Kitwanga: Kuna kundi linalomshauri vibaya Rais Samia

Kitwanga: Kuna kundi linalomshauri vibaya Rais Samia

Tunahitaji taasisi imara zaidi kuliko wote
Taasisi haijengwi na majengo au vitabu ni watu. Pole kama hulijui hilo. Na lazima wawe na kiongozi na kwa mfumo wa katiba yetu hilo ni jukumu la Rais pekee mpaka hapo tutakapo amua vinginevyo.
 
Mtu yeyote anaweza kumshauri rais. Lakini rais anao washauri wake pale Ikulu. Kwa hiyo ukisema rais anashauriwa vibaya,una maana hana washauri wazuri pale Ikulu. In fact wale washauri wake wa Ikulu, I noticed,wamemshauri raid awapeleke Washington DC na wapi sijui,kwa hiyo sasa rais hana washauri tena.
Rais mstaafu hawezi kuwa mshauri. Rais mstaafu atakuwa hana kitu kipya cha kusema. Ni kwa ajili watu wanafilisika mawazo ndio wanatimuliwa Ikulu( yoyote ya dunia hii).
And besides,kushauri Ina maana kufuatlia events kwa karibu,kwa detail nyingi,jambo ambalo Kikwete hawezi kupata muda.
Na Sukuma Gang wanaotajwa ni kina nani? Huyu Kitwanga ni Msukuma?
Hii sio kuwagawa watu ,kuwaita Sukuma Gang,Msoga Gang? Watu wengine wanaitwa wafuasi wa Magufuli. Wafuasi wa Magufuli vipi? Kuna mfuasi wa Magufuli zaidi ya Samia ambaye alichaguliwa na Magufuli kuwa Mgombea Mwenza?
Kwa hiyo Mama Samia anajitayarisha kuifumua serikali yake,na Kitwanga anazungumza maneno ya tahadhari,Ina maana rais inahofiwa ataivuruga nchi na teuzi zake za kesho au kesho kutwa.
Na kwa nini rais asifanye early retirement leo,ili kesho awatangaze wakuu wa mikoa wapya? Ama sivyo watu kama Kitwanga wataendelea kusema,mwangalieni huyu rais,anataka kutuletea balaa.
Unasema watu wanavyosubiri,wanakwenda kwa waganga wa jadi kutoa kafara?
Kutoa kafara siyo tatizo. Tatizo ni watu wanakutana kila jioni,wanasema,weka bia pale,weka konyagi pale. Haya sasa tumjadili huyu Rais Samia na teuzi zake.
 

Hapa kidiplomasia, Kitwanga amemwambia Rais anafanya mambo hovyo hovyo au anakosea kosea katika mambo yake.

Mara nyingi sana watu wanatumia lugha ya kuwasema vibaya washauri wa Rais ili kumwambia Rais haupo sawa, unakosea.

Wataalamu mnaweza kunisahihisha.
Mkuu,

Hili jambo nilishawahi kulisema kitambo sana hapa.

Watanzania wanamuheshimu sana rais, hususan CCM.

Wengi hawawezi kusema hapa rais kakosea.

Watakachosema ni hiki kimsemo cha "Rais anania nzuri ila washauri wake wanamshauri vibaya".

Ukifungua code hapo kwa kanuni za Rais wa zamani wa US Harry Truman za "The Buck Stops With Me" kama kanuni ya kirais, hata kama ni kweli rais anashauriwa vibaya, rais kukosa mfumo wa kuchekecha ushauri na kukataa ushauri mbaya inaonesha rais mwenyewe analkosea.
 
Sukuma Gang wanapita kipindi kigumu sana dadeq zao
Si Kweli,

Wananchi maskini wenye kupokea ujira wa siku chini ya 10,000 ndo wanapitia Hali ngumu.

Kibarua wa kiwandani anaelipwa 7000 per day ndo anasota.

Anunue Mchele 3,500, sukari kilo 3000, mkaa 2000, kibiriti 100, mafuta ya kupikia Lita 6000, Kodi ya nyumba 50,000 Kwa mwezi, maji 10,000 Kwa mwezi, sabuni mche 3000, luku 5000,nk nk.

Ni wananchi ndo wanasota, ktk makundi ya WAKULIMA, biashara, waajiriwa, vibarua nk.
 
Huyaoni matatizo ya mama yupi?
Au mama yako mzazi?

Nchi ya watu milioni sitini,unataka watembelee unavyojisikia wewe?

Na tutajuaje kama anaowasema kitwanga ndio kina wewe?

Shat ap [emoji67]
View attachment 2527543
Voicer:
Shirikisha ubongo wako japo kidogo, muacheni Mama yetu mpendwa, mama shupavu, mama wa shoka na Jemedari wetu Mkuu, Dr. Samia Suluhu Hassan apige kazi yake vyema ya kuiletea nchi yetu maendeleo

Tumewazoea nyie, kila kitu ni kulalamika tu Kitwanga wenu huyo ana nini cha maana, nchi iliwashinda kuendesha alafu leo anatwambia nini

Kipindi chao walijawa viburi sana, akina sie nani alitujua? Muacheni jamani leo natembea kifua mbele nikijiamini ndani nchi yangu bila shida yoyote.
 
Rais anaweza kuonekana dhaifu lakini anapoamua kushughulikia watu kwa mamlaka yake huwa tunakuja humu jukwaani na kuanza kulialia tukisema rais huyu ni dikteta,

Hayati JPM aliamua kutokuwa dhaifu na mpaka miaka miwili akiwa kaburini bado wapo watu wanaoulalamikia uongozi wake.

SSH sio dhaifu kama tunavyodai, ameruhusu uongozi wake uheshimu demokrasia na amewapa watu uhuru wa kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu.
Samia ni dhaifu mno,she's misfit to the position!
 
Kitwanga anasema kuna kundi ambalo limejipenyeza kwa rais na kila mahala linamshauri vibaya Rais.

==========


WAZIRI wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, amesema kuna kundi linalomzunguka Rais Samia Suluhu Hassan ambalo limekuwa likiweka vigingi kwa watu, wakiwamo wataalamu, wanaotaka kushauri kuhusu mambo mema ya kuipeleka nchini pazuri zaidi.

Kitwanga amesema mbali na kuweka vigingi kwa watu wenye nia njema, kundi hilo limekuwa likiwaona tishio, hivyo kuwachafua, ili kulinda masilahi binafsi. Amemwomba Rais kuwa makini na kundi hilo.

Kitwanga alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo mbalimbali yanayoendelea nchini na kwamba ameona kuna umuhimu wa kumshauri Rais Samia kupitia vyombo vya habari.

Alisema kundi hilo limejipenyeza katika kila sekta zikiwamo taasisi za umma na kwamba lengo lake ni kuharibu nchi kwa maslahi binafsi.

Chanzo: Nipashe
Niliiangalia intavyuu, alikuwa amelewa chakari
 
Kitwanga anasema kuna kundi ambalo limejipenyeza kwa rais na kila mahala linamshauri vibaya Rais.

==========


WAZIRI wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, amesema kuna kundi linalomzunguka Rais Samia Suluhu Hassan ambalo limekuwa likiweka vigingi kwa watu, wakiwamo wataalamu, wanaotaka kushauri kuhusu mambo mema ya kuipeleka nchini pazuri zaidi.

Kitwanga amesema mbali na kuweka vigingi kwa watu wenye nia njema, kundi hilo limekuwa likiwaona tishio, hivyo kuwachafua, ili kulinda masilahi binafsi. Amemwomba Rais kuwa makini na kundi hilo.

Kitwanga alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo mbalimbali yanayoendelea nchini na kwamba ameona kuna umuhimu wa kumshauri Rais Samia kupitia vyombo vya habari.

Alisema kundi hilo limejipenyeza katika kila sekta zikiwamo taasisi za umma na kwamba lengo lake ni kuharibu nchi kwa maslahi binafsi.

Chanzo: Nipashe

Yeye wakati akiwa Waziri alimshauri nn JPM? Je Alimshauri vizuri? Hata baada ya kutimuliwa uwaziri, kwanini hakuita waandishi wa habari na kusema watu walikuwa wanapotezwa, kuuawa, watu walikuwa wanaokotwa kwenye masulfate, kuporwa mamilioni na serikali ya JPM wazi wazi, bureau de change kuvamiwa na fedha kuchukuliwa na kikosi cha JPM.. Na mambo ya ajabu ajabu kumtumia Musiba kuwatukana watu, etc etc

Kitwanga hana kabisa legitimacy & sifa ya kumshauri Mh. Rais Samia..
 
Taasisi haijengwi na majengo au vitabu ni watu. Pole kama hulijui hilo. Na lazima wawe na kiongozi na kwa mfumo wa katiba yetu hilo ni jukumu la Rais pekee mpaka hapo tutakapo amua vinginevyo.
Ukimuuliza watu gani, anaweza dai tubadilishe Katiba tuweke Wazungu, kana kwamba wao ndio Taasisi.

Fikra na mawazo yabadilike. Tulipiga hatua nne tumerudi tatu.

Hatahivyo, hiyo moja tunaona matunda yake ingawaje wanaosuasua hawakubali. Makusanyo na mapato ya kodi ni juu n.k Vyama mbadala vinanyooka.
 
Labda naye Rais ni mwanakikundi. Lakini huyu ni mlevi, si wa kumtilia maanani.
 
Hapana, si kweli, labda kwenu tu.

Upanga tulikuwa na duka la baba Taybal, kulikuwa na duka la wahindi nimewasahau jina Four Flats jeshini watoto wa Muhimbili Primary tulikuwa tunakwenda kununua Peramaziwa.

Uswahilini kulikuwa na maduka ya watu binafsi. Hayakuwa mengi kama sasa lakini yalikuwapo.

Mkuu hii habari imeandikwa na Shivji katika kitabu chake "Development As Rebellion: A Biography of Julis Nyerere" si habari ya vijiweni.
Una umri gani?
Unajua RTC?
 
Kwamba Hadi yule Mzee asiye na wizara maalum naye anatoa ushauri mbaya au anashauri bt hasikizwi?

Maombi juu ya nchi, viongozi na KANISA ndo yatalitoa Taifa letu ktk mkwamo tuliopo.

Amen
Hao ndio wamechoka. Wanaongea ni wajumbe tu.
 
Yani rais hata kama kweli anashauriwa vibaya, akiukubali ushauri, kosa ni lake.

Rais anatakiwa kuwa na njia za kuhakiki ushauri anaopewa.

Nyerere alishauriwa na washauri wake ataifishe maduka yote, yani maduka yote mpaka ya Uswahilini yawe ya ushirika au chama.

Akamfuata Mzee mmoja anaitwa Songambele, Mzee wa Dar tu wa chama, yani hakuwa hata katika washauri rasmi wa rais. Lakini Nyerere alimfuata kama Mzee wa kitaa anayeyajua mambo ya kitaa.

Nyerere akamwambia Mzee Songambele, nimeshauriwa hivi na washauri wangu, kwamba tuyafanye maduka yote yawe ya umma, unaonaje?

Mzee Songambele akamwambia chonde chonde usifanye hivyo baba, tutaadhirika mtaani, wenyewe tunajua tunavyojistiri kwenye viduka vyetu hivi, usifanye hivyo. Hao washauri wako hawajui maisha ya mtaani.

Nyerere akautupa ushauri aliopewa na washauri wake wasomi, akaenda na maneno ya Mzee Songambele, Mzee wa Dar ambaye yuko connected kitaa.

Hapo utaona rais kajiwekea namna ya kuhakiki ushauri anaopewa, hakubali kila kitu anachoshauriwa.

Rais akikubali ushauri mbaya, kosa ni la rais, kwa sababu rais anatakiwa kuhakiki ushauri kabla ya kuukubali.
Ahaa kumbe Mwanamvua hana uwezo wa kuhakiki...
Ndio maana basi mambo hayaeleweki....
 
Nadhani wanachukua reference kwenye management ya mfumko wa bei ya mazai ya chakula. Kimsingi haitakiwi serikali kupuuzia uwezo wa wananchi wake kupata chakula kwa bei inayohimilika. Mfumko wa bei ni kati ya maeneo yanayomgusa mtu wa chini kabisa ambaye ndiye mpiga kura halisi kwa nchi hii(by observation and experience).
Swala lingine ni management ya mikopo inayokopwa kutoka nje. Inapelekwa wapi? Mimi binafsi sina shida na nchi kukopa lakini tatizo langu ni inaelekeza wapi mikopo inayokopa?
Eneo lingine muhimu kulingazia ni initiatives zinazoendelea ndani ya Shirika la Umeme Tanesco. Kwa majina ni matamu lakn je usimamizi ukoje?
Mfano Trilioni 4 zilizoahidiwa, zimeelkezwa wapi? T 11 zilizoombwa zinaelekezwa wapi?
Je, kipande cha SGR cha Tabora kwenda Mpanda, ni nani huyo aliyeahidi kukijenga halafu tukatane akipitisha bidhaa zake? Ni bidhaa gani hizo?
Je, nani huyo aliyejitolea kutujengea barabara ya kulipia kutoka Dar hadi Morogoro? Na tumejiuliza maswali muhimu kwa miundo mbinu muhimu kama hizo kujengewa kwa kulipia baadaye?
Je, kuwahamisha wamaasai kutoka Ngorongoro nao ulikuwa ushauri mzuri? Tafiti zimeheshimiwa?
Na, je proposal yake ya kutaka mchakato wa ajira urudi kwa mashirika. Najua alisema kuhusua ajira za muda kama za REA na Tanesco kwa miradi maalum lkn One can read the tone. Anataka ajira zirudi kwa mashirika na taasisi badala ya kufuata mtiririko kupitia UTUMISHI. Nani anamshauri mazaa baadhi ya vitu?
Nchi haiendesheki bila Bureaucracy.
Ndani ya serikali, inatakiwa kama jambo linahitajika let say July, basi mchakato wake uanze January. UTUMISHI na sekretariat ya ajira hawacheleweshi. Mashirika na taasisi wanachelewa kuomba wenyewe.
Mama asielekeze nchi kwenye ubanana republic au laisez affair capitalism.
 
Back
Top Bottom