Kinachoendelea Kigoma kuibua wachawi ni udhalilishaji, upuuzi na uchonganishi

Kinachoendelea Kigoma kuibua wachawi ni udhalilishaji, upuuzi na uchonganishi

Viongozi wote wa kigoma hawalioni hili ?

Tusema viongozi wa CC wamelipitisha, mtu unalazishwa kutoa afu5 na fimbo juu . Asee [emoji119]
Huyo muweka uzi ni muongo. Mtu halazimishwi kutoa fedha. Fedha zinachangwa kwa hiari. Na fedha hizo ni kwaajili ya wanaowasaidia hao wataalamu kufanya shughuli yao. Hao wataalamu hawachukui hata mia mbovu.
 
Wanakijiji wa Kigoma Wana maoni gani? Ikipigwa kura ya maoni Huko Kigoma.

Kwamba kamchape wake au wasije?

Wananchi wengi watakuwa upande gani? Unavyohisi wewe
Wananchi ndio wanawachangia hawa jamaa kwa hiari yao. Hakuna analazimishwa na fedha hizo ni kwaajili ya wanaowasaidia hao wataalamu kufanya shughuli yao. Hao wataalamu hawachukui hata mia mbovu.
 
Narudia tena ni Udharilishaji, Upuuzi, Ushenzi,Uchonganishi na Utapeli.

Nimefika mkoa wa Kigoma Tokea Majuzi nilicho Kikuta huku Sielewi Huku ninchi Nyingine au ni Tanzania hii hii !

Kuna kitu kinaitwa  KAMCHAPE, hawa wapuuzi nani kawaleta, Hili kweli nani kalipa Baraka kufanyika karibu mkoa mzima wa Kigoma?

Kinachofanyika Ni Udhalilishaji na Uchonganishi kwa jamii.

Kwanza Wanachangisha Tsh 5,000 kila kaya kwa lazima sio ombi.

Kisha Wanapita kila nyumba Eti wanatoa Uchawi na wachawi! Tena utake usitake lazima.

Wakifika kwako wanasema hapa kuna uchawi Lazima uchapwe kisha unanyolewa Nywele Mbele ya umati wa watu kisha kunyweshwa Kile wanachoKiita Dawa hautakuwa mchawi tena!

Nimefuatilia kinachofanyika pale ni Mazinga Ombwe na Kujipatia Pesa kwa Utapeli!

Wakati Yakifanyika hayo Kijiji Jirani, Nyie mnaanza jiandaa na kama mwenyekiti hata Wakaribisha hao watu au kuchangisha hizo pesha kila kaya naye Anajumuishwa kwenye Kundi moja la Wachawi !

Kuna vitu vya Ajabu sana Vinafanyika mpaka nimeshikwa na Butwaa. Nimeuliza nikaambiwa Serikali Ndio Imeruhusu hili Lifanyike Mkoa mzima kweli?

Mbona Sioni Dodoma na Mbeya Kwanini Kigoma?

Kwasasa zoezi limepamba Moto Vijiji vya Nyarubanda, Kalinzi, Mukigo, Muhinda, Nyaruboza, Rukoma, Igalula, Mgambo, Katumbi, Kalya Nk.

Huko kumechafukwa hali ni mbaya na lisipofanyiwa kazi na kuacha litaleta shida kwa watu


Pia soma
- Mfahamu 'Kamchape' mkamata wachawi na shughuli zake kwa ujumla kutokea hapa Mkoani Kigoma
Tulia wakimaliza Kigoma wataenda mikoa mingine.
Haya ni mambo ya kiroho zaidi Sio kimwili,wewe kama sio mchawi unaumia Nini.
Acha hao wapumbavu waadabishwe
 
Haya yanafanyika hata huko songwe na chunya.Ni nani huwa anawaruhusu hawa wapuuzi? Hivi wakuu wa mikoa na wilaya ambao ndo wakuu wa ulinzi na usalama kazi yao ni nini dhidi ya kuwalinda wananchi hasa kwenye upuuzi kama huu?


Tanzania nchi ya hovyo sana
Kama wanatoa kwa hiari Yao shida nini,mbona watu wanatoa kanisan kwa hiari
 
Haya yanafanyika hata huko songwe na chunya.Ni nani huwa anawaruhusu hawa wapuuzi? Hivi wakuu wa mikoa na wilaya ambao ndo wakuu wa ulinzi na usalama kazi yao ni nini dhidi ya kuwalinda wananchi hasa kwenye upuuzi kama huu?


Tanzania nchi ya hovyo sana
Kigoma wananchi wapinga agizo la DC wataka uchawi ukomeshwe.

Hiinili niliona kwenye taarifa ya habari, azamu tv, wananchi wakiandamana kumpinga DC kukataza watu wanaojifanya wanatoa uchawi, muda mwingine wananchi tunawaingiza viongozi kwenye moto, hebu nenda you tube, andika maneno ya hapo juu, uone juhudi za DC kuxuzuia hii.
 
Wanakijiji wa Kigoma Wana maoni gani? Ikipigwa kura ya maoni Huko Kigoma.

Kwamba kamchape wake au wasije?

Wananchi wengi watakuwa upande gani? Unavyohisi wewe
Wengi Wana unga mkono wachapwe
 
Huyo mganga si ayatume majini yake yaende Benki yeyote ya karibu yakachukue hela kuliko kuanza kuchangisha wananchi ambao ni choka mbaya?
 
Narudia tena ni Udharilishaji, Upuuzi, Ushenzi,Uchonganishi na Utapeli.

Nimefika mkoa wa Kigoma Tokea Majuzi nilicho Kikuta huku Sielewi Huku ninchi Nyingine au ni Tanzania hii hii !

Kuna kitu kinaitwa  KAMCHAPE, hawa wapuuzi nani kawaleta, Hili kweli nani kalipa Baraka kufanyika karibu mkoa mzima wa Kigoma?

Kinachofanyika Ni Udhalilishaji na Uchonganishi kwa jamii.

Kwanza Wanachangisha Tsh 5,000 kila kaya kwa lazima sio ombi.

Kisha Wanapita kila nyumba Eti wanatoa Uchawi na wachawi! Tena utake usitake lazima.

Wakifika kwako wanasema hapa kuna uchawi Lazima uchapwe kisha unanyolewa Nywele Mbele ya umati wa watu kisha kunyweshwa Kile wanachoKiita Dawa hautakuwa mchawi tena!

Nimefuatilia kinachofanyika pale ni Mazinga Ombwe na Kujipatia Pesa kwa Utapeli!

Wakati Yakifanyika hayo Kijiji Jirani, Nyie mnaanza jiandaa na kama mwenyekiti hata Wakaribisha hao watu au kuchangisha hizo pesha kila kaya naye Anajumuishwa kwenye Kundi moja la Wachawi !

Kuna vitu vya Ajabu sana Vinafanyika mpaka nimeshikwa na Butwaa. Nimeuliza nikaambiwa Serikali Ndio Imeruhusu hili Lifanyike Mkoa mzima kweli?

Mbona Sioni Dodoma na Mbeya Kwanini Kigoma?

Kwasasa zoezi limepamba Moto Vijiji vya Nyarubanda, Kalinzi, Mukigo, Muhinda, Nyaruboza, Rukoma, Igalula, Mgambo, Katumbi, Kalya Nk.

Huko kumechafukwa hali ni mbaya na lisipofanyiwa kazi na kuacha litaleta shida kwa watu


Pia soma
- Mfahamu 'Kamchape' mkamata wachawi na shughuli zake kwa ujumla kutokea hapa Mkoani Kigoma
Haya mambo si ndiyo yalimfanya Ali Hassan Mwinyi mpaka ajiuzulu u Waziri wa Mambo ya Ndani?

Waziri wa sasa naye anafanya nini? Polisi wanafanya kazi gani huko?
 
Huyo mganga si ayatume majini yake yaende Benki yeyote ya karibu yakachukue hela kuliko kuanza kuchangisha wananchi ambao ni choka mbaya?
Bank zote freemason wamezindika hakuna jini Wala mchawi anaweza chukua Hela bank.
Hata mchawi tu ndani achukui Hela akichukua tu hawezi toka ndani ya nyumba anakuwa amekiuka kanuni
 
Kuna mama mmoja mtu mzima mwenye umri mkubwa kuweza kuitwa bibi alichanjwa chale kwa lazima eti uchawi wake ukose nguvu akitaka kuloga. Mama wa watu alivuja damu njingi. Ilikuwa kila nyumba wakipita zingine wanasema hakuna uchawi na zingine wanasema kuna uchawi, wanafukua sehemu fulani ya nyumba wanaibuka na kitu kama pembe ya myama wanasema ni uchawi, mwenye nyumba anakamatwa na kuchanjwa chale kwa lazima
 
Usikie tu uchawi na wachawi, hawafai kutengamana na jamii. Hukumu ya mchawi ni kuuwawa. Hawa ndiyo visababishi vya umasikini. Utakuta wanaroga watoto wanashindwa kwenda shule. Wachawi wanakwamisha maendeleo ya watu. Kwa maoni yangu washughulikiwe kwa nguvu ili waache uchawi. KAMCHAPE OYEE

Kwa akili hizi Bora bandari iuzwe tu. Bado mpo zama za ujima
 
Mheshimiwa Makamu bila shaka anayajua yanayoendelea huko kwake, atarekebisha.
 
Hivi hii kisheria imekaaje??? Serikali inaruhusu hii kitu kweli??
 
Back
Top Bottom