Unaamua kuchutama? Acha kuabudu shetani. Njoo kwa Yesu umwabudu Mungu Muumba wa Mbingu na nchi, alieymfufua Yesu Kristo Katika wafu. Yesu ndiye Njia kwlei na uzima. Mtu haendi kwa Mungu isipokuwa kwa njia ya Yesu.Mbumbumbu mzungu wa reli 😁😁😁
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unaamua kuchutama? Acha kuabudu shetani. Njoo kwa Yesu umwabudu Mungu Muumba wa Mbingu na nchi, alieymfufua Yesu Kristo Katika wafu. Yesu ndiye Njia kwlei na uzima. Mtu haendi kwa Mungu isipokuwa kwa njia ya Yesu.Mbumbumbu mzungu wa reli 😁😁😁
Unaamua kuchutama? Acha kuabudu shetani. Njoo kwa Yesu umwabudu Mungu Muumba wa Mbingu na nchi, alieymfufua Yesu Kristo Katika wafu. Yesu ndiye Njia kwlei na uzima. Mtu haendi kwa Mungu isipokuwa kwa njia ya Yesu.
Baada ya kumuumba msaidizi sindio alirubuniwa na shetani😅 akawa wakala wa shetani!Kabisa. Lkn vp mpango wa Mungu kumuumbia mwanamume msaidizi toka ubavuni ilikuwa ni njama ya sheitwan? Ima mana Mungu hakuliona hilo gap?
Eeh shetani humuingilia mwanamke akilini ili kuharibu nyumba yako. Usiposimama imara kupambana nae umeishaShetani ni kweli anapitia kwa mwanamke mm alibadilishwa mke akaniambia maneno na yalifanya kazi maneno hayo kama yalivokusudiwa nilichogundua kumbe ilikua sio maneno yake ilikua ni nguvu ya shetani baada ya kunifika mpaka mke tuliachana
KIFOMULA; ROHO YA MUNGU HUMSHUKIA MWANAUME WAKATI ROHO ZA KISHETANI HUMSHUKIA MWANAMKE.
Anaandika Robert Heriel.
Hatuandiki kumkashifu yeyote Ila tunaandika kufundisha na kuleta Uelewa wa mambo katika ulimwengu wa kiroho na elimu ya kimwili.
Katika Dunia hii zipo pande mbili zinazolingana. Juu na chini. Kushoto na kulia, Giza na Nuru, wema na ubaya, mwanaume na Mwanamke, Mtawala na mtawaliwa. Mungu na Shetani.
Pande hizo zinazokinzana zote zina kanuni zake na ni nadra Sana kutumia kanuni za upande mwingine.
Ni ngumu Sana Mungu kuongea moja Kwa moja na Mwanamke. Kama ilivyokuwa ngumu Kwa Shetani kuongea moja Kwa moja na Mwanaume.
Kama ingekuwa ni Kemia. Ni kwamba hakuna chemical Reaction baina ya Mungu na Mwanamke halikadhalika Shetani na Mwanaume.
Mungu au roho za Mungu huona kazi kubwa kumtumia Mwanamke katika shughuli za hapa na pale za kiutendaji. Kama ilivyo kaa Shetani au roho za kishetani huona kazi kubwa kumtumia mwanaume na hapa nazungumzia mwanaume kamili na halisi mwenye roho na tabia za kiume.
Shetani afikapo mahali popote pale hufikia Kwa mwanamke. Hata akiingia kwenye familia yoyote Ile basi hufikia Kwa mwanamke Kwanza ili atende kazi zake.
Mungu afikapo mahali popote hufikia Kwa mwanaume. Humuita mwanaume na ndio hufanya kazi zake.
Kimsingi, ili shughuli za Mungu zifanikiwe Kwa upesi basi mfumo utakaopaswa kutumiwa ni mfumo Dume kwani Mungu ndio mfumo wake.
Na ili shughuli za kishetani zifanikiwe Kwa upesi Sana basi yapaswa mwanamke atumike na mfumo jike utumike haraka.
Hii ni kusema, endapo dunia itafuata mifumo jike ni kwamba ufalme wa Mungu umeanguka na Shetani atakuwa yupo incharge.
Ndio maana kimsingi, ni kosa la jinai na kubwa Kuruhusu Mwanamke aongoze ibada za kiungu hasa Mungu Mkuu. Mwanamke kuongoza Ibada za kiroho kitafsiri ni kuwa ni agenda za kishetani zitapenyezwa na ushetani utakuwa dhahiri.
Au haya mwanaume akiongoza lakini akatumia mifumo ya Mfumo jike na kusikiliza sauti za kike ni kwamba Shetani ata-operate na mambo yataanza kwenda mrama.
Kifamilia, haipaswi Mwanamke awe kiongozi wa Familia. Mwanaume ndiye anayepaswa kuongoza familia.
Mwanamke kuongoza Familia ni laana. Na ni tafsiri kuwa familia hiyo ni base muhimu ya kishetani.
Sisemi Kama mtu nisiyefikiria umuhimu wa Wanawake, Hasha! Ila nazungumzia roles za msingi katika kanuni za ukinzani wa uwili.
Najaribu Kueleza Jambo hili ili wenye akili na maarifa wajue nini chakufanya.
Mwanaume kamili na halisi, mwenye roho ya Mungu, anayetumia mifumo ya Mungu Mkuu kamwe hawezi ongozwa ibada na Mwanamke kwani Kwa kufanya hivyo ni kukubali kuongozwa na Shetani na kutawaliwa na shetani hata Kama Mwanzoni ataona mambo ni mazuri lakini mwishoni lazima ubaya ujitokeze.
Wakati mwingine unaweza ukashangaa kuona Wanaume wazima wamesimamisha suruali zao wakiongozwa ibada na Mwanamke. Kwa kweli inahuzunisha
Ni Dalili ya kukosa akili na kutojitambua.
Mwanamke anaweza kuongoza wanawake wenzake, au kuongoza watoto wenye umri chini ya miaka 15 au ambao bado hawajaona manii/Shahawa zao.
Lakini mwanaume yeyote aliyeona Shahawa zake, mwenye uwezo wa kuzalisha hapaswi kuongozwa na Mwanamke katika mambo ya kiroho.
Mimi Taikon sisemi haya kuwaumiza au kuwadharau wanawake Ila naongea Jambo la kweli linaloigharimu Dunia.
Mungu hufikia Kwa wanaume na hutenda Kwa mfumo Dume. Shetani hufikia Kwa Wanawake na hutumia mfumo jike.
Sishangai dunia ya sasa ikikazania haki Sawa na kuondoa mfumo dume. Sababu ni kuwa Shetani haupendi mfumo dume Kwa sababu haumsapoti na unamchelewesha.
Nanipumzike sasa.
Ni Yule Mtibeli kutoka Nyota ya Tibeli.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Maandiko yanasema, Wakati ulipofika kwa Mungu kuukomboa ulimwengu, alimtuma Malaika aende kwa Mariam na kumwambia atazaa mtoto kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na mtoto atamuita Yesu na ndio ataokoa ulimwengu. Swali, kwanini kwa jambo kubwa kama hilo ambalo Mungu amelitenda hapa duniani akwenda kwa Joseph mume wa Mariam kwanza na kuamua kuanzia kwa Mwanamke (Mariam) kiasi ambacho madhehebu mengine yamempa hadi ‘uungu’ huyu mama? Tuanzie hapo.
Wewe ni kichaa msomi. Na mpo wengi Tanzania, tushawazoea.
Meneja Robert 2021/2022 utatufikisha kanani tumechoka ila SALAMA
Unapambana nae vipi shetani mkuu na pengine amejianda tangu ukiwa mdogo hujui au ndoa kaimiliki tangu awali hujui na roho zetu naamini ipo sehemu ya shetani au katika nafsi zetu.Eeh shetani humuingilia mwanamke akilini ili kuharibu nyumba yako. Usiposimama imara kupambana nae umeisha
Dah noma kweli sema shetani humuingilia mke kupitia jini mahaba! Ndoa nyingi zimevunjika kwa style hioUnapambana nae vipi shetani mkuu na pengine amejianda tangu ukiwa mdogo hujui au ndoa kaimiliki tangu awali hujui na roho zetu naamini ipo sehemu ya shetani au katika nafsi zetu.
Mimi binafsi nikiwa mdogo nilikwenda sehemu mabondeni nikaanguka mti nilirudi nyumbani wazee wakapandisha shetani kama nilipata tatizo lakin palepale dakika 10 kila kitu kikaa sawa na kila mtu akaendelea na shuhuli yake na maisha yakaendelea yakaendelea sikuwahi kujua chochote kuhusu shetani mpaka tumeishi na mke miaka 16 nimeshangaa mke hafla anasikia sauti anaongozwa na shetani jinsi ya maisha yetu yanavokwenda nikamuhisi mke anaanza kugeuka kabisa kama sasa yeye ndio anitawale mimi na kujiongoza nifanye nini au vip mkuu haikuchukua muda ndoa ikaachika kwa ugomvi mkubwa na mimi nilimkatalia kabisa kusikiliza sauti za ndani za kishetani.
MilionsDah noma kweli sema shetani humuingilia mke kupitia jini mahaba! Ndoa nyingi zimevunjika kwa style hio
Mtoa mada ametimiza tu wajibu wake akiwa kama Mwanafasihi nguli! Hivyo siyo sahihi sana kukimbilia kwenye kichaka cha kutaka kulazimishwa kuheshimiwa kwa sababu tu ya uanawake wenu!Ndugu, jitahidi kuwa na hekima na busara walau kwa muda mfupi!! Nakuona umejaa kejeli, husuda, ubinafsi, majivuno,ujuaji ,chuki, sifa ,dharau n.k kuhusu wanawake, kwa kifupi umeathiriwa na mfumo dume!!! Huu ni ujinga na unaweza kuondolewa kwa kuelimishwa.
Huwezi kuwadhalilisha mama zetu,dada zetu ,bibi zetu na shangazi zetu halafu tukuache tu eti kisa ni 'mwanafasihi nguli' (kwa unavyojiita na kujipachika )??? Au wewe mwenzetu umezaliwa na mwanaume?? Hivyo vitabu vyote ukivichunguza kwa kutumia fikra tunduizi na kwa umakini wa hali ya juu ,utakuja kugundua vyote vimejaa mfumo dume.
Angalia jamii za Mashariki ya Kati (Wayahudi ,Waarabu,Waajemi n.k) zilikuwa zinamchukuliaje kiumbe anayeitwa mwanamke katika mila na tamaduni zao kwa nyakati hizo, ukitoka hapo nenda Ulaya,Asia,Afrika n.k.
Swali: Unaweza kuzitenganisha vipi mila ,tamaduni pamoja na dini??? Usijibu kwa kutumia mhemko,tumia fikra tunduizi!!!
Ujumbe: Mpe heshima yake mwanamke (mama yako) ambaye Amekubeba kwenye tumbo lake au wewe mwenzetu hukubebwa kwenye tumbo??