Uchaguzi 2020 Kamati ya Maadili yatolea ufafanuzi adhabu dhidi ya Lissu kumfungia kampeni. Yasema ameadhibiwa na Kamati ya Vyama 15 vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu

Naona Katibu wa kamati ya maadili ya tume ya uchaguzi Dr Kavishe bado amemkalia kooni mgombea urais wa Chadema Tundu Lisu.

Dr Kavishe amesema kinachogombea ni chama cha Chadema ambacho kimemdhamini Tundu Lisu kwa nafasi hiyo hivyo Tundu Lisu atapaswa kutumikia adhabu ambayo kimsingi Chadema wameikubali.
Dr Kavishe amenukuliwa na ITV akisema adhabu ya Chadema kupitia kwa Tundu Lisu ni halali kabisa.

Maendeleo hayana vyama!
 
Ni kweli kabisa kama alivyosema, Adhabu hii ni halali kabisa.

Kikubwa aitumikie tu kama alivyoadhibiwa.
 
Watanzania wanataka uhuru na haki ndani ya nchi yao. Watanzania hawataki kuonewa na kunyanyaswa na kutukanwa ndani ya nchi yao. Ndiyo maana kipindi cha miaka 5 ya Meko amejisifu kuwa kafanya maendeleo sana, lakini why this REJECTION ? Sasa hivi haongelei tena madaraja na madege
 
Ukijifanya unajua sana ndio hivi sasa,

Yeye alifikiri pekeake ndio anajua sheria pekeake
 
Inavyoonekana hata ndani ya chadema lisu anajiona yupo juu ya kila mtu anafanya atakavyo, mbowe kajiweka mbali na huu msala, maana baada ya uchaguzi watz watarudi hapa kuanza kuattack strategies za lisu anazozitumia sasa
 
Limetepeta kama nini?
 
Kwanza kabisa, kwa nini kamati itoe ufafanuzi? Simply means ni kweli uamuzi wake haueleweki na kweli kwamba hoja za Lissu zina mashiko. Kama kamati ina uhakika kuwa ilifuata utaratibu na imempa Lissu haki ya rufaa ilitakiwa ikae kimya isubiri reaction ya Lissu ione kama anapeleka rufaa, au anatekeleza adhabu au anaendelea na kampeni then utaratibu ufuatwe kwa mujibu wa sheria.
Lakini kitendo cha kutoa ufafanuzi tayari ni weakness. Na ufafanuzi sio sehemu ya uamuzi hivyo huwezi kutekeleleza ufafanuzi.
Mfano ni kama jaji amesikiliza kesi akatoa hukumu, anakuwa ameshamaliza haruhusiwi kutoa maelezo eti ufafanuzi wa hukumu zaidi na nje ya kilichoandikwa kwenye hukumu hiyo. Hivyo ambaye hajaridhika huchukua hatua ya kukatarufaa.
 
Lissu anafanya makusudi kuvuruga uchaguzi, kwani anajua hawezi kushinda. Tamanio lake ni kuleta vurugu ili kuchafua nchi kwa wahisani ionekane Tanzania hakuna haki wala demokrasia. Hila zake hazitafanikiwa.

Usipende reply ukiwa chooni
 
Watanzania wanataka uhuru na haki ndani ya nchi yao. Watanzania hawataki kuonewa na kunyanyaswa na kutukanwa ndani ya nchi yao. Ndiyo maana kipindi cha miaka 5 ya Meko amejisifu kuwa kafanya maendeleo sana, lakini why this REJECTION ? Sasa hivi haongelei tena madaraja na madege
 
Lissu anafanya makusudi kuvuruga uchaguzi, kwani anajua hawezi kushinda. Tamanio lake ni kuleta vurugu ili kuchafua nchi kwa wahisani ionekane Tanzania hakuna haki wala demokrasia. Hila zake hazitafanikiwa.
Aliyeweza kuiba 1.5T na kisha kufukuza CAG mchana kweupe anashindwaje kuiba kura ambazo ni siri? Subiria uone mawakala wa vyama vingine watakavyonimwa nakala za matokeo ndo utajua nani mwenye nia ya kuvuruga utulivu aka amani ya nchi
 
Watanzania wanataka uhuru na haki ndani ya nchi yao. Watanzania hawataki kuonewa na kunyanyaswa na kutukanwa ndani ya nchi yao. Ndiyo maana kipindi cha miaka 5 ya Meko amejisifu kuwa kafanya maendeleo sana, lakini why this REJECTION ? Sasa hivi haongelei tena madaraja na madege
 
Nadhani Robert anachangia Sana kumpa huyu jamaa kiburi. Ametamba twiter kuwa yeye ndie aliemshauri asitii.
 
Lissu anafanya makusudi kuvuruga uchaguzi, kwani anajua hawezi kushinda. Tamanio lake ni kuleta vurugu ili kuchafua nchi kwa wahisani ionekane Tanzania hakuna haki wala demokrasia. Hila zake hazitafanikiwa.
Tatizo lake kubwa hivi sasa mbinu zake zimejulikana na ameamua kufanya makusudi. Anasubiriwa tu wahenga walisema ''subira yavuta heri.''
 
Mataahira sijui mkoje!!! yaani Lissu anavunja kanuni, anaadhibiwa hamtaki!! sasa ataongozaje nchi kama hataki kufuata Kanuni??
TL anafahamu kabisa hawezi kushinda, wewe subiri tu, anaweza kuwa disqualified kwa sababu anafanya makusudi, kupigwa kwake risasi na njama zao na Chadema ndio zinawatesa hivi sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…