Kenya: Ilikuaje hadi mtu mmoja anaua watu 42 bila polisi kujua?? Je muuaji ni mwerevu kuliko vyombo vya usalama?

Kenya: Ilikuaje hadi mtu mmoja anaua watu 42 bila polisi kujua?? Je muuaji ni mwerevu kuliko vyombo vya usalama?

Watupumzishe Jamani. Kwa hiyo muuaji alikuwa anangojea watu waandamane ndiyo aanze kuua?.

Polisi wametafuta mtu wa kumtupia mzigo, wao ndiyo wanahusika.
Vyombo vya habari vinadai alilazimishwa kukiri.
Na wakili wake anasisitiza serikali iseme ukweli
 
Sio maigizo ni true,lakini chanzo cha kujulikana ni huyo mwenye hiyo Youtube Channel Senior Dave ndie aliyevumbua baada ya kuwakuta jamaa na demu wake na kuwafanyia challenge Loyalty Test,kisha akawashirikisha Polisi ndio ukamataji wa watuhumiwa wengine ukaendelea
Kwaiyo anakua na kibali cha kuwahoji na kuwapiga piga hivo
 
Kwahiyo kuna mtu kabisa anakaa akiamini bwana huyu kaua watu 42 alafu akawa anawatupia karibu na kituo cha polisi kwa muda wote huo? Mwili mmoja, wa pili, wa tatu mpaka kumi zilizo nne, kisha mbili kama nyongeza, sio baharini, ah-ah, karibu na kituo cha polisi.

Tuwe serious.
 
Kuna jambo limejificha hapo, miili kukutwa karibu na kituo cha polisi, kwanini iwe sasa, je omondi nae aliuwawa na huyu? Miili ya wanawake mna uhakika ni wanawake au walivalishwa nguo za kike kupoteza maboya, kwanini iwe ni baada ya maandamano? Yani mtu mmoja aue watu wote hao awatupe karibu na kituo cha polisi bila kushtukiwa!!! Haiwezekani km inawezekana basi ni uzembe wa serikali, na pengine bila kelele za wananchi na hali tete ya maandamano kutishia serikali huenda mauaji hayo yangeendelea,, Ruto atoke tu kashachemka
 
Serial killers are everywhere. And are very smart up stairs, eg is British Dr Harold Frederick Shipman. He killed 250 mostly wealthy old women.
Alikua anawaua kisa nn

maana sehemu kubwa serial killer wanaua kutokana na trauma,sexual affairs ndo maana nyingi unakuta zinahusiana na sex
 
Mjinga kabisa wewe
Heeeh ameongea maoni yake naweza kumuunga mkono 40%
Kulikua na kesi nyingine ya watu 400 kufa inahusiana na imani za dini wengi wao walikuta hawana viongo vya mwilini.


Imagine had watu wanafika 400 ndo usalama wajue
Does it make any sense
 
Kuna jambo limejificha hapo, miili kukutwa karibu na kituo cha polisi, kwanini iwe sasa, je omondi nae aliuwawa na huyu? Miili ya wanawake mna uhakika ni wanawake au walivalishwa nguo za kike kupoteza maboya, kwanini iwe ni baada ya maandamano? Yani mtu mmoja aue watu wote hao awatupe karibu na kituo cha polisi bila kushtukiwa!!! Haiwezekani km inawezekana basi ni uzembe wa serikali, na pengine bila kelele za wananchi na hali tete ya maandamano kutishia serikali huenda mauaji hayo yangeendelea,, Ruto atoke tu kashachemka
Kati hayo maswali
Swali jingine kwann ni wote wanawake??
Wengine wanasema ni biashara ya ovaries na kidney
 
Kwahiyo kuna mtu kabisa anakaa akiamini bwana huyu kaua watu 42 alafu akawa anawatupia karibu na kituo cha polisi kwa muda wote huo? Mwili mmoja, wa pili, wa tatu mpaka kumi zilizo nne, kisha mbili kama nyongeza, sio baharini, ah-ah, karibu na kituo cha polisi.

Tuwe serious.
Inafikirisha
 
Back
Top Bottom