Kocha wa Makipa Simba SC na wengine 8 wakamatwa na Dawa za Kulevya
Hebu wataje wafanyabiashara wakubwa watano wa kitanzania wenye fedha safi na halali. 😂😂. We taja tu. Uzuri humu jf wapo watu wazima wenye mafaili mengi ya watu 😂😂😂 hebu wataje watano tu 😂
Wa kutaja ni wewe unaesema wana makando kando na sio mimi mkuu.

Wote ambao serikali haijawatia mkononi basi biashara zao ni halali, huu unazi wa kuendekeza kua ili uwe tajiri lazima ufanye biashara haramu sijui mmeutoa wapi.

Hiyo ni mentality ya kivivu, kutaka shortcut. Na hii sio kwa hawa matajiri wakubwa tu hata wale wanaojiweza kitaa mnawananga kua ni wachawi, majambazi nk.
Acha uvivu mzee, tafuta utajiri.
 
Twende mbele, turudi nyuma. Jamaa kafaidi like tako 😂😂. Na binti wa watu kawa muislamu kabisa na kaacha kupost tako mtandaoni. 😂😂😂😂. Mwamba kafaidi kwelikweli na inasemekana alimtia mimba na kuzaa nahisi tayari. 😂😂
Kwa kweli jamaa kafaidi ndio raha yenyewe hiyo mwanawane. Ate hela ule warembo maana warembo wenyewe hawan upendo wabachotaka ni hela tuu
 
Wa kutaja ni wewe unaesema wana makando kando na sio mimi mkuu.

Wote ambao serikali haijawatia mkononi basi biashara zao ni halali, huu unazi wa kuendekeza kua ili uwe tajiri lazima ufanye biashara haramu sijui mmeutoa wapi.

Hiyo ni mentality ya kivivu, kutaka shortcut. Na hii sio kwa hawa matajiri wakubwa tu hata wale wanaojiweza kitaa mnawananga kua ni wachawi, majambazi nk.
Acha uvivu mzee, tafuta utajiri.
Naomba unisamehe sana, tajiri. Nimekosa sana mkuu 🙏
 
Na El Chapo aliwahonga kweli hadi rais wa nchi [emoji28][emoji28][emoji28]
Sasa mwanawane shipment moja kama hiyo tayari ni billion 24 nashindwaje kuhonga rais.

Wee jamaa ana jeshi lake kabisa na vifaa vya kivita kabisa, military grade amunition unashindana nae vipi.
Mie bwana nasema tuu wacha vijana wapambane kama mtu anaona anaweza tokea huko wacha afanye tuu maana hawa tunaotegemea kufight hiyo vita wenyewe wanaendesha hiyo biashara
 
Meki alikuwa anakula million kumi kwa mwezi ajabu sana
Kwa lile Bata la Wachezaji wa Cambiaso Soccer Academy, Hadhi yao na Mengineyo sishangai leo kusikia kuwa kumbe Mmiliki ni Drug Baron na anashirikiana na Watu wengine.

Shikamoo sana Kocha wa sasa wa Kagera Sugar FC Mecky Mexime ( ambaye ulikuwa Kocha wa Cambiaso Soccer Academy) kwa kuwa Mjanja, Kushtuka, kutoa Ushirikiano na kusepa Mapema kabka ya Msala Kukukuta.
 



Watuhumiwa tisa akiwemo Kocha wa Makipa wa Klabu ya Soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam Muharami Said Sultan wanashikiliwa na Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya kilo 34 aina ya heroin.

Akizungumza leo Jijini Dar Es Salaam Novemba 15, 2022 Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Kusaya amesema Mamlaka hiyo imekuwa ikifanya operesheni maeneo mbalimbali nchini kuanzia Oktoba hadi Novemba mwaka huu na kufanikiwa kukamata watuhumiwa wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Akifafanua zaidi Kamishina Jenerala Kusaya amewataja wanaoshikiliwa kwa tuhuma hizo ni Kocha wa Makipa wa Simba Muharam Said Sultani(40) mkazi wa Kigamboni na kufafanua kwamba Muharam amewahi pia kuichezea timu ya Simba.

Wengine ni Mfanyabiashara na Mmiliki wa Kituo cha Soka cha Cambiasso Sports Academy kilichopo Tuangoma wilayani Kigamboni Alhaj Kambi Zeber Seif maarufu kwa jina la Kambiasso au Alhaj Kambi mbali ya kumiliki kituo hicho cha soka ana miliki kampuni ya Safia Group of Companies inayomiliki magari ya kusafirisha abiria (daladala) kutoka Dar es Salaam kwenda Mkoa wa Pwani.

Pia Mamlaka hiyo inamshikilia Said Abeid Matwiko ambaye anaishi Magole A Kivule na kazi yake ni fundi selemala,mwingine ni Maulid Mohamed Mzungu maarufu kwa jina la Mbonde (54) mkazi wa Kisevule ambaye kazi yake ni mkulima.

Amewataja watuhumiwa wengine ni John Andrew John (40) mkazi wa Magore-Kitunda ambaye ni mfanyabiashara na amekuwa na jukumu la kutafuta vijana wenye vipaji na kuwapeleka kituo cha Soka Kambiasso, Pia wanamshikilia Seleman Matola Said(24) mkazi wa Temeke –Wailes Matola ni mtoto wa dada yake na mtuhumiwa Alhaj Kambi.

Mwingine ni Hussein Mohamed Pazi(41) mkazi wa Kibugumo wilayani Kigamboni ambaye ni mfanyabiashara na mtuhumiwa wa tisa ni Ramadhan Rashid Chalamila(27)ambaye ni mfanyabiashara. “Watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani wakati wowote kuanzia sasa.

You gonna be rich ask me
Waves-endless-ocean-gif.gif
 
Mwarami Said Mohamed Sultan mchezaji wa zamani wa Taifa Stars, Simba SC, Clube Ferroviário de Maputo ya Mozambique pia Ferroviario za Pemba na Nampula zote za Mozambique.

AT THURSDAY, NOVEMBER 26, 2009

Huyu ndiye kipa mpya wa timu ya taifa ya bara a.k.a Kilimanjaro Stars Mohamed Mwalami anayechezea klabu ya Ferroviaro ya Maputo, Msumbiji. Anachukua nafasi ya kipa Shaaban Dihile ambaye ametemwa.

Kipa mwingine ni Shaaban Kado wa Mtibwa Sugar. Kwa habari kamili ya kikosi kinachoondoka asubuhi hii kuelekea Kenya kwenye michuano ya Chalenji inayoanza Jumamosi 28, 2009.​

18 Jul 2014​

KIPA SIMBA SC ABWAGA MANYANGA​

Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
KIPA wa zamani wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya Simba, Mwarami Mohammed ‘Shilton’ amestaafu soka na sasa anataka kuwa kocha.

Mwarami mwenye umri wa miaka 35, amesema kwamba ameona bora kutungika glavu zake kwa heshima kwa sababu umri umeenda.

“Nimecheza kwa muda mrefu, tangu mwaka 1997 nacheza Ligi Kuu, ni miaka mingi na ninaona mwili umechoka. Ni wakati wa kupumzika kwa heshima sasa,”amesema.
Mwarami Mohamed amestaafu soka
Mwarami amestaafu akiwa anachezea Ferroviario de Maputo ya Msumbiji ambayo alijiunga nayo baada ya kuchezea Ferroviario za Pemba na Nampula.

Kabla ya kwenda Msumbiji, nchini Tanzania, Mwarami alichezea timu za Coastal Union ya Tanga, Simba SC ya Dar es Slaam, Kariakoo United ya Lindi na Reli Morogoro.

“Nataka kuwa kocha, nimeanza kuafuatilia vyuo vya kwenda kusomea ukocha, lakini kwanza nitapata kozi za awali hapa hapa nchini kwa kuanzia,”alisema


15 November 2022
TAARIFA YA SIMBA SC : MWARAMI MOHAMED SIYO MWAJIRIA WA SIMBA SC

 
Jidanganye Mo ni tapeli mzoefu toka enzi ya ubinafsishaji. Zile mali ni umafia wa Baba yake Gulamabbas na mjomba wake Azim. Tafuta wazee wa zamani wakupe mkanda mzima wa umafia wa familia ya akina dewji [emoji23][emoji23][emoji23]
Baba yako alikuwa wapi muda huo?
 
Back
Top Bottom