Jua Kali latawala Tanzania: Hali ya Hewa kila Mkoa na Uzoefu wako ni upi?

Jua Kali latawala Tanzania: Hali ya Hewa kila Mkoa na Uzoefu wako ni upi?

Fuh
Takwimu za hivi majuzi zinaonyesha joto limeongezeka sana kwa viwango vya kutisha, katika sehemu mbalimbali duniani.

Here are some of the hottest recorded temperatures in 2024:
Ouargla, Algeria – 51.3°C
Basra, Iraq – 52.6°C
Ahvaz, Iran – 53.0°C
Kuwait City, Kuwait – 52.1°C
Jacobabad, Pakistan – 51.2°C
Delhi, India – 49.9°C
Phoenix, USA – 48.3°C
Seville, Spain – 47.6°C

Viwango hivyo vya joto lililopitiliza havijawahi kushuhudiwa tangu wanasayansi waanze kutunza record za viwango vya joto.

Wanasayansi wanasema ongezeko hili la joto linatokana na mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na shughuli za binadamu, kama vile uzalishaji wa gesi joto kutoka viwandani na ukataji miti.

Biblia, iliishatabiri juu ya kuongezeka kwa joto. Katika Ufunuo wa Yohana 16:8-9 tunasoma juu ya mabakuli ya ghadhabu ya Mungu yatakayomwagwa juu ya jua...

"Kisha malaika wa nne akamwaga bakuli lake juu ya jua. Jua likapewa nguvu ya kuwachoma watu kwa moto wake. Basi, watu wakaunguzwa vibaya sana; wakamtukana Mungu aliye na uwezo juu ya mabaa hayo. Lakini hawakutubu na kumtukuza Mungu."

Ni ajabu sana. Watu wanaunguzwa, badala ya kutubu dhambi ndio wanakazana kumtukana Mungu na kusema eti hayupo.

Joto hili kali si jambo la kawaida—wanasayansi wamethibitisha kuwa limeongezeka kwa kasi, na Biblia ilishatabiri nyakati hizi. Huu ni wakati mwafaka wa kutubu maovu na kumrudia Mungu, na kujiandaa kwa ujio wa Yesu Kristo(Ufunuo 22:12).

Chonde, chonde, kama hujaokoka, usisubiri hadi iwe too lateDuh
 
Viwango hivyo vya joto lililopitiliza havijawahi kushuhudiwa tangu wanasayansi waanze kutunza record za viwango vya joto.
Hawa wanasayansi nao, mwaka 2020 na 2021 huko Marekani joto liliwahi kufika hadi 54.4⁰C. Wao walikuwa hawajaanza kutunza tu hizo records?
 
Hawa wanasayansi nao, mwaka 2020 na 2021 huko Marekani joto liliwahi kufika hadi 54.4⁰C. Wao walikuwa hawajaanza kutunza tu hizo records?
Joto la 2024 limewekwa katika muktadha wa joto kali zaidi duniani kwa wastani, si kwa rekodi ya joto la juu zaidi kihistoria. Hiyo inamaanisha kwamba wastani wa joto katika sehemu mbalimbali duniani mwaka 2024 ulivunja rekodi za awali, lakini haimaanishi kuwa lilifikia kiwango cha juu kuliko kile cha Death Valley mwaka 1913 (56.7°C).
 
Joto la 2024 limewekwa katika muktadha wa joto kali zaidi duniani kwa wastani, si kwa rekodi ya joto la juu zaidi kihistoria. Hiyo inamaanisha kwamba wastani wa joto katika sehemu mbalimbali duniani mwaka 2024 ulivunja rekodi za awali, lakini haimaanishi kuwa lilifikia kiwango cha juu kuliko kile cha Death Valley mwaka 1913 (56.7°C).
Sawa nimeelewa. Hiyo ya 1913 hata wao tu wanapingana
 
Dar tupo na nyie hadi joto liniue mje
 

Attachments

  • IMG_20250303_171405_582.jpg
    IMG_20250303_171405_582.jpg
    719.1 KB · Views: 2
Mbeya Jana mvua imeshuka kubwa na kibaridi juu, hapa Kuna upepo mzuri labda mida ya saa sita hadi kumi ndo huwa Kuna joto,ila saizi nipo kuota moto na sweta nimevaa
 
Back
Top Bottom