Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Ndugu William Mshumbusi & Kalamu1;

1. Tutabishana sana lakini ukweli wa mambo ni kuwa, miradi (projects) zinazoendeshwa na kusimamiwa na serikali moja kwa moja huwa mwisho wa siku zinaishia kwenye massive failure kwa sababu ya kuingiza SIASA ZETU MBOVU na ambazo huzaa tatizo jingine la UONGOZI/MANAGEMENT mbovu zisizo na ubunifu lakini zenye nia ovu za kuteketeza (kuiba) mtaji na faida kidogo yote inayopatikana kutokana na shughuli za mradi huo kwa kushirikiana na wanasiasa (watawala) ambapo mwisho wa siku shirika/kampuni/mradi unakufa kifo cha kawaida kabisa...

2. Rejea mifano ya viwanda vyote vilivyojengwa wakati serikali ya awamu ya kwanza ya Nyerere, vyama vya ushirika SHIRECU, NYANZA, TARECU nk nk. Vyote hivi vilikufa kifo cha kawaida tokana na tatizo hili nililolieleza hapo juu...

Mifano mingine iliyo hai kabisa na inavyoendelea hata sasa ni; angalia TANESCO, NHC, MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII YOTE ni shida tupu na yote yanajiendesha pasipo ufanisi huku watawala wa kisiasa wakiyaingilia na SIASA ZAO MBOVU na kuyavuruga vuruga kiasi cha kuyafanya yajiendeshe kwa hasara kubwa na kushindwa Ku - deliver kwa wateja wao...

Ndo kusema kuwa, ishu siyo nchi kukosa wataalamu wa nyanja zote i.e management, uchumi, fedha nk bali ni SIASA CHAFU na UONGOZI WA HOVYO WA TAIFA HILI..

3. Sasa ili ku solve tatizo hili sisi kama nchi ni lazima kujengwa kwa taasisi imara na huru zenye kujiendesha zenyewe pasipo kuingiliwa na siasa za watawala...

Ni ngumu sana kwa DG mfano wa TANESCO au hata UDART kujisikia yuko huru na akafanya iwapo hana uhakika wa nafasi yake kwa sababu anakuwa hajui Rais au PM amelalaje Leo na ataamua nini juu ya hatima yake...

Asanteni..
Nimekuelewa
 
Sasa si hata huko kukusanya kodi uliona wakiwa wanashindwa?

Sikubaliani nawe kamwe juu ya hayo mawazo ya kusema "Tokea uhuru mpaka leo hakuna sehemu linapofanikiwa..., ni madudu tu kila siku."

Unachanganya mambo mengi hapa pengine bila kujua.

Kushindwa kwa mambo mengi yaliyofanyika hapa tokea uhuru sababu zipo nyingi sana, hata zisizohusu maamuzi ya serikali. Kama wewe huwezi kulitambua hilo, basi maana yake ni kwamba mawazo yako umeyagandisha sehemu moja tu, na huna uwezo wa kupambanua hali zinazohusiana katika kufifisha mafanikio.
Ni vigumu sana kujadili jambo na mtu wa aina hiyo.
Acha porojo

Nitajie shirika moja la serikali lililofanya biashara na likafanikiwa

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mada muhimu kweli kweli, lakini wachangiaji wanachungulia tu na kupita zao! Wanatafuta mada za CCM na CHADEMA!

Mimi sikubaliani na wewe juu ya hiyo dhana ya serikali haifanyi biashara.

Usiifanye kuwa 'dogma', au kama kitu ulichokaririshwa.

Hata kama ulisikia ikisemwa hivyo, kwa nini usiweke muda ujaribu kutazama uhalisia na ukweli wake ukoje?

Sasa mimi nakushauri uanze kulitazama hilo kwa jicho la pili; acha kufumba jicho moja, yafungue yote mawili ili upate picha nzuri.

Ni hivi: kuna kizuizi gani kinachofanya serikali isiweze kufanikisha kuendesha miradi hiyo yote uliyoitaja?

Kwani haina watu wenye uwezo wa kuifanya. Kama wapo, ni nini kinazuia wasifanye hiyo kazi kwa ufanisi?

Na kama hawapo, serikali haiwezi ikamwajiri, ndiyo kuajiri kampuni kwa mkataba inayoweza kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi? Sijasema serikali ibinafsishe, kama wewe unavyotaka.

Lakini la muhimu hapa ninalolisisitiza, ni hii dhana potofu ya kwamba serikali haiwezi kufanya mambo yake kwa ufanisi.

Kuna sababu zipi...., hizo sababu haziwezi kuondolewa?

Kila mara imekuwa ni kutafuta visingizio tuuu kwa kushindwa tu kutimiza wajibu mliopewa kuutimiza.

Hapa ndipo nilipopenda Magufuli apafanyie udikteta wake haswa haswa...! Hali ingebadilika tu baada ya muda.

Haya mashirika makubwa ya ujenzi na mengine toka China tunayoona yametapakaa duniani kote, mbona haya yalikuwa ni mashirika chini ya serikali?
Wao waliweza vipi?

Una point ya msingi - kuwa serikali iondoe matatizo yanayosababisha kushindwa kwa hii miradi! Bahati mbaya hukutaja hata jambo moja unalodhani ni kikwazo. Lakini tukiangalia miradi mingine kama viwanda ya Nyerere, ATC, reli ya kati, TAZARA, bandari, mabasi na kadhali - ilishindwa!!! Sababu kubwa sio kukosekana kwa wataalamu, vifaa, uongozi nk - sababu ni hii - ustahamilivu wa udhaifu ili kufaidisha siasa (patience for failure/mismanagament). Serikali imekuwa ikikwepa hata kuonesha tu miradi hii inashindwa (rejea magawio ya ATC, TTCL na wengine). Ustahamilivu wa kushindwa umekuwa mkubwa mno na wa maana ili kufaidisha siasa za serikali. Njia nzuri ni kuiondoa serikali katika uendeshaji ili stahamilvu hiyo iishe. Kuiondoa serikali simaanishi wayauze au wabinafsishe. Ninamaanisha wawe sehemu ya umiliki kama ambavyo watakuwa wamiliki wengine wenye hisa! Serikali anaweza kuwa mmiliki mkubwa tu (51%) na wana hisa wakawa na 49%. Ni hawa 49% ndio watakaoendesha mashirika haya kwa ufanisi!! Ndio hao watakataa hasara. Ndio hao hawatataka faida za kisiasa ziharibu uwekezaji wao. Air Rwanda kwa mfano inamilikiwa na Rwanda 51% na Qatar Airways 49%. Baada ya miaka minvi ya hasara, sasa Rwanda sio mwendeshaji wa shirika tena. Inaitwa PPP (public private partnership).

Mambo haya yamejaribiwa na kufanikiwa sehemu mbalimbali duniani. Uwekezaji wa kiraia ndio uwekezaji salama unaoweza kubakiza sehemu kubwa ya faida ndani ya nchi!!

Faida za kisiasa ni hasara kwa uchumi!! Tuwezeshe raia kuachana na siasa na wawe wazalishaji. Serikali ibaki na kazi ya kukusanya kodi, kutunga sheria na kudhibiti shughuli za hao raia.
 


Mbona halmashauri ya jiji la London ndio ☝️linaendesha London under ground, asilimia kubwa ya mabasi London, Trams, trains na njia nyingine nyingi za usafiri.

Na tena njia za mabasi zikiaribika sio serikali inayolipia matengenezo wao, train serikali itajenga reli deni wanalipa wao; hakuna dezo.

Issue Tanzania ni management sio serikali kuendesha; isitoshe kuna huduma zingine serikali inazishikilia ili kuhakikisha unafuu au kuzipeleka mahala ambapo wawekezaji awataki kwenda. Nyie mkishaona serikali imewekeza ndio mnaibuka aiwezi kazi.

Website yao inasema London underground asilimia 41% ya matumizi yao yanatoka kwa walipa kodi. Na wanasema mapato yao wanatumia kuiendesha hiyo kampuni na bado hayatoshi. Ina maana inaendeshwa kwa hasara ila kwa sababu ni huduma wapiga kura wanaiona muhimu serikali inaendelea kuisaidia.

 
Una point ya msingi - kuwa serikali iondoe matatizo yanayosababisha kushindwa kwa hii miradi! Bahati mbaya hukutaja hata jambo moja unalodhani ni kikwazo. Lakini tukiangalia miradi mingine kama viwanda ya Nyerere, ATC, reli ya kati, TAZARA, bandari, mabasi na kadhali - ilishindwa!!! Sababu kubwa sio kukosekana kwa wataalamu, vifaa, uongozi nk - sababu ni hii - ustahamilivu wa udhaifu ili kufaidisha siasa (patience for failure/mismanagament). Serikali imekuwa ikikwepa hata kuonesha tu miradi hii inashindwa (rejea magawio ya ATC, TTCL na wengine). Ustahamilivu wa kushindwa umekuwa mkubwa mno na wa maana ili kufaidisha siasa za serikali. Njia nzuri ni kuiondoa serikali katika uendeshaji ili stahamilvu hiyo iishe. Kuiondoa serikali simaanishi wayauze au wabinafsishe. Ninamaanisha wawe sehemu ya umiliki kama ambavyo watakuwa wamiliki wengine wenye hisa! Serikali anaweza kuwa mmiliki mkubwa tu (51%) na wana hisa wakawa na 49%. Ni hawa 49% ndio watakaoendesha mashirika haya kwa ufanisi!! Ndio hao watakataa hasara. Ndio hao hawatataka faida za kisiasa ziharibu uwekezaji wao. Air Rwanda kwa mfano inamilikiwa na Rwanda 51% na Qatar Airways 49%. Baada ya miaka minvi ya hasara, sasa Rwanda sio mwendeshaji wa shirika tena. Inaitwa PPP (public private partnership).

Mambo haya yamejaribiwa na kufanikiwa sehemu mbalimbali duniani. Uwekezaji wa kiraia ndio uwekezaji salama unaoweza kubakiza sehemu kubwa ya faida ndani ya nchi!!

Faida za kisiasa ni hasara kwa uchumi!! Tuwezeshe raia kuachana na siasa na wawe wazalishaji. Serikali ibaki na kazi ya kukusanya kodi, kutunga sheria na kudhibiti shughuli za hao raia.
Mkuu nimepata shida kidogo kukuelewa huko juu kuhusu "ustahimilivu..."; kidogo nibwage manyanga chini!

Unazungumzia umiliki, kama huo wa Rwanda? Mbona umeishia hapo mkuu, umejaribu kuangalia "The Pride of Africa" wanavyofanya?

Hata kama hutaki kuangalia mfano huo na mingi mingine huko nje ya mipaka yetu, mbona unajisahaulisha kirahisi rahisi..., hapa hapa nyumbani una uhakika hapajawahi kuwepo na mpango kama huo, tena sio katika shirika hilo hilo la ATC pekee, na mashirika mengine kibao yaliyowahi kuwa na washiriki na serikali kubaki na hisa kadhaa. Hivi unadhani pendekezo lako ni jipya?

Haya, sote tunajua, at least nategemea kuwa unajua: hivi ni nani anayemiliki na kuendesha Ethiopian?

Haya mambo tunayajadili hapa wakati mwingine tukitumia hisia tu tunazozipata toka kwa watu na hatuyafikiri kwa kina tukaangalia hasa ni kwa nini serikali ijihusishe kwenye baadhi ya haya mambo.

Unajua, mimi nitakubaliana nawe moja kwa moja kuhusu kujiondoa kwa serikali kabisaaaa kwenye haya mambo iwapo kama hawa binafsi tunaowalilia watatoa huduma safi kabisa na wananchi wafaidike na huduma hizo.

Lakini historia inaonyesha, sio hapa pekee, bali na kwingine pia, kuna mambo ambayo ni lazima serikali iyabebe hata kama ni kwa mzigo mkubwa. Tulikuwa na IPTL hapa iliyotupatia taabu kweli kweli. Mara hii tumejifanya kusahau? India hawakuja hapa na kutaka kuua kabisa reli? Mifano ipo chungu nzima, na hiyo si pekee hata kama tungesema akina Mo waendeshe mashirika haya, kuna athari chungu nzima ninazoweza kueleza ni jinsi gani bado tutakuwa tumekwama.
 
Website yao inasema London underground asilimia 41% ya matumizi yao yanatoka kwa walipa kodi. Na wanasema mapato yao wanatumia kuiendesha hiyo kampuni na bado hayatoshi. Ina maana inaendeshwa kwa hasara ila kwa sababu ni huduma wapiga kura wanaiona muhimu serikali inaendelea kuisaidia.

Sina hakika kama British Airways ni tofauti na hao, na hata BBC!
 
Website yao inasema London underground asilimia 41% ya matumizi yao yanatoka kwa walipa kodi. Na wanasema mapato yao wanatumia kuiendesha hiyo kampuni na bado hayatoshi. Ina maana inaendeshwa kwa hasara ila kwa sababu ni huduma wapiga kura wanaiona muhimu serikali inaendelea kuisaidia.

Ebu onesha hiyo sehemu waliposema hayo.

Nilichoona mimi mapato yao ni service fees, government grants (mikopo ya serikali ya kibiashara yenye riba nafuu), wanakopa bank, paid advertising and other toll charges za barabara zilizochini ya jiji.

I doubt kama serikali itatumia kiasi icho cha pesa kuendesha underground, be it ni sensitive kwa uchumi wao.

The mere fact wanakwambia 80% ya profit wanarudisha kwenye kuboresha miundombinu ina maana hiyo profitable organisation isiyotegemea government subsidies.
 
Ebu onesha hiyo sehemu waliposema hayo.

Nilichoona mimi mapato yao ni service fees, government grants (mikopo ya serikali ya kibiashara yenye riba nafuu), wanakopa bank, paid advertising and other toll charges za barabara zilizochini ya jiji.

I doubt kama serikali itatumia kiasi icho cha pesa kuendesha underground, be it ni sensitive kwa uchumi wao.

Mbona umeshaiona hiyo sehemu tayari? Labda kama huoni kwamba government grants na mikopo ya European Investment Bank vyote ni hela za walipa kodi. Hela za serikali ni hela za walipa kodi.
 
Mbona umeshaiona hiyo sehemu tayari? Labda kama huoni kwamba government grants na mikopo ya European Investment Bank vyote ni hela za walipa kodi. Hela za serikali ni hela za walipa kodi.
Grant ni mkopo nafuu unaotolewa na serikali na unalipwa; nani kakwambia ni hela ya bure hiyo.

Fungua hiyo statement nenda kaangalie kwenye notes za current na non current liabilities utaona grants ni madeni.
 
Ethiopia Airlines ilikuwa Shirika pekee la ndege la Ethiopia kati ya 1950 hadi 2002. Unahitaji kuwa TANESCO ndio ushindwe kujijenga na uendelee kupata hasara ukiwa mwenyewe sokoni.

Usiongelee IPTL aliyekuwa supplier tu na ambaye ni dili la wanasiasa.Ongelea TANESCO ambayo haijawahi kutoka mikononi mwa serikali, haijwahi kupata faida na huduma zake ni tia maji tia maji tu siku zote. Na vigogo wa serikali hawataki kusikia suala la sekta binafsi kwenye umeme!!!

Kama una mashaka na Huduma kutoka kampuni binafsi nenda Agha Khan, Regency, Kairuki. Nenda Feza, St Mary's, ISM, St Anthony. Angalia wanafunzi wanaotoka shule za kata na hao kutoka st st, Angalia usafiri wa dalaldala za binafsi ulivyo na uhakika kuliko hizo daladala za mwendokasi, Angalia usafiri wa mikoani kwa mabasi ambako serikali haina hata basi moja la abiria.

Serikali iliwaindoa Maxmalipo kwenye mwendokasi,wakati huu tiketi zinachanwa na huduma ya kadi imekufa. Sasa hivi ni miaka miwili hilo dude lao la E-government bado liko linajenga mfumo wa kielectronic.Two damn years!!!.
Mkuu nimepata shida kidogo kukuelewa huko juu kuhusu "ustahimilivu..."; kidogo nibwage manyanga chini!

Unazungumzia umiliki, kama huo wa Rwanda? Mbona umeishia hapo mkuu, umejaribu kuangalia "The Pride of Africa" wanavyofanya?

Hata kama hutaki kuangalia mfano huo na mingi mingine huko nje ya mipaka yetu, mbona unajisahaulisha kirahisi rahisi..., hapa hapa nyumbani una uhakika hapajawahi kuwepo na mpango kama huo, tena sio katika shirika hilo hilo la ATC pekee, na mashirika mengine kibao yaliyowahi kuwa na washiriki na serikali kubaki na hisa kadhaa. Hivi unadhani pendekezo lako ni jipya?

Haya, sote tunajua, at least nategemea kuwa unajua: hivi ni nani anayemiliki na kuendesha Ethiopian?

Haya mambo tunayajadili hapa wakati mwingine tukitumia hisia tu tunazozipata toka kwa watu na hatuyafikiri kwa kina tukaangalia hasa ni kwa nini serikali ijihusishe kwenye baadhi ya haya mambo.

Unajua, mimi nitakubaliana nawe moja kwa moja kuhusu kujiondoa kwa serikali kabisaaaa kwenye haya mambo iwapo kama hawa binafsi tunaowalilia watatoa huduma safi kabisa na wananchi wafaidike na huduma hizo.

Lakini historia inaonyesha, sio hapa pekee, bali na kwingine pia, kuna mambo ambayo ni lazima serikali iyabebe hata kama ni kwa mzigo mkubwa. Tulikuwa na IPTL hapa iliyotupatia taabu kweli kweli. Mara hii tumejifanya kusahau? India hawakuja hapa na kutaka kuua kabisa reli? Mifano ipo chungu nzima, na hiyo si pekee hata kama tungesema akina Mo waendeshe mashirika haya, kuna athari chungu nzima ninazoweza kueleza ni jinsi gani bado tutakuwa tumekwama.
 
BBC sio shirika la kutengeneza faida. Linaendeshewa kwa license fee ambayo ni kama kodi inayotozwa kwa kila mtu anayemiliki TV Uingereza.

British Airways ni shirika binafsi lilo kwenye soko la hisa la Uingereza.
Sina hakika kama British Airways ni tofauti na hao, na hata BBC!
 
Kusema 80% ya profit wanarudisha kwenye kuboresha miundombinu haina maana hiyo ni profitable organisation isiyotegemea government subsidies ina maana hiyo ni sera yao pale wanapopata faida. Sio ajabu ukakuta aini hiyo ya maneno hata TANESCO au ATCL kwenu.
Ebu onesha hiyo sehemu waliposema hayo.

Nilichoona mimi mapato yao ni service fees, government grants (mikopo ya serikali ya kibiashara yenye riba nafuu), wanakopa bank, paid advertising and other toll charges za barabara zilizochini ya jiji.

I doubt kama serikali itatumia kiasi icho cha pesa kuendesha underground, be it ni sensitive kwa uchumi wao.

The mere fact wanakwambia 80% ya profit wanarudisha kwenye kuboresha miundombinu ina maana hiyo profitable organisation isiyotegemea government subsidies.
 
Sekta binafsi ndio solution sababu serikali kila kitu ni siasa hivyo biashara hawaziwezi.

Wauze hiyo company.
Kweli kabisa ikishindikana basi ni serikali kuwa na hisa tu kwenye shirika kuliko kuendelea kula hasara, manake kwa nchi zetu especially za Africa, mara nyingi watu wafanyao kwenye mashirika yetu yanayoendeshwa na serikali, huwa hawana uchungu wowote na pesa inayotumiwa na kama shirika linajiendesha kwa ufanisi au kwa hasara, kwani wafanyakazi wao alimradi wanakuwa na uhakika wa mshahara mwisho wa mwezi na kuangalia wapi penye upenyo wa ufisadi wao wachote basi... manake wanaona btw ni mali ya umma tofauti na kama shirika lingekuwa linaendeshwa na private entities, ambao wanakuwa serious kuhakikisha linakuwa na tija...tofauti kabisa na mashirika yanaendeshwa na serikali zetu za kiafrika, ambazo zinakuwa zinaingiza siasa na kutotumia watu sahihi, kwenye mambo ya kiutendaji, na hata ktk mambo mengine ya msingi ambayo yanahitaji utaalamu uliobobea kwenye eneo husika. Mifano michache ya matatizo kama haya, nimeyaona kwa mashirika ya ndege ya huku kusini mwaka Afrika, ya SAA na pia shirika la ndege la Air Namibia ambayo kwa muda mrefu, yaliendelea kuwa ' bail out' kila mwaka kwa pesa za serikali pamoja na kuingiza hasara miaka mfululizo, kwa sababu nyingi zikiwepo za kisiasa na mashirika kuingiliwa na serikali kwenye uendeshaji....na tayari kama Air Namibia bunge na serikali wamenyoosha mikono na limevunjwa( liquidated) na huku South Africa ,SAA inapumulia mashine... Mie ninashauri nchi zetu bado ni maskini, na tujaribu tuwe na priorities na kufanya mambo ambayo tulio na uwezo nayo kwa kipindi husika.... kazi iendelee.
 
Mada muhimu kweli kweli, lakini wachangiaji wanachungulia tu na kupita zao! Wanatafuta mada za CCM na CHADEMA!

Mimi sikubaliani na wewe juu ya hiyo dhana ya serikali haifanyi biashara.

Usiifanye kuwa 'dogma', au kama kitu ulichokaririshwa.

Hata kama ulisikia ikisemwa hivyo, kwa nini usiweke muda ujaribu kutazama uhalisia na ukweli wake ukoje?

Sasa mimi nakushauri uanze kulitazama hilo kwa jicho la pili; acha kufumba jicho moja, yafungue yote mawili ili upate picha nzuri.

Ni hivi: kuna kizuizi gani kinachofanya serikali isiweze kufanikisha kuendesha miradi hiyo yote uliyoitaja?

Kwani haina watu wenye uwezo wa kuifanya. Kama wapo, ni nini kinazuia wasifanye hiyo kazi kwa ufanisi?

Na kama hawapo, serikali haiwezi ikamwajiri, ndiyo kuajiri kampuni kwa mkataba inayoweza kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi? Sijasema serikali ibinafsishe, kama wewe unavyotaka.

Lakini la muhimu hapa ninalolisisitiza, ni hii dhana potofu ya kwamba serikali haiwezi kufanya mambo yake kwa ufanisi.

Kuna sababu zipi...., hizo sababu haziwezi kuondolewa?

Kila mara imekuwa ni kutafuta visingizio tuuu kwa kushindwa tu kutimiza wajibu mliopewa kuutimiza.

Hapa ndipo nilipopenda Magufuli apafanyie udikteta wake haswa haswa...! Hali ingebadilika tu baada ya muda.

Haya mashirika makubwa ya ujenzi na mengine toka China tunayoona yametapakaa duniani kote, mbona haya yalikuwa ni mashirika chini ya serikali?
Wao waliweza vipi?
Hayo yalifanywa kwenye TRC ,kuna tija ilipatikana?

Wakati wa JK alijaribu kwa kuleta watanzania waliokuwa nje ya nchi kwenye sekta binafsi kama TIC,NSSF,NHC nk nk walijitahidi lakini mwendazake alivyokuja akadai hawezi lipa salary kubwa na hadi leo hii mashirika yamejifia huko

Tukubali serikali iwe na hisa tuu ila shughuli za uendeshaji zifanywe na sekta binafsi tena kipaombele iwe watu wa ndani ndio wawe investors
 
Kifupi NI kuwa biashara za serikali zinaubunifu hafifu na hazina tija waanaajiliwa kwa vyeti kuendesha biashara na sio kwa uwezo na UBUNIFU.
Mfano ttcl walijenga ofisi kila mahala na kuajili wahandisi, mafundi na meneja lkn. Voda ,tigo na halotel wanahudumia minala na kuudha bidhaa kwa kutumia mawakala na tenda
Hakuna mtu ataweka jita kwenye kitu ambacho hakifaidishi yeye binafsi.

Kwenye uchumi wa soko kuna dhana ya kwamba mtu anavyojibidiisha kujinufaisha binafsi,in turn anafaidisha na wengine third part
 
Mkuu, ahsante kwa mchango wako, lakini dhana hii ni potofu kabisa.

Kwa nini watu wote hao walioko serikalini wote wawe hawana ubunifu, ila hawa wengine ndiko kuwe na wabunifu?

Umetoa mfano huo wa TTCL, ukalinganisha na TIGO, VODA na HALOTEL - hivi kweli unaweza kusema kwamba wafanyakazi walioko TTCL hawana ubunifu kama hao walioko kwenye mashirika hayo? Ushahidi wa hili ni upi?

Serikali wangetaka mashirika yao yafanye vizuri ingewezekana sana!

Basi tu, hatujapata viongozi ambao wana nia ya kuyafanya haya mashirika yawe imara. Ni mambo ya uzembe tu na kukosa usimamizi unaotakiwa kuyawezesha mashirika yafanye kazi vizuri.
Graduate wa master au degree hajawahi fanya biashara na hana exposure anaanzia wapi kuwa mbujifu?

Ukinolewa kutoka sekta binafsi ukaja sekta ya umma ndio unaweza kuwa mbunifu,,

Nimewahi fanya Kazi sekta binafsi kwa miaka 2 tena kwenye kampuni ya Kenya hapa hapa Bongo uchumi ulivyovurugika ikafungasha nikatafuta Kazi serikali,to be honest huku serikali no one cares ni mwendo wa kufukuzia posho tuu na kufanya Kazi kwa mazoea, wanasema sio Kazi ya baba yako chukua chako sepa na vile mishahara ni midogo

Pia tatizo ni ajira za kudumu bora zingekuwa za mkataba ingeleta tija kidogo
 
Kusema 80% ya profit wanarudisha kwenye kuboresha miundombinu haina maana hiyo ni profitable organisation isiyotegemea government subsidies ina maana hiyo ni sera yao pale wanapopata faida. Sio ajabu ukakuta aini hiyo ya maneno hata TANESCO au ATCL kwenu.

78AFC0D6-B0DB-40F4-8631-7E09E812A9D0.jpeg



Umeona hapo ☝️mwaka jana walitengeneza faida ya £671.2 million.

Yes kuwekeza 80% back ni sera yao kwa sababu kampuni ni 100% mali ya serikali hawana interest na dividend bali kutoa merit good zenye ubora na kuboresha maslahi ya wafanyakazi. Ndio maana wanarudisha kwenye kujiboresha.

6A8EDBF4-7863-44FB-99A0-EF0E5CA25190.jpeg

Tazama hapo ☝️ juu tena utaona aina ya grants wanazopata zifuatilie zote kupitia google utaona ni za kulipa. Kuwa mali ya serikali aina maana wanaendeshwa kwa subsidies.

Grants ni sources of finances za kawaida sana nchi za wenzetu, hata taasisi binafsi zinapata provided serikali inataka kusaidia sector fulani, wanao qualify kwenye hiyo industry can apply.

Acha kumsikiliza huyo jamaa alieni quote anaunga unga tu ubishi wala ajapitia hiyo statement yenyewe aliyoileta.

PS. British Airways sio mali ya UK kwa sasa inamilikiwa na ‘International Airline Group’ (AIG) shirika lilisojaliwa Spain.
 
Back
Top Bottom