Kuhusu Katiba Mpya: Hoja ya Rais Samia haina mashiko
Hiyo ya kupoza hapa na pale ni jambo zuri lakini ni short term. Kwa mfano akishamaliza kuondoa Mabaya ya Magufuli then yeye ana nini cha kuoffer?. Ni lazima asimame sasa ajipambanue kwa ujasiri kuonyesha anajua Taifa linahitaji nini. Asiangalie utswala wake wa miaka mitano au Tisa anayoweza kukaa nadarakani. Aangalie miaka 50 au 100 ijayo...
Huenda anaisujudia hii iliyopo kwakua ndio umemfanyia "nipige tafu"
 
Siku 100 mama aanze mchakato wa katiba kweli?!! Mimi sio CCM lakini nakataa.

Mama amekuta nchi imeoza,imefungwa kila kona,inanuka uozo,ni lazma aifungue kwanza,aanze kuitibu ndipo mambo mengine yafuate.

Katiba mpya sio wapinzani au watanzania tu wanaitaka ila hata mama mwenyewe SSH ni muhimu kwake kwa manufaa ya nchi yake Zbar. Zbar haina tofauti na jimbo ndani ya nchi, haina maamuzi yake yenyewe,imecheleweshwa kimaendeleo na viongozi uchwara.

Sasa mtawala kapatikana wa wa Zanzibar na hana uhakika wa kuchaguliwa tena na chama chake,akishindwa tena unategemea ni lini huu mtego wa muungano fake utaondoka? Labda aje afe Rais mwingine madarakani.

SSH anawavutia kasi tu.
 
Chini ya Ibara ya 3 ya Katiba ya nchi yetu, Tanzania inafuata mfumo wa vyama vingi vya siasa tangu mwaka 1992. Utekelezaji wa majukumu ya vyama vya siasa ikiwemo mikutano ya hadhara hautegemei hali ya uchumi tulionao. Mikutano ya hadhara ya kisiasa ni haki ya kikatiba.
 
Mumewauliza wananchi kama wanataka Katiba mpya au wanataka uchumi? Wananchi wengi, tunataka uchumi, tupate mkate wetu wa leo na kesho, mambo ya Katiba ni yenu nyinyi wanasiasa, sisi wananchi bora mkono uwende kinywani. Hebu anzeni nyinyi wanasiasa muwaulize wananchi, hata kwa kupiga kura, kwenye maeneo yenu.
Mkuu; haya ni mawazo na tabia ya kizembe.
 
Mumewauliza wananchi kama wanataka Katiba mpya au wanataka uchumi? Wananchi wengi, tunataka uchumi, tupate mkate wetu wa leo na kesho, mambo ya Katiba ni yenu nyinyi wanasiasa, sisi wananchi bora mkono uwende kinywani. Hebu anzeni nyinyi wanasiasa muwaulize wananchi, hata kwa kupiga kura, kwenye maeneo yenu.
Kwani wanasiasa sio wananchi? Au wewe unapoongelea wananchi unamaanisha kiumbe gani. Hata hivyo yote unayojinasibu nayo bila muongozo kamwe usifikiri yatafanikiwa.vinginevyo msome mtoa mada umuelewe.
 
Mama umeanza vizuri lakini jana umechafua hali ya hewa.

Fikiria tena mama etu kabla hujachelewa.

Kikwete aliweza na alitoa uhuru 100% kwa wanasiasa kujiachia na uchumi wa mtu mmoja mmoja ulikuwa fresh.

Kumbuka miongoni mwa sababu za kuchukiwa Magu ni pamoja na mambo hayo mawili, fanya leo kesho aijuae ni Mungu pekee.

Kila la heri namuomba Mwenyezimungu akufunue macho uone na uwe kiongozi na siyo MTAWALA.

Tchaoooo!
 
Hakuna asiyejua kua ikipatikana katiba mpya hasa ile ya mzee Warioba itaondoa nafasi zote za Wakuu wa Wilaya na mikoa, Wakurugenzi hawatasimamia tena uchaguzi. CCM wanajua kabisa wamechokwa na wananchi wanategemea zaidi kubebwa bebwa zaidi na vyombo vya dola.

Hawa vijana wa ccm wao ni bendera upepo wanaona katiba ikipatikana watakosa ulaji. Licha ya katiba kutajwa katika ilani yao lakini wamegeuza hili suala
 
1625038214225.png
 
kuandika katiba mpya ni mchakato unao hitaji fedha nyingi.
kwa sasa nchi yetu imeshuka kiuchumi kutokana na janga la korona, hivyo ni busara kwa sasa kama taifa kiongozi wetu na sisi wanachi tukajikita kujenga uchumi wetu.
katiba ni mchakato unao hitaji muda.
hivyo naungana na Rais kwa sasa kulingana na hali ya kiuchumi tuliyo nayo tufanye jambo moja kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna asiyejua kua ikipatikana katiba mpya hasa ile ya mzee Warioba itaondoa nafasi zote za Wakuu wa Wilaya na mikoa, Wakurugenzi hawatasimamia tena uchaguzi. CCM wanajua kabisa wamechokwa na wananchi wanategemea zaidi kubebwa bebwa zaidi na vyombo vya dola.

Hawa vijana wa ccm wao ni bendera upepo wanaona katiba ikipatikana watakosa ulaji. Licha ya katiba kutajwa katika ilani yao lakini wamegeuza hili suala
1625038348588.png
 
kuandika katiba mpya ni mchakato unao hitaji fedha nyingi.
kwa sasa nchi yetu imeshuka kiuchumi kutokana na janga la korona, hivyo ni busara kwa sasa kama taifa kiongozi wetu na sisi wanachi tukajikita kujenga uchumi wetu.
katiba ni mchakato unao hitaji muda.
hivyo naungana na Rais kwa sasa kulingana na hali ya kiuchumi tuliyo nayo tufanye jambo moja kwanza.
Kilichoshuka ni kasi ya ukuaji wa uchumi, lakini uchumi wetu bado unakua.

Usisahu kuwa tuko uchumi wa kati!
 
kuandika katiba mpya ni mchakato unao hitaji fedha nyingi.
kwa sasa nchi yetu imeshuka kiuchumi kutokana na janga la korona, hivyo ni busara kwa sasa kama taifa kiongozi wetu na sisi wanachi tukajikita kujenga uchumi wetu.
katiba ni mchakato unao hitaji muda.
hivyo naungana na Rais kwa sasa kulingana na hali ya kiuchumi tuliyo nayo tufanye jambo moja kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom