Kijana kamkimbia mchumba wake alietaka kumuoa baada ya kujua kwao kuna walemavu ni sawa?

Kijana kamkimbia mchumba wake alietaka kumuoa baada ya kujua kwao kuna walemavu ni sawa?

Mimi kuna ukoo naujua uliachiwa laana huko enzi za mababu zao miaka 1910,babu huyo alimdhulumu mjane ....babu alizaa watoto wakiume watatu na wao wakaja kuoa,ila kila tumbo wakiume mmoja chanel kichwani zilipotea wakiwa wamemaliza udsm na wanafanya kazi kabisa,laana zipo
Ndugu yangu hiyo laana ya mwaka 1910 uliiona wakati inatolewa [emoji3][emoji3]

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Kuna jamaa aliwahi kuwa na mahusiano na mdada mpaka wakawa wanaishi kama mume na mke bila ndoa. Bahati nzuri binti alikuwa anajulikana hadi kwa ndugu wa jamaa. Binti akapata ujauzito akajifungua mtoto albino. Jamaa alishindwa kuruka kwani mtoto sura ilikuwa ni yake kabisa. Ila ilibidi abreak up na yule dada kwa kudai kuwa kwao hawana mtu wa aina hiyo.
Basi kuna siku akamtembelea babu yake mzaa baba kijijini kwa sababu babu yake alikuwa anajua kuwa jamaa ana mke akamuuliza habari za mkewe. Jamaa akamwabia babu yake kuwa ameachana na mkewe kwa sababu amebaini kuwa amemletea kiumbe kisicho cha kawaida kwenye ukoo wao. Babu akauliza ni nini hicho? Jamaa akafungua kuwa binti amemzalia albino jambo ambalo kwenye ukoo wa halijawahi kutokea.
Babu yake kusikia hivyo alisikitika sana, akamwambia huyo mtoto uliyemkataa ni babu yangu. Babu akamweleza kuwa babu yake mzee baba alikuwa albino. Na alieleza kuwa katika familia ya babu yake walikuwa watoto watano watoto wawili akiwemo babu wa babu yake walikuwa albino.
Aliendelea kueleza kuwa babu yake huyo alioa na kuzaa watoto sita akiwemo baba wa babu yake na watoto wote walikuwa kawaida.
Babu alimwambia hiyo ni asili yao kabisa.
 
Kuna jamaa aliwahi kuwa na mahusiano na mdada mpaka wakawa wanaishi kama mume na mke bila ndoa. Bahati nzuri binti alikuwa anajulikana hadi kwa ndugu wa jamaa. Binti akapata ujauzito akajifungua mtoto albino. Jamaa alishindwa kuruka kwani mtoto sura ilikuwa ni yake kabisa. Ila ilibidi abreak up na yule dada kwa kudai kuwa kwao hawana mtu wa aina hiyo.
Basi kuna siku akamtembelea babu yake mzaa baba kijijini kwa sababu babu yake alikuwa anajua kuwa jamaa ana mke akamuuliza habari za mkewe. Jamaa akamwabia babu yake kuwa ameachana na mkewe kwa sababu amebaini kuwa amemletea kiumbe kisicho cha kawaida kwenye ukoo wao. Babu akauliza ni nini hicho? Jamaa akafungua kuwa binti amemzalia albino jambo ambalo kwenye ukoo wa halijawahi kutokea.
Babu yake kusikia hivyo alisikitika sana, akamwambia huyo mtoto uliyemkataa ni babu yangu. Babu akamweleza kuwa babu yake mzee baba alikuwa albino. Na alieleza kuwa katika familia ya babu yake walikuwa watoto watano watoto wawili akiwemo babu wa babu yake walikuwa albino.
Aliendelea kueleza kuwa babu yake huyo alioa na kuzaa watoto sita akiwemo baba wa babu yake na watoto wote walikuwa kawaida.
Babu alimwambia hiyo ni asili yao kabisa.
Basi sawa ikawaje sasa ndugu yangu nafuatilia kwa ukaribu kabisa

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Yeye akipata ulemavu hapo ukubwani alipo atalelewa na nani?
Suala la kupata ulemavu lipo muda wowote, Lakini kujua sehemu fulani kuna ulemavu na wewe unakwenda kujitafutia matatizo yasiyo ya lazima ni ukosefu wa akili.

Kulelewa atalelewa na yeyote tu.
 
Kabisa kama mtu hana elimu lazima aseme uchawi umehusika kumbe ni science tu.

Haya mambo yangefikaga huku kwetu ingekuwa nafuu sana japo ki Africa Africa umwambie mtu mtoto anaonekana ana shida hii na hii na option iliyopo ni abortion hawezi kukuelewa.

Sembuse tu mtu anaambiwa mimba imetunga nje ya kizazi inatakiwa itolewe kwa usalama wa mama na bado anagoma.
Kwanza Afrika umtembelee mama mjamzito halafu uanze story za kumwambia mzazi kwamba mtoto ana atakuwa na shida fulani.

Watakwambia wewe ndio mchawi mwenyewe...😂
 
Angetoka kimya kimya tuu bila kuongelea ulemavu, kuna karma dunia hii na umeumbwa hujaumbika, yeyote anaweza kuwa mlemavu any minute
 
Mbona huu mjadala ni very sentive...kupitia hapa watu watajifunza ni magonjwa yapi yanarithiwa kabla hawajajiingiza wazima wazima..
Huyo nae kavurugwa..
watu kama hawa lazima wawepo ili jukwaa lisikae kizembe
 
Tushatembelea na bado tunaendelea kutembelea boss maana kuna clinic ya kila mwezi pale MUHIMBILI na CCBRT (dawa)
Dogo shida alizaliwa akapata homa ya manjano ikapelekea akalazwa miezi kadhaa pale temeke
Baada ya kutoka akawa yupo sawa ila sasa shida ikaanza wakati wa miezi ya kukaa kitako ndio ikajulikana kama dogo anashida
Na hospital wamesema kwamba ana utindio wa ubongo na kwamba tatizo haliponi kwa uwezo wao kama madokta hawana dawa labda tu apone kwa uwezo wa Mungu
"tatizo haliponi kwa uwezo wao"

Naelewa uchungu unaoupata kwa kauli hiyo hasa inapotoka kwa madaktari, maana binafsi ni mlemavu wa viungo

Na kwa mujibu wa madaktari sikupaswa kuishi hadi leo hii. Walinitabiria kwamba sintofika 2005

Lakini baada ya kuingia kwenye utu uzima na kulijua neno la Mungu na kulikiri hasa ule mstari usemao "lisilowezekana kwa binadamu kwa Mungu linawezekana"

Mstari ulinitia nguvu sana huo nikawa nakiri uzima kwamba"sintakufa bali nitaishi nami nitayasimulia matendo makuu ya Mungu "



Pole na usife moyo iko siku Mungu atakurejeshea furaha yako juu ya mwanao
 
Binafsi mimi naona kijana kakosea, hakuwa sahihi, mkasa huu hapa nawapeni.

Kuna kijana mdogo wa kiume miaka 26 tupo nae kazini alikuwa kwenye uchumba na binti wa miaka 22, wote ni wasomi binti kamaliza degree mwaka jana.

Kijana alikuwa tayari kabisa mwezu huu kwenda kujitambulisha nyumbani kwa binti ili amuoe.

Wiki 3 ziliyopita kijana alipata safari ya kikazi kwenye mkoa anakotokea huyo binti, alikaa huko kama wiki hivi

Huko alipofika na kuamua kuchagua malazi ni mitaa karibu na nyumbani kwa huyo binti, katika kujichanganya na wakazi wa hapo akitoka kazini aliulizia kama wanamfaham mzee wa binti akaongezea na maelezo ya ziada, wakamwambia ni mtaa huo huo tu na wanaijua familia ya hapo.

Kijana ikabidi aanza kukamua intelejensia, akagundua kuwa pale nyumbani kwa binti kuna wanafamilia wawili wana matatizo ya kutosikia vuzuri na kuna mwengine huwa yupo ndani tu ana matatizo ya akili tangu mdogo.

kuna wawili wengine hawana shida wamesoma na wana kazi na biashara zao.

Hapa sasa nitaongea zaidi kama yeye mwenyewe alivyojitetea, ndipo penye kuamua kazingua au lah, twendeni pamoja.

Kijana ni kama alipata mstuko akataka kumuacha binti kienyeji ila alishindwa, ikabidi amuweke wazi kwamba anampenda lakini anachukua tahadhari hawezi kurisk kumuoa sababu ndoa bila watoto ni ngumu na anahofia alichokigundua kwenye familia anayotokea huyo binti, alimwambia kwamba mtu yeyote anaweza kupata ulemavu muda wowote maana hujafa hujaumbika, pia mtu yoyote anaweza kupata mtoto mlemavu maana hakuna anaemuumba mtoto atakavyo lakini yeye anahofia kwamba uwezekano wa kupata mtoto mlemavu utaongezeka zaidi endapo wao wakipata mtoto kwa kuhofia kwamba ulemavu wa wanafamilia ni magonjwa ya kurithi, hivyo hata kama binti ni mzima yawezekana karithishwa genes / genetics zinazoweza kuleta mtoto mwenye ulemavu, sababu ya zaida ambayo hakumwambia binti ni kwamba anahofia kuna mambo ya kiafrika kwenye mila au matambiko yaliyowahi kudanyika huko zamani yanarithishwa,

Alimwambia binti wanaweza kuwa na mahusiano mengine ila si kwenye kupata watoto, Binti hakumwelewa kabisa ikawa ndio mwisho hapo.

Je, ni sawa?
Huu uzi tuwapelekee wahindi na waarabu wao watakua na majibu mazuri
 
Basi sawa ikawaje sasa ndugu yangu nafuatilia kwa ukaribu kabisa

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Jamaa ilibidi amrudie yule dada waliyezaa naye, wafunga ndoa maisha yakaendelea. Walifanikiwa kupata watoto watatu mmojawapo ndiyo huyo albino mwingine alikuwa na character za kialbino kwenye macho na ngozi kwa mbali lakini hakuwa albino. Mtoto wa tatu alikuwa kawaida kabisa.
 
Kumuacha ni sawa kabisa, probably style ya kumuacha mtu wa namna hiyo ndio inatakiwa iwe strategic.

Hata zamani wazee hawakuoa familia zenye magonjwa ya kurithi kama kifafa, familia zenye mikosi(mlango wa saba), familia ambazo wanawake hawakudumu kwenye ndoa. Walifanya sana hivyo, sio ajabu wala.
 
Mkuu ww unaonekana unaelewa sana haya mambo ya magonjwa ya kurithi..Nami naomba niulize hapa. Hivi ukoma(leprosy) nao pia huwa ni ugonjwa wa kurithi, genetically?
Isivyo bahati siufahamu kivile huo ugonjwa ila nachofahamu sio wa kurithi, kama kuna mengineyo wataalamu watakuja kujazia nyama
 
Ni kweli kabisa....Hujafa hujaumbika...

Mimi jana tu..kuna sehemu nilikuwa natoka...hakuna usafiri wowote unapita..hata boda hakuna...

Ikatokea Bajaji nikaisimamisha...kupanda Kuna mdada mzuri tu amekaa katikati na Mmama..ni mtu na Mama yake.

Kumbe yule Dada amepata Ugonjwa wa Akili...Mama yake ametoka kumchukua Zanzibar huko..Na Bajaj walikuwa wamekodi... walinibeba tu ili kunisaidia...

Yule Dada alikuwa anapiga kelele Bajaj nzima,mara anilalie, apige makofi, aimbe, anafika mahali anataka kama kuruka...Nikataka kumwambia Dereva anishushe tu...

Ghafla nikaingia Imani nikajiuliza angekuwa ndugu yangu ningevumila..Acha na hapa nivumilie..Ikabidi niwe namsaidia Mama yake kumshika akitaka kuruka..

Hii Dunia inatupasa kukaa kwa utulivu na adabu kubwa sana....Unaweza kujiona mkamilifu sababu halijakupata..ila likikupata ndiyo utajua kupatana nalo.
Ubarikiwe dada. [emoji120][emoji120]
 
Ukiachana tu changamoto za kumlea, naamini kama mzazi kila ukimtazama unajisikia uchungu sana kwakuona kwamba anateseka bila makosa.

Mwaka jana mwanangu wa kiume wa 3 kuzaliwa, 5 years alipata changamoto ya mifupa ,serious bactrial infection kwenye mfupa mkubwa wa mguu karibu na goti. Ilikua ni ishu sana.. alikua halali usiku hospital kutwa kicha kakunja mguu analia sanaa .

Daktar alinambia kitaalam hapo maumiv anayoyasikia ni kama upigwe panga kwenye mguu.. aisee acha tu, mbaya zaid wakasema kuna uwezekana ikatokea eneo la maungio ya mifupa gotini ikaathirika na mguu ukashindwa kukua hivyo kubaki na mguu mfupi mmoja na kuwa mlemavu...

Aisee...usiku akilala mwanangu nilikua nikimtazama machozi yananitoka nalia peke yangu. 🥲🥲.
NIkawa namwambia Mungu naomba kama inawezekana hii hali ihamishie kwangu, mwanangu bado mdogo sana kwa haya maumivu.

It took us 4 months with alot of money mpaka dogo kuja kukaa sawaa.
Alikua anapigwa doz nzito za antibiotics kias kwamba leo hii hiv vi antibiotics vya kawaida akinywa anapoumwa kawaida tu, huwa ni kama havifanyi kazi.

Daktar alinambia it will take time mwil kurud sawa toka usugu wa madawa..


Kuwa mzazi ni kaz sana Mungu atusaidie wazaz na walez wotee.
Intelligent businessman we endelea tu kupiga selfie dogo [emoji23] haya mambo sidhan kama utayaweza

Jitahidi jumpa juice zinazodetoxify

Na poleni sana kwa kuuguza
 
Back
Top Bottom