Mkuu mazingira ya Kenya yaliletwa na Wakenya walio upande wa Raila, kwani Uhuru aliogopa shari toka kwa wafuasi wake. Kinachofanyika sasa ni makubaliano yasiyo wazi ya mama Samia na viongozi kadhaa wa cdm. Na sio makubaliano ya ccm na cdm. Ifahamike ccm bara ndio wenye nguvu, huyo mama hana ushawishi bali analindwa na cheo cha urais alichokipata kwa bahati mbaya. Hivyo anachofanya ni kuwahadaa wapinzani ili atawale bila kelele, kisha makubaliano hayo yatumike kama udhaifu wa cdm. Rejea ule utapeli wa Magufuli muda mfupi kabla ya uchaguzi mkuu, kati yake na Mbatia na Lipumba na alichokifanya kwenye uchaguzi.
Naona wazi cdm wakiingizwa mkenge kwa mtazamo wa Mbowe kutokana na alichoongea na mama Samia, lakini hapo kuna mazingira ya Mbowe kufaidika binafsi, na kidogo sana cdm kama taasisi. Bado nina kumbukumbu mbaya ya ujio wa Lowassa ndani ya cdm, na alichokuwa anaoongea Mbowe kwenye utetezi wake wa kumpokea Lowassa. Matokeo ya kumpokea Lowassa ni kuharibu haiba ya cdm,na kibaya zaidi aliishia kupandikiza siasa za kikondoo. Leo hii Lowassa hayupo karudi ccm, na cdm imebaki na siasa za uwoga. Mnao amini siasa za maridhiano ya maneno matupu sitaki kuwazuia, lakini ukweli ccm hawawezi kukubali maridhiano ya mezani bila mivutano. Muda utasema kwenye hii shaka yangu.