Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hawajitolei maisha yao kutulinda, wanalipwa ili kutulinda. Hii ni kazi waliyoamua wao kuomba ili waajiriwe kuifanya. Hivyo wanatekeleza majukumu yao.Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
nimeamini siku moja tu inatosha kuprove ujuha wa professorMnaoandika hovyo msifikiri JF haina limit ya kuwalinda.
Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana.
Eleweni kuwa hii mitandao hakuna pakujificha na hakuna kinachofutika hata wewe ukifuta.
Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
Asiesikia la mkuu huvunjika guu, hakuna marefu yasio na ncha, safari 1 huanzisha nyingine, za mwizi 40, Simba mwenda Pole ndio hula..., Za kuambiwa changanya na Zako,msije mkasema hakukumbushwa
Kula chuma hiko
---
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema siku saba zilizotolewa kusalimisha mavazi yanayofanania na sare za jeshi kwa hiari zimeisha, hivyo jeshi litaingia kuzisaka nguo hizo kwa wananchi.
Kaimu mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano na Msemaji wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda amesema jeshi halina utani katika suala hilo, kwani katazo hilo ni kwa mujibu wa kifungu cha 99 cha Sheria ya Ulinzi wa Taifa (NDA) Sura ya 192 sheria namba 24 ya mwaka 1966 yaliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 pamoja na kifungu cha 178 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16 na kifungu cha 6 cha Sheria ya Usalama wa Taifa.
“Muda wao wa kusalimisha kwa hiari umeisha, kama mtu atakuwa hajasalimisha basi tutazifuata wenyewe, na mtindo upi tutatumia kuzichukua kwa wananchi tunajua wenyewe,” amesema Kamanda Ilonda.
Ameongeza kuwa sheria inakataza kutengeneza, kuagiza, kuuza na kutumia sare za JWTZ au zinazofanana na sare hizo bila kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika.
Tatizo mnaongea sana tena Kwa matusi na kejeli.Kwanza wajue kabisa wanavunja katiba na sheria za nchi.
Chombo PEKEE ambacho kina idhini kikatiba kufanya msako au upekuzi ni Jeshi la polisi, ikiwa nchi haiko katika hali ya hatari.
Hatujawahi kusikia kwamba Tanzania katika kambi yoyote ya Jeshi, kumeibiwa sare za Jeshi na hivyo wanaanza msako kizikamata.
Hatujaskia kwamba Kuna fununu au taarifa kwamba Kuna watu au kikundi Cha watu au kampuni imeingiza sare za Jeshi Tanzania ama Kwa Nia ovu au ya kibiashara.
Hakuna mahali katika sheria za nchi askari wa Jeshi anaruhusiwa au kupewa mamlaka ya kufanya upekuzi au upelelezi juu ya makosa ya uhalifu isipokua jukumu lao ni kuhakikisha mipaka ya nchi Iko salama muda wote.
Hii inaleta picha nyingine tofauti inayofuatana na ya Jeshi la polisi kutuambia watu flani walipanga uhaini. Hivyo tuamini kwamba ndani ya muda mfupi hata ndani ya Jeshi kulikua na sura ya uasi na Kwa maana hiyo askari wa Jeshi wameiba sare na kuwapatia wananchi au paramilitaries Kwa ajili ya kujiandaa na Mapinduzi husika.
Nchi inakua banana republic na Kwa maana hiyo Kila mtu anaonesha tentacles, mnafanya nchi ionekane kituko duniani Kila uchwao,. Sijui ni elimu Gani Hawa watu wanasomea hawajui Sheri, katiba na wajibu wao.
Law enforcement ni jukumu la polisi sio jeshi. Labda kwa watumishi wa jeshi tu ndio wana vitengo vyao vya sheria na mahakama za jeshi.Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana
Nani anajitolea?Wamelazimishwa kujitolea?
😁😁😁😁 huo muda wa police kufanya hivyo umeisha, na ukishaona hawa wameingilia jambo ujue kazi ipo. Uzuri walitoa tangazo na siku za kufata maelkezo. Kama ulikaza shingo acha livunjike sasa. Vaa wakukute ili ujue wanaweza kukamata au watakwambia usubiri police waje kukukamata 🤣🤣🤣🤣
[emoji3] kweli hili swali muruwaUtakuwepo posta muda huo au unaombea misiba kwa wenzio tu?
Watapindua wapi wanakula michapati pale wanatoka vitambi tu[emoji3][emoji3] nina kishamba changu nimekosa pesa yakunilimia wakanisaidie kung'oa visiki tu.Wenzao wanapindua serikali huko wao wanasaka sare huku [emoji28]
I don't condone mapinduzi ila hii ni task ya kiboya sana.
Hivi kuingia mtaani sheria inawaruhusu? Au wanataka kuvunja Sheria ili washtakiwe
Sio kazi tu hata akili hazimoUna maanisha jeshi letu halina kazi?
Wangekuwa wanajua intelligence, tungeibiwa rasilimali zetu? Mavazi tu mtu ana adhibiwa kuliko aliyekwiba twiga, waende Niger wakafanye kazi.Intelligence mpaka ya kujua nguo za watu kabatini Kweli wataweza,
Kwahiyo wakishampata?? Tulieni wanajeshi sio Mungu.!!!Mnaoandika hovyo msifikiri JF haina limit ya kuwalinda.
Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana.
Eleweni kuwa hii mitandao hakuna pakujificha na hakuna kinachofutika hata wewe ukifuta.
Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.