Uchaguzi 2020 Kauli mbiu ya Uhuru na Kazi yampaisha Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Kauli mbiu ya Uhuru na Kazi yampaisha Tundu Lissu

Mshaurini aachane nayo atawainua wenye nayo. Amekosa Slogan hata aokoteze za TANU na CCM? Atasababisha waanze kuvaa sare zao za kuwasha mwenge.

Screenshot_2020-08-19-19-36-25-1.png
 

Attachments

  • Screenshot_2020-08-19-19-36-25-1.png
    Screenshot_2020-08-19-19-36-25-1.png
    180.8 KB · Views: 1
Hii kaulimbiu aliitumia Mwalimu Nyerere mara baada ya Tanganyika kupata uhuru.

Watu walifurahi sana kupata uhuru wakafikiri kupata uhuru maana yake serikali itawafanyia kila kitu.

Kuna mzungu mmoja wa TANU - sikumbuki vizuri nani, inawezekana Derek Bryceson, akaanzisha kaulimbiu ya "Uhuru na Jasho".

Mwalimu Nyerere akaipenda, akaibadilisha kidogo na kuifanya iwe "Uhuru na Kazi".

https://www.google.com/url?sa=t&sou...FjACegQIARAB&usg=AOvVaw2W7ef6-8Dc1zb76RELjZNn
 
Uhuru upi?

Hivi mwananchi wa nanjilinji kule ukiongelea juu ya uhuru si anakushangaa?

Hilo la uhuru atawapata viongozi wenzie wa pale ufipa
Swali lilipaswa kuwa Uhuru upi? Comment zilizofata zimekuwa conclusive
 
Kipenga cha kuanza mbio (za kampeni) hakijapulizwa. Yeye kaishaanza kukimbia ovyo ovyo. Wenzake wametulia wakiangalia silaha alizo nazo (anazotumia kuwashawishi wananchi wampe kura).

Hivyo washindani wake anawapa fursa ya kuzijua silaha alizonazo (weakness zake) na na hivyo kuwapa fursa ya kupanga aina ya silaha watakazotumia kumwangamiza (kujibu mapigo anayofanya sasa hivi). Kwanza kipenga cha kuanza mbio hizo kitakapopulizwa jamaa huu atakuwa tayari ameshachoka ile mbaya na alishamaliza silaha zake zote.

Hivyo subiri kuona jinsi kipenga cha kuanza mbio hizo kitakapopulizwa atakavyoangamizwa kwa silaha nzito nzito, hapo washindani wake watakapoanza kujibu mapigo (ya kushawishi kura za wananchi). Mbaya zaidi washindani wake wako 16 kutoka majeshi (vyama) mbali mbali. Hashindani na jeshi la ccm pekee bali na majeshi (vyama) 16! Kuna majeshi ya Bernard Membe (Jasusi mbobezi), Lipumba (Professa mbobezi wa Uchumi wa dunia), Mbatia ( mbobezi wa majanga ya dunia) na mabobezi mengine ya kadhalika na kadhalika ya dunia! Yaani jamaa ajiandae tu kurudi ughaibuni kuendelea na matibabu yake na kuichafua nchi yetu mbele ya jumuiya za kimataifa kama alivyozoea kutufanyia. Ila urais haiwezekani hata kidogo. Ubunge nao wakina Ndungai walishamalizana naye!
....relax man..., silaha unazijua?
 
Kama mna wanachama wengi kwanini mnaogopa tume huru ya uchaguzi?
Hatujawahi kuwa na tume ambayo sio huru, haya maneno ya kukaririshwa na wanaoshindwa,wakati mwengine muwe mnawauliza wenyeviti wenu wa hizo Sacco's Kama tume sio huru mbona Kila chaguzi mnapata ongezeko la kura za uraisi na wabunge pia wanaongezeka idadi kwanini kusiwe inapungua tu, halafu Kama tume sio huru unashiriki uchaguzi wa Nini?
 
Dhana ya Uhuru zaidi kujiamulia mambo yao wenyewe ni dhana yenye maana pana sana. Watu jamii ya waislam wanaamini nadharia ya Serikali kutokuwa na dini ni nadharia iliyowekwa ili kuzuia ustaarabu wa dini yao kustawi.

Tundu anapaswa kusema bila kutafuna maneno endapo ataendeleza ukandamizwaji huo au kuweka wazi ili apate kura za wenye dini inayokandamizwa.

Huwezi kuwakandamiza watu kwa muda mrefu pasipo wao kuzinduka. Binafsi najaribu kuwaza ni jinsi gani CHADEMA itatatua tatizo hili. Watu wanajifunza asili yao na pale wanapojihisi wanabaguliwa huwa tayari kutetea haki zao na ikibidi ghasia hutokea.

Kwani watu hubadilika na kamwe hawatoridhika kujiona wao no jamii ya daraja la pili iwapo kuna chama kinaweza kuwapa Uhuru wa kujiamulia mambo hao ikiwemo utamaduni wao.
 
wanachama hai wa CCM mpaka jana Ni 18.2 milion hapo bado kura za wapenzi tu ambao sio wanachama, kwani ukiambiwa CCM Ni chama kikubwa na kina mizizi mpaka vijijini ulikuwa unafikiri Nini

Wapinzani wenu wana 22 Million na bado mashabiki wao.
 
Hatujawahi kuwa na tume ambayo sio huru, haya maneno ya kukaririshwa na wanaoshindwa,wakati mwengine muwe mnawauliza wenyeviti wenu wa hizo Sacco's Kama tume sio huru mbona Kila chaguzi mnapata ongezeko la kura za uraisi na wabunge pia wanaongezeka idadi kwanini kusiwe inapungua tu, halafu Kama tume sio huru unashiriki uchaguzi wa Nini?
Watanzania wote wanajua tume ya uchaguzi ya Tanzania sio huru, labda kama wewe unaishi Burundi. Hilo sio swala la kubishana kabisa sababu liko wazi na halihitaji degree kulifahamu otherwise elimu yako ni ile ya kukalili na sio ya uelewa.

Hatuwezi kususia uchaguzi mkuu sababu ndio utaamua mustakabali wa maisha yetu ya miaka 5 ijayo.

Mwaka huu mwizi asijaribu kuiba kura, atakatwa mkono.
tapatalk_1596824683065.jpg
tapatalk_1585594105790.jpg
 
Watanzania wote wanajua tume ya uchaguzi ya Tanzania sio huru, labda kama wewe unaishi Burundi. Hilo sio swala la kubishana kabisa sababu liko wazi na halihitaji degree kulifahamu otherwise elimu yako ni ile ya kukalili na sio ya uelewa.

Hatuwezi kususia uchaguzi mkuu sababu ndio utaamua mustakabali wa maisha yetu ya miaka 5 ijayo.

Mwaka huu mwizi asijaribu kuiba kura, atakatwa mkono. View attachment 1542391View attachment 1542396
Usiseme watanzania sema Wana Sacco's wa chadema
 
Mshaurini aachane nayo atawainua wenye nayo. Amekosa Slogan hata aokoteze za TANU na CCM? Atasababisha waanze kuvaa sare zao za kuwasha mwenge.

View attachment 1542362
Uhuru na Kazi' ndicho watu Wanachotaka kusikia kwa sasa.ingelikuwa wananchi hawataki kusikia juu ya Uhuru wao usingewaona kwenye mikutano yake
 
Back
Top Bottom