Kampuni Kutoka China Kujenga Daraja la Dar- Zanzibar

Kampuni Kutoka China Kujenga Daraja la Dar- Zanzibar

Jemedari mkuu Magufuli angelikuwa hai ningeamini hilo jambo linawezekana bila upembuzi yakinifu lakini hawa waliopo ni michakato tu!
Upembuzi yakinifu ni hatua muhimu sana kabla ya kufanya uwekezaji. Kuna wakati tulinunua boti ya kufanya safari za Dar Bagamoyo bila upembuzi yakinifu, bila shaka tunajua hasara tuliyopata.
 
Kwa kuwa kama ilivyo kawaida yetu kila awamu lazima iache alama yake, na miradi mingi mikubwa serikali ya sasa inayofanya ni ile iliyoachwa na Magufuli.

Ngoja tuone miradi mikubwa ya awamu hii itakuwa ni ipi, naona huu wa daraja la Dar - Zanzibar utakuwa kama tulivyoona ule wa Kigongo - Busisi ulioasisiwa na mwendazake kule Mwanza, kila mtawala lazima apakumbuke nyumbani kwanza.

Kama ikitokea siku ujenzi huo ukaanza, naona huo ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa biashara ya boti za kusafirisha watu, mwendo hapo utakuwa ni magari tu yanapishana kwenda Zanzibar.
Hawez kujenga huo mradi nchi Ina Hali ngumu na miradi iliyopo Bado inatakiwa pesa nyingi kukamilisha
 
Serikali imeanza mazungumzo na Kampuni ya China Overseas Engineering Group Company (COVEC) ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika ujenzi wa daraja litakalo unganisha Tanzania Bara na Zanzibar.

Naibu Waziri wa Uchukuzi Godfrey Kasekenya amesema bungeni leo Aprili 28, 2023 kuwa Mazungumzo hayo yameanza Machi 11, 2023 na yalihusisha wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Ujenzi kwa upande wa Tanzania Bara na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa upande wa Zanzibar.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mwantum Dau Haji aliyetaka kujua mpango wa serikali kujenga daraja hilo, Naibu Waziri Kasekenya amesema bado mazungumzo yanaendelea na serikali inakusudia kujiridhisha na teknolojia zinazotumika katika ujenzi wa madaraja makubwa kabla ya kuanza ujenzi.

“Daraja hili litajengwa kwa kushirikiana na sekta binafsi kwa utaratibu wa PPP (Public-Private Partnership),” amesisitiza Kasekenya.

#HabarileoUPDATES
View attachment 2602214
Mwaka jana walisema ifikapo mwezi wa 4 mwaka 2023 wataanza ujenzi wa daraja pale Jangwani.
Wameshaanza?
 
Wachina Wana reserve kubwa sana ya Hela, hawataki zikae hivihivi, wanataka zizalishe, na wai-annex Dunia na uchumi wao, sisi tunaona daraja, wao wanaona wanaongeza sphere of influence, they are extending territorial influence, a sort of neo colonialism.

Our treasury will be paying bills, mirija itakuwa inanyonya kupeleka china.

M ona hawaleti teknolojia wafungue viwanda? Mbona hawaombi ardhi walime, huku ndiko Kuna ajira za watu wengi, na ni huko ndio tutapata export.

Ukijenga daraja maana yake unaanza biashara ya ku-import kutoka china labour, building materials, na daraja likiisha ndio basi tena, halizalishi kitu. Halafu daraja kwa ajili ya watu milioni moja walioko zenji?

May be kama wanatujengea for free
 
Haya madaraja tuliyonayo urefu usiozidi meter kumi maintance costs inatushinda yanachakaa mpaka yanasombwa na mvua.

Hilo daraja la baharani ambalo litakuwa battered na weather elements usiku na mchana 365 ili lidumu zinahitajika gharama kubwa za upkeep ndio tutaweza.

Huko serikalini kuna vitimbi vya ‘Masakuu na Utoro’ngo’ngo’ afadhali.
 
Hizi ndo hoja muhimu kwa nchi.

Tumezoeshana hoja za nani anataka urais, mara huyu kachepuka, mara fulani pisi kali......

Turudi hapa tujadili maendeleo ya nchi yetu.

Daraja lijengwe nitaomba nifanye jogging ya kwenda zenji na kurudi
Kujenga hilo daraja sio rahisi. Huo mradi kwa harakaharaka unaweza kugharimu trillion 30. Trilion 30 kujenga tu daraja kwa nchi hii bado sidhani kama tuna huo msuli
 
Kujenga hilo daraja sio rahisi. Huo mradi kwa harakaharaka unaweza kugharimu trillion 30. Trilion 30 kujenga tu daraja kwa nchi hii bado sidhani kama tuna huo msuli
Kiukweli haufai,hakuna Nchi iliyoendelea ilianza na mamiradi yasiyo na Tija kama hayo
 
Kampuni ya China Overseas Engineering Group imeonesha Nia ya kujenga Daraja la km 40 Kati ya Dar na Zanzibar,Naibu Waziri Kasekenya amesema Bungeni..

My Take
Kama Daraja hili litajengwa linaweza kutumia nusu ya gharama za Kujenga SGR.

Swali Je Tunalihitaji Kwa Sasa?
Daraja Dar to Znz!!
Meli zitapitaje kuja Dar kutoka mataifa mengine....
 
Kiukweli haufai,hakuna Nchi iliyoendelea ilianza na mamiradi yasiyo na Tija kama hayo
Hata kama kungekua na tija, bado hatuna uwezo wa kujenga daraja moja kwa gharama hizo.

Nimeona umbali wa daraja unaweza kufanana na wa lile la Tianjin. gharama za Tianjin bridge za kule china, wao walitumia trilion 50. Hapo kil akitu wanazalisha wao, huku karibu kila kitu tunaagiza si inaweza kufika trilion 80.
 
Waliowahi kwenda .Jee huko kwao wameshajenga daraja la kupita mkondo mkali kama wa magogoni au Nungwi.
Miradi ya Viongozi wa Tanzania inashangaza sana ,just imagine anachoongea huyu bwana hapa kina logic kabisa ila wenye akili ndogo Huwa hawaelewi
 
Back
Top Bottom