Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Urais ni zao la wakati.. Na sio kutaja majina kabla ya wakati..Wakati utakapofika ni vyema matatizo ya nchi yakaainishwa.. Kisha tukachagua mwenye uwezo wa kuyatatua matatizo hayo kati ya wale watakaokuwa wamejitokeza..
 
Shida ya Lissu anasahau kuwa hii Katiba ya Nyerere ya 1977 imempa nguvu nyingi Rais, anarakiwa kulifahamu na kulitii hilo kwanza kabla ya mambo mengine. Mfano, Lissu alichangia sana kuvunjila kwa mchAkato wa uandishi wa Katiba mpya 2015 kwa kung'ang'ania Lazima, lazima, lazima serikali 3. Mambo yote mule yalikuwa safi ikiwemo tume huru ya uchaguzi na uchaguzi kuhojiwa mahakamani lakini watanzania waliikosa katiba mpya kipindi kile kwasababu ya akina Lissu kutoka nje na kuunda UKAWA. Angekuwa mtu mwenye staha angekubali kwa kuvumilia Katiba mpya nzuri lakini yenye muungano wa serikali 2 na akishaupata Urais angekuwa na nguvu za kuandika tena Katiba yenye serikali 3 au muungano wa mkataba kama wanavyotaka. Lakini walikuwa na jazba kubwa sana ya kutaka vitu vyote leoleo.

..kilichowazuia Ccm 2014 kutuletea katiba yenye mambo mzuri isipokuwa serikali 3 ni nini?

..au kitu gani kinawazuia Ccm kutupatia katiba nzuri sasa hivi wakati wameshikilia mihimili yote?
 
Urais ni zao la wakati.. Na sio kutaja majina kabla ya wakati..Wakati utakapofika ni vyema matatizo ya nchi yakaainishwa.. Kisha tukachagua mwenye uwezo wa kuyatatua matatizo hayo kati ya wale watakaokuwa wamejitokeza..
Hapata, baba wa taifa (RIP) aliwahi kusema, wale wote wanaotaka kuwa wagombea lazima wajulikane mapema ili watu wapate muda mrefu wa kuwajadili. Alisema kuwa kama CCM ikishamtangaza mgombea wao itakuwa tayari imeshamtangaza Rais wa nchi hii kwa 99.99%. Bahati nzuri CCM tayari wameshamtangaza mgombea wao 2025 mapemaa kuwa ni Rais Mama Samia, hivyo ni vema na wagombea wa upinzani wakajulikana mapemaa ili wananchi tupate muda wa kuwafahamu na kuwachambua vya kutosha kama hivi tunavyofanya kwa mama Samia na Lissu. Hii ni afya kwa wapiga kura, wagombea na taifa pia, wasichukie watu wanapowadadavua mapema madhaifu na mazuri Yao.

Uchaguzi wa Marekani ni 2024, mchAkato rasmi wa wagombea bado lakini watu tayari wanawadadavua Trump na Biden kwakuwa Trump kaonyesha Nia ya kuhombea tena kupitia Chama chake Cha republican.
 
Hapata, baba wa taifa (RIP) aliwahi kusema, wale wote wanaotaka kuwa wagombea lazima wajulikane mapema ili watu wapate muda mrefu wa kuwajadili. Alisema kuwa kama CCM ikishamtangaza mgombea wao itakuwa tayari imeshamtangaza Rais wa nchi hii kwa 99.99%. Bahati nzuri CCM tayari wameshamtangaza mgombea wao 2025 mapemaa kuwa ni Rais Mama Samia, hivyo ni vema na wagombea wa upinzani wakajulikana mapemaa ili wananchi tupate muda wa kuwafahamu na kuwachambua vya kutosha kama hivi tunavyofanya kwa mama Samia na Lissu. Hii ni afya kwa wapiga kura, wagombea na taifa pia, wasichukie watu wanapowadadavua mapema madhaifu na mazuri Yao.

Uchaguzi wa Marekani ni 2024, mchAkato rasmi wa wagombea bado lakini watu tayari wanawadadavua Trump na Biden kwakuwa Trump kaonyesha Nia ya kuhombea tena kupitia Chama chake Cha republican.

..Samia hana uwezo wa kushindana na Lissu kwa hoja.

..Lissu ni msomi mzuri kuliko Samia na ana uelewa mpana wa masuala mengi ya kiuongozi na kiutawala.

..Lissu pia ana historia ya kutetea wanyonge wa nchi yetu na ni mwanasiasa ambaye hajachafuka kwa rushwa.

..Samia amemzidi Lissu kwasababu yuko ndani ya serikali hivyo dola na mifumo yote inambeba.
 
Hii nzito sana
Nchi inatawaliwa na mbulu….ziii
Tunayataka wenyewe
Guinea Leader anewaambia wa western ‘stop lecturing us… military intervention is….. UN General Assembly last week
Western model of democracy is not for Africa… Yes indeed sio kabisaaa.

ujinga wetu umetufikisha hapa…
Hata hiyo 'democracy' huko kwao imegota.
 
Wanazo zote na za ziada ndio maana uchaguzi wa mwaka tulimshauri Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Ila kwa uchaguzi wa 2025, niliwaomba Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! hivyo iwapo CCM itamsimamisha mgombea Mwanamke, TL asigombee maana itakuwa ni aibu kushindwa na Mwanamke!.

Unless kama sauti hii ni yake YEYE, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke then TL agombee, wapambane!.

P
Bwana Mayalla, kwamba TL akishindwa na mwanamke itakuwa ni aibu??? Hii comment yako imeniacha na maswali mengi Sana....kwamba:

Kama ni aibu kwa Tundu Lisu, je, ni aibu kwa Watanzania wote wanaume kuongozwa na mwanamke?

Je, mwanamke ni kiumbe thaifu dhidi ya mwanaume, au una maana gani?

Je, una lengo la kudharirisha wanawake?
 
Hii nzito sana
Nchi inatawaliwa na mbulu….ziii
Tunayataka wenyewe
Guinea Leader anewaambia wa western ‘stop lecturing us… military intervention is….. UN General Assembly last week
Western model of democracy is not for Africa… Yes indeed sio kabisaaa.

ujinga wetu umetufikisha hapa…

..hii tuliyonayo Tz ni demokrasia yetu pekee, sio demokrasia ya magharibi.

..demokrasia ya Tz tume ya uchaguzi inateuliwa na mwenyekiti wa chama tawala.

..demokrasia ya Tz wasimamizi wa uchaguzi ni makada wa chama tawala.

..demokrasia yetu haifanani hata kidogo na demokrasia ya magharibi.

..Watz tuache kutafuta visingizio huko nje mambo yanapotuharibikia.
 
..Samia hana uwezo wa kushindana na Lissu kwa hoja.

..Lissu ni msomi mzuri kuliko Samia na ana uelewa mpana wa masuala mengi ya kiuongozi na kiutawala.

..Lissu pia ana historia ya kutetea wanyonge wa nchi yetu na ni mwanasiasa ambaye hajachafuka kwa rushwa.

..Samia amemzidi Lissu kwasababu yuko ndani ya serikali hivyo dola na mifumo yote inambeba.
Watu wanataka maji, hospital, barabara, umeme, chakula, mkongo, ajira na amani hawataki maneno na uelewa wa Ulaya sijui sheria. Sheria zote muhimu sana kwetu ziko kwenye Katiba ya nchi.
 
Bwana Mayalla, kwamba TL akishindwa na mwanamke itakuwa ni aibu??? Hii comment yako imeniacha na maswali mengi Sana....kwamba
Hakunaga mashindano yoyote kati ya mwanaume na mwanamke, wanaume wanatakiwa kushindana na wanaume wenzao, wanawake na wanawake wenzao. Mwanaume ukishindana na mwanaume mwenzio ukashindwa, its normal umezidiwa, lakini mwanaume ukishindana na mwanamke ukashindwa kiukweli ni aibu!. Hii sio mara yangu ya kwanza kushauri mtu asigombee kuepuka aibu ya kushindwa!. Uchaguzi wa 2015 kwa Zanzibar, nilishauri hivi, Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein hawakusikia wakamsimamisha na kweli ali... ilibidi Jecha kuokoa jahazi kwa kupindua meza!. Mwanaume rijali uneyesimama kushindwa na mwanamke anayechuchumaa ni aibu!. Sometimes bora kufa kishujaa huku umesimama kuliko kuishi huku umepiga magoti!. Lissu ni shujaa msimuaibishe!
Kama ni aibu kwa Tundu Lisu, je, ni aibu kwa Watanzania wote wanaume kuongozwa na mwanamke?
It's the other way round, yaani kitendo cha Mwanamke kuongoza nchi ni credits kubwa sana kwa Mwanamke kufuatia mfumo dume kuwa vitu Mwanamke hawezi, ukiwemo urais!, hivyo huyu Mwanamke ame wa prove wrong kwa kuonyesha uwezo kuliko wale wanaume 4!. Je, kuna kazi za kike na za kiume? Fupa hili lililowashinda wanaume wanne, mwanamke mmoja ataliweza?
Je, mwanamke ni kiumbe thaifu dhidi ya mwanaume, au una maana gani?
Hili mbona sio swali ni jibu, kwani wewe unaonaje kuhusu strengths na weaknesses kati ya mwanamke na mwanaume, wanafana?. Mwanamke ni kiumbe dhaifu ila kuna wanawake wa shoka, they are strong than men!. Wanawake wengine wenye kujitambua kuhusu strength of a woman, they use that strength and becomes above men!. Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?
Je, una lengo la kudharirisha wanawake?
No sina lengo la kudhalilisha wanawake bali kumuepushia aibu huyu shujaa wetu, mtu kushindwa na Mwanamke ni aibu ya mwaka, ambayo itapelekea ahamie kule jumla!.
P
 
Hakunaga mashindano yoyote kati ya mwanaume na mwanamke, wanaume wanatakiwa kushindana na wanaume wenzao, wanawake na wanawake wenzao. Mwanaume ukishindana na mwanaume mwenzio ukashindwa, its normal umezidiwa, lakini mwanaume ukishindana na mwanamke ukashindwa kiukweli ni aibu!. Hii sio mara yangu ya kwanza kushauri mtu asigombee kuepuka aibu ya kushindwa!. Uchaguzi wa 2015 kwa Zanzibar, nilishauri hivi, Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein hawakusikia wakamsimamisha na kweli ali... ilibidi Jecha kuokoa jahazi kwa kupindua meza!. Mwanaume rijali uneyesimama kushindwa na mwanamke anayechuchumaa ni aibu!. Sometimes bora kufa kishujaa huku umesimama kuliko kuishi huku umepiga magoti!. Lissu ni shujaa msimuaibishe!

It's the other way round, yaani kitendo cha Mwanamke kuongoza nchi ni credits kubwa sana kwa Mwanamke kufuatia mfumo dume kuwa vitu Mwanamke hawezi, ukiwemo urais!, hivyo huyu Mwanamke ame wa prove wrong kwa kuonyesha uwezo kuliko wale wanaume 4!. Je, kuna kazi za kike na za kiume? Fupa hili lililowashinda wanaume wanne, mwanamke mmoja ataliweza?

Hili mbona sio swali ni jibu, kwani wewe unaonaje kuhusu strengths na weaknesses kati ya mwanamke na mwanaume, wanafana?. Mwanamke ni kiumbe dhaifu ila kuna wanawake wa shoka, they are strong than men!. Wanawake wengine wenye kujitambua kuhusu strength of a woman, they use that strength and becomes above men!. Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?

No sina lengo la kudhalilisha wanawake bali kumuepushia aibu huyu shujaa wetu, mtu kushindwa na Mwanamke ni aibu ya mwaka, ambayo itapelekea ahamie kule jumla!.
P
Kule mashuleni na vyuoni wanaume hawashindwi na wanawake darasani, kwenye tafiti/machaposho?
 
Kule mashuleni na vyuoni wanaume hawashindwi na wanawake darasani, kwenye tafiti/machapisho?
Wanashindwa ila sio aibu kwasababu ni mitihani ni mashindano kwa wote hujui unashindana na nani, hivyo mwanamke akiibuka kidedea, ni wewe tuu ndio unajiaibikia ndani yako kushindwa na demu, lakini hauabiki na jamii, lakini hii ya kujua CCM itasimamisha Mwanamke 2025, halafu Chadema ikasimamisha mgombea mwanaume, mwanaume huyo akishindwa na mwanamke ni aibu!.
Nimewashauri Chadema na wapinzani Iwapo Watanzania wataamua 2025 twende na Mwanamke, mnaonaje tukiwashauri CHADEMA wasimamishe Mwanamke? Maana Mwanaume kushindwa na Mwanamke ni aibu!
P
 
Watu wanataka maji, hospital, barabara, umeme, chakula, mkongo, ajira na amani hawataki maneno na uelewa wa Ulaya sijui sheria. Sheria zote muhimu sana kwetu ziko kwenye Katiba ya nchi.
..samia na ccm yake wameshindwa kutuletea yote hayo uliyoyataja, pamoja na katiba bora, hivyo wanastahili kupumzishwa.
 
Mtu yeyote ambaye hayuko mentally stable hana sifa zozote zinazomqualify kuwa rais. Tuweni serious na urais wa nchi, tafadhali.
 
Rais wa nchi yetu awe na sifa zipi?

Je, ni nani anazo sifa nyingi za kuwa Rais ajae? Je, Tundu Lissu anazo sifa hizo pia?
Sifa anazo tele kwa mujibu wa katiba yetu. Mpeni kura za ndio
 
Wanashindwa ila sio aibu kwasababu ni mitihani ni mashindano kwa wote hujui unashindana na nani, hivyo mwanamke akiibuka kidedea, ni wewe tuu ndio unajiaibikia ndani yako kushindwa na demu, lakini hauabiki na jamii, lakini hii ya kujua CCM itasimamisha Mwanamke 2025, halafu Chadema ikasimamisha mgombea mwanaume, mwanaume huyo akishindwa na mwanamke ni aibu!.
Nimewashauri Chadema na wapinzani Iwapo Watanzania wataamua 2025 twende na Mwanamke, mnaonaje tukiwashauri CHADEMA wasimamishe Mwanamke? Maana Mwanaume kushindwa na Mwanamke ni aibu!
P
Ni kweli kaka, hata baba alikuwa ananiambia usishindane na dada zako kwenye kwenda kuchunga ng'ombe, na na mama aliwaambia dada zangu msishindane na kaka yetu kwenye kupika na kuosha vyombo, hata pocket money ya shule dada walikuwa wakipewa kubwa kuliko mimi kwasababu ambazo nilikujaelezwa baadae sana. Ni heri akapima kina cha maji kwa kutumbukiza fito badala ya kuyapima kwa kutumbukia mwenyewe. Mama Samia ni mmoja tu tangu tupate Uhuru miaka zaidi ya 60 iliyopita, wacha amalizie miaka yake 5 mingine kisha turudi kwenye mminyano wa wavaa kaptura menyewe kwa menyewe.
 
Shida ni kiburi,Jeuri,dharau na ubishi pamoja na ubabe kisu anachotumia kuwachinjia mahasimu wake akiwamaliza ataturudia sisi wanyonge tutaburuzwa mpaka basi.

Sifa za Rais lazima awe muungwana asimamie mifumo yote ijiendeshe kwa Sheria tulizokubaliana waajiliwa na wateuliwa wote watimize wajibu wao.

Kila Mwananchi atende wajibu wake na ajione kwamba ni mwenye nchi hii na vizazi vijavyo vinayo haki ya kunufaika na matunda yatakayopatikana.
 
Rais wa nchi yetu awe na sifa zipi?

Je, ni nani anazo sifa nyingi za kuwa Rais ajae? Je, Tundu Lissu anazo sifa hizo pia?
Ni nani huyo aliyewahi kum-rule out TL kuwa hana sifa za kuwa Rais wa JMT?
 
HIZI ZOTE NI POROJO MFU. Kinachotakiwa ni kuwa na uchaguzi huru na wa haki utakaowezesha Watanzania kuchagua Rais wanayemtaka, period. Wao ndio wanajua sifa za Rais wanayemtaka. Watanzania wana haki HATA ya kukosea katika uchaguzi ilimuradi anayechaguliwa akiharibu, wawe na uwezo pia wa kumbadili kwa kura katika uchaguzi unaofuatia. Ikibidi hata kumchukulia hatua za kisheria.
Mkuu 'Drifter', nisingeweza kuliweka hili vizuri kuliko ulivyolieleza hapa mwenyewe. Ninakupongeza sana kwa uwezo wako huu wa kujieleza vizuri.

Sasa tunaona jitihada zinazofanywa kwa maksudi kabisa, kuwachanganya akili wananchi kwa mbinu zilizochoka kama zinavyowasilishwa na haya makundi yanayozileta kwenye jukwaa hili na kwingineko, kujaribu kuvuruga tu akili za wananchi wasitumie haki yao ya kuwachagua viongozi wanaowataka wenyewe.
 
Back
Top Bottom