Kilimanjaro: Naomba tumsaidie Mwanafunzi Sifika Daniely Ruben apate haki yake na arudi shule

Kilimanjaro: Naomba tumsaidie Mwanafunzi Sifika Daniely Ruben apate haki yake na arudi shule

Si sawa kwa walicho nifanyia, mtoto hawezi kupewa adhabu kwa makosa ya wazazi wake. Ingawaje mimi ni RC, lakini sikubaliani na ile rushwa waliyoniomba. Miaka ya 1994, ilikuwa fedha ndefu hadi bibi yangu ikabidi auze mali zake huku asomesha toka kwangu. Jibu langu huwa ni rahisi sana... Mbegu ya haradari iliyotupwa juu ya miamba huwa haizai.... pambana na hali yako mzee maana uliniacha na hali yangu. Ni hayo tu. mauvimu ni mengi kwa kweli, kama hujapitia maisha ya kuponda kokoto, kuuza matunda, kupika vibaragashia, we acha tu ndugu, shukuru Mungu alikuepusha na maisha hayo.
Makosa huwa yanatokea, na kila binadamu hufanya makosa, lakini mwanadamu mwenye busara huwa hapendi kuona makosa yanajirudia, ikiwa unaweza kumuonea huruma binti asiyekuhusu vipi kutomsaidia mtu anayekuhusu?

Hao ndugu zako hawana kosa kama wakihitaji msaada na wewe unauwezo wasaidiye ili waje kujisaidia wenyewe, maisha haya yana changamoto nyingi, shukuru wewe umefanikiwa lakini umepitishwa kwenye njia ngumu, ndiyo naweza kusema waokozi wa watu huwa wanapitia magumu sana na inavyoonyesha wewe ndiye mwokozi wa familia yenu.

Katika maisha mzazi si mtu wa kuzinguana naye jinsi itakavyokuwa ni mzazi wako tu, tambua nawe ni mzazi au utakuwa mzazi yanaweza kukutokea makubwa kuliko baina yako na mzee wako, hivyo rudisha moyo wako kwa kumsamehe mzee wako na wasaidiye ndugu zako utaona jinsi maisha yako yatakavyobarikiwa.
 
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.

"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.


Nimeitoa kwa Yericko Nyerere

View attachment 2761440View attachment 2761442
Anafanyiwa kazi mkuu
 
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.

"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.


Nimeitoa kwa Yericko Nyerere

View attachment 2761440View attachment 2761442
Hao watu ni wauaji. Hii nchi kuna watu wamekula kesho za watu wengi sana na ndio hao unakuta wanapitisha miswada mibovu bungeni.
 
Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda okoa mstakabali wa maisha ya binti huyu.

"Kaka Yericko pole na Majukumu, Naomba kaka nisaidie, mtoto huyu kwenye picha anaitwa SIFIKA DANIELY RUBEN, naomba apate Haki zake, Ipo hivi kaka, Nilikuwa natafuta binti wa kazi za ndani, Nikapata binti kutoka Hedaru, alipofika nikamuhoji ili kujua ametoka wapi hasa, na familia yake ipoje.

Akaniambia amemaliza Form Four, Ana Division One ya 10, Nikamuuliza Kwanini hujaenda shule, Akasema shule aliyopangiwa wameuza jina lake, Alipoenda kuripoti aliambiwa nafasi yake haipo. Nimeumia Kiukweli naomba nisaidie kwa wahusika binti apate haki yake, Mimi sina kipato kikubwa lakini kwa shule ya serikali nitamsomesha, lakini anapataje haki yake maana mimi kumpeleka shule binafsi uwezo sina.

Shule aliyomalizia Form Four ni MKOMBOZI SECONDARY SCHOOL ipo Hedaru Wilaya Ya Same. Shule aliyopangiwa aripoti Form Five Inaitwa NAMWAI HIGH SCHOOL Ipo Mkoa wa Kilimanjaro Sanya Juu,
Na Mchepuo aliopangiwa ni PCM
Namba yake ya Mtihani ni S.P. 0708/0136

Naomba Nisaidie Huyu Mtoto apate haki Yake Arudi shule Mimi nilitaka mfanyakazi ndo nimeletewa Huyo na Moyo wangu Umekosa Amani Nafasi yake Imeuzwa Kisa Alichelewa Kurepoti shule Wazazi wake Hawana Msaada Tena Maana Baba yake ni masini kabisa, na Mama Yake mzazi kwa sasa ni Mgojwa. Naomba Nisaidie apate hake yake Mimi Nitamsomesha Kwa hikihili kipato changu kidogo Nilichojaliwa".

Namba ya Mlezi +255 686 001 667

Na Yericko Nyerere
 

Attachments

  • Screenshot_20230925-165518_Lite.jpg
    Screenshot_20230925-165518_Lite.jpg
    208.1 KB · Views: 1
  • Screenshot_20230925-165534_Lite.jpg
    Screenshot_20230925-165534_Lite.jpg
    163.3 KB · Views: 1
Maelezo mengiiii lkn kifupi hamna mwanafunzi anayehitaji msaada hapo na huyo aliyempokea pia hana uwezo wa kureason. Zama hizi hicho kitu hakipo kwa mifumo iliyopo HAIWEZEKANIKI hlf mtoto asome afaulu kwa hhsyo matokeo ndo akimbilie kwenye uhausigeli yaaani amekosa kaakili kabisa kawapi pa kupeleka tatizo lake mpaka aamue kukimbilia huko? Basi huo ufaulu aliopata ni non sense na elimu hiyo haina maana kwake.
Kuna mtoto alifaulu kama huyu na ni binti, alikuwa amepata kibarua cha kazi za ndani Dsm

Yule mama akamuhoji kama hivi na ndipo aliguswa na kumpeleka kwenye media ili aweze saidiwa arejee shule

Baba yake ni mgonjwa hanyanyuki kitandani huko dodoma na yeye ndio binti mkubwa na mama ana majukumu makubwa ya kuwa baba kumuuguza baba na kuhudumia wengine

Manispaa ya Dodoma chini ya Mtaka kama sikosei kipindi kile walichukua jukumu la kumsomesha

Na binti ndoto zake ni aje kuwa dkt kwa ajili ya kija kumsaidia mzee wake ambaye amelala kitandani kwa muda sasa

Watu wana pitia changamoto nyingi sana

Na kuna yule mwingine alishindwa kwenda chuo kawa ana shindwa kuvunja kokoto na mama yake, media zikapaza sauti na spika kipindi hicho ni ndugai alichukua jukumu hilo
 
Usaidizi kwa haraka bint huyu unahitajika na hasa kwa wahusika na aliyefanya uhuni sheria zichukuliwe dhidi yake afisa elimu mkoa alikosoma.binti huyo
 
Mtoto muongo sana jina lake anaitwa SIFAEL TAWEL ELIREHEMA na alipata daraja 0, hakusoma masomo ya sayansi alikuwa anasoma masomo ya sanaa. Nimeweka na photoentry yake pamoja na ya SIFIKA RUBEN
View attachment 2761730
Wa Tanzania tunapenda sana ushabiki kwa vitu vya kijinga sana ujue ....hii yaarifa si mtu wa kwanza kukanusha kwamba huyu mtoto ni muongo na kwa taarifa zilizopo mtandaoni kutoka kwa.mdau mmoja kwamba huyu dogo si mara yake ya kwanza kudanganya kuwa kafaulu kaporwa matokeo ..hivi watoto wa kike kwa uongo mnawajua nyie yani anapindisha ukweli unaendana kabisa kumbe uongo mtupu..kwa karne hii kweli nani ananunua jina?vipi mmefatilia background ya Matokeo yake kabla ya hayo ya necta?form four graduant na ufaulu huo option ya mwisho kabisa iwe kufanya kazi za .ndani?inafikirisha na maswali mengi yasiyo na majibu as long as suala hii imeachiwa mamlaka husika wacha ifanye kazi yake lakn binafsi siamin kabisa kama kaporwa matokeo
 
Bint namfahamu vzr ni wa hedaru mtaa wa kongei, ngoja tunyamaze muda utaongea ukweli [emoji40]
 
Bint namfahamu vzr ni wa hedaru mtaa wa kongei, ngoja tunyamaze muda utaongea ukweli [emoji40]
Funguka mzee labda pengine kaporwa ufaulu wake labda Kwa kubadilishiwa namba Kwa vile wazazi hawana kipato ?uchunguzi kutoka Kwa wanafunzi waliosoma pamoja utatupa majibu nani alikuwa mwanafunzi Bora zaidi ya mwingine sababu division one ya 10 na zero vimeachana sanaa lazima aliye kuwa kimeo anafahamika hapo
 
Taarifa iliyotumwa na Mkuu wa shule aliyosomea ni kwamba huyo binti amedanganya, Mkuu wa shule ameweka viambatanisho. Jina halisi ni Sifaeli Tawel na siyo Sifika Daniel. Namba yake ya mtihani ni 0850/0135 na siyo 0850/0136. Huyu alidanganya na hilo suala limeshatatuliwa. Huyu binti alipata div. 0
 
  • Thanks
Reactions: HLM
Ndugu, we acha tu. Binafsi hali hiyo ilikwisha nipata. Nilinyimwa joining instructions ya Makoko seminari kule Musoma kisa tu baba yangu hafuati misingi ya ukatoliki. Siwezi sahau tukio lile. Niliponda mawe, nikauza kokoto na kupata fedha ili nitoe rushwa ya kumuhonga mtu wao (anaitwa Padre Masaga)... sijui siku hizi yuko wapi. Huyu Kiumbe nilimchukia hadi sasa kwa jinsi alivyonifanyia ili nipate joining instruction ya makoko seminari kisa tu makosa ya baba yangu kuto kukubari misimamo ya RC. Nimefauli lakini naadhibiwa kwa makosa ya mzee wangu. Siwezi sahahu.
Seminary lengo lao la kwanza ni wito wa upadre, na wito unaanzia nyumani, Sasa kama mzee hasapoti huo wito ni kwamba familia haiingia katika mfumo wao, Hivyo walikua sahihi, kanisa linaanza na Familia.

Zipo familia Baba ni Muislamu ila alisapoti wanae katika ukatoliki na walisoma seminary bila shida.
Hapo issue kubwa ni hio Rushwa Huyo padri bogas alizingua.
 
Khaa sasa seminary lengo lao la kwanza ni wito wa upadre, na wito unaanzia nyumani, Sasa kama mzee hasapoti huo wito ni kwamba familia haiingia katika mfumo wao, Hivyo walikua sahihi,
Zipo familia Baba ni Muislamu ila alisapoti wanae katika ukatoliki na walisoma seminary bila shida.
Hapo cha issue kubwa ni hio Rushwa Huyo padri bogas alizingua.
Wito tulikuwa nao ktk familia. Dingi alisomea huko huko seminari na baba yake dingi alisaidia kuitafsiri biblia yote toka English hadi kibantu chao…
Anyway- sikujali Ndugu zangu walifanya nini, nilicho sikitika ni hilo Jambo la rushwa- huyu Padre Masaga Kama yumo humu Kwa kweli ujue ulinikwaza sana hata sasa nikiyakumbuka iliyonifnyia napata maumivi ya moyo sana.
Nimekusamehe ila kusahau ni mtihani…
 
Hapana mambo kama haya inabidi yawekwe public ili ushenzi kama huu ukomeshwe.

Hafu hawa ndio walimu ambao watu wanataka waboreshewe maslahi na mashahara.

Hii ndiyo Tanzania sasa nchi ambayo kila mtu kambare ukimkuta kitengo chake.
Umekurupuka ndugu
 
Back
Top Bottom