Kiteto: Wakulima mji wa Kibaya wagomea bei ndogo ya mnada zao la mbaazi

Eka moja inatoa gunia moja sasa utalima eka ngapi ili upate pesa ya maana, au mnachanganya na mazao y a nje
 
Tatizo wakulima pia hawana mmoja, mkigoma kuuza wengine wanauza tena bei ndogo
Kangomba tulisha wakataa...

Wachimbaji wadogo wa dhahabu huwezi walangua, wanafahamu soko linavyoenda kuanzia soko la dunia, dar, nairobi nk

Hawa watu wq kiteto, kondoa wasikilizwe wasaidiwe na wauze kwa bei nzuri, wahindi wasiwasumbue... hili zao wqnunuzi wakuu wahindi wana peleka kwao
 
Nunua wewe au zitunze usubiri bei nzuri zaidi

Sent from my TECNO KB8 using JamiiForums mobile app
 
Changamoto Kuna Binge Moja zamani alikuwa Kwa Haji dalali ndio anawapeleka puts watu wote pale amekula deal na watu wachache wapige Hela ,
 
DC Wa Kiteto Tunataka utoe majibu , kwanini watu wasipeleke Kwenye soko la Uhakika wa Bei kubwa , watu Tunataka Soko la Dar es salaam kama hasara Wacha tupate sisi tupo tayari kulipa Ushuru na Tusafirishe Mazao yetu wenyewe
 
Gharama anazochajiwa mnunuzi mbazi Wilayani Kiteto ni zaidi ya Tshs 160/ unaambiwa Hadi Kuna tozo ya mtunza ghala Tshs Kwa kg 40/, Vyama vya ushirika, mifumo, Halimashauri, Na hao hakuna kitu chochote walichomsadia mkulima,,
Tunataka kufahamu mchango wao kwenye sector ya kilimo Kwa Kiteto.
 
Bei ya Mbazi kwenye Mnada Kiteto kuwa Ndogo Kuna hangiwa na Tozi mbalimbali anazotozwa mnunuzi wa Mbazi kwenye Mnada Tozo zida zidi Tshs 160/ Kwa Kg Moja
Ushuru wa Halimashauri
Mtunza ghala analipwa zaidi ya Tshs40/ Kwa kg Moja
ACU - Chama ushiri Arusha.( Na Kiteto ipo mkoa wa manyara)
AMCOSI.
Hivi vyote ndio vinashusha Bei ya Mbazi Eli kufidia hizi tozo ambazo zinatozwa Kwa mnunuzi na yeye ana adjust Bei Eli aweze kumudu gharama za Tozo.
 
Wakulima wa Mbazi Leo Tena saa 4 asubuhi watakutana na Mkuu wa Wilaya Kiteto kujuwa Hatima ya Mbazi zao. msimamo wao Bado upo pale pale ama wapewe Bei nzuri au Kibali Cha kusafirisha Mbazi Zetu kwenda kwenye Soko la Dar es salaam
 
Wakulima wa Mbazi Leo Tena saa 4 asubuhi watakutana na Mkuu wa Wilaya Kiteto kujuwa Hatima ya Mbazi zao. msimamo wao Bado upo pale pale ama wapewe Bei nzuri au Kibali Cha kusafirisha Mbazi Zetu kwenda kwenye Soko la Dar es salaam
acha ujinga unaona mbazi ni kitu cha kuringia sokoni
 
Gharama za usafiri Kwa Semitrela la kupakia Gunia 300 ni 1.5M ukigawa gharama zake za ote ni chini ya 70kwa KG? Na tofauti ya Soko la Kibaya ni zaidi 200/ Kwa kg chikulua mtu ana KG 60000 mara Tshs 200 ni zaidi ya Tshs 12M jee hiyo ni ndogo
Umeweka gharama za labor, warehouse, chakula na malazi? Au ukifika Dar tu unauza juu ya gari unarudi kwenu?
 
Umeweka gharama za labor, warehouse, chakula na malazi? Au ukifika Dar tu unauza juu ya gari unarudi kwenu?
Dunia ya Sasa huna haha ya kusafiri Kuna magari mengi tu hapa Kibaya mjini, unapakia mzigo wako na idadi ya kg zako gari linapikelewa sokoni Kwa Haji ama Barracuda na dalali Wa haya Mazao ni Moja tu Anaitwa Malick baada ya masaa mawili ama matano muamala unasoma kwenye akaunti
 
acha ujinga unaona mbazi ni kitu cha kuringia sokoni
Mbazi no Moja ya Mazao muhimu sana Kwa Uchumi wa Nchi kama likipewa kipaumbele litaongeza Fedha za Kigeni , Unajuwa Balance of payment? Sasa mbazi inakwenda kuongeza kitu pale kwenye Export, wewe inabaki Dola hamna hujue jinsi ya kupata Dola kwenye Uchumi ni pamoja na kuongeza uzalishaji wa haya mazao
 
Kwahiyo dalali Malick atakuuzia kwa 2,400 na kukutumia net bila kuweka commission yake?
 
Hao "watu" unaotaka wapewe vibali vya kusafirisha mbaazi kupeleka Dar ni wakulima au madalali?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…