Kila siku wako Misikitini na Makanisani wakihubiri siasa lakini wa kwanza kusema tusichanganye dini na siasa

Wakuu Mimi n maamuma TU katika sheria lakn nashangaa Sana katiba yetu inasema kila mtanzania Ana haki ya kutoa maoni kwa Jambo lolote lihusulo nchi yetu

Wiki hii kanisa katoliki limetoa maoni kupitia baraza la MAASKOFU yaani TEC na wameorodhesha vifungu Tata vya mkataba ambavyo wao wanaona Kama vinafaa kurekebishwa maajabu anatokea mtu anasema Ni udini TU unaowasumbua hawa MAASKOFU

Mm nilitegemea watajibu kadiri ya maswali yaliyoulizwa juu ya vipengele Tata lakn mtu anakimbilia kusema udini

USHAURI wangu n vema wakajibu hoja iliyopo mezani kuliko kujikita kwenye udini
 
Huyu ni shehe au sio shehe.

 
Yaani ni ajabu sana kwa kweli jk kakosea sana
 
Huyo Sheikh kwa uhakika wake. Masheikh lazima wafate mafundisho sahihi ya Mtume.
 
Walioanzisha utetezi wa dini kwenye mkataba huu ni CCM, sijui walitaka kumtisha nani na kwa faida ya nani?
 
Nahitimisha kusema hivi hawapendi raisi muislamu kupingwa
 
Dini na siasa vyote mlaji wao ni mwananchi unavitenganishaje?
Dini na siasa unazitenga vipi? Tuchukulie walioleta dini walijitenga na siasa? Kwa upande wa Waislamu, Mtume Muhammad alipigana vita vingi vya Badr, Uhud, Khandak na Hunayn, je alichanganya dini na siasa? Kwa Wakristo Yesu alikemea maovu ya watawala mpaka akasulubiwa, je alichanganya dini na siasa? Kwa kifupi dini na siasa unazitenga vipi?
 
Kikwete atueleze je udini unaingiaje katika kupinga mkataba wa bandari? Na je ni dini gani itanufaika na huu mkataba wa DPW na TPA?

Tunataka tuelezwe uzuri au ubaya wa mkataba huu na siyo kujificha nyuma ya kichaka cha siasa na dini!
Kazi kweli kweli
 
Ebo! Kwa hiyo ulitaka katika kuhoji wasitumie katiba kama reference! Hujui katiba ndiyo mwongozo uliokubalika katika kuendesha siasa na utawala wa nchi hii!

Sasa kama nyie waislam hamtaki kujua yaliyomo katika mkataba mnapata wapi uhalali wa kuhoji waraka wa maaskofu ambao unakosoa mkataba?

Ukweli ni kuwa mashehe wenu walio wengi hawana elimu ya kutosha hata kuelewa mkataba wenyewe na ndiyo sababu wamebaki kulalamika kuwa kuna udini wakati hoja ni kuwa mkataba ni mbovu na wa kifisadi! Maaskofu wanapojaribu kuwaelimisha namna serikali ilivyopotoka mnaona ni uchochezi dhidi ya serikali!

Ningefurahi kama wewe ingejikita katika kujadili vifungu vya mkataba badala ya kutaka kujadili mafundisho ya Yesu Kristo!

Mtu ye yote ambaye anaamini kuwa dini na siasa havitangamani basi hajui anachojua. Nchi zote zinazotawaliwa kwa Sheria ya kiislamu zinachanganya dini na siasa mfano Iran, Iraq, Pakistan, Saudi Arabia, Afganistan nk.
 
Ebo! Kwa hiyo ulitaka katika kuhoji wasitumie katiba kama reference! Hujui katiba ndiyo mwongozo uliokubalika katika kuendesha siasa na utawala wa nchi hii!
Sahihi kabisa unajua maana ya kufata dini ? Maana lazima utumie misingi ya dini yako kama muongozo katika kuyaendea mambo. Maana yake kutumia katiba kama marejeo wewe unakuwa hufati dini sababu katiba no matokeo ya maoni ya watu ambayo yana mapungufu mno.

Usiwe unakurupuka kijana, tumia akili kuhoji mambo.

Umekubalika na kina nani ? Kwanini Kuna dini ? Maana ya dini ni nini ?

Kwahiyo nyinyi Wakristo muongozo wenu ni Katiba au Biblia ?

Ndio maana nasema hivi Maaskofu akili ndogo sana.
 
Maoni yako ni mazuri Sana lakini wakati CCM inajifungamanisha na Dini hamkusema.
 
Kikwete atueleze je udini unaingiaje katika kupinga mkataba wa bandari? Na je ni dini gani itanufaika na huu mkataba wa DPW na TPA?

Tunataka tuelezwe uzuri au ubaya wa mkataba huu na siyo kujificha nyuma ya kichaka cha siasa na dini!
Kikwete ni mtu asiyejali chocho ndo maana alingia mikataba ya hovyo hovyo ,halafu anataka mpaka karne hii tuendele na haiyo na iana hiyo ya mikataba kwa kuwa yeye na wajukuu. Wake wana uhakika wa maisha
 
Sasa kama maaskofu wamerejea katiba katika hoja zao ni vipi mnabwabwaja kuwa wameingiza dini katika siasa?

Dini zipo ili kutoa miongozo ya kiroho kwa binadamu na kila mtu ana dini yake. Uislamu ni dini yako na si ya watu wote.

Wakristo wanafuata vyote biblia kwa mambo ya kiroho na katiba kwa mambo ya utawala na maendeleo. Bahati mbaya kwenu waislamu mambo yenu ya kutaka kutumia Sharia hayana nafasi Tanzania hivyo lazima mfuate katiba. Ndiyo sababu Sheikh Mselemu alifungwa na Kikwete na hamkufurukuta mpaka alipoachiwa na Samia baada ya kusota zaidi ya miaka 7.

Nakushauri wewe ndiye unapaswa kutumia akili kuihoji serikali na siyo kutumia Sharia ambazo hazina nafasi katika utawala wa nchi hii!
 
Kikwete ni mtu asiyejali chocho ndo maana alingia mikataba ya hovyo hovyo ,halafu anataka mpaka karne hii tuendele na haiyo na iana hiyo ya mikataba kwa kuwa yeye na wajukuu. Wake wana uhakika wa maisha
Kikwete ni mtu wa hovyo sana anajali tumbo lake tu!
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…