Kinachomsumbua Dkt. Slaa ni udini na chuki binafsi kwa Rais Samia

Kinachomsumbua Dkt. Slaa ni udini na chuki binafsi kwa Rais Samia

uwe unafanya hivyo hata na kwa wanasiasa wa chama chako. Ondoeni kibanzi machoni penu, kemeeni udini, ukanda, ukabila na mengine ya kipuuzi. Kama wanasiasa wenu wapuuzi msipowakemea sisi waumini wakija kwenye nyumba zetu za ibada tutawakemea
CCM huwezi kuikuta ikihamashisha Udini na ndio sababu ndani ya CCM mtu wa dini yoyote ile na kabila lolote lile anaweza kuwa Kiongozi na kuteuliwa kugombea nafasi yoyote ile.
 
Unaweza niwekee video hata ya Dakika moja ikimuonuesha dkt Slaa akikosoa jambo lolote lile katika awamu iliyopita?
Niwekeee wewe ya Jk.

Enzi za mkapa hukuwepo mdogo wangu Dr Slaa akikosoa serikari ya Mkapa kwenye Mremeta,Buzwagi,Mgodi wa makaa wa kiwira
Hivi vitu huvijui kichwa kitakuuma mbuzi wewe
 
Niwekeee wewe ya Jk.

Enzi za mkapa hukuwepo mdogo wangu Dr Slaa akikosoa serikari ya Mkapa kwenye Mremeta,Buzwagi,Mgodi wa makaa wa kiwira
Hivi vitu huvijui kichwa kitakuuma mbuzi wewe
Nimesema niwekee video ya Dkt Slaa hata ya nusu dakika akikosoa jambo lolote lile katika utawala uliopita. Jibu swali hilo.
 
Hivi unamuona Slaa kweli ana akili nzuri!! Akikuangali tu unajua huyu hamna kitu. Nani ambaye anaenda upadre kafaulu. Upadre ni alternative ya waliofeli kama ualimu

Wewe ndiyo hakuna unachoelewa kabisa!!

Miaka yote Seminary schools za Kanisa Katoliki ndiyo zimekuwa zinaongoza kwa ufaulu Tanzania, mpaka Serikali ikaamua zisiwekwe kwenye orodha ya Sekondari kwa sababu zinaiabisha Serikali, halafu wahitimu wake wawe na elimu ndogo!!

Wakati ule zilipokuwa zinachanganywa na sekondary schools nyingine, ilikuwa kawaida kuona katika top 10 ni seminary schools pekee, na labda shule 2 normal private school na 1 ya Serikali.

Hivi unajua kuwa ukitaka kwenda upadre kama umesoma sekondari za kawaida, ukapata chini ya division 2, hawakupokei? Ni kwenye mazingira maalum wanaweza kumchukua wa division 3 inayoegemea divison 2. Chini ya hapo huwezi kupokelewa kwenda kusomea ukasisi wa Roman Catholic church.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kama ni Wafuatiliaji wazuri wa siasa za nchi hii mtakubaliani nami na ukweli kuwa Dkt. Slaa amekuwa na Udini mkubwa sana ndani ya kifua chake. Amekuwa na chuki binafsi sana kila inapotokea utawala uliopo madarakani ni wa upande wa pili yaani Uislamu. Amekuwa ni mtu mwenye chuki, vurugu na mzushi wa masuala mbalimbali ili kuwachafua viongozi wetu hasa Rais pamoja na kumchonganisha na Wananchi.

Unaweza muangalia Dkt Slaa wa wakati wa Mheshimiwa Kikwete, wakati wa Hayati Dkt Magufuli na wakati huu wa Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan. Utagundua ya kuwa anaongozwa zaidi na Udini pamoja na chuki binafsi kwa Mheshimiwa Rais.

Hali hiyo imempa upofu wa akili na macho katika kujadili hoja. Ndio sababu unaona anakuwa akizusha mambo mbalimbali ya uongo na uchonganisha kwa lengo la kutaka kuifanya serikali ichukiwe na wananchi. Jiulize kama umewahi kumuona au kumsikia Dkt Slaa akikosoa kitu chochote kile katika utawala uliopita. Unafikiri ni kwanini? Jibu ni Udini tuu ndio muongozo wake. Ndio maana kwa Udini wake yupo tayari kuzusha lolote na kusema uongo wowote ule ili serikali ichukiwe na kuleta taharuki pale inapokuwa ikiongozwa na muislamu.

Lakini ni huo huo Udini wa Dkt Slaa anaweza kufumbia macho kitu chochote kile na kutetea kila jambo ikiwa tu ni wa upande wa Dini yake. Ndio maana katika uzushi anaoongea huwezi ukaona akiweka ushahidi wa aina yoyote ile mezani kuthibitisha madai yake ya uzushi na uongo. Hawezi akaweka nyaraka yoyote ile kuthibitisha maneno yake.

Watanzania tunapaswa kumpuuza na kukataa kabisa kuingia katika mtego wa Dkt Slaa wenye lengo na ajenda ya chuki binafsi na Udini kwa kutunga vitu vya kizushi na uongo. Tumkatalie zidi ya ajenda zake chafu za kumchafua Mheshimiwa Rais na tumkemee kwa nguvu zote. Tumwambie kama ana ushahidi wa lolote lile anapokuwa akizungumza hadharani basi atuwekee kwanza ushahidi.

Napenda kumalizia kwa kusema kuwa dkt Slaa hata fanikisha ajenda zake za Udini na chuki binafsi kwa Mheshimiwa Rais, na wala hatafanikiwa kumchafua kwa namna yoyote ile kama ambavyo amekuwa akifanya jitihada za kutaka kumchafua Rais wetu na kumjengea taswira mbaya kwa wananchi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Wewe tutakuondowa kwenye uchawa, mama anamalizia term ya Magufuli, mwaka 2025 ndio tunaanza awamu ya kwanza ya mama yetu kipenzi, mwaka 2030 ndio awamu yake ya pili mpaka 2035 tunamuongeza mitano tena ya shukrani.
 
Wewe ndiyo hakuna unachoelewa kabisa!!

Miaka yote Seminary schools za Kanisa Katoliki ndiyo zimekuwa zinaongoza kwa ufaulu Tanzania, mpaka Serikali ikaamua zisiwekwe kwenye orodha ya Sekondari kwa sababu zinaiabisha Serikali, halafu wahitimu wake wawe na elimu ndogo!!

Wakati ule zilipokuwa zinachanganywa na sekondary schools nyingine, ilikuwa kawaida kuona katika top 10 ni seminary schools pekee, na labda shule 2 normal private school na 1 ya Serikali.

Hivi unajua kuwa ukitaka kwenda upadre kama umesoma sekondari za kawaida, ukapata chini ya division 2, hawakupokei? Ni kwenye mazingira maalum wanaweza kumchukua wa division 3 inayoegemea divison 2. Chini ya hapo huwezi kupokelewa kwenda kusomea ukasisi wa Roman Catholic church.
Siyo kila anayekuw padre lazima apitie seminari.
 
Basi wewe ni msahaulifu sana au ulikuwa haujaanza kufuatilia siasa za nchi hii. Hivi mara hii umesahau vurugu za dkt Slaa wakati wa Mheshimiwa Kikwete?
Nadhani wewe ulikuwa hujaingia katika siasa! Kwa kauli lipi ya Dk.Slaa aliyomsema kwa habari ya udini?
 
Siyo kila anayekuw padre lazima apitie seminari.
Mapadre wanaandaliwa seminari, mtu mwenye wito wa upadre lazima atasoma seminari.

Hoja yako wewe ni sawa na Papa siyo lazima awe Kadinari lakini ni nadra kwa padre kupata daraja la Upapa bila kupitia Uaskofu.
 
Mapadre wanaandaliwa seminari, mtu mwenye wito wa upadre lazima atasoma seminari.

Hoja yako wewe ni sawa na Papa siyo lazima awe Kadinari lakini ni nadra kwa padre kupata daraja la Upapa bila kupitia Uaskofu.
Siyo lazima. Wapo mapadre wengi hawakupitia seminari. Na siyo kila aliyepitia seminari lazima awe padre. Wale vipanga seminarini hawawi mapadre wanaenda vyuo vikuu ila wale dhaifu seminarini ndo wanaenda upadre kama last resort. Mi ni msinari najua hilo
 
Lazima uelewe kuwa hakuna bandari iliyouzwa bali kuna mkataba wa miaka 30 kuwapa wawekezaji,tena siyo bandari nzima au eneo lote la bandarini.tofauti na kauli za wapotoshaji wachache wenye chuki binafsi na ubaguzi wanaosema kuwa bandari zote zimeuzwa. Unaikumbuka kauli ya dkt Slaa alipoulizwa juu ya kupigwa risasi kwa Lissu? Unakumbuka alisema nini?

Wewe kweli ni punguani. Unaandika vitu ambavyo huna uelewa kabisa.

Wewe unaongelea mkataba mtoto wa bandari ya Dar, ambao ni utekelezaji wa mkataba mkuu IGA. IGA inatamka wazi kuwa DPW ndiyo watakuwa wawekezaji pekee kwenye bandari zote za Tanzania. Na mkataba huo utendelea kuwa hai mpaka biashara ya bandari itakapokoma. Wewe unajua biashara ya bandari itakoma lini?

Ninyi machawa msio na akili ni mashetani na wasaliti wakubwa wa Taifa. Hata hawa wanaofanya huu uhayawani watakuwa wanawadharau kwa sababu wanajua kuwa akili zenu zinapofushwa kwa ujira mdogo sana. Watu wanaongelea mambo ya msingi kwa Taifa, ninyi mnakuja na maneno yenu ya kijuha na ujinga kwa sababu ya kurushiwa vihela vidogo na watawala waliokosa uzalendo kwa nchi, wanaotumika kama agents wa mataifa ya kiarabu.

Dunia nzima, hao DPW hawajawahi kusaini mkataba wa kishetani kama huo waliosaini na hawa watawala waliopofushwa kwa rushwa na uelewa mdogo.
 
Siyo lazima. Wapo mapadre wengi hawakupitia seminari. Na siyo kila aliyepitia seminari lazima awe padre. Wale vipanga seminarini hawawi mapadre wanaenda vyuo vikuu ila wale dhaifu seminarini ndo wanaenda upadre kama last resort. Mi ni msinari najua hilo
Tunashindwa kuelewana lugha tu, upadre ni calling, mtu mwenye wito wa upadre anasoma seminari otherwise kama alikosa admision seminari.

Nina washkaji wengi tu waseminari wala hakuna padre huwa tunakutana pale Sealander club.
 
Mshaurini dkt Slaa aache Udini na chuki binafsi kwa Mheshimiwa Rais. Embu nikuulize swali hilo. Je umewahi kumsikia Dkt Slaa akikosoa chochote kile katika utawala uliopita?


Broo huijui hii nchi wala Siasa za ndani na za kimataifa kama Dr. Slaa.

Hujui falsafa ya ukristo wala uislam kama Dr. Slaa.

Huijui CCM wala upinzani kama Dr. Slaa. Hujui Diplomasia wala Demokrasia kama Dr. Slaa .

Humjui Dr. Samia na Serikali yake kama Dr Slaa

Mwisho kabisa Dr Samia hakujui kama anavyomjua Dr. Slaa.

Iko hivi:-
Nchi za magharibi wakishirikiana na nchi Tajiri za Kiarabu zenye ushirika wa karibu na nchi za kimagharibi hasa Marekani wakishirikiana na Wafanyabiashara wakubwa wa silaha duniani , waporaji wa rasilimali za Afrika na kwingineko, wauza madawa ya kulevya na wawekezaji wahuni na walaghai wote wanatengeneza ugaidi kupitia Dini na Kabila. Kongo kwenye wakristo wengi na wapagani wengi hawa Wahuni wa kishetani na mashoga na adui wa Kizazi cha Mwanadamu waefanikiwa kuwaangamiza mamilioni ya Waafrika kupitia Ukabila.

Iko wazi kuwa Kwa sasa Wahuni hao na mawakala wa setani duniani wanatumia uislam maeneo yenye waislam wengi kutengeneza ugaidi kwa baadhi ya nchi za Afrika na Asia . Kwa nchi za Afrika zaidi wanatumia Ukabilla.

Kwa nini Marekani na maswahiba zake wanatumia Uislam kwenye nchi zenye waislam wengi, ? Jibu ni kwa sababu wanajua kuwa uislam ni dini iliyojengwa kiitikadi tangu utotoni. Yaani uislam unajengwa kama mfumo wa maisha kisiasa ,kijamii na kiuchumi.
Ni rahisi kumrubuni mtu aliyejengika kiitikadi tangu utotoni katika misingi ya kuona kuwa hakuna zaidi ya kila anachokiamini.Ndio maana sehemu kama Tanzibar hakuna Lugha za makabila zaidi ya kiswahia hawaamini katika ukabila zaidi ya uislam.
Karne zilizopita Ugaidi ulifanywa zaidi na Wakristo hasa Wakatoliki huko Ulaya na Amerika ya kusini kutokana na jinsi dini iilivyokuwa imejengwa kiitikadi. Kwa sasa hali imebadilika wala Mabepari wanaona ukristo umegawanyika na hauna tena wafia dini.
Ni wazi kuwa kwa sasa CCM haikubaliki bila kutumia dini. Kuna magroup mengi ya whasap watu wanatumia siasa za hovyo za kusema kuwa Eti Dr. Samia anapingwa kwa sababu ni muislam.
Na kwa sababu wale Wahuni na wezi wa kimataifa wamefanikiwa kutudanganya kwa kutumia fedha na misaada kwenye taasisi na NGOs wanaaminika kwa haraka mana wale wasubiri misaada wanaona kazi ni nzuri mana pesa za bure zinapatikana sasa bila kujua kuwa uhalifu wa kimataifa hupitia fedha za misaada.

Watu wamempinga Magufuli Mpaka wakapigwa Risasi na bado wanaendelea kumpinga Mama Samia bila kujali ni Dini gani. Watu wanapigania Rasilimali za Taifa hili alizoziumba Mungu na sio Mama Samia.
Sasa hivi ameaminisha watu kuwa yeye ndiye ameiumba ardhi na utajiri wa Tanganyika na watu wanampigia magoti. Mungu hakuwa mjinga kuwaweka kila watu kwenye eneo lao na rasilimali za kutosha . Ukiwa Rais ni lazima ukubali kukosolewa na hata kutukanwa.
Kinacholeta uchawa huu ni Katiba mbovu . Watu wanajipendekeza kwa sababu katiba inamfanya Rais kuwa zaidi ya Mungu. Anaweza akaamka asubuhi akamtajirisha mtu na kumpa cheo kikubwa na kumvurugia mwingine maisha kama anavyoona yeye bila kuulizwa.
Lakini pakiwa na katiba bora mambo ya udini,ukabila ,uchawa na uchama yatapungua sana.
Hawa wanaoeneza hisia za udini wanatafuta uteuzi tu. Kenya palikua na ukabila sana lakini umeanza kufutika baada ya katiba mpya. Siasa zinajijenga kwa misingi ya hoja sio dini na ukabila.

Dr. Slaa amefanya kazi na Serikali ya CCM Dr.Samia akiwa Makamu wa Rais. Serikali sio Samia yeye ni kiongozi na mtawala . Akikosea atasemwa na serikali yake.
Dr Slaa ni mwanasiasa na mwanaharakati sijawahi kumsikia akizungumzia mambo yanaayohusiana na itikadi za kidini. ?

Wakristo tangu Mwalimu Nyerere walimpinga sana mpaka wengine wakahama nchi . Mwinyi hivyohivyo ,mkapa hivyohivyo aliambiwa na Mrema kuwa ameuza Migodi na wenyeji wakafukiwa kwenye mashimo wakiwa hai. Akaja Kikwete hivyo hivyo akapingwa alipouza Gesi na kuwapiga kwa mabomu Watu wa kuisini kisha gesi kupewa wageni na mpaka leo nchi ni maskini na tozo ndizo zinajenga mashule na barabara badala ya gawio la gesi kama tulivyoambiwa na tukawalaumuwamakonde na kufurahia walipokua wanavunjwa miguu.
Ugaidi ukaanza kutengenezwa. Magufuli akakuta hali ya ugaidi iko juu karibu na kuvuruga nchi. Yote chanzo ni mikataba ya hovyo na misaada saada.
Dr. Slaa ana haki ya kuhoji masuala yanayohusu Tanganyika mana ndiyo nchi yake pekee. Mama Samia ana nchi mbili Zanzibar na Tanganyika na ni Rais wa Tanganyika kwenye koti la Muungano au Tanzania .

Ni wazi kuwa Mleta Mada unachochea Chuki za kidini lakini mwisho wake utashindwa kwa sababu kizazi hiki hata huko Uarabuni hawapiganii maslahi ya mtu mmoja wala dini yake bali uhuru wao na maslahi ya Taifa kwa manufaa ya wengi.
Wawekezaji waje wajenge viwanda ,sio malori ya kubeba mizigo na mabasi na Bandari ,wanyama ambao wapo bure porini hawana hata kazi kubwa ya kuwatunza kama ngombe au kuku. Tunawapa misitu ili wafanyeje? Tunawapa ardhi kubwa ambayo ndio urithi wa maskini kwenye nchi waliyoumbiwa na Mungu. Halafu watu wakae kimya.

Yaani umffukuze mmasai mwenye nyumba ya matope na Ngombe halafu umlete Mwarabu mwenye Magari ,Mandege ,mabunduki, Mahoteli n.k eti ndiye anayetunza mazingira . ?
Inakuja kweli kwenye akili ya dini ya mtu au ni janga la kitaifa kwa miaka ijayo.

Mikataba yote mibovu imeleta madhara makubwa kwa watu maskini na wazawa. Kuanzia kwenye migodi mpaka kwenye hifadhi.

Wewe Mleta mada hebu Jiulize Kama JPM alipingwa na kwa kiwango kikubwa alilinda sana Rasilimali za nchi na kupinga sana ufisadi maisha yake yote tangu akiwa waziri wa ujenzi kwa watawala waliokuwa wamejimilikisha magari ya umma na kuweka namba za kiraia huku wakiwa wanatumia madereva wa serikali na kafuta ya serikali kwa shughuli binafsi JPM angesafiri na kuuza rasilimali za nchi kama ilivyo leo kelele zake zingekuaje ukiunganisha na Kelele za kipindi cha Kikwete?
Huoni kuwa JPM ameiokoa sana CCM mpaka leo ina watu kama Majaliwa , Makonda,Polepole,Ndugai,Mpina,Chalamila, na hata wabunge kama Mdee aambao wanaweza kutoa hoja zenye kufikirisha ?
Yaani JPM angeendeleza mbinu zile zile za kupiga bakuli na kugawa rasilimali za umma kwa mawakala wa mashoga duniani ! Hali ya CCM ingekuwa mbaya sana na uchumi ungeporomoka sana kipindi cha Korona .

Tusisingizie udini kwenye maslahi ya nchi. Lisemwalo lipo na Dr. Slaa hajawahi kukosea katika kutoa hoja zake juu ya ufisadi .
 
Tippu_Tip.jpg

Huyu Mzee aliuza Mababu zetu huyu Mama tisipompiga Stop nae atatuuza.

Tusipokuwa Makini Watanganyika tutauzwa Uarabuni.
 
Wewe kweli ni punguani. Unaandika vitu ambavyo huna uelewa kabisa.

Wewe unaongelea mkataba mtoto wa bandari ya Dar, ambao ni utekelezaji wa mkataba mkuu IGA. IGA inatamka wazi kuwa DPW ndiyo watakuwa wawekezaji pekee kwenye bandari zote za Tanzania. Na mkataba huo utendelea kuwa hai mpaka biashara ya bandari itakapokoma. Wewe unajua biashara ya bandari itakoma lini?

Ninyi machawa msio na akili ni mashetani na wasaliti wakubwa wa Taifa. Hata hawa wanaofanya huu uhayawani watakuwa wanawadharau kwa sababu wanajua kuwa akili zenu zinapofushwa kwa ujira mdogo sana. Watu wanaongelea mambo ya msingi kwa Taifa, ninyi mnakuja na maneno yenu ya kijuha na ujinga kwa sababu ya kurushiwa vihela vidogo na watawala waliokosa uzalendo kwa nchi, wanaotumika kama agents wa mataifa ya kiarabu.

Dunia nzima, hao DPW hawajawahi kusaini mkataba wa kishetani kama huo waliosaini na hawa watawala waliopofushwa kwa rushwa na uelewa mdogo.

Chaa ajabu hawajaleta Teknolojia yoyote mpaka sasa wanachofanya ni kuuanya pesa za ndani na kuata mtaji . Tunatumia mikopo ya nje kuwawekea mazingira mazuri waliotukopesha ili waje wavune pesa zao waondoke huku watanzania wakiendelea kulipa madeni.

Ni sawa na yake ya kukopa pesa za ujenzi wa Barabara au madaraja na kisha kuwapa Tenda ya ujenzi wale wale uliowakopesha na pesa zote zinarudi kwao. Badala ya kuajiri wataalam wa chache na Tenda kuwapa wazawa kutasababisha hata wataalamu walioko nje kurudi kulijenga Taifa lao.

Hawa wakiona Ngozi nyeupe wanajua ndio malaika wameshuka kutoka Mbinguni kuja kuijenga Tanzania. Kumbe ni mashetani yanayowaza kumaliza kizazi cha bimadamu kwa kuleta ushoga ,magonjwa ,vita ,uroho wa madaraka ,rushwa ,ufisadi na kulinda maslahi ya wachache kupitia vyombo vya dola.
 
Siyo kila anayekuw padre lazima apitie seminari.
Kwa hiyo anapitia wapi? Au huelewa kabisa mfumo wa Kanisa?

Unadhani unaweza kuchomoka tu kutoka popote ukasema unataka kuwa Padre?
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kama ni Wafuatiliaji wazuri wa siasa za nchi hii mtakubaliani nami na ukweli kuwa Dkt. Slaa amekuwa na Udini mkubwa sana ndani ya kifua chake. Amekuwa na chuki binafsi sana kila inapotokea utawala uliopo madarakani ni wa upande wa pili yaani Uislamu. Amekuwa ni mtu mwenye chuki, vurugu na mzushi wa masuala mbalimbali ili kuwachafua viongozi wetu hasa Rais pamoja na kumchonganisha na Wananchi.

Unaweza muangalia Dkt Slaa wa wakati wa Mheshimiwa Kikwete, wakati wa Hayati Dkt Magufuli na wakati huu wa Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan. Utagundua ya kuwa anaongozwa zaidi na Udini pamoja na chuki binafsi kwa Mheshimiwa Rais.

Hali hiyo imempa upofu wa akili na macho katika kujadili hoja. Ndio sababu unaona anakuwa akizusha mambo mbalimbali ya uongo na uchonganisha kwa lengo la kutaka kuifanya serikali ichukiwe na wananchi. Jiulize kama umewahi kumuona au kumsikia Dkt Slaa akikosoa kitu chochote kile katika utawala uliopita. Unafikiri ni kwanini? Jibu ni Udini tuu ndio muongozo wake. Ndio maana kwa Udini wake yupo tayari kuzusha lolote na kusema uongo wowote ule ili serikali ichukiwe na kuleta taharuki pale inapokuwa ikiongozwa na muislamu.

Lakini ni huo huo Udini wa Dkt Slaa anaweza kufumbia macho kitu chochote kile na kutetea kila jambo ikiwa tu ni wa upande wa Dini yake. Ndio maana katika uzushi anaoongea huwezi ukaona akiweka ushahidi wa aina yoyote ile mezani kuthibitisha madai yake ya uzushi na uongo. Hawezi akaweka nyaraka yoyote ile kuthibitisha maneno yake.

Watanzania tunapaswa kumpuuza na kukataa kabisa kuingia katika mtego wa Dkt Slaa wenye lengo na ajenda ya chuki binafsi na Udini kwa kutunga vitu vya kizushi na uongo. Tumkatalie zidi ya ajenda zake chafu za kumchafua Mheshimiwa Rais na tumkemee kwa nguvu zote. Tumwambie kama ana ushahidi wa lolote lile anapokuwa akizungumza hadharani basi atuwekee kwanza ushahidi.

Napenda kumalizia kwa kusema kuwa dkt Slaa hata fanikisha ajenda zake za Udini na chuki binafsi kwa Mheshimiwa Rais, na wala hatafanikiwa kumchafua kwa namna yoyote ile kama ambavyo amekuwa akifanya jitihada za kutaka kumchafua Rais wetu na kumjengea taswira mbaya kwa wananchi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Maslahi ya nchi hayana udini wewe usiwe unajadili hoja usizozoweza unaonekana hamnazo
 
Back
Top Bottom