Uwez sema asiemuamini Allah atachomwa moto wakat hiyo dini imaenza juzi tu miaka ya 1400 iliyopita, na kabla yake kuna maelfu ya imani zilikuwepo kabla yake.
Unajua kama wewe ni MJINGA katika hili ? Ukikataa unakuwa MPUMBAVU.
Nani amekwambia UISLAMU umeanza mwaka 1400 ?
Mitume na manabii wote walikuwa Waislamu.
Sasa ni imani gani ambayo ilikuwepo kabla ya UISLAMU ?
Mungu yupo lkn si huyo mnaemuabdu ktk magenge yenu ya dini.
Umejuaje kama Mungu yupo ?
Mbingu na motoni hazipo na hazitowai kuwepo maana ziliundwa na hao wana dini ili kuwatisha watu na kuwafanya waoga na watumwa wa imani.
Umejuaje kama mbingu na moto haupo ? Unao ushahidi juu ya hili ?
Muumba wa kweli hana haja na dini ili umjue, bali kufuata sheria za uumbaji, upendo kwa viumbe wake na kutii sheria za , jamii yako unayokuzunguka.
Unaweza kuniambia malengo ya wewe kuwepo hapa Duniani kupitia hizo sheria za uumbaji ?
Unazijuaje hizo sheria za uumbaji ?
Kupinga mafundisho ya dini isiwe kigezo cha kumuita mtu mpagani, maana hata wew unakuwa mpagani kwa kuikana imani ya uafrica na kukumbatia imani za mtu mweupe ambazo ni uongo na copy ya ile origin ya imani za babu zako.
Imani ya Uafrika ni ipi na msingi wake ni upi ?
Naomba unitajie mambo matatu tu ambayo hizi imani tulizo letewa zime copy toka kwenye imani za mababu zako ?
Kimsingi imani na dini zote si sahihi maana ukifuatilia zote kiundan zinamakosa na zote zipo chini ya lengo moja na muanzilishi mmoja aliekuwa na targets zake kwa jamii fulani.
Imani gani uliyo ifatilia wewe ukaikuta ina makosa ? Naomba utolee mfano imani ya Uislamu. Onyesha kosa hata moja, ukiweza kuonyesha kosa hata moja mimi nitaomba hii ID yangu ifungiwe na wewe utakuwa shahidi.
Hakuna ukwel ktk dini ndiomaana mnapingana ninyi kwa ninyi.
Ulichoandika hapa nina uhakika hujakifikifia kiunadani. Kupingana baina ya mtu na mtu au mwingine na mwingine, kuna sababu nyingi sana, moja wapo ni mmoja akawa mjinga (kama ulivyo wewe) na mwingine akawa muelevu, au wote mkawa wajinga juu ya jambo husika.
Kiuhalisia dini zote asili yake ni imani za kishirikina ambazo ziliabudiwa na mababu wa kiafrika ya kale yaani misri na sehem zingine baran Africa, na baada ya ujio wa races za watu weupe na kuanza kustaharabika wakazicopy hizo imani na kuzistaharabisha kwa kubadili histories, majina na wahusika wa hizo imani na ndipo ujio wa dini na misahafu ukaanzia hapo.
Ukionyesha ukweli wa hiki ulichokiandika mimi nitaomba hii ID ifungiwe. Nilichokiona watu kama nyinyi msipo ulizwa maswali ya msingi mtazidi kupotea na kuwapoteza wajinga wenzenu. Yaani unaandika mambo ya uongo kuanzia mwanzo mpaka mwisho, tena unaandika mambo ambayo tukikuomba ushahidi huwezi kuutoa mpaka unakufa.
Huu ujasiri huwa mnautoa wapi ?