Je, Rais Magufuli alikuwa na Pacemaker au Defibrillator? Ilidukuliwa?
Mkuu kwanza hongera sana kwa andiko lako zuri,umeandika vyema na kwa utulivu kiasi,ingiwa mwishoni umehitimisha kwa namna ambayo haina afya sana kwa msomaji wako,kuhusiana na kumshutumu mtoa taarifa juu ya kutoonekana kwa rais (Tundu Lisu).

Kwanza inapaswa utambue kuwa kutoa taarifa(baada ya kupata tetesi) haimfanyi mtoa taarifa kuhusika na tukio moja kwa moja.

Pili,kwa kiwango cha upinzani juu ya serikali,umaarufu na madhila aliyokutana nayo mtoa taarifa,ni wazi kuwa lazima atakuwa na vyanzo vya kuaminika kutoka kwenye system juu ya mambo mengi yanayoendelea humo,unaweza kujiuliza kwanini,lakini jibu la hakika ni kuwa,sio wote waliopendezwa na yaliyotokea juu yake mchana ule kule Dodoma,kumbuka ana marafiki wengi ndani na nje ya utumishi wa umma aliokuwa amehudumu kwa kipindi kirefu,hivyo kuleak kwa taarifa na kuzipata ni jambo rahisi.

Tatu,kumhususisha mtoa taarifa na majasusi ambao walitaka sijui Magufuli ashindwe uchaguzi sio sahihi,sote tulikuwa hapa nchini ,kilichotokea kwenye uchaguzi huo kinajulikana kabisa bila mashaka kwamba haukuwa na credibility yoyote ya kuitwa uchaguzi huru na wa haki(Rejea tamko la Election Observers kutoka East Africa). Upinzani wa Lissu sio wa kutiliwa mashaka kuwa anatumika sijui na mabeberu,amekuwa ni mwanaharakati long ago,kabla hata hajaingia kwenye siasa(Rejea Issue ya North Mara - Nyamongo).

Nne,taarifa za kuchafuliwa kwa mtu huyu zimepigiwa debe na watu wasio na creadibility ya kutoa taarifa kama Cyprian Musiba mara baada ya kwenda ughaibuni kwa ajili ya matibabu zaidi,hapo ndipo ilipanza kusikika oooh anatumiwa na mababeru,sijui wanadhamini matibabu yake ili aje kupinga maendeleo yanayoletwa na Mh hayati Magufuli nk,kwa mtu mwenye akili hapa atajiuliza maswali matatu kama sio matano.
1.Je,kutibiwa nje ya nchi ni kosa,na nini kilipelekea yeye kupigania uhai wake ndani na nje ya nchi,kuna uchunguzi wowote juu ya tukio la kutaka kuuwawa kwa risasi nyingi mchana kweupe katika very monitored area?
2.Serikali iligharamia matibabu yake akagoma?.
3.Hapa nchini kuna hospital ambayo ingeweza kumtibu kwa kiwango cha majeraha yake?.
4.Je,ni mwanasiasa wa kwanza kutibiwa nje?
5.Mtoa taarifa (Cyprian Musiba na wenzake) ni watu wa mlengo gani?

Mwisho,upo ushahidi wa kisayansi kuwa ni kweli pacemaker inaweza kuwa hacked, LAKINI hakuna hata mtu mmoja amewahi ku be hacked, zaidi sana anayefanya hacking sharti awe mita chache kutoka alipo mgonjwa(within 20 feet),hili linaondoa uwezekano wa watu kutoka nje kumonitor pacemaker ya rais,swali fikirishi ikiwa kweli imehakiwa na kupelekea kifo cha rais,ni nani huyo?(maana lazima awe mtu aliye kwenye compaund ya victim,na uhusika wa Lissu unatokea wapi?.

NB.Chochote kinawezekana katika ulimwengu wa ujasusi,visasi na madaraka(siasa).



View attachment 1733034View attachment 1733035
Screenshot_20210324-075759_1.jpg
 
Haha hahah haha.
Magufuli alikuwa a walking dead, hakuwa na afya, alikuwa very much short tempered, alikuwa na dalili zote za kufika ukingoni mwa maisha.
Pacemaker haikufanyi uishi milele.
Pia Magufuli hakuwa threat kwa dunia hadi wamuue.
Kama PSU walijua njia rahisi ya adui kumdhuru raisi ni kupitia kudukua pacemaker yake, walichukua tahadhari gani kuiwekea Artificial Intelligene security Ili Kama iki sense kwamba inaingiliwa itoe taarifa?
Waliiwekea backup system gani ili kama ikiwa hacked backup ifa ye kazi?

Mbona majibu ya maswali yako yapo kwenye hii story ya jamaa inaonekana hujitambui [emoji2373]
 
Hakuna mwanadamu anayeweza kumuua mwingine bila Mungu kuachilia, na Mungu huachilia ili aweze kufanya malipizi kwa sifa na utukufu wake kama alivyofanya kwa Samson hata kwa Yesu

Kama wapo waliopewa pesa ili kumuua kama Yudas alivyofanya kwa Yesu, wakumbuke tuu kwamba

"Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa." Mathayo 26:24
 
Nitashangaa kama seriki ya CCM chini ya Mh Rais Samia inatamuacha Tundu Lissu salama bila kumwajibisha.Anatakiwa akamatwe atuambie hao waliyompa information ( from America and sound Africa) na Lengo Lao ilikuwa nini? Walijuaje?
Ingekuwa mimi condition ya kurudi Tanzania na kuitwa Mtanzania ni kuwataja hao informa wake.
Wazo zuri sana! Lakini Ni Mkuki kwa nguruwe? Hiyo Serikali ambayo inapotezea uchunguzi wa aliyemimina risasi Zaidi 30 kwa Lisu, ijihangaishe kumchunguza Tundu Lisu kuhusika na kifo cha Jiwe kilicho sababishwa na kukatika kwa Umeme kwenye moyo wa Jiwe?
 
Wazo zuri sana! Lakini Ni Mkuki kwa nguruwe? Hiyo Serikali ambayo inapotezea uchunguzi wa aliyemimina risasi Zaidi 30 kwa Lisu, ijihangaishe kumchunguza Tundu Lisu kuhusika na kifo cha Jiwe kilicho sababishwa na kukatika kwa Umeme kwenye moyo wa Jiwe?

Unajua kuna watu wanastahili kabisa kufa we kila unalofanya zuri yeye anaforce lionekane baya kwa wananchi mara cjui anapeleka umbeya USA kwamba Tz huko nini kinaendelea huyo msaliti wa nchi yetu [emoji706][emoji706] kabisa
 
Yote uloelezea yanaweza kuwa ni kweli lkn huyu Magufuli alikuwa mgonjwa zamani aliwahi kufanyiwa opearation wa moyo toka anasoma lkn nyumbani watu ni wajinga sana wao ni ushabiki tu japo mtu hapati chochote hana maslahi na jambo lolote pili Magu alikuwa kisirani sana kampuni ngapi kazitia hasara kufunga mikataba yao japo hasara ni ya Tanzania wao wanakwenda kushtaki koti za kimataifa wanapewa pesa zao lkn lengo kwa kampuni ni kuonesha project zao kwa ajili ya kupata kazi nyengine .Sasa watu wengi wanafikiria huu ulimwengu wote duniani ni sawa sawa tu kama uko kariakoo , hawajui kama kuna vita ya kila aina unaweza kubadilishiwa prescription yako ya dawa unazotumia na wadukuaji na ikawa ni sumu kwako so afya ya kiongozi yyote yule mwana siasa ajue ni silaha kwake unaweza kumalizwa mara moja tu .
Jamaa alijitengenezea maadui wengi Tu bila sababu za msingi , sometyme na kiburi tuu, maamuz ya kukurupuka tumepata hasara ya kuyalipa makampuni mengi tuu, alikuwa anakopa hela huko nje alaf anatudanganya ni Fedha za ndani , ametukaba na mikodi mingi Sana ya kuumiza na akaminya mzunguko wa hela , lakni pesa yote anapeleka kwenye miradi ya ajabu ajabu tuu.....

Matajiri wengi Tu kawatia hasara , alitamani wote tuwe tunapata hela ya Kula tuu, alaf mtu akiteseka na upambanaji wa mtaani ndo anashangiliwa et anapambana , unapambana nin wazee unaishia kupata hela ya Kula tuu...

Majengo mengi Tu yamebaki kama popo Dar es salaam , wakat Kikwete anatoka madarakani Dar es salaam ilikuwa fastest growing city in sub Saharan Africa...lakn Leo ipo wapi ? Makampuni ya nje yalikuwa yanakimbizana kuwekeza bongo , mji umekufa Kwa maamuz ya hovyo hovyo tuu

Alifanikiwa kuwabrainwash Sana watanzania wengi Kwa sababu wengi Elimu Yao inatia mashaka they can't think beyond ....

Alichofanikiwa Tu ni miundo mbinu ya barabara na majengo ya umma hcho ndo naweza kumsifu Ila Nyanja nyingine ni terrible .... Ni kweli tulimshangilia wakat anaingia madarakani lakn the guy was not smart enough aisee ......

Kwangu Mimi still Kikwete na ufisadi wake wote alikuwa far better kuliko JPM

Kuhusu Afya yake Mwamba ilianza kuzorota kitambo tuu , na hii ilimstua hata Makonda akaamua kuachia ofisi , hapa mwishoni mwishoni Hali yake ilibadirika ....tunaweza kusingizia vitu vingi lakn yeye Kwa Hali yake ya Afya alikuwa vulnerable Sana na Korona , ... Apumzike Kwa Amani
 
Unajua kuna watu wanastahili kabisa kufa we kila unalofanya zuri yeye anaforce lionekane baya kwa wananchi mara cjui anapeleka umbeya USA kwamba Tz huko nini kinaendelea huyo msaliti wa nchi yetu [emoji706][emoji706] kabisa
Basi nimekuelewa vizuri kiongozi,aliyestahili kufa kweli kafa,asiyestahili kabaki,God is really awesome,his love is low down and upper above,glory to his name [emoji120]
 
Back
Top Bottom