Kinana: Rais wa Tanzania aliyekula kiapo hawezi kufanya jambo ambalo halina maslahi na nchi yake

CCM njooni mmsikilize Kinana kuna jambo la maana.

Your browser is not able to display this video.

---
Kinana avunja ukimya kuhusu Bandari

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdurhaman Kinana, amezungumzia mjadala wa uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam huku akiweka wazi kuwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoingoza haiwezi kuuza bandari hiyo na kuhoji Rais auze bandari kwa maslahi yapi.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Mkendo Musoma Mjini Kinana alianza kwa kueleza kuwa liko jambo la bandari linazungumzwa na mjadala mkubwa, unaendelea kuwa mrefu, mjadala mpana.

“Nataka niwahakikishie msiamini kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyekula kiapo eti atafanya jambo ambalo halina maslahi na nchi. Haiwezi kutokea, Rais ambaye tangu amechukua usukani amefanya mambo mengi mazuri, kwa nini aende kuuza bandari, sababu ni
ipi?

Ili apate nini, ili iweje na ukisikiliza huu mjadala usikilizeni kwa makini na mmeshausikiliza, wote tunaoutetea, wanaopinga pamoja na wanaokosoa hakuna anayesema kwamba kusiwe na uwekezaji hata mmoja kwani wote wanakubali kwamba kuna haja ya kuwekeza na lengo ni moja tu kuongeza ufanisi na kuongeza mapato.

“Serikali imesema tunakwenda kufanya kazi hii kwa nia njema ya kuongeza ufanisi, kuongeza mapato tuweze kufanya shughuli nyngi zaidi za maendeleo. Wamejitokeza watu wameanza kuhoji, wako wanaohoji kwa nia njema ya kujenga ya uzalendo, hatuwezi kusema kila anayehoji anania mbaya,” alisema.

Anachofanya Rais ni kuwa mtulivu kusikiliza kila hoja kuchambua kila hoja, kutathimini kila hoja, ili muda utakapofika tupate uwekezaji ulio bora zaidi kwa manufaa ya Watanzania. wako waliopeleka mjadala huu katika udini, wengine katika muungano Bara na Visiwani, hakukua na sababu,”alisema Kinana.

Alifafanua kuwa uwekezaji huo ni wa kiuchumi hivyo unatakiwa kujadili kwa hoja,hoja itasikilizwa, hoja yako itajibiwa , pale itakapotakiwa kufanyiwa kazi itafanyiwa kazi kwa maslahi mapana ya nchi.

“Sasa niseme yafuatakayo hakuna anayekataa ,wale wanaopinga na wanaonga mkono, hakuna anayekataa uwekezaji , Serikali inaendelea kusiliza hoja ,maoni na hofu zinazotolewa.

“Chama chetu kimeagiza kwamba wananchi wasikilizwe kwa kila ngazi , kwa kila sehemu, Serikali inaendelea kusikiliza.Sina mashaka hata kidogo kwamba Rais atatoa uamuzi wa busara katika jambo hili na hata uamuzi huualipoufikia kuwekeza katika Bandari ni kwa sababu moja tu ya maslahi mapana ya watanzania na nchi sio kwasababu nyingine yoyote.

“Najua tuko watu wengi tuko vyama vingi ndio wakati muafaka sasa likitokea jambo kila mtu anatatafuta namna ya kulitengeneza kwa namna ambayo linakuwa na manufaa kwake. Kwa hiyo ukipiga kelele sana nchi imeuzwa …imeuzwa …imeuzwa ungependa watu waamini kwamba imeuzwa.

"Hakuna bandari inauzwa, inauzwaje? kwanini iuzwe ?Bandari ya Musoma hapa inauzwaje”, kwa bei ipi ? kwasababu ipi? Ili iwe vipi hakuna sababu, naomba tuwe watulivu. Naomba tuwe na imani na Serikali yetu tuwe na imani na Rais wetu ,tumuamini kwamba kila jambo analofanya ni kwa maslahi ya Taifa letu.
 
78, hao wapo hapo kulinda masilahi binafsi ya JK
MTU wa miaka 78 anatuongaza kuelekea wapi?
Ni wazo gani la kimaendeleo ambalo alikosa nafasi ya kulitoa alipokua waziri Hadi tutegemee alilete Sasa?
Wasira atakua na wazo gani jipya ambalo hakutuambia tangu aanze uongozi miaka ya sabini. Sana Sana anatuongaza twende huko anakoelekea kwa Sasa. Maandiko yanasema miaka yetu ni sabini hapa duniani, ikizidi Sana Ni sabini na Saba, baada ya hapo......
 
hawa ni vijana wa JK
 
Nimependa tamko hili.Lakini kiongozi wa Chama ni kama amechekelewa kidogo kutoa muongozo huo.Ilikuwa vema angeelekeza haya kabla ya Bunge kuidhinisha mkataba.

Nimependa tamko hili.Lakini kiongozi wa Chama ni kama amechekelewa kidogo kutoa muongozo huo.Ilikuwa vema angeelekeza haya kabla ya Bunge kuidhinisha mkataba.
Nimependa tamko hili.Lakini kiongozi wa Chama ni kama amechekelewa kidogo kutoa muongozo huo.Ilikuwa vema angeelekeza haya kabla ya Bunge kuidhinisha mkataba.
Bunge lipo sehemu gani?
 
Wanachoshindwa kuelewa ni kua watu hawapingi uwekezaji bali wanapinga mkataba mbovu,
 
Sijasoma content bali heading tu, nadiriki kusema.. Hawez enda kinyume wala kupinga baadhi ya vifungu.
 
Sasa mpaka Katia Saini mkataba kuukubali ,,,,si ameona una maslahi au,,lakini wananchi tumesema nooo ,
 
Waliouza Loliondo na mikataba ya hovyo kwenye madini na gesi hawakula kiapo? Majizi ni majizi tu.
 
Yaliyotokea huko nyuma viapo havikuwepo.unaweza kula kiapo lakini kwa kuwa na uelewa mdogo na kutokuumiza kichwa ukasini hovyo hovyo
 
Biashara ya meno ya tembo ni haramu
Anauwawa mnyama mpole tena mkubwa mwenye uzito wa kilo 7000 kwa ajili ya pembe zake zenye kilo 30 !!!!! 🙄🙄🙄. Wenye kazi hizo Mungu wa mbinguni anawaona ! Na hawatapata peace of mind katika maisha yao yote wakiwa na hizo pesa haramu !!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…