Kikwete ni mmoja ya Marais ambao miaka Ijayo watoto wetu watatushangaa sana kuwa ilikuaje....

sasa hivi tunaotaka katiba mpya tunachambwa,kusutwa na kutukanwa,yeye kama mzee wa nchi kakausha tu. unaweza kudhani Hii nchi haina wazee
Hiyo inakuonyesha kwamba kiongozi wa namna hiyo hakuwa na uchungu na maslahi ya nchi hii. Hata huo mchakato alioruhusu ufanyike haukuwa moyoni mwake kabisa; kwamba anatafuta njia ya kuinufaisha Tanzania.

Linganisha hali hiyo na ile ya Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, hata baada ya kung'atuka.

Hawa wenzetu, uongozi ni kutafuta sifa na kujinufaisha, ndivyo vipaumbele vyao; ndio msukumo wa kusaka uongozi.
 
Hao watoto watakuwa wajinga sana.
Kama watashindwa kuilaumu ccm na hizo lawama wakamtwisha JM Kikwete basi dunia itawashangaa.
Urais hutokana na mfumo. Huwezi kumpata Rais makini kwenye mfumo chakavu!
 
Acha kujivunia umasikini, sema pesa za Watanzania . Unakuwa kama Jiwe.
 
Kikwete ni adui wa wananchi wanaojitambua!!!

Na huyu ndiye mentor wa Rais aliye madarakani hivyo atajitahidi kurudia ufisadi alioufanya wakati wa utawala wake vis a vis Katiba Mpya!!!
Mimi namlaumu kikwete kwa kumleta Jiwe
 
Kikwete ni adui wa wananchi wanaojitambua!!!

Na huyu ndiye mentor wa Rais aliye madarakani hivyo atajitahidi kurudia ufisadi alioufanya wakati wa utawala wake vis a vis Katiba Mpya!!!
Hauna lolote, Kikwete aliwaonya ukawa kwa kuchezea nafasi ya mchakato aliyoitoa. Wao walikuwa biz na vipengele visivyo na uharaka kwa wakati ule. Nadhani shida yao ilikuwa posho, ndiyo sababu wali complicate mambo sana.
 
Hongera mleta Mada ur clever!
Huenda topic hii ika mwamsha Mzee JK, atoe ushauri Sahihi! Kwa maslahi ya Taifa letu, waugwana wote hawapendi Katiba yetu isiyo na meno mdhibiti kiongozi na fairness kwa Zanzibar.
Kwani kiswahili hakitoshi mpaka utumie lugha usiyoijua???
 
Uko sahihi lakini mambo ya kuitana masikini sijui wanyonge siyo poa. Umasikini ni laana, pinga kwa nguvu zako zote hilo jambo na wala usijivunie kuitwa masikini au mnyonge.
 
Kikwete ni adui wa wananchi wanaojitambua!!!

Na huyu ndiye mentor wa Rais aliye madarakani hivyo atajitahidi kurudia ufisadi alioufanya wakati wa utawala wake vis a vis Katiba Mpya!!!
Najua mnasubiri afe ili mje na mapambio kibao ya kumsifu, hakuna rais alietupa maisha yenye unafuu kama Kikwete, Ebu angalia mfumuko wa bei uliopo saizi tangu enzi za mwenda zake mpk hapa kwa Mama Samia, Enzi za JK ata mawaka walikula bata na kamisheni za kufa mtu lkn kaja yule Jamaa wa Chato kavuluga kila kitu lkn bado mnampa mzee wa watu lawama kila siku. Khs mchakato wa katiba mzee hana kosa maana aliefuata mbele yake ndie alietakiwa kuendeleza ule mchakato lkn baada ya kuingia madarakani akaona nchi tamu akauweka mchakato prmbeni sasa hapo mlitaja JK afanyeje?

Ebu watanzania tuache lawama zisizo ba kichwa wala miguu ili tuweze kuijenga chi yetu kwa umoja na mshikamano.
 
Hauna lolote, Kikwete aliwaonya ukawa kwa kuchezea nafasi ya mchakato aliyoitoa. Wao walikuwa biz na vipengele visivyo na uharaka kwa wakati ule. Nadhani shida yao ilikuwa posho, ndiyo sababu wali complicate mambo sana.
Kikwete ilibidi ahujumu ule mchakato kwani kama ile katiba ingefanikiwa asingepona kuwajibika kwa ufisadi aliofanya kuanzia kuuza wanyama pori mpaka ushirika wake na HOME SHOPPING CENTRE Kuingiza makontena bila kulipa Ushuru na wao kunufaika pamoja!! Ndio maana kupoteza ushahidi HOME SHOPPING CENTRE ikabid kubadili jina kuwa GSM kabla ya Kikwete kuondoka madarakani!!
Hiyo ndiyo sababu kubwa ya yeye kuhujumu Katiba Mpya , na isingekuwa hivyo yaliyompata Rafiki yake ZUMA kule South Africa na akina Gupta , yangempata yeye na wakina HOME SHOPPING CENTRE kwasababu kile walichofanya Ilikuwa STATE CAPTURE!!
 
Hapo ndipo uwezo wako wa kufikiri ulipoishia.
 
Tunapojadili mada kama hizi tusaidie Taifa basi. Mzee Kikwete kazi yake iliishia nje ya Bunge la Katiba. Hakuwa mbunge, Mwenyekiti wala Makamu wa Bunge la Katiba. Alitimiza wajibu wake wa kimamlaka kwa mipaka. Tuwaulize wabunge wakiwemo wa UKAWA! πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™
 
Kikwete tena!!!!

Basi na wewe mtoa mada watoto wako na wajukuu watakushangaa zaidi kwamba ulikuwa bwege kiasi gani haukuweza hata kuwa waziri au mbunge au mfanyabiashara mkubwa katika maisha yako yote na badala yake uliishia Tu kuwa mfuatiliaji WA Wanaume wenzio, mzushi, mwenye wivu a.k.a husda na maskini uliyekosa hekma kiasi kwamba ukoo wote umeambukizwa hiyo tabia na umebaki hauna mbele wala nyuma.
 
Wabongo vichwa panzi sana aisee, JK anaingiaje kwenye mchakato wa Katiba wakati mlianza kubishana bungeni mle mpaka wengine kumtukana JK Nyerere... JK aliwaachia mchakato mezani mkaanza ubishi usio na maana.

Akaja Mchato JPM akawaambia hataki kusikia upuuzi na ukileta fyoko anakuletea fyoko na wote mkaufyata tena...sasa mmeanza tena ubishi wenu..

Tatizo moja la wanasiasa wa Tanzania hasa upinzani wanafikiri wanachowaza wao ndio watanzania wote wanawaza..... ile katiba ilikuwa ngumu kuptikana maana tayari watu walitaka kulazimisha kila agenda yao ikubalike....
 
Chuki dhidi ua kikwete itakuua

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Ni Rais mbovu kabisa kuwahi kutokea Tanzania tokea tupate Uhuru. Cha kusikitisha kuna Mazuzu wengi Wanamkumbali na walikuwa Wakimpenda huyu Mswahili ambaye wana CCM walimpitisha mwaka 2005.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…