jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 20,419
- 39,217
Mungu anataka fungu la kumi la nini kama kila kitu ni chake na yeye ni muweza wa yote
Peleka kwa yatima au wajane mkuu.
Wote ni watafutaji pesaUlitaka ziwepo baa na kumbi za starehe?
sasa walawi wanahusiana vipi na mimi msandawe?Kama huwelewi maandiko omba uelekezwe,fungu la 10 lilitolewa maalumu kwa wana walawi waliokua ni makuhani na waangalizi wa hekalu,ambao hata katika urithi wa ardhi hawakupewa,hivyo ili waishi na kuendelea kuhudumia hekalu fungu la 10 lilipelekwa hekaluni
Acha uongo kwahiyo kanisa ni ghala?Leteni zaka kamili Ili kiwemo chakula katika nyumba yangu....zaka ni ya Mungu peleka madhabahuni....wahitaj utawasaidia Kwa pesa tofaut na zaka
Kwahiyo zaka mnayotoa inafanya uinjilishaji na utume? Wapi umeona hiiNdio utulie tuwekane sawa,huo utamaduni na muongozo uliingia hadi katika kanisa la kwanza la kristo,kila sehemu ya 10 ya mapato yalipelekwa kani sana ili kuipa nguvu kazi ya utume na uijilishaji,na hii inafanyika hadi sasa.
Bila hivyo kazi ya utume na uinjilishaji ingekuwa ngumu ndio maana kanisa linaendelea kusisitiza utoaji wa zaka kwa lengo hilo.
Wanawalawi kwa sasa hawapo ila ile kazi yao sasa ni sawa na inayofanyika katika kanisa la leo.
Soma na sura ya 14 anzia mstari wa 22 hadi mwisho paleKumbukumbu 26:12
“Utakapokwisha kutoa zaka, katika zaka zote za maongeo yako mwaka wa tatu, ambao ndio mwaka wa kutolea zaka, umpe zile zaka Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane, wapate kula ndani ya malango yako na kushiba;”
Nani unamjua ww kabarikiwa kwa kutoa zaka?Peleka madhabahuni utaona jinsi utakavyo barikiwa kuwasaidia yatima sio mbaya unaongezewa dhawabu zaidi ila asilimia ya Mungu ni ya Mungu
Kwanini ipelekwe huko na wasipewe ambao tunadhani wanahitajiMkuu hiyo ela pelekea watu wenye uhitaji, japo fungu la kumi linapaswa kwenda kanisani.
Nakuomba hiyo pesa pelekea watoto wenye kuishi mazingira magumu, kama utashindwa kufanya hivyo kula mbuzi choma mpaka hiyo pesa iishe.
Kama ni mkristo agiza kitimoto nusu nusu mpaka pesa iishe utaongeza afya na utapata nguvu ya kutafuta nyingine.
Wako brainwashed hawatakuelewaKuikamilisha maana yake TO PUT AN END OF. Kuweka NUKTA.. Biblia inasema Kristo ni MWISHO wa sheria. Wakristo hawapo chini ya Torati..
Pili, Kama mnafuata Torati kwa nini hamuifuati yote mnachagua tu fungi la kumi?
Tatu, wewe ni myahudi? Kabila lako ni lipi kati ya yale 12?
Mchungaji wako ni Kuhani? Ni kuhani wa kabila gani? Ni wapi Mungu amemuagiza mchungaji wako apokee zaka?
Watakupa kale ka andiko Yesu akiwachana mafarisayo ili tu kulazimisha mambo yaoHakuna sehemu yesu amezungumxia Zaka mkuu acha kuongopa...
Hivi huwa hamuoni Aibu kuongopa kwa ajiki ya maslahi yenu binafsi
Mafundisho ya wapi haya ni kwa mujibu wa maandiko ganiKIBIBLIA fungu la kumi linatakiwa liende kanisani hakuna MBADALA ..hiyo inaitwa ZAKA (TITHES) maana yake ni kurudisha Kwa Mungu madhabahuni.....yatima ,masikini etc wanapelekewa sadaka..na makanisa mengi fungu la kumi ni Kwa ajili ya kulipa mishahara wachungaji ...wewe peleka kanisani umeshamaliza sehemu yako mbele za Mungu ...kama unadhani kanisa unalosali halistahili kupelekewa sadaka either ni la nabii fake etc basi unasali sehemu sio sahihi....Hifadhi vizuri ZAKA zako Kwa uaminifu tafuta kanisa sahii peleka...
Wengine wana hadi namba za lipa pesa!Fungu la Mungu au fungu la mchungaji? Hawa hawa manabii wetu wa siku hizi uwapelekee fedha halafu useme umepeleka kwa Mungu? Hawa hawa kina Gwajima na Mzee wa Upako au kina Mwamposa? Kina 'nabii'' Malisa?
Hakuna Walawi bongo.Kama huwelewi maandiko omba uelekezwe,fungu la 10 lilitolewa maalumu kwa wana walawi waliokua ni makuhani na waangalizi wa hekalu,ambao hata katika urithi wa ardhi hawakupewa,hivyo ili waishi na kuendelea kuhudumia hekalu fungu la 10 lilipelekwa hekaluni