Kudai Israeli ni Taifa la Mungu huku Wayahudi wakimkaata Yesu, ni ushahidi hizi dini zimejaa uongo mwingi

Kudai Israeli ni Taifa la Mungu huku Wayahudi wakimkaata Yesu, ni ushahidi hizi dini zimejaa uongo mwingi

Imani inafanya watu wasihoji, na ndio maana hata Wafuasi wa Kibwetere hawakuhoji matokeo yake wakaangamia.
Suala la msingi ni kwamba imani ipi?

Imani ya Ukristu inamhitaji muumini aelewe na kuhoji kile anachofundishwa, kabla hajaridhia kukifuata.

👉 Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza Maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. -Matendo ya Mitume 17:11

Dini yoyote inayosomesha imani dufu -- kufuata tu bila kujua sababu ya fundisho husika -- ni utapeli.

👉 Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. -1 Petro 3:15
 
Kabla sijaenda mbali, kwanza nikiri mimi ni Mkristo ila Ukristo wangu sio sababu ya kutohoji hata kama mtasema imani yangu ni ndogo.

Tukirudi kwenye mada, huku kwetu ukimpinga Kristo, hutaeleweka na utachakuliwa kuwa ni mwenye dhambi na unatahiili kuombewa.

Hata hivyo, cha kushangaza ni sisi sisi tunaodai Israel ni Taifa telule la Mungu huku Wayahudi wakiwa hawamkubali Yesu na wengi wa hao Wayahudi wameukaa kristo. Ajabu sana!

Kwa kifupi, jambo hili linaweza kuwa ni ushahidi tosha kuwa katika hizi dini, kuna mambo ya kutunga katika hivi tunavyovitta vitabu vitakatifu na huenda ni maandiko/aya zote ni uongo au baadhi ya maandiko/aya ndio za uongo .

Pia, nawaza,Tulia watanzania wengi hawamkubali, lakini huko nje ya nchi wamemkubali na kumpa cheo kikubwa tu. Je, ndio yale yale ya Wayahudi kumkataa Yesu na sisi huku kumkubali kama Mwana wa Mungu?

Hakika maswali ni mengi kuliko majibu.
Nina mashaka na uislam kushikamana sana na waarabu, ukiwa na free mind lazima uone utata.
 
kasome kwanza bible usiwe kama andazi.

bible imeandika wazi,Yesu alikataliwa na hao wayahudi,ndio sababu hata ya kuuawa kwake.
"Yesu alikataliwa na hao wayahudi" sasa hili taifa teule limetokea wapi?
Enyi wagalatia jitafakarini!!!!
 
Tatizo ni wapokeaji wenyewe au aina ya dini au namna dini husika ilivyofikishwa kwa watu.

Historia iko wazi kwamba mahali popote ambapo Ukristu halisi ulipenya, watu walipata maendeleo makubwa na kwa kasi sana.

Wanasayansi, wanasiasa, wasomi, wanasanaa na viongozi mashuhuri asilimia kubwa msingi wa mafanikio yao ni Ukristu.

Ulaya na Marekani ni mifano miwili.
Unaposema “misingi ya mafanikio yako ni ukristo” unamaanisha kitu gani?

Fuatilia vyema utafahamu mifumo yote ina watu wenye mafanikio na walioleta mabadiliko makubwa duniani.

Iwe ni Christians, Muslims, Budhas, Hindus, Chinese etc etc.

Fuatilia, kama hujui uliza.
 
Sikuhtaji kusoma content ya trd...!
Tangu nifahamu ya kwamba YESU alizaliwa nazareth na alisurubiwa btrhem na bado mpaka leo wakazi wa huko uyahudini hawamwamini na kumtukuza YAHWE wamapokeo!!?, nikajiona mi ni mjinga sana kutukuza elimu ya nadharia ingali imeelekeza chimbuko ni wapi lakini kulekule chimbukoni wanaidis na kuikataa!!!
Huu ni UZWAWA!!

Halafu bado hadi leo hii kuna wajinga wanaendelea kutuaminisha eti Israel taifa teule na wanaenda kuhiji na kutoa sadaka!!

Kumbe ndo maana wazungu wanaendelea kuja AFRICA na mikataba yao ya KIPUMBAVU coz wanapitia mlemle kwenye akili za mababu zao kwamba bado tumelala!!!

Na Bethlehemu na Nazareth na pia Galilaya nadhani ni miji ipo upande wa Palestina kwa ramani ya sasa hivi! Damascus ya kwenye biblia ipo Syria, Jangwa la Sinai lipo Misri, Babylon ipo Iraq.
 
Ukristo umetungwa baadae xn baada ya yesu mwili wake kuacha dunia.
Mafundisho yote muhimu yajengayo msingi wa imani ya Ukristu, Mwana wa Adamu aliyafundisha kikamilifu kwa muda wa miaka 3.5 akiwa na wanafunzi 12++

👉 [18]Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

[19] Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

[20] na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, Mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. ~Mathayo 28:18-20
 
Point yangu ni kuwa matatizo ya Africa yanaletwa na sisi Waafrika wenyewe. Wazungu walitufanyizia na wameshaondoka ila watawala wengi wa kiafrika wamegeuka kuwa wakoloni weusi.
Kwani mimi kuna sehemu nimesema matatizo yetu waafrika yameletwa na wengine?

Ndo maana nimesema utumwa wa kinguvu uliisha, lakini upo wa ki hiyari na pia “mental slavery”

Utumwa wa kiakili umechangia kwa kiasi kikubwa zaidi kwenye hali iliyopo Africa hususan viongozi wale ambao nao ni zao la wananchi wenyewe.
 
Jewish people ! Jews ! = wayahudi !
They believe in Moses = Musa !
They have unique believe rather/more than what proclaimed of moses miracles!
Musa alipomkabidhi Haruni kuwaongoza wakimbizi, ilifikia hatua jamaa(Haruni) alishindwa kuwadhibiti kuumba/kuchonga masanamu ambayo hao wakimbizi(wanaIsrael-mayahudi) wanayatukuza na kuyaamini hadi leo ikiwemo Sanduku la Agano.
Halafu sisi wamatumbi tumeizika na kuikataa mizizi yetu ya mibuyu, mironge, mikwizingi, minyaranyanyara, miarovera, midimu, mikunungu, mikuzwingi, minangari na migagani
 
Kabla sijaenda mbali, kwanza nikiri mimi ni Mkristo ila Ukristo wangu sio sababu ya kutohoji hata kama mtasema imani yangu ni ndogo.

Tukirudi kwenye mada, huku kwetu ukimpinga Kristo, hutaeleweka na utachakuliwa kuwa ni mwenye dhambi na unatahiili kuombewa.

Hata hivyo, cha kushangaza ni sisi sisi tunaodai Israel ni Taifa telule la Mungu huku Wayahudi wakiwa hawamkubali Yesu na wengi wa hao Wayahudi wameukaa kristo. Ajabu sana!

Kwa kifupi, jambo hili linaweza kuwa ni ushahidi tosha kuwa katika hizi dini, kuna mambo ya kutunga katika hivi tunavyovitta vitabu vitakatifu na huenda ni maandiko/aya zote ni uongo au baadhi ya maandiko/aya ndio za uongo .

Pia, nawaza,Tulia watanzania wengi hawamkubali, lakini huko nje ya nchi wamemkubali na kumpa cheo kikubwa tu. Je, ndio yale yale ya Wayahudi kumkataa Yesu na sisi huku kumkubali kama Mwana wa Mungu?

Hakika maswali ni mengi kuliko majibu.
😆😆😆😆
 
Ukatoriki ulifikaje Rome-Italy na kuwa dhehebu la kwenye ukristo.
Anglican wamekuaje waingereza na ni christians.
Lutheran pia nao ni vipi.
Mwamposa, Gwajima, Mzee wa upako nk wanatofauti gani na hao wengine kuanzia Vatican mpaka pale church of London.

Biblia imeanzia pale mashariki ya kati Israeli, na biblia hiyohiyo inasema Israeli ndio Taifa teule.. na sio Tanzania wala Kenya..

Yaani Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi atuumbe wooote na mataifa yetu halafu aibariki Israeli na waIsraeli.
Nimejaribu kukuelewa, ila nimeshindwa. Maana haionekani kama unauliza au unajibu.

Ni kama sentensi zako zinauliza, lakini mwishoni hakuna kiulizo. Sasa hapo ni ngumu sana kueleweka.

Kinachoshangaza zaidi, wadau wamekufurahia. Sijui wanafurahia vile ambavyo umeandika sentensi tata au la?
 
Salary Slip:

Kwa nini usiende kwenye source? Mkuu Salaery Slip. ni aibu kama wewe Mkristo unashindwa kupata majibu yako toka kwenye Biblia, hii sio kwako tu, ni kwa muumini wa dini yoyote ile, nikiwa Mwislamu lazima niitee dini yangu toka kwenye source yake, yaani Quran..

Watu wengi dini wamerithi tu, kwa vile wazazi walikuwa Wakristo basi ndio umekua Mkristo, au kwa sababu Wazazi wangu ni Waiislamu na mimi ni Muislamu.....kwa njia hii watu wengi ni very shallow mno katika Imani zao.

Mkuu Salary Slip, just take your time go to the source, Bible......start with the New Tastement.....itajibu kirahisi majibu yako!

Kuna vitu vya msingi katika imani ya Kikristo unavikosa. Jibidishe, ili kujijengea ufahamu katika imani yako.

Maswali machache na mafupi ya kawaida:

1) Kwa kadiri ya maandiko, Waisrael waliwahi kuadhibiwa na Mungu kwa kwenda kinyume na maagizo yake, mara ngapi?

2) Mara ngapi baada ya Waisrael kumkosea Mungu, na kisha kuadhibiwa kwa kupigwa na maadui zao, na hatimaye kutiwa utumwani, aliwatumia manabii, na kisha waisrael baada ya kukiri uovu wao na kumrudia Mungu, aliwaokoa kwa mkono wenye nguvu na ushindi mkubwa dhidi ya maadui zao?

3) Kwa kadiri ya maandiko, kutokana na uovu na makosa yao, je, kuna wakati Mungu aliwahi kuwaambia Waisrael kuwa kwa sababu ya kosa hili, kuanzia leo ninyi siyo Taifa teule?

4) Kwa kadiri ya maandiko, hata sisi tusio Waisrael, mara ngapi tumeanguka katika dhambi? Je, kuanguka kwetu katika dhambi, kumetufanya tusiwe wana wa Mungu?

5) Ukisoma biblia vizuri, maneno mengi ya manabii na Masiha Yesu, amezungumza sana juu ya Wayahudi kutompokea Masiha, na hivyo Mungu kuwaadhibu kutokana na kosa hilo. Anazungumzia juu ya mfalme kuwatuma watumishi (manabii), lakini wayahudi kuwakataa; kisha kuamua kuwatumia mtoto wake (Yesu) akitarajia watamheshimu na kumsikiliza, lakini wakaamua kumwua. Na anawauliza, je mfalme atawatenda nini watu wa namna ile? Nao wanajibu kuwa atawaangamiza. Kiimani, hata yale ya kuangamizwa na Hitler au Hamas, yaweza pia kuwa adhabu ya Mungu kwaajili ya kumkataa masiha. Kwa kadiri ya unabii, kuna siku watamkiri Kristo, na utakuwa mwisho wa mateso na maangamizi yao.

Ni sawa na mfalme, awe na wanawe wakorofi. Wakiwa wakorofi anaweza kuwakasirikia. Akiwa amewakasirikia, ninyi wengine mtaonekana ni wazuri kuliko wanawe watukutu. Lakini ninyi wengine, mkafanya jitihada ya kuwabadilisha watoto wale, hata wakarudia katika hekima, mfalme atawashukuru sana hawa waliowasaidia watoto wake hadi wakarudi katika kujitambua. Baada ya watoto wale kurudi katika hekima, ni dhahiri nafasi yao bado itakuwa ya juu kuliko ninyi mliowasaidia hata wakawa watu wema, na si ajabu wale waliowasaidia watoto hawa kurudia katika hekima wakapata thawabu kubwa kwa kazi hiyo njema, kuliko waliowatendea uovu wakati wa kipindi chao cha uovu.
Ina maana mmeshindwa kumuelewa mleta mada ya kuwa ametambua chanzo cha huu uwongo umeanzia kwenye hiyo bibilia mnayomtaka akaisome tena....
Ukiwa na akili timamu ya utashi wa kujitambua kama binadamu lazima utatambua kuwa dini zote ni pilika za wajanja ambazo watu weusi mmeshupaza shingo kujifanya mnazijua kuliko waliozileta mpaka wanawaonea huruma kwa misaada ya kila kukicha.....
 
Shida watu wakipata pesa kidogo au wakiwa na afya njema huwa hawaoni uwepo wa Yesu wala Mungu subiri awe kwenye shida, hata Babu Oseya(mwanamziki) wakati yupo gerezani alituma ujumbe kuwa siku akitoka gerezani atamtukuza MUNGU na kumtumikia lakini baada ya kutoka akarudi kule kule. Lisu alipigwa risasi 38 lakini hakufa hapo hapo kuna watu wakipigwa hata na manati wanakufa.

Sasa mambo ya akina Lissu yanaingiaje kwenye mada hii? Duh!
 
Shida watu wakipata pesa kidogo au wakiwa na afya njema huwa hawaoni uwepo wa Yesu wala Mungu subiri awe kwenye shida, hata Babu Oseya(mwanamziki) wakati yupo gerezani alituma ujumbe kuwa siku akitoka gerezani atamtukuza MUNGU na kumtumikia lakini baada ya kutoka akarudi kule kule. Lisu alipigwa risasi 38 lakini hakufa hapo hapo kuna watu wakipigwa hata na manati wanakufa.

Wengine waseme risasi 16 ikiwa ni pamoja na Yeye Lissu mwenyewe alisema, leo tena zinakuja risasi 38, kesho tutaambiwa risasi 200 yote mradi ni kumkuza mtu! Mimi najua hata tembo tu angepigwa risasi tano angekufa hapo hapo, sembuse binadamu apigwe risasi 16 au 38 mnazotuambia abaki? Na wakati dereva aliyekuwa naye hapo hapo jirani kwenye gari isimpate hata risasi ya kumparua hata mguu au mgongo tu? Mimi ningekuwa nachunguza hili tukio ningekomaa kwanza na huyo dereva!
 
Dini hizi ni utapeli mtupu!

Zimelifanya bara la Africa kuwa bara la hovyo kuliko yote na watu wake hovyo zaidi.
Waliokuwa brainwashed watakupinga ila unasema ukweli mtupu, turudi imani zetu za kale..
 
ukielewa maana ya imani,utagundua kuhoji ni dalili ya ugonjwa wa akili.

imani inakuelewa uamini Mungu aliumba mtu kwa matope,akawaje na nyama??huhoji hili wewe mbioooo mpaka kwenye uteule wa israeli.

bangi bila msosi.
Hapo tatizo siyo kuhoji, bali majibu unayopewa.

Kwa mfano, sayansi ikikwambia umetokana na nyani, hapo utaelewa nini?

Ni lazima tukiri kwamba kuna mambo tusiyoweza kufafanua kibinadamu, na hapo ndipo tunakutana na imani katika miujiza ya Mungu.
 
Wengine waseme risasi 16 ikiwa ni pamoja na Yeye Lissu mwenyewe alisema, leo tena zinakuja risasi 38, kesho tutaambiwa risasi 200 yote mradi ni kumkuza mtu! Mimi najua hata tembo tu angepigwa risasi tano angekufa hapo hapo, sembuse binadamu apigwe risasi 16 au 38 mnazotuambia abaki? Na wakati dereva aliyekuwa naye hapo hapo jirani kwenye gari isimpate hata risasi ya kumparua hata mguu au mgongo tu? Mimi ningekuwa nachunguza hili tukio ningekomaa kwanza na huyo dereva!
Sema wewe sasa alipigwa ngapi? au alikatwa na mapanga?
 
Ina maana mmeshindwa kumuelewa mleta mada ya kuwa ametambua chanzo cha huu uwongo umeanzia kwenye hiyo bibilia mnayomtaka akaisome tena....
Ukiwa na akili timamu ya utashi wa kujitambua kama binadamu lazima utatambua kuwa dini zote ni pilika za wajanja ambazo watu weusi mmeshupaza shingo kujifanya mnazijua kuliko waliozileta mpaka wanawaonea huruma kwa misaada ya kila kukicha.....

Technocrat :

Hajaanzia kwenye Biblia Mkuu, kama angeanzia kwenye Biblia hilo swali lake angeli frame tofauti kabisa! Amekiri ni Mkristo, Mkristo gani hata hajui ABC ya imani yake? Hajakiri kabisa Biblia imemchanganya.......

Hiyo hoja yako haya dini zote ni pilika pilika za wajanja....hiyo ni mada tofauti mkuu......Mababu zetu walikua na dini zao za asili ....nani mjanja aliyewaanzishia hizo imani....hiyo ni mada tofauti mkuu....Maana itabidi tuanze Antropology 101...Uone imani ya dini kwa mwanadamu ilivyo sehemu ya mwanadamu.
 
Onyesha ushahidi

Kasome kwenye tourati ndiyo utagundua kuwa Wayahudi wanamkataa Yesu kwa kusisitiza kuwa Yesu siyo mwana wa Mungu kwa vile Mungu hakuzaa mtoto na pia hakuna kitu kinaitwa utatu mtakatifu. Hiyo ni tosha kabisa kujibu swali lako. Pia wanakuambia Yesu siyo Mungu.
 
Sikuhtaji kusoma content ya trd...!
Tangu nifahamu ya kwamba YESU alizaliwa nazareth na alisurubiwa btrhem na bado mpaka leo wakazi wa huko uyahudini hawamwamini na kumtukuza YAHWE wamapokeo!!?, nikajiona mi ni mjinga sana kutukuza elimu ya nadharia ingali imeelekeza chimbuko ni wapi lakini kulekule chimbukoni wanaidis na kuikataa!!!
Huu ni UZWAWA!!

Halafu bado hadi leo hii kuna wajinga wanaendelea kutuaminisha eti Israel taifa teule na wanaenda kuhiji na kutoa sadaka!!

Kumbe ndo maana wazungu wanaendelea kuja AFRICA na mikataba yao ya KIPUMBAVU coz wanapitia mlemle kwenye akili za mababu zao kwamba bado tumelala!!!
Unangoja hadi wengine waamini ndipo wewe uamini?

👉 Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki. ~Yohana 20:29
 
Back
Top Bottom