Kufanya biashara na Watanzania mtandaoni ni taabu sana

Kufanya biashara na Watanzania mtandaoni ni taabu sana

mwingine alikuja inbox maswali mengi nikawa namjibu kama ilivyopaswa.
kaomba na picha za kutosha nikamtumia ile bidhaa ilikuwa juu ya meza. mwisho wa siku ananiuliza "hiyo meza vipi huuzi?"๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ๐Ÿ˜‚

Yaani tutoke kwenye kujadili bidhaa husika tuanze kujadili meza tena.
๐Ÿ˜† ๐Ÿ˜† ๐Ÿ˜†
Unamjibu tu hapana na kumrudisha kwenye point ya msingi.
 
kwa kifupi alivyoniuliza kuhusu meza sikujibu na hakunitext tena. Nahisi aljishtukia.
๐Ÿ˜† ๐Ÿ˜† ๐Ÿ˜†
Unamjibu tu hapana na kumrudisha kwenye point ya msingi.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kuna muda wahindi nawaonaga wana dharau ila huwa nawaelewa muda mwingine. huwa wanataja bei then wanaendelea na mambo yao hawakutazami usoni.

Wabongo pasua kichwa sana.
 
Elimu ya customer care mkuu unamaanisha nini kuweza kuvumilia ujinga wa wengine..

Ili kupunguza maswali unaweka maelezo yote yaliyoshiba tena kwa msisitizo ili mtu akija inbox basi aje kama mnunuzi. kama sio mnunuzi ni alipite tu tangazo.
Huna elimu ya customer care mkuu.
Tuko tofaut na uelewa unatofautiana.
 
Biashara online hata Sellers wenyewe wana mbambamba na ugaigai ,ukijichanganya tu wanasepa na mshiko ,kwahiyo lazima uhoji sana ili kujua kama ni muuzaji kweli au tapeli ,na mara nyingi matapeli hawataki kuhojiwa sana ukimdadisi sana tu lazima apanic.
Kwaiyo mtoa mada ni tapeli?
 
Sijui hata nani kawaloga. Unaweka maelezo yote kamili bei na njia ya mawasiliano etc.

Anakuja mtu anakuuliza maswali ambayo majibu yake kwenye maelezo ulishaweka. Yaani mwisho wa siku ni usumbufu tu. Anakwambia naomba picha zaidi wakati picha za kutosha umeshaweka kwenye tangazo. Mwingine anauliza bei tena wakati bei umeshaweka.

Anakuja anakusumbua maswali kibao mwisho wa siku anakwambia eti niidhani hivi na vile. Una muuliza ina maana maelezo ya bidhaa hukusoma kwenye Tangazo?

Ingawa wateja serious wachache sana pia huwa wapo tena hawanaga mambo mengi ni anakuja tu moja kwa moja anauliza discount na njia ya kuipata.
Au anakumbia kwa sababu nina namba yako nitakutafuta, ukiona hivi jua hakuba munuzi hapo
 
Wauzaji pia sio waaminifu.. ndo maana wateja tunakua na maswali mengi ili kujiridhisha na huduma mkuu..
Imagine kuna mzgo nmeagiza kutoka dar tangu J3 ya wiki iliyopita, ila cha ajabu mpaka leo muuzaji hajautuma.

Uaminifu wenu ni ZERO
Online business huwa na enjoy kufanya na Wazungu na Wahindi basi, wabongo hapana
 
Elimu ya customer care mkuu unamaanisha nini kuweza kuvumilia ujinga wa wengine..

Ili kupunguza maswali unaweka maelezo yote yaliyoshiba tena kwa msisitizo ili mtu akija inbox basi aje kama mnunuzi. kama sio mnunuzi ni alipite tu tangazo.
Mkuu wabongo kwenye online sio kabisa, na bado saaa kwenye Delivery hapo ndio balaaa, anakumbia mfano niletee kuku walio.chinjwa watatu dakika za mwisho ndio unampelekea anakumbia nimepata shida hapa nitachukua mmoja tu au wawili. Acha kabisa
 
Elimu ya customer care mkuu unamaanisha nini kuweza kuvumilia ujinga wa wengine..

Ili kupunguza maswali unaweka maelezo yote yaliyoshiba tena kwa msisitizo ili mtu akija inbox basi aje kama mnunuzi. kama sio mnunuzi ni alipite tu tangazo.
Hata kwenye Delivery hakikisha anakupa pesa kwanza, unaweza juta ni washenzi sana sory
 
Sijawahi kuona wafanyabiashara wapuuzi kama wa Online katika hii nchi! Anaweka product na kazi yake tu ila specifications hamna na bei haweki anataka umpigie simu au uende inbox. Sasa unauza kitu ambacho thamani yake huijui ama! Hii tabia inakera mno mbadilike.
Mimi nisha fanya naweka kila kitu, hadi Delibery freee bado ni changamoto kwa kifupi Wazunvu na Wahindi nawakubali sana,
 
Una tatizo la anger management. Hufai kuwa kitengo cha Customer Service utakuwa unaharibu sana. Kwa msaada zaidi soma types of Customers. Mi ukinilitea mawenge nakupa spana live bila chenga na biashara inakufa.

Jenga mentality mteja ni kama mtoto tu, kuna wanaoelewa fasta na kuna wanaochelewa kuelewa.
Sasa chukulia mfano, Mtu kakupa Oda sawa niandalie lets say kuku watatu uniletee Jumamosi na wachinjwe kabisa, unaandaa na mmeisha kubaliana bei, unashangaa Dakika za mwisho either anakumbia amepepata tatizo la gjafla hachukua wote au unapeleka anataka punguzo tena na mmeisha kubaliana mwanzoa, isha nitokea sina idadi kwa Wabongo ila Wazungu na Wahindi fresh kabisa,
 
Jiwe gizani

Wasumbufu wameguswa hapo juu

Ukiona blue ticks kwenye whatsap yangu unaweza ukaacha kabisa online business

Mtu anakuja na screenshot yenye bei Halafu anakuuliza bei gani?

Umeandika location anauliza unapatikana wapi

Picha umeweka anaomba picha zaidi

Wengine wanaomba mpaka feedback kutoka Kwa wateja wengine [emoji119]
Hili nalo ni tatizo au anataka utaje bei kwa kila anaye coment, mimi huwa nawapotezea mazima yaani anaona wa juu yake umemtajia bei na yeye anataka umtajie kwenye coment yake,
 
Nakiri hili wengi wa wauzaji wana hii shida.
Kingine hawazijui vyema bidhaa wanazo ziuza, hili bila shaka hata upande wa physically umeligundua.

Ila hili nimelizungumzia kwa upande wangu. Unakuta nimeweka kila kitu bayana. lakn kinachonishangaza mtu anakuja kukuuliza maswali ambayo kwenye description nilishaweka.

Kuokoa muda nishanunua vitu vingi online kama maelezo yameshiba basi sinaga mambo mengi ni simu tunajadili bei then mzigo unaletwa.
Au anaomba namba ya simu na umeweka kwenye maelezo
 
Nakiri hili wengi wa wauzaji wana hii shida.
Kingine hawazijui vyema bidhaa wanazo ziuza, hili bila shaka hata upande wa physically umeligundua.

Ila hili nimelizungumzia kwa upande wangu. Unakuta nimeweka kila kitu bayana. lakn kinachonishangaza mtu anakuja kukuuliza maswali ambayo kwenye description nilishaweka.

Kuokoa muda nishanunua vitu vingi online kama maelezo yameshiba basi sinaga mambo mengi ni simu tunajadili bei then mzigo unaletwa.
Au anakuuliza mimi nipo Kigoma napataje? Ukimjibu nitakutumia hutamuona tena,
 
Back
Top Bottom