Kilimanjaro: Naomba tumsaidie Mwanafunzi Sifika Daniely Ruben apate haki yake na arudi shule

Kilimanjaro: Naomba tumsaidie Mwanafunzi Sifika Daniely Ruben apate haki yake na arudi shule

Kwa walichokufanyia naamini unaona ni sawa mzee alivyogomea misimamo yao
Si sawa kwa walicho nifanyia, mtoto hawezi kupewa adhabu kwa makosa ya wazazi wake. Ingawaje mimi ni RC, lakini sikubaliani na ile rushwa waliyoniomba. Miaka ya 1994, ilikuwa fedha ndefu hadi bibi yangu ikabidi auze mali zake huku dingi amekaza shingo.

Nachosema ni kwamba, huyo binti anahitaji msaada wa hali na mali na hiyo ya yeye kwenda kutafuta u house girl ni njia mojawapo ya kutatua changamote zake.

kwangu mimi, niliponda kokoko, nikauza maembe, machungwa, mananasi, nikapalilia mashamba ya watu na kuuza vitumbua na vubaragashia vya ndizi na unga wa sembe ( kama ulisha wahi visikia) lakini bado sikufua dafu. Ila kwa kuwa nilikuwa determined, niliweza kutoboa kwa nguvu zangu binafsi na msaada kidogo wa bibi yangu (RIP) aliyeuza baadhi ya mali zake ili tu nipewe joining instructions.

Haya ya dingi, sikukubaliana na misimamo yake maana alitakiwa kuweka mbele maslahi ya watoto wake mbele na wajibu huo wazazi wengi hawautaki, ni maslahi yao kwanza. Baada ya hapo akaoa tena mke wa pili na kufyatua watoto lukuki na sasa anataka msaada wa kuwasomesha toka kwangu. Jibu langu huwa ni rahisi sana... Mbegu ya haradari iliyotupwa juu ya miamba huwa haizai.... pambana na hali yako mzee maana uliniacha na hali yangu. Ni hayo tu. mauvimu ni mengi kwa kweli, kama hujapitia maisha ya kuponda kokoto, kuuza matunda, kupika vibaragashia, we acha tu ndugu, shukuru Mungu alikuepusha na maisha hayo.
 
Ndugu, we acha tu. Binafsi hali hiyo ilikwisha nipata. Nilinyimwa joining instructions ya Makoko seminari kule Musoma kisa tu baba yangu hafuati misingi ya ukatoliki. Siwezi sahau tukio lile. Niliponda mawe, nikauza kokoto na kupata fedha ili nitoe rushwa ya kumuhonga mtu wao (anaitwa Padre Masaga)... sijui siku hizi yuko wapi. Huyu Kiumbe nilimchukia hadi sasa kwa jinsi alivyonifanyia ili nipate joining instruction ya makoko seminari kisa tu makosa ya baba yangu kuto kukubari misimamo ya RC. Nimefauli lakini naadhibiwa kwa makosa ya mzee wangu. Siwezi sahahu.
Imani na dini ni vitu viwili tofauti, wengi wana dini,lakini Imani hawana kama huyo Padri aliyekupiga pin kisa life style ya Dingi wako, alafu kama wwe umeamua kufanyia ibada zako kwenye nyumba za Ibada kwa nini ulazimishe na wengine hadi vikwazo vya kiuuchumi kuwekeana!!??
 
Ulikosa shule za serikali?
Nilivuka madarasa kwa uwezo wangu wa darasani na hivyo mitihani ya darasa la saba haikuwa bado. Kwa maana nyingine, nilifanya mtihani wa seminari nikiwa darasa la sita - mwaka mmoja kabla ya wa serikali LY . Yote kwa yote, sababu ya kuvuka darasa ni ili nikwepe elfu 40 ya wakati ule maana dingi alikwisha telekeza familia ya watoto 10 na kutafuta familia nyingine. Mama alikuwa ni mkulima tu.
 
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.

"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.

Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. Nimeumia Kiukweli naomba nisaidie kwa wahusika binti apate haki yake, Mimi sina kipato kikubwa lakini kwa shule ya serikali nitamsomesha, lakini anapataje haki yake maana mimi kumpeleka shule binafsi uwezo sina.

Shule aliyomalizia Form Four ni MKOMBOZI SECONDARY SCHOOL ipo Hedaru Wilaya Ya Same. Shule aliyopangiwa aripoti Form Five Inaitwa NAMWAI HIGH SCHOOL Ipo Mkoa wa Kilimanjaro Sanya Juu,
Na Mchepuo aliopangiwa ni PCM
Namba yake ya Mtihani ni S.P. 0708/0136

Naomba Nisaidie Huyu Mtoto apate haki Yake Arudi shule Mimi nilitaka mfanyakazi ndo nimeletewa Huyo na Moyo wangu Umekosa Amani Nafasi yake Imeuzwa Kisa Alichelewa Kurepoti shule Wazazi wake Hawana Msaada Tena Maana Baba yake ni masini kabisa, na Mama Yake mzazi kwa sasa ni Mgojwa. Naomba Nisaidie apate hake yake Mimi Nitamsomesha Kwa hikihili kipato changu kidogo Nilichojaliwa".

Nimeitoa kwa Yericko Nyerere

View attachment 2761440View attachment 2761442
Hakikisha na yeye hajakudanganya.
Sio tunasumbua watu kumbe mtoto hataki shule ama alifeli kabisa.
 
Imani na dini ni vitu viwili tofauti, wengi wana dini,lakini Imani hawana kama huyo Padri aliyekupiga pin kisa life style ya Dingi wako, alafu kama wwe umeamua kufanyia ibada zako kwenye nyumba za Ibada kwa nini ulazimishe na wengine hadi vikwazo vya kiuuchumi kuwekeana!!??
Jambo la imani ni gumu sana ndugu yangu, laniki nimejifunza kitu. Tangu siku hizo mpaka sasa, Mungu hajawahi kunitupa ktk ombi lolote ninalomuomba (baya au Zuri) hata bila kwenda kanisani. Shukrani kwange yeye Muumba aliye ndani ya nafsi yangu ayasikiaye maombi yangu bila kuchoka na kunipa matamanio yangu kila nimkimbiliapo... usicheze na maombi ukiwa umenuia. Mungu ni msikilizaji mzuri sana.. jua tu namna ya kuongea naye na si lazima kwenda kanisani , hata kimoyomoya anakusikiliza na kujibu tu.
 
0788174071
Namba ya waziri wa elimu hiyo mpigie . Duh Kuna watu wanyama kiasi hicho Karne hii aisee
Usihngaike kumpigia Mkenda huwa hapokei Simu!! Kila wakati Simu yake imezimwa hataki usumbufu!! Hao ndio mawaziri wa Samia.
 
Uongo mkubwa.

1.Matokeo gani yanaanza na SP?

2.Angalieni namba za usajili za taarifa ya yeriko na taarifa ya haya matokeo. Namba 2 tofauti. Hizi ni shule mbili tofauti.
 
Mtoto muongo sana jina lake anaitwa SIFAEL TAWEL ELIREHEMA na alipata daraja 0, hakusoma masomo ya sayansi alikuwa anasoma masomo ya sanaa. Nimeweka na photoentry yake pamoja na ya SIFIKA RUBEN
Screenshot_20230925-114209_Drive.jpg
 
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.

"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.

Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. Nimeumia Kiukweli naomba nisaidie kwa wahusika binti apate haki yake, Mimi sina kipato kikubwa lakini kwa shule ya serikali nitamsomesha, lakini anapataje haki yake maana mimi kumpeleka shule binafsi uwezo sina.

Shule aliyomalizia Form Four ni MKOMBOZI SECONDARY SCHOOL ipo Hedaru Wilaya Ya Same. Shule aliyopangiwa aripoti Form Five Inaitwa NAMWAI HIGH SCHOOL Ipo Mkoa wa Kilimanjaro Sanya Juu,
Na Mchepuo aliopangiwa ni PCM
Namba yake ya Mtihani ni S.P. 0708/0136

Naomba Nisaidie Huyu Mtoto apate haki Yake Arudi shule Mimi nilitaka mfanyakazi ndo nimeletewa Huyo na Moyo wangu Umekosa Amani Nafasi yake Imeuzwa Kisa Alichelewa Kurepoti shule Wazazi wake Hawana Msaada Tena Maana Baba yake ni masini kabisa, na Mama Yake mzazi kwa sasa ni Mgojwa. Naomba Nisaidie apate hake yake Mimi Nitamsomesha Kwa hikihili kipato changu kidogo Nilichojaliwa".

Nimeitoa kwa Yericko Nyerere

View attachment 2761440View attachment 2761442
Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. [emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kitu kama hicho, uuze jina la mtu ili iweje!?,acheni kutupanda kichwani,cheti cha form 4 kina picha na sura ya mhusikae,huyo aliyenunua jina atapata wapi cheti cha form four baada ya kuhitimu form six!?
Hili nalo neno.
 
Back
Top Bottom