Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

Hivi unadhani kanali hakua na mawazo Kama yako,kua dogo kajichanganya,ngoja nimnyooshe awe na adabu,matokeo yake yeye yupo mochwari?
Kuwa makini,mkuu.
Hujanielewa nimesema usijenge chuki kitu cha kwanza kinachopelekea migogoro ya Askari na raia ni chuki za raia kwa Askari, hio sio sahihi na haikubariki kwanini ujenge chuki kiasi cha kuona kwamba aliefanya mauaji ya kumuua Askari yupo sahihi km sio ujinga ni nini?
 
mtu anaua wanajeshi watatu anaenda kijijini kwao anaeleza hali halisi kwababu.

babu anamwambia punzika miezi mitatu mjukuu wangu halafu rudi mjini ukapige kazi bila hofu.

unarudi mjini mamboyote saafi kabisa hatawale waliokuwa wanakufata nyumbani nakusumbua mkeo na watoto hawaji tena na rodi unaingia Kama kawaida

dogo kafeli pakubwa mnooo hadi nimekasirik
 
Mungu alituumba tupendane na kuthaminiana lakini haya mavitu ya ulimwengu huu Vyeo,pesa,mali vinatuvimbisha makiburi mpaka tunakuwa kama wehu na kusahau utu wa mwenzetu na kujiona sisi ni bora zaidi ya mwingine. Pole kwa pande zote Mbili kwa maumivu tofauti ktk sakata hili.
 
Kwa hio na wewe utafanya hivyo unaua alafu unakimbilia kwa Babu au sio? Chuki za kijinga
 
Hakuna mwanaume rijali yuko tayari kuvumilia ukhanithi , yaani wewe ukurupuke tu baada ya kuvombiwa gongo huko vichochoroni na kuanza kuzaba mtu vibao ,una akili una kamasi ?
Watu wawe na heshima aisee hata kama ni kupishana kauli ,huna haki ya kwenda kushambulia mtu physically .
Unayemshambulia ana haki ya kujibu mapigo , wewe uwe askari au kikaragosi yoyote lazima utiwe adabu ukifanya hivyo unless ukutane na boya
 
Safi sanaaa ukishindwa kuikotrol bangi wacha usaidiwe.
 
Ofcourse ujanja wa kujitoa mikononi mwa wenye macho hawana
 
Haya kama ndivyo nilivyosoma basi haikuwa kazi ya jeshi ni kazi ya polisi, tunategemea muhusika apelekwe kwenye vyombo vya sheria.

Dereva kaua bila kukusudia, temper ililetwa na dereva aliyetumia madaraka yake kumtesa kijana wa watu.

Afisa wa jeshi kapoteza maisha kizembe sana mno, unatumia madaraka hata pasipostahili, kuna watu hawapendi kuonewa

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Na wewe unahisi ungefanikiwa kufika mkata baada ya kuua? Punguza ujinga
 
Uwe unaelewa wewe mpumbavu , huyo bodaboda anekuta njia imezibwa akauliza kwanini ameziba njia ?
Huyo askari zuzu akaanza kumpiga makofi ,ni nani alikuwa na makosa hapo ?
Muwe mnatumia akili ninyi kondoo
 
...Pamoja na uzibaji wa njia Sijui walijibishana nini kama muwajuavyo madereva bajaji na boda, keno akamlamba kibao kijana akaon sio kweli kaenda kweny bajaj yake katafuta silaha kaichukua, kwamba hapa naenda kujeruhi, kamchoma nayo" unasema kaua bila kukusudia? Basi Sheria ni pana aisee
 
Acha kua biased, usiegemee upande kila mmoja ana makosa kwa kiasi chake Ila alievuka mpaka ni aliechukua maamuzi ya kuua baada ya kuzidiwa nguvu kwenye one vs one na kuchezea mambata, kata funua za kutosha unakimbilia bisibisi? Tulia unabishana na Askari? Haya sasa baada ya kuua unapata faida gani?
 
Uwe unaelewa wewe mpumbavu , huyo bodaboda anekuta njia imezibwa akauliza kwanini ameziba njia ?
Huyo askari zuzu akaanza kumpiga makofi ,ni nani alikuwa na makosa hapo ?
Muwe mnatumia akili ninyi kondoo
Unauhakika jamaa kaziba tu njia dereva kaja kuuliza tu akapigwa kibao hivyo tu ndo ilivyokua? Anayeongelewa hapo ni keno sio Cpl wa mizinga
 
Maafisa wa jeshi ni watu very smart,na wastaarabu nashangaa huyu kanali ni wa jeshi gani,Jeshini watu wanaokurupuka ni kina fulani siwataji
Angalizo:
CO Lugalo,MP commander,lolote litalompata huyu kijana mjiandae kujibu,tunataka kijana afikishwe kwenye vyombo vya sheria na sheria ifate mkondo wake,na pia kazi ya kumkamata ni ya polisi siyo ya kwenu.


Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Unaandika hivi wewe kama nani unajiexpose kifala mno.Akifa huyo jamaa ijapokuwa ni mtuhumiwa,unajua kwamba jeshi(taasisi) inaweza kuwajibishwa mbele ya mahakama? Uzuri kikosi husika kinafahamika.Acheni kujipa kazi ya mahakama ya kutoa adhabu.

Eimu zenu ndogo mno na hata sheria ndogo ndogo hamzijui,mtaweza kuijua Katiba ya nchi na tuikeleza kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…