JWTZ: Tutaingia Mtaani kuzisaka Sare zetu kwa Wananchi

JWTZ: Tutaingia Mtaani kuzisaka Sare zetu kwa Wananchi

Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
Hawajitolei maisha yao kutulinda, wanalipwa ili kutulinda. Hii ni kazi waliyoamua wao kuomba ili waajiriwe kuifanya. Hivyo wanatekeleza majukumu yao.

Ni sawa na mwalimu anavyolipwa ili afundishe watoto wa mwanajeshi. Au daktari anavyolipwa ili aokoe maisha ya watu. Kama daktari hajalipwa, hawezi kuokoa maisha mtu.

Hata wanajeshi bila kulipwa, hawawezi kulinda usalama wa nchi. Acha watekeleze wajibu wao kwa mujibu wa katiba.
 
Mnaoandika hovyo msifikiri JF haina limit ya kuwalinda.

Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana.

Eleweni kuwa hii mitandao hakuna pakujificha na hakuna kinachofutika hata wewe ukifuta.

Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
nimeamini siku moja tu inatosha kuprove ujuha wa professor
aliye jifanya mwerevu kwa miaka 100!
wewe ajuza kwa umri wako na heshima yako nusu kenda
uliyojitwalia kwa miongo mingi,unaipoteza kizembe
kwenye utawala wa Mama Abdul!

so sad!
😒😒
 
W
Asiesikia la mkuu huvunjika guu, hakuna marefu yasio na ncha, safari 1 huanzisha nyingine, za mwizi 40, Simba mwenda Pole ndio hula..., Za kuambiwa changanya na Zako,msije mkasema hakukumbushwa
Kula chuma hiko
---

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema siku saba zilizotolewa kusalimisha mavazi yanayofanania na sare za jeshi kwa hiari zimeisha, hivyo jeshi litaingia kuzisaka nguo hizo kwa wananchi.

Kaimu mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano na Msemaji wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda amesema jeshi halina utani katika suala hilo, kwani katazo hilo ni kwa mujibu wa kifungu cha 99 cha Sheria ya Ulinzi wa Taifa (NDA) Sura ya 192 sheria namba 24 ya mwaka 1966 yaliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 pamoja na kifungu cha 178 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16 na kifungu cha 6 cha Sheria ya Usalama wa Taifa.

“Muda wao wa kusalimisha kwa hiari umeisha, kama mtu atakuwa hajasalimisha basi tutazifuata wenyewe, na mtindo upi tutatumia kuzichukua kwa wananchi tunajua wenyewe,” amesema Kamanda Ilonda.

Ameongeza kuwa sheria inakataza kutengeneza, kuagiza, kuuza na kutumia sare za JWTZ au zinazofanana na sare hizo bila kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika.

Wamenusa harufu ya mapigano yatakayochochewa na mapinduzi wameanza kujihami, ipo siku tu CCM na viongozi wenu mtalia na kusaga meno kwenye hii nchi.
 
Kwanza wajue kabisa wanavunja katiba na sheria za nchi.

Chombo PEKEE ambacho kina idhini kikatiba kufanya msako au upekuzi ni Jeshi la polisi, ikiwa nchi haiko katika hali ya hatari.

Hatujawahi kusikia kwamba Tanzania katika kambi yoyote ya Jeshi, kumeibiwa sare za Jeshi na hivyo wanaanza msako kizikamata.

Hatujaskia kwamba Kuna fununu au taarifa kwamba Kuna watu au kikundi Cha watu au kampuni imeingiza sare za Jeshi Tanzania ama Kwa Nia ovu au ya kibiashara.

Hakuna mahali katika sheria za nchi askari wa Jeshi anaruhusiwa au kupewa mamlaka ya kufanya upekuzi au upelelezi juu ya makosa ya uhalifu isipokua jukumu lao ni kuhakikisha mipaka ya nchi Iko salama muda wote.

Hii inaleta picha nyingine tofauti inayofuatana na ya Jeshi la polisi kutuambia watu flani walipanga uhaini. Hivyo tuamini kwamba ndani ya muda mfupi hata ndani ya Jeshi kulikua na sura ya uasi na Kwa maana hiyo askari wa Jeshi wameiba sare na kuwapatia wananchi au paramilitaries Kwa ajili ya kujiandaa na Mapinduzi husika.

Nchi inakua banana republic na Kwa maana hiyo Kila mtu anaonesha tentacles, mnafanya nchi ionekane kituko duniani Kila uchwao,. Sijui ni elimu Gani Hawa watu wanasomea hawajui Sheri, katiba na wajibu wao.
Tatizo mnaongea sana tena Kwa matusi na kejeli.
Kiufupi tu
JF ni ndogo sana.
 
Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana
Law enforcement ni jukumu la polisi sio jeshi. Labda kwa watumishi wa jeshi tu ndio wana vitengo vyao vya sheria na mahakama za jeshi.

Kwa wananchi, kama mtu kavunja sheria (mathalani kumiliki mavazi ya vyombo vya ulinzi na usalama), basi akamatwe na apelekwe mahakani apewe adhabu inayostahili.
 
So sad! Nchi ilipofikia inahitaji msaada mkubwa wa jeshi, lakini jamaa wanajiweka bize na vitu visivyo na msingi kabisa.
 
Hawana la kufanya hawa mbunga zinachukuliwa Wamasai wanafukuzwa wapo kimya. Jeshi taratibu linakwenda kuchukua nafasi ya kudharauliwa. Usishangae Slaa ama Mwambukisi wamekutwa na sare za jeshi. Ule mtaro wa kutoka bahari kuja Jangwani Magomeni kuchafu sana wanatakiwa kusafisha jiji. Ama wakalime mashamba ya Alizeti. Bogus maamuzi ya hili jeshi.
 
Bandari inauzwa wapo kimya wanapokea posho nono nono tu, madini na wanyama wetu kila kukicha vinaporwa, eti mkaanze kusaka nguo za mfanano na zao, nguo zenyewe za elf 5, nendeni Gabon huko mkaombe kazi!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Ujinga mtupu.Kizazi kinabadilika.Hivi kwa miaka ya 70s huko,ungekuta watu wanahojihoji kuhusu hilo suala?Mambo yanabadilika.
😁😁😁😁 huo muda wa police kufanya hivyo umeisha, na ukishaona hawa wameingilia jambo ujue kazi ipo. Uzuri walitoa tangazo na siku za kufata maelkezo. Kama ulikaza shingo acha livunjike sasa. Vaa wakukute ili ujue wanaweza kukamata au watakwambia usubiri police waje kukukamata 🤣🤣🤣🤣
 
Wenzao wanapindua serikali huko wao wanasaka sare huku [emoji28]

I don't condone mapinduzi ila hii ni task ya kiboya sana.
Watapindua wapi wanakula michapati pale wanatoka vitambi tu[emoji3][emoji3] nina kishamba changu nimekosa pesa yakunilimia wakanisaidie kung'oa visiki tu.

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Hivi kuingia mtaani sheria inawaruhusu? Au wanataka kuvunja Sheria ili washtakiwe

Sheria inawezekana haiwa ruhusu. Lakini sheria ipi? Kama ni hii Katiba ya JMT iliyoandikwa na mawazo ya watu 20 tu ambao walikuwa wananjua Nyerere JK na wakijua anataka nini na anayo matamanio gani katika kuliongoza Taifa.

Na katika kuandika kwao wakafikiria Taifa hili siku zote litaongozwa na Watu wanaofanana na Nyerere JK.

Sasa unategemea nini kama ikitokea wajeda wakaingia mtaani kwa maslahi mapana ya nchi ambayo haya onekani kutendewa haki na Katiba ya JMT???
 
Mnaoandika hovyo msifikiri JF haina limit ya kuwalinda.

Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana.

Eleweni kuwa hii mitandao hakuna pakujificha na hakuna kinachofutika hata wewe ukifuta.

Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
Kwahiyo wakishampata?? Tulieni wanajeshi sio Mungu.!!!
 
That’s police work. Hilo, kama jinai zote zinazofanywa na raia, ni jukumu la kipolisi. JWTZ, ikibidi, wanatakiwa kuwasiliana na jeshi la polisi kuhusu mikakati ya kufanikisha kazi hiyo kwa ufanisi zaidi. Sio kuingia mitaani. Hiyo siyo state of emergency na Rais hajatangaza.

Ni nchi modeli ya “banana republic” tu ndio utaona jeshi linafanya kazi ya polisi. Nchi makini huwezi kuona wanajeshi waliovaa combat fatigues wanazagaa mitaani, kuzoeana, kupambana au kutishiana na raia. Ni aibu kwa taifa.
 
Back
Top Bottom