Kama upo mtaani muda mrefu bila kazi, tatizo ni wewe!

Kama upo mtaani muda mrefu bila kazi, tatizo ni wewe!

Acha niwapelekee moto wazembe wazembe wanadeka kama yatima.

Dunia hii ukileta unyonge unanyooshwa tu hahahahaha.
Maisha ya kutoboa sio kulipa geto la self na smart tv! Umeweza kulipa kodi ya geto unahisi umetoboa? Acha mbwembwe bamdogo bado una safari ndefu!

Waliotoboa watoto wanasomesha shule IST huko na wanamiliki ma investment ya maana huko kwenye ma Real estate na ma T bonds!
 
Acha niwapelekee moto wazembe wazembe wanadeka kama yatima.

Dunia hii ukileta unyonge unanyooshwa tu hahahahaha.
Yani mtu unalala ndani huombi kazi ukakosa unaropoka tu ajira ngumu kisa unasikia story za waliokosa!

Siku hizi hata ukiwa na connection utaulizwa kitu gani unaweza kufanya (skills) tunarudi tena pale pale kwenye ujuzi! Ukishajibu hilo swali ndo linakuja swali la vyeti ila swali namba moja ni ujuzi unao!

Yaani ili uajiriwe au kujiajiri upate wateja unatakiwa uwe na Thamani flani (skill) ambayo itamvutia mteja au mwajiri unatakiwa uwe mtabe wa kitu flani yani piga ua garagaza kitu flani uwe nacho ambacho unasema kabisa hapa kwenye hiki hakuna wa kunitisha!

Vijana wengi wapo nusu nusu unakuta anajua hiki kidogo na kile kidogo sasa waajiri hawataki mtu wa kuja kufanya majaribio kazini au kuja kujifunzia kazini, kazini sio Shule au Chuo, watu wanataka product wanataka kazi ugonge show utengeneze faida sasa ukiwa nusu nusu unalia lia ajira ngumu lazima uone kila mtu ana roho mbaya
 
Yani mtu unalala ndani huombi kazi ukakosa unaropoka tu ajira ngumu kisa unasikia story za waliokosa! Siku hizi hata ukiwa na connection utaulizwa kitu gani unaweza kufanya (skills) tunarudi tena pale pale kwenye ujuzi! Ukishajibu hilo swali ndo linakuja swali la vyeti ila swali namba moja ni ujuzi unao! Yani ili uajiriwe au kujiajiri upate wateja unatakiwa uwe na Thamani flani (skill) ambayo itamvutia mteja au mwajiri unatakiwa uwe mtabe wa kitu flani yani piga ua garagaza kitu flani uwe nacho ambacho unasema kabisa hapa kwenye hiki hakuna wa kunitisha! Vijana wengi wapo nusu nusu unakuta anajua hiki kidogo na kile kidogo sasa waajiri hawataki mtu wa kuja kufanya majaribio kazini au kuja kujifunzia kazini, kazini sio Shule au Chuo, watu wanataka product wanataka kazi ugonge show utengeneze faida sasa ukiwa nusu nusu unalia lia ajira ngumu lazima uone kila mtu ana roho mbaya
Wewe hata uwe na ujuzi gani training muhimu!
 
Ni kawaida kutafuta wa kumbebesha mizigo.

Kama sio ndugu tutalaumu marafiki.

Tutaamia kwa serikali au chama tawala.

Tukifika mwisho tatizo anakuwa Mungu hajapanga ndio akili zetu vijana wa kitanzania.

Ukiletewa mnaijeria mpambane nae unataka huruma unalaumu elimu yetu au migration.

Yani ilimradi tu wewe uwe safe hahahaha.
Wewe ndio nakwambia kama ipo ipo tu! Kazi sio kupambana mzee, ukiona unapambania sana kitu jua hakikua riziki yako! Riziki ina flow tu na tena inakujaga upande wako bila hata force kubwa
 
Motivisheni spika maisha sio rahisi kihivyo
 
Yani mtu unalala ndani huombi kazi ukakosa unaropoka tu ajira ngumu kisa unasikia story za waliokosa! Siku hizi hata ukiwa na connection utaulizwa kitu gani unaweza kufanya (skills) tunarudi tena pale pale kwenye ujuzi! Ukishajibu hilo swali ndo linakuja swali la vyeti ila swali namba moja ni ujuzi unao! Yani ili uajiriwe au kujiajiri upate wateja unatakiwa uwe na Thamani flani (skill) ambayo itamvutia mteja au mwajiri unatakiwa uwe mtabe wa kitu flani yani piga ua garagaza kitu flani uwe nacho ambacho unasema kabisa hapa kwenye hiki hakuna wa kunitisha! Vijana wengi wapo nusu nusu unakuta anajua hiki kidogo na kile kidogo sasa waajiri hawataki mtu wa kuja kufanya majaribio kazini au kuja kujifunzia kazini, kazini sio Shule au Chuo, watu wanataka product wanataka kazi ugonge show utengeneze faida sasa ukiwa nusu nusu unalia lia ajira ngumu lazima uone kila mtu ana roho mbaya
watu wanakuwa wakali sababu hawataki kutoka kwenye comfort zone.

Maana ukishazungumzia ujuzi inabidi kujifunza na kujifunza ni kunahitaji muda na akili, hapo ndio kijana wa kitanzania anaona unamtukana ukimwambia bado hatoshi kwenye mapambano ya ajira.

Mwingine anakwambia sio lazima kuajiriwa nitajiajiri anafikiri kwenye kujiajiri ndio hatuitaji skills ukiwezeshwa mtaji ndio umemaliza kila kitu.

Skills + Connection = Money

More skills more money

Kama hauna skills ulimwengu wa sasa ajira ni ngumu sana kupata. Hata wanaotoboa kwenye ujasiriamali walikubali kuinvest kupata ujuzi flani.

Jifunze jifunze jifunze kisha jifunze tena mpaka uwe competent lazima utaona mabadiliko. Uzuri tunaishi ulimwengu mwepesi kila kitu kipo mtandaoni either bure au kwa kulipia. Au nenda kwa wanaojua upate ujuzi umekaa kitaa miaka mitano bila kazi ila unaona unapoteza muda kujifunza kitu kwa miezi sita.

Imagine una kampuni yako unatafuta watafiti. Wanakuja watu wawili mmoja anajivunia tu kuwa na degree ya udsm, mwingine maybe ana degree ya teophil kisanji university ila ni hustler wa kitaa anakuja na package ana degree, anaweza kutrain watu, anaweza kudesign research tools kama questionnaires, interview guides etc, anaweza kutumia digital tools like google forms, kobo, tangiline etc...anaweza kufanya analysis ya data, anaweza kufanya presentation ya data, anaweza kuandika technical report.

Hapo ni wazi mmoja ataondoka kwenye interview akisema Mungu ajanijalia acha niendelee kusubiri kudra.
 
Wewe ndio nakwambia kama ipo ipo tu! Kazi sio kupambana mzee, ukiona unapambania sana kitu jua hakikua riziki yako! Riziki ina flow tu na tena inakujaga upande wako bila hata force kubwa
Kazi ni vita unatakiwa uwe na silaha.....kazi za kuflow zenyewe zimebaki hizi za kutembeza mabeseni mjini matokeo yake ukiona classmate unajificha kwenye msingi.

Ili uwe na kazi nzuri unatakiwa upambane.

Kuna watu hata skill ya kawaida ya kutengeneza CV kwao ni mtihani.

Mtu hata kujieleza yeye ni nani ni mtihani na anajua nikienda interview piga ua tell me about yourself siwezi acha kuulizwa.
 
Waacheni hao ni graduates waliopata ajira juzi wana moto sana,kama motivation speaker.

Dunia ina mambo mengi sana ila kama umetoka chuo juzi au jana hauwezi yaelewa yote.

Mimi ukiniuliza ufanye nini ili upate ajira nitakwambia mtangulize Mungu wako,fanya maombi,funga na toa sadaka haitochukua hata hiyo miezi miwili utapata kazi.

There is a dark side in every one life,Godies is only one protector from that sides.

Kutokufanikiwa katika mambo uyapangayo maana yake nyota yako imechafuka unaitaji kuisafisha sasa hapo kazi kwako.
 
Waacheni hao ni graduates waliopata ajira juzi wana moto sana,kama motivation speaker.

Dunia ina mambo mengi sana ila kama umetoka chuo juzi au jana hauwezi yaelewa yote.

Mimi ukiniuliza ufanye nini ili upate ajira nitakwambia mtangulize Mungu wako,fanya maombi,funga na toa sadaka haitochukua hata hiyo miezi miwili utapata kazi.

There is a dark side in every one life,Godies is only one protector from that sides.

Kutokufanikiwa katika mambo uyapangayo maana yake nyota yako imechafuka unaitaji kuisafisha sasa hapo kazi kwako.
Mtoa mada atakua na umri mdogo. Kuna mengi hajayaona. Hajui. Ni kumpuuza tuu.

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Achana na story za motivesheno spika wewe sio Elon Musk au Jack Ma hao ni gifted.

Ona sasa huna kazi hauna mradi wowote unajifariji na story za kina Jack Ma na umri unakwenda unaonekana boya tu kitaa sababu hauna maisha
ww una nn kinachokufnya uongee utumbo hapa jf, motivatinal speakers wana mada kma zako mshamba na pumba, etii huna kazi wala mradi nitafute nikuoneshe acheni kuon watu wapuuz hapa jf mkachukulia poua kila mtu pungaa wee....etii #sinzapazuri we c barmedi unajiita majina ya bar
 
Back
Top Bottom