Katika ulimwengu wa kishirikina, nguo yako ni wewe

Mkuu maisha yako yamefanana sana na yako.
Mimi niliacha kuswali nikiwa form 2 hapo ndio nikawapa upenyo wachawi.
Nilivyoingia form 3 nikawa nayumba sana kimasomo wakati form 1 na 2 nilikuwa naongoza.
Kufika form 5 nilifaulu ila sio kwa viwango vile ambavyo watu walikuwa wanangojea surprise.
Nikaja kupitwa na watu ambao nilikuwa nawafundisha kila siku topics mbalimbali,badae tukaingia advance ndio wenge likaongezeka nikawa sijielewi.
Lakini hadi kufikia hapo bado nikawa sijashtuka chochote ni kama nilifungwa hivi,baadae nikaungaunga nikaingia chuo.
Baada ya kuingia chuo nikawa nakoswakoswa kudisco kila mwaka,kwa mfano unakuta GPA iko chini ya pass mark ukifuatilia unagundua kuna marks za somo moja zimesahaulika hazijahesabiwa.
Nikaja kushtuka niko chuo mwaka wa pili tena kuna jirani ndio alitushtua alimfuata mzee akamuuliza mbona huyu mwanao anakula vizuri milo yote lakini kila siku anazidi kukonda tu bila sababu,yaani nilikuwa kama mgonjwa aliyeugua TB kwa muda mrefu,mabega yamepanda hapo ndio nikashtuka na kuanza kuhangaika kwa wataalamu kuombewa.
Nikaingia mwaka wa 3 chuo nikiwa na afya nzuri na muonekano wenye nuru nikamaliza salama.
Baadae nikaingia mtaani kupambana ikawa vita inaendelea nikishtuka najipanga hivyo hivyo nikatoboa kiasi chake
 
Ile ishu yako iliisha vipi je alirejea nyumbani
 
Amna mkuu, ukistukia mchongo, unajipanga upya muhimu ni kuusoma mchezo, ukitaka kujua unaishije waangalie sana waliokuzunguka utajua tu. Unaweza kujua upo sawa kumbe ni kinyume chake, meditation inasaidia sana
Tufundishe meditation mzee.Wengine wanasema meditation ni nguvu za giza
 
Nguo inatumiwa kwa sample kama sample zingine like nywele,nyayo, choo, dam, nk. Sema nguo inatumika coz ni sample rahisi kupatikana. Sema inatokana na utaalam wa mtu . Wale wakongwe wanachukua kimvuli boss.
 
yes hii ina ukweli. zamani nlikua napenda sana kuwatumia watu random nguo zangu used na viatu as watu wa kijijin ndugu mbali mbali wanaomba...siku nlipigwa stop na dingi hahah na hakunipa sababu. sasa naelewa.
Hivi kumbe vipo na watu tiyari wanajua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…