JWTZ: Tutaingia Mtaani kuzisaka Sare zetu kwa Wananchi

JWTZ: Tutaingia Mtaani kuzisaka Sare zetu kwa Wananchi

LOlote wanalofanya jeshi, nyuma yao yupo Amiri Jeshi Mkuu.

Yeye ndo ametoa maagizo wananchi washughulikiwe na jeshi wanatafuta namna ya kukinukisha
Yan katuma SS tushughulikiwe , kumbe wezanke wamepiga U-turn
 
Boss, Maoni yangu yamemlenga kuruta anayekutana na raia aliyevaa nguo inayofanana na jeshi mtaani na siyo sababu halisi ya hiyo OP.
Kwani kuruta ni soldier 🤣
 
Asiesikia la mkuu huvunjika guu, hakuna marefu yasio na ncha, safari 1 huanzisha nyingine, za mwizi 40, Simba mwenda Pole ndio hula..., Za kuambiwa changanya na Zako,msije mkasema hakukumbushwa
Kula chuma hiko
---

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema siku saba zilizotolewa kusalimisha mavazi yanayofanania na sare za jeshi kwa hiari zimeisha, hivyo jeshi litaingia kuzisaka nguo hizo kwa wananchi.

Kaimu mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano na Msemaji wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda amesema jeshi halina utani katika suala hilo, kwani katazo hilo ni kwa mujibu wa kifungu cha 99 cha Sheria ya Ulinzi wa Taifa (NDA) Sura ya 192 sheria namba 24 ya mwaka 1966 yaliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 pamoja na kifungu cha 178 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16 na kifungu cha 6 cha Sheria ya Usalama wa Taifa.

“Muda wao wa kusalimisha kwa hiari umeisha, kama mtu atakuwa hajasalimisha basi tutazifuata wenyewe, na mtindo upi tutatumia kuzichukua kwa wananchi tunajua wenyewe,” amesema Kamanda Ilonda.

Ameongeza kuwa sheria inakataza kutengeneza, kuagiza, kuuza na kutumia sare za JWTZ au zinazofanana na sare hizo bila kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika.
Mtu avae swat ya marekani mseme sare zenu
 
Kwani kuruta ni soldier 🤣
Hahaha. Ushaelewa lakini. Hata hivyo, ukipata nafasi ya kazi jeshini, siku ya kwanza kabisa ukiwa unawasili unatambuliwa kama mwanajeshi.
 
Mnaoandika hovyo msifikiri JF haina limit ya kuwalinda.

Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana.

Eleweni kuwa hii mitandao hakuna pakujificha na hakuna kinachofutika hata wewe ukifuta.

Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
Kwamba tusiongee??Labda wakutake wewe Shangazi yao...ila ni ushamba, km hawana kazi wakaombe mechi ya kirafiki uko Somalia
 
Mnaoandika hovyo msifikiri JF haina limit ya kuwalinda.

Nawashauri muwache kuongea kijinga, wakimtaka mtu hapa JF wana uwezo wa kumpata ndani ya muda mchache sana.

Eleweni kuwa hii mitandao hakuna pakujificha na hakuna kinachofutika hata wewe ukifuta.

Chezeeni vingine, msichezee watu wanaojitolea maisha yao kutulinda.
Akili zako ndio kama hizi wacha dp world waje
 
Nawakubali sana Hawa Jamaa,ila zoezi hili wasijetengeneza chuki na raia kwa kupiga,nitawazereuu kama pongo wetu. Viva JWTz
 
Nchi inawajinga wengi sana, yani hawa jwtz wamekosa jambo LA maana LA kufanya, wanaona kusaka nguo zinazofanana na za jeshi ni jambo LA maana sana!
Yaani mtu ni luteni, kwa elimu yote aliyonayo, mchango wake anaoutoa kwa nchi ni kusaka raia wanaovaa nguo kama za jeshi!? Akili za matope kabisa,
Badala ya kuwaza jinsi ya kutatua changamoto kwenye nchi, mfano wakiweka mkakati wa kutumia vijana wa jkt, wafungwa, tekunolojia kuzalisha sukari na ngano ya kutosha, tusiagize tena kutoka nje, jwtz ifahamike Afrika nzima kwa ku miriki kiwanda cha kuzalisha sukari, mafuta, ngano!
Mnaingia MOU na sekta binafsi, tuna kuwa na akiba ya nafska ya kulisha Afrika nzima!
Au kubadilisha matumizi ya kuni na kuwa gesi kwenye magereza yote,
Au kwenda mbali zaidi kuanzisha karakana ya kuzalisha vitu vya IT, au assembling plant ya magari,
Kwenye branches za majeshi kuna, Airwing,navy, na army(infantry), sasa hv imeongezeka Cyber na space, bongo zipo? Hawa Kenge wanachowaza ni kupiga watu mitama na kunyangsnya leso na kaptura, akili finyu kabisa,
Mwanajeshi tena unakuta wapo zaidi ya mmoja, mnatesa raia, na mnaona ufahari kabisa!
Hii ndio shida ya ku recruit failures wa form four.
Stupid kabisa. Yanaenenda kama mambuzi
ni mambuzi na makenge tuu hawana jipya zaidi ya kutishia raia...lango Muhimu l nchi linauzwa wameshindwa hata kupenyeza sabotage ishindikane wanasaka
vitambaa vya makamasi mtaani.
 
Nyumba 100 unazijua mzee?
Vitongoji vitatu hivyo.
Watu zaidi ya mia tano,uwe unafikiri kabla hujaandika.
Tukio lilitokea ndio, ila Nyumba 100 hapana.
Mkuu, jaribu kufatilia hili swala, lilikuwa ni jambo baya Sana na la maudhi
 
Asiesikia la mkuu huvunjika guu, hakuna marefu yasio na ncha, safari 1 huanzisha nyingine, za mwizi 40, Simba mwenda Pole ndio hula..., Za kuambiwa changanya na Zako,msije mkasema hakukumbushwa
Kula chuma hiko
---

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema siku saba zilizotolewa kusalimisha mavazi yanayofanania na sare za jeshi kwa hiari zimeisha, hivyo jeshi litaingia kuzisaka nguo hizo kwa wananchi.

Kaimu mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano na Msemaji wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda amesema jeshi halina utani katika suala hilo, kwani katazo hilo ni kwa mujibu wa kifungu cha 99 cha Sheria ya Ulinzi wa Taifa (NDA) Sura ya 192 sheria namba 24 ya mwaka 1966 yaliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 pamoja na kifungu cha 178 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16 na kifungu cha 6 cha Sheria ya Usalama wa Taifa.

“Muda wao wa kusalimisha kwa hiari umeisha, kama mtu atakuwa hajasalimisha basi tutazifuata wenyewe, na mtindo upi tutatumia kuzichukua kwa wananchi tunajua wenyewe,” amesema Kamanda Ilonda.

Ameongeza kuwa sheria inakataza kutengeneza, kuagiza, kuuza na kutumia sare za JWTZ au zinazofanana na sare hizo bila kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika.
Kwanza wajue kabisa wanavunja katiba na sheria za nchi.

Chombo PEKEE ambacho kina idhini kikatiba kufanya msako au upekuzi ni Jeshi la polisi, ikiwa nchi haiko katika hali ya hatari.

Hatujawahi kusikia kwamba Tanzania katika kambi yoyote ya Jeshi, kumeibiwa sare za Jeshi na hivyo wanaanza msako kizikamata.

Hatujaskia kwamba Kuna fununu au taarifa kwamba Kuna watu au kikundi Cha watu au kampuni imeingiza sare za Jeshi Tanzania ama Kwa Nia ovu au ya kibiashara.

Hakuna mahali katika sheria za nchi askari wa Jeshi anaruhusiwa au kupewa mamlaka ya kufanya upekuzi au upelelezi juu ya makosa ya uhalifu isipokua jukumu lao ni kuhakikisha mipaka ya nchi Iko salama muda wote.

Hii inaleta picha nyingine tofauti inayofuatana na ya Jeshi la polisi kutuambia watu flani walipanga uhaini. Hivyo tuamini kwamba ndani ya muda mfupi hata ndani ya Jeshi kulikua na sura ya uasi na Kwa maana hiyo askari wa Jeshi wameiba sare na kuwapatia wananchi au paramilitaries Kwa ajili ya kujiandaa na Mapinduzi husika.

Nchi inakua banana republic na Kwa maana hiyo Kila mtu anaonesha tentacles, mnafanya nchi ionekane kituko duniani Kila uchwao,. Sijui ni elimu Gani Hawa watu wanasomea hawajui Sheri, katiba na wajibu wao.
 
Kwamba tusiongee??Labda wakutake wewe Shangazi yao...ila ni ushamba, km hawana kazi wakaombe mechi ya kirafiki uko Somalia
Somalia ni pamoto kule.Mtu akienda,kurudi ni majaaliwa.Sasa BATTLE kama hizo,hazitiliwi maanani,badala yake anakunjwa na kupigwa mitama,mtanzania ambaye hajajifunza hata matumizi ya silaha wala ngumi.Na huyo mtanzania,akipigwa,aliyempiga anaonekana MWAMBA,wakati aliyepigwa hana mafunzo yoyote.Somalia kule baadhi wana mafunzo,ndo inatakiwa mtu aonyeshe UMWAMBA kwa wale wasomali.
 
Back
Top Bottom