Daktari W Sindabhalla
JF-Expert Member
- Jan 29, 2017
- 600
- 580
kwa sehemu upo sawa Mkuu,Sasa ukiwa na hekima bila pesa hayo yotendo huwa kinyume chake watu wote watakuona sisimizi hata wazazi wako watasema tumezaa kutoa minyoo tumboni,ndugu zako watakudharau hadi basi,acha tu wenye pesa wajivune hujui walinyanyasika vipi walipokua wakitia mawazo ya hekima wakiwa makapuku na yakapuuziwa na kudhihakiwa... ufukara ni mbaya sana ndugu yangu!
kwa sehemu upo sawa Mkuu,
isipokuwa, kuwa na hekima ama kuitafuta HEKIMA si kuwa MASIKINI.
Wala haimaanishi kwamba wenye HEKIMA ndio masikini.
Hivyo, ni heri kuwa na Hekima,
maana ni rahisi Fedha kumfuata mwenye Hekima.
Nadhani tunashindwa kumuelewa Suleiman na mawasiliano yake na Mungu, na tunashindwa kutofautisha mtu mwema na mtu Mwovu, Suleiman alifanikiwa kuwasiliana na Mungu kwa utu wema wake tena akiwa mfalme akaulizwa apewe nini yeye akiwa mfalme tayari anakazi ya kumuingizia kipato na mtu mwema pia kwenye kazi yake na maisha yake ndipo alipoomba hekima Ili aitumie kwenye maamuzi atakayokuwa anafanya yawe ya hekima na kuacha kuomba mabaya kama kuua maadui zake au mambo mabaya ila aliridhika na kazi aliyokuwa nayo na kuomba aongezewe hekima ndipo Mungu akambariki kwa kuwa mtu mwenye Mali nyingi kwa kuchagua kuwa mwema badala ya kuomba mambo mabaya, Sasa mtu huna kazi alafu uulizwe upewe nini alafu ujibu hekima Sasa hizo hekima ukipewa uzunguke nazo kutoa hekima bila kazi siutazeeka ukiwa masikini? Hao wakina Trump ni kweli wanamali lakini tunawapima kwa wema au ubaya wao maana sasa tunamfumo wa sheria ndiyo zinazotumika kurekebisha watu wabaya na pia tunakuwa na watu wema na watu wabaya katika maamuzi yoyote yanayofanyika katika ngazi zote hivyo watu wanatakiwa kuangalia maana yoyote yanayofanyika je yatakuwa yenye haki au wema au yatakuwa yenye chuki au mabaya tofauti ni kipindi cha Mfalme Suleiman yalitoka kwa Mfalme pekee mpaka kwa mambo ya kifamilia kitu kutenda katika wema bila kuongozwa na nguvu ya ziada kutoka ndani ilikuwa ngumu kutoa majibu ya haki ndipo Suleiman akaomba Hekima yaani kutendea watu wake Wema na siyo ubaya kwa mambo yatayokuja mezani kwake kutolea maanamuzi.Donald Trump alitangulia kutengeneza ela kwanza lakini hekima zikagoma kumuijia akiwa na ela.
William Ruto alitangulia kutengeneza ela kwanza lakini hekima zikamgomea akaingiza nchi kwenye machafuko ya damu 2008 na kubaki kwenye historia hiyo mbaya.
Hiyo ni tofauti ya wema na ubaya, au watu wema na watu wabaya wakikaa pamoja nini watafanya na siyo Hekima aliyoomba Mfalme Suleiman, watu wawe na hela ila wawe wema na Hekima aliyoomba Suleiman ilikuwa ni kutenda wema au kutoa maamuzi yenye haki Sasa Kuna watu wameshindwa kutofautisha hekima ambayo ni haki ya kumtendea mtu anayestahili na maarifa au elimu ya kujielewa aliyonayo mtu.Yafuatayo yatajiri:
Wenye fedha:
1. Watauana kwa kuibiana fedha na wake/waume zao.
2. Watakosa ubunifu kwa kuwa hawana hekima.
3. Watahujumiana.
4. Hawatatembeleana.
Wenye hekima:
1. Watabuni vitu kutokana na hekima zao.
2. Wataamua magomvi kwa hekima hivyo watakuwa na amani.
3. Watapendana na kutembeleana hivyo watashirikiana.
4. Watakuwa na maendeleo kwasababu hawataibiana hekima.
Nimeipenda sana hii comment yako, we live in the world where people have forgotten what's real matters in our life.Wale ni waasisi wa bara la giza! Wameanza kuitafuta nuru miaka hio ambapo civilization ilikuwa hakuna mpaka ikaanza kuingizwa nchini taratibu!
Jamii by far zilitegemea sana solidarity for protection against inhumanity acts na socialization. Dunia ika evolve na kuletewa civilization ika mature na kuwa utandawazi kwa sasa inter culture imetamalaki. Waliotuletea civilization concepts ndio waliotuharibia yale mazuri yote ya hekima.
Kitambo kidogo about 25 years ago ilikuwa ni kawaida kwa watoto wa mitaa ya jirani kucheza pamoja kwenye open spaces around the street. Kukaribishana kula pamoja muda wa mchana haikuwa tatizo.Kilichopelekea hii situation ilikuwa ni hekima tu ya wazazi.
Kumuadhibu mtoto wa jirani ilikuwa ruksa sio kwa kuwa wazazi wake hawakumpenda mtoto ila kulitakiwa kuwe na equity katika malezi ya watoto ili kujenga jamii iliostaarabika na yenye hekima. Leo hii gusa mtoto wa mtu uone moto wake kwanza hata kumuona hutamuona wazazi wengine wanalea vibaya watoto wanajikuta wanafuga watoto washenzi wa tabia na ndio hawa hata hekima tu ndogo za maisha ya kuishi na watu tofauti kwenye jamii hawana. Unamuozesha binti akikaa miezi 6 anaachika arudi kwao au akapange mtaani aendelee kudanga. Watoto wa kiume ndio hawa mashoga na wengi waliokosa weledi hata wa kujisimamia na familia zao mpaka waombe msaada kwa mama😅
Leo hii wewe watoto wako unawaruhusu hata wakacheze nje tu? Umefunga maukuta na mageti alarm cameras ili tu watu wasiwe na access ya kuja kwako. Hii ni picha halisi tu kwamba ile hekima ya kuishi kama social beings haipo, solidarity hamna hata kidogo! Mtu akija kwako hata ndugu unaona kero kama kaja kukumalizia chakula ila utamaduni ulikuwa hivyo 25 yrs ago about 2 decades and a half!
Watoto waliozaliwa 2000’s mpaka kufikia leo ukizungumzia social lifestyle ya kitaani hawaijui hata kidogo. Wamezaliwa wakafugwa kama broilers. 😅 They know nothing about life and its roots!
Hakuna mwenye hekima asiye na Pesa.Sasa ukiwa na hekima bila pesa hayo yotendo huwa kinyume chake watu wote watakuona sisimizi hata wazazi wako watasema tumezaa kutoa minyoo tumboni,ndugu zako watakudharau hadi basi,acha tu wenye pesa wajivune hujui walinyanyasika vipi walipokua wakitia mawazo ya hekima wakiwa makapuku na yakapuuziwa na kudhihakiwa... ufukara ni mbaya sana ndugu yangu!
kwahiyo, hapo napata ufahamu kwamba hekima aliyoiomba Sulemani, ilikuwa ni kitendea kazi ktk ofisi yake ya Kifalme. ASANTE kwa ufahamu huo.Nadhani tunashindwa kumuelewa Suleiman na mawasiliano yake na Mungu, na tunashindwa kutofautisha mtu mwema na mtu Mwovu, Suleiman alifanikiwa kuwasiliana na Mungu kwa utu wema wake tena akiwa mfalme akaulizwa apewe nini yeye akiwa mfalme tayari anakazi ya kumuingizia kipato na mtu mwema pia kwenye kazi yake na maisha yake ndipo alipoomba hekima Ili aitumie kwenye maamuzi atakayokuwa anafanya yawe ya hekima na kuacha kuomba mabaya kama kuua maadui zake au mambo mabaya ila aliridhika na kazi aliyokuwa nayo na kuomba aongezewe hekima ndipo Mungu akambariki kwa kuwa mtu mwenye Mali nyingi kwa kuchagua kuwa mwema badala ya kuomba mambo mabaya, Sasa mtu huna kazi alafu uulizwe upewe nini alafu ujibu hekima Sasa hizo hekima ukipewa uzunguke nazo kutoa hekima bila kazi siutazeeka ukiwa masikini? Hao wakina Trump ni kweli wanamali lakini tunawapima kwa wema au ubaya wao maana sasa tunamfumo wa sheria ndiyo zinazotumika kurekebisha watu wabaya na pia tunakuwa na watu wema na watu wabaya katika maamuzi yoyote yanayofanyika katika ngazi zote hivyo watu wanatakiwa kuangalia maana yoyote yanayofanyika je yatakuwa yenye haki au wema au yatakuwa yenye chuki au mabaya tofauti ni kipindi cha Mfalme Suleiman yalitoka kwa Mfalme pekee mpaka kwa mambo ya kifamilia kitu kutenda katika wema bila kuongozwa na nguvu ya ziada kutoka ndani ilikuwa ngumu kutoa majibu ya haki ndipo Suleiman akaomba Hekima yaani kutendea watu wake Wema na siyo ubaya kwa mambo yatayokuja mezani kwake kutolea maanamuzi.
Ni kweli maana ili zibaki mkononi ni lazima kupanga matumizi kwa hekima!!Pesa hazikai kwa mtu asie na busara
Ndio kuna kitu wanaita "Nidhamu ya fedha" Ukikosa nidhamu ya fedha ,fedha hazikai mkononi zitakimbia zote!!Ni maneno ya kufarijiana ukweli ni kamba pesa ina hitaji discipline ya hali ya juu kama huwezi kua nayo pesa utazisikia kwa majirani
Hakuna mwenye hekima asiye na Pesa.
Kama Mao Tsetung alivyoweka kwapani US$ 13 ml na Fidel Castro $ 900 ml na wote kukaa na hekima kichwani. Huku mwenzao Nicolae Ceausescu akipokea mshahara wa 18.000 Romanian lei sawa na US$ 1200 kwa exchange rate ya mwaka 1989, akidhaniwa yeye na Mwl Nyerere ndiyo Marais Wajamaa waliojilipa mishahara midogo kuliko wote kwenye urais wao.Weka pesa kwapani,
Kaa na Hekima kichwani. Utaona raha ya Dunia.
Like the Roman Catholic Clerics.If you are President of the richest country on earth being poor is a choice not inanyway an outcome.
Hekima haikai kwenye roho ya ubaguzi, udukuzi na jeuri.Nani kakwambia Trump hana hekima?
Hekima yake ndiyo ilimfanya Mike Tyson akamuajiri, baada ya yeye Trump kupata pesa nyingi pesa hizo zikabomoa hekima yake. Kumbe pesa zinaharibu hekima lakini hekima haziharibu pesa, bora basi hekima kuliko pesa kama ni hivyo.Trump hana hekima ila kwa alipofikia kiuchumi hamna kitu ambacho atafanya kisiwe influential!
Not that kwamba yeye ni mtu mwenye hekima ila ni mtu ambaye ana ushawishi wa kifedha.
Sawa mkuuHekima yake ndiyo ilimfanya Mike Tyson akamuajiri, baada ya yeye Trump kupata pesa nyingi pesa hizo zikabomoa hekima yake. Kumbe pesa zinaharibu hekima lakini hekima haziharibu pesa, bora basi hekima kuliko pesa kama ni hivyo.
Zawadi za Nyerere za kustaafu walikubaliana na Mama Maria wakazichukuwa wakazipeleka Mwanza kuanzisha kituo cha yatima na zingine wakasaidia maskini wa Butiama ikiwemo kukodisha mashamba Butiama na kuanzisha kilimo cha kufa na kupona na mazao ya shamba waligawa kwa wanakijiji bure kwa wasiojiweza na kwa bei ndogo sana kwa wanaojiweza. Mimi nimeishi sana Butiama.Nyerere alikua na pesa za kufa mtu. Kumbuka kipindi anastaafu, alizawadiwa ng'ombe na vitu vingi sana sema mzee yule hakujionyesha.
Nkrumah hakustaafu, alipinduliwa na waliompindua walimfuata huko huko Misti kwa wakwe zake kummalizia.
Mandela alikua na pesa
Kwahiyo Obama alikuwa zoba mbele ya John McCain Senator tajiri wa Arizona kwenye kinyang'anyiro 2008?Ukiwa na hekima huku huna hela unaonekana zoba tu
Karl Marx? Plato? Socrates? Aristotle? Pythagoras? Newton?Huwezi kuwa na Hekima ukawa kapuku.Ukiona mtu hana hela hiyo ni indication moja wapo kuwa hekima haimo kwake.
Of course yes, power turned to be Litmus Test for his wisdom; the test that he did not pass.Amekuwa madarakani tumeona actions zake
Unamuona Trump mwehu eti? hivi unaweza kua US president huna akili?