Kampuni ya ICTE kutoka Ufilipino imeshinda tenda kuendesha bandari ya Darbun, SA kwa miaka 25

Nani kakataa kubinafsisha , watu wanapinga vifungu vya mkataba , Gazeti la Uhuru la hao hao CCM , na hata kama South Africa wamebinafsisha si Kwa mikataba ya kihuni kama hii...
 


 
Tusifanye mambo kwa vile wengine wamefanya makubaliano ni muhim zaidi kuliko kukurupuka.

Mkataba wa hao wafipino na South Africa ungeuambatanisha ingependeza.
 
Mtetezi mwingine wa kampuni ya kikoloni huyu hapa. Bora walafi wetu wanaopiga huko bandarini tunawamudu na tuna uwezo wa kuwatoa haraka sana kuliko huyo mkoloni wa kiuchumi. Afrika kusini ilizoea tabia za mkoloni kitambo sana na ilichelewa kupata uhuru kisha ina uzoefu wa kuishi na mkoloni hadi leo anaishi naye kama mwananchi mzawa. Kijana unawakumbuka vizuri makaburu na siasa zao lakini? Ok, sawa hawa masultani unataka waje kutawala uchumi wetu? Kama tutaweza kuwavumilia vitendo vyao na tukaishi nao kama wazawa tu waje na wapewe bandari zote wafanye kwa ufanisi sisi tutaenda kuchunga ng'ombe huko mbugani. Kijana naona unataka kutawaliwa kwa kuwa huna uwezo wa kusimamia rasimali zako na ukafanya kwa ufanisi
 
Kwa mtindo huo wa kuiga iga na kufuata namna mataifa mengine yanavyowekezwa na mataifa ya nje tutajikuta hatuna mipaka wala utaifa. Wenye nguvu na uchumi mkubwa ndio watakuwa wanawekeza kwenye mataifa yasiyo na ufanisi wa kuendeleza rasimali zake. Watakuja hata wengine kuwekeza kwenye akili zetu mradi tu wapate maslahi yao.
 
We mzee tunza heshima YAKO
 
Kama bandari yetu imekaliwa na kampuni ya Kifisadi wanashindwa nini kuitoa na kuweka isiyo ya kifisadi?

Je Afrika kusini wamebinafsisha mpaka ardhi?
Haina ukomo wa muda?
Imewapa bandari za bahari na Maziwa?
Haitatozwa kodi?
Wamepewa mpaka reli na barabara zinazoingia bandarini nk nk

Hao Uhuru ni Madalali wa bandari tu,mktaba wa kijinga kama huu hatuukubali.
 
Akili Zako hazina Akili kabisa.. kwani watanzania wamepinga kubinafsishwa Kwa bandari au wamepinga aina ya mkataba tulioingia?..
 
Umeandika pumba,na hii inathibitisha kua uwezo wako wakufikiri umetawaliwa na chuki pamoja na mawazo ya toka enzi za ujima.
 
Huyu mwamba huwa anaongea vitu Bila logic ilimradi apate attention kama demu vile..[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Akili zako fupi kama kimo chako
 
Umeandika pumba,na hii inathibitisha kua uwezo wako wakufikiri umetawaliwa na chuki pamoja na mawazo ya toka enzi za ujima.
watetezi mko wengi mliopigwa upofu msione athari za uwekezaji huo kwa taifa. Mnachoona ni ufanisi tu kwa tamaa zenu kwamba nanyi mtapata shea au ngawira humo
 
Wazalendo wa kweli daima tutakuwa wazalendo wa kulinda rasimali za taifa kwa vizazi vijavyo. Hatuwezi kuiga namna mataifa mengine yanavyowekezwa
 
watetezi mko wengi mliopigwa upofu msione athari za uwekezaji huo kwa taifa. Mnachoona ni ufanisi tu kwa tamaa zenu kwamba nanyi mtapata shea au ngawira humo
Fuatilia vitu ambavyo ubongo wako unaweza kuvielewa,issue ya investment ni kubwa sana kwa akili yako kuielewa,hata kukuelewesha ni kazi bure tu.
 
Kiukweli ili gazeti la UHURU nilizuri sana kwa kufungia vitumbua na chapati halitoi rangi rangi kama yale kichina
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…