Kulikoni, mpakani na Rwanda sisi ni shamba la bibi?

Kulikoni, mpakani na Rwanda sisi ni shamba la bibi?

Ni kweli!. Nilipita Rusumo tarehe 05/01/2023 kuelekea Kigali na baadae Gisenyi. Naelewa kuwa Rwanda ni nchi ndogo sana kuilinganisha na Tanzania kwenye ujenzi wa miundombinu, Lakini wenzetu linapokuja suala la ujenzi wa barabara wanasimamia kweli kweli na matokeo ni kazi iliyotukuka.
Kutoka Rusumo hadi Kigali barabara ile iko kwenye viwango vya juu sana, alama za barabarani za wima na zilizochorwa zinaonekana wazi, taa za barabarani zipo hadi Kigali. Mitaro mingi imefunikwa na cha msing zaidi ni nidhamu kwenye uendeshaji unaofuata sheria kwa kiwango kikubwa.
Kuna barabara chache sana zinazoweza kushindana na zile za Rwanda, Barabara zote zilizojengwa na Strabag zinaweza kushindana, kuna barabara moja mpya imejengwa kutoka Kabingo hadi Nduta Junction pamoja na barabara kadhaa zilizojengwa Mbeya na Tabora.....Barabara nyingi zilizojengwa siku za nyuma ni aibu tupu!.🥹
🥹
 
Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya.

2. Upande wa Rwanda taratibu zote katika kila idara yaani forodha, afya, polisi, immigration, usalama nk ni wazi na hakuna rushwa.

3. Waliopo kwenye eneo la serikali mpakani upande wa Rwanda ni wale tu wanaohusika kwa shughuli rasmi za hapo. Yaani wafanyakazi, mawakala wa forodha, mawakala wa bima za magari, wasafiri wavukao nk.

4. Hakuna anayeweza kuvuka kuingia Rwanda pasipo sababu wala idhini ya idara zote husika za huko yaani immigration, usalama na polisi.

5. Upande wa Rwanda wafanyakazi maisha ni kula kwa viwango vya mishahara yao.

6. Kuhusiana na Tanzania itoshe kusema huku ndiko kwenye ulaji wa urefu wa zile kamba zetu. Yaone magari ya wafanyakazi huku. Ama Kwa hakika wanalamba asali kweli kweli.

7. Eneo la serikali huku limesheni hadi wasiohusika. Kuvuka kuja Tanzania ni bwerere ambapo kama hata wapiga debe kutoka Rwanda wanajifanyia shughuli zao Tanzania kwa raha zao tumebakiza nini?

Yapo mengi ya kushangaza ila itoshe kusema kwa hakika sisi ni shamba la bibi.

Tuendelee kulea hali hizi hadi lini?
'Tuendelee kulea hali hii hadi lini?"

Nadhani jibu la swali lako liko wazi mkuu 'brazaj'.

Hadi hapo sisi wananchi tutakapoamua kuondoa uozo wa hawa viongozi tulionao, na kuweka wanaojali maslahi yetu na ya nchi yetu.

Kwani wao Rwanda wamewezaje?
 
Halafu anatokea Dogo mmoja kaishia Kigali tu analeta uzi, muulize ni mkoa/mji gani mwingine anaujua nje ya Kigali anaanza kugoogle 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Inawezekana kabisa wewe hukuelewa mada inahusu nini.

Hebu eleza tu yanayotokea hapo mpakani pekee upande wa Rwanda na upande wa Tanzania, kama unazuzuka sana na ukubwa wa sehemu.

Unahitaji 'resource' kubwa kiasi gani kuhakikisha taratibu za mpakani zinafuatwa?
 
Inawezekana kabisa wewe hukuelewa mada inahusu nini.

Hebu eleza tu yanayotokea hapo mpakani pekee upande wa Rwanda na upande wa Tanzania, kama unazuzuka sana na ukubwa wa sehemu.

Unahitaji 'resource' kubwa kiasi gani kuhakikisha taratibu za mpakani zinafuatwa?
Soma para ya kwanza halafu uje
 
'Resources'? are you crazy!
Hapa hata ungepewa resources zote unazofikiri wewe, hali haiwezi kuwa tofauti na ilivyo sasa.

Ubovu katika uongozi ndiyo kitu pekee kinachosababisha haya yote. Siyo swala la kuwa au kutokuwa na 'resources'.
Jobless ndio your argument zilivyo ingia uone mziki ulivyo
income vs needs halafu angalia nipaumbele
 
Jobless ndio your argument zilivyo ingia uone mziki ulivyo
income vs needs halafu angalia nipaumbele
Mkuu, usirukeruke hovyo hapa kama panzi. Usilete utoto katika jambo lisilohitaji utoto.
Soma para ya kwanza halafu uje
Hivi kweli unajua kusoma na kuelewa unachosoma?

Hiyo unayoita "paragraph ya kwanza" iko wapi?

Mada inazungumzia "mpakani", kwani hapo mpakani hakuna miundo mbinu?

Inahitaji 'resource' kiasi gani kuboresha hali ya hapo mpakani?

Lakini hata hilo la miundombinu si mhimu, kama ungeelewa kinachozungumziwa kwenye mada. Wewe huoni utendaji kati ya sehemu hizo mbili ni tofauti pia?

Watu kama wewe, ndio hasa mnaosababisha ubovu wa nchi hii.
 
Mkuu, usirukeruke hovyo hapa kama panzi. Usilete utoto katika jambo lisilohitaji utoto.

Hivi kweli unajua kusoma na kuelewa unachosoma?

Hiyo unayoita "paragraph ya kwanza" iko wapi?

Mada inazungumzia "mpakani", kwani hapo mpakani hakuna miundo mbinu?

Inahitaji 'resource' kiasi gani kuboresha hali ya hapo mpakani?

Lakini hata hilo la miundombinu si mhimu, kama ungeelewa kinachozungumziwa kwenye mada. Wewe huoni utendaji kati ya sehemu hizo mbili ni tofauti pia?

Watu kama wewe, ndio hasa mnaosababisha ubovu wa nchi hii.
Naona mtoa mada umekuja na ID Nyingine aana unayouliza mtoa mada alishayajibu acha ujuaji
 
Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya.

2. Upande wa Rwanda taratibu zote katika kila idara yaani forodha, afya, polisi, immigration, usalama nk ni wazi na hakuna rushwa.

3. Waliopo kwenye eneo la serikali mpakani upande wa Rwanda ni wale tu wanaohusika kwa shughuli rasmi za hapo. Yaani wafanyakazi, mawakala wa forodha, mawakala wa bima za magari, wasafiri wavukao nk.

4. Hakuna anayeweza kuvuka kuingia Rwanda pasipo sababu wala idhini ya idara zote husika za huko yaani immigration, usalama na polisi.

5. Upande wa Rwanda wafanyakazi maisha ni kula kwa viwango vya mishahara yao.

6. Kuhusiana na Tanzania itoshe kusema huku ndiko kwenye ulaji wa urefu wa zile kamba zetu. Yaone magari ya wafanyakazi huku. Ama Kwa hakika wanalamba asali kweli kweli.

7. Eneo la serikali huku limesheni hadi wasiohusika. Kuvuka kuja Tanzania ni bwerere ambapo kama hata wapiga debe kutoka Rwanda wanajifanyia shughuli zao Tanzania kwa raha zao tumebakiza nini?

Yapo mengi ya kushangaza ila itoshe kusema kwa hakika sisi ni shamba la bibi.

Tuendelee kulea hali hizi hadi lini?
Sasa unauliza kama ni shamba la bibi wakati mwenye nchi unamjua...au we unamuona ni mdada
 
Kwanini kujiachia kuwe Tanzania tu? Zingatia:

4. Hakuna anayeweza kuvuka kuingia Rwanda pasipo sababu wala idhini ya idara zote husika za huko yaani immigration, usalama na polisi.

7. Eneo la serikali huku limesheni hadi wasiohusika. Kuvuka kuja Tanzania ni bwerere ambapo kama hata wapiga debe kutoka Rwanda wanajifanyia shughuli zao Tanzania kwa raha zao tumebakiza nini?

Huu siyo unaoitwa urafiki wenye mashaka?

Au kwetu ndiko nchi kufunguliwa kwenyewe?
Mimi nimevuka ule mpaka kutoka pale rusumo upande wa tz kwenda upande wa Rwanda bila document yoyote, nikafika baa ya amarembo kunywa bia za mitzig bila kikwazo chochote, wewe mgeni tu ndio huwezi kuligundua hilo, pale mpakani Kuna makubaliano ya Ujirani mwema, madc Wana vikao vyao
 
Mtoa mada ametembelea border moja alafu anakuja na conclusion kwamba tz ni shamba lá bibi ,ni kuulize umeshawahi tembelea border ya tunduma, Nakonde what is your take on that? Maana ukienda upande wa nakonde hapaeleweki ila ukija tunduma kumependeza na watazania ndio wanafanya shughulii nyingi za uchumi upande wa Zambia hapo utasemaje? labda ni kupe somo kidogo border inakuwa nzuri kiuchumi kwa wakazi wa eneo lille pale ambapo panakuwa hakuna sheria kali za kutoka na kuingia kwa raia wa nchi zote mbili kwa baadhi ya kilometres mfano mzuri ni border ya tunduma nakonde raia wanaishi peaceful sababu ya business interaction ya raia wa nchi zote mbili mtazania akita anaenda kununua mafuta ya kupakaa upande wa Zambia na mzambia akitaka anakuja nunua mchele upande wa Tanzania .kwa upande wa border Rwanda tz kuachia warwanda kuja kufanya kazi tz hivyo ndivyo inapaswa kuwa kwa nchi pande zote kwa baadhi ya kilometres free border movement ili ku create business opportunities kwa wakazi wa maeneo hayo ya mipakani.
 
Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya.

2. Upande wa Rwanda taratibu zote katika kila idara yaani forodha, afya, polisi, immigration, usalama nk ni wazi na hakuna rushwa.

3. Waliopo kwenye eneo la serikali mpakani upande wa Rwanda ni wale tu wanaohusika kwa shughuli rasmi za hapo. Yaani wafanyakazi, mawakala wa forodha, mawakala wa bima za magari, wasafiri wavukao nk.

4. Hakuna anayeweza kuvuka kuingia Rwanda pasipo sababu wala idhini ya idara zote husika za huko yaani immigration, usalama na polisi.

5. Upande wa Rwanda wafanyakazi maisha ni kula kwa viwango vya mishahara yao.

6. Kuhusiana na Tanzania itoshe kusema huku ndiko kwenye ulaji wa urefu wa zile kamba zetu. Yaone magari ya wafanyakazi huku. Ama Kwa hakika wanalamba asali kweli kweli.

7. Eneo la serikali huku limesheni hadi wasiohusika. Kuvuka kuja Tanzania ni bwerere ambapo kama hata wapiga debe kutoka Rwanda wanajifanyia shughuli zao Tanzania kwa raha zao tumebakiza nini?

Yapo mengi ya kushangaza ila itoshe kusema kwa hakika sisi ni shamba la bibi.

Tuendelee kulea hali hizi hadi lini?
Hao hao unaowaona wanashangaa shangaa, sijui wapiga debe, ndio haohao wanaomfanya Kagame ashindwe kuigusa Tanzania, hakuna aliye hapo kwa bahati mbaya, jaribu tu utaona kilichomtoa kanga manyoya
 
Hao hao unaowaona wanashangaa shangaa, sijui wapiga debe, ndio haohao wanaomfanya Kagame ashindwe kuigusa Tanzania, hakuna aliye hapo kwa bahati mbaya, jaribu tu utaona kilichomtoa kanga manyoya

Itoshe kusema hujui ulisemalo.
 
Mtoa mada ametembelea border moja alafu anakuja na conclusion kwamba tz ni shamba lá bibi ,ni kuulize umeshawahi tembelea border ya tunduma, Nakonde what is your take on that? Maana ukienda upande wa nakonde hapaeleweki ila ukija tunduma kumependeza na watazania ndio wanafanya shughulii nyingi za uchumi upande wa Zambia hapo utasemaje? labda ni kupe somo kidogo border inakuwa nzuri kiuchumi kwa wakazi wa eneo lille pale ambapo panakuwa hakuna sheria kali za kutoka na kuingia kwa raia wa nchi zote mbili kwa baadhi ya kilometres mfano mzuri ni border ya tunduma nakonde raia wanaishi peaceful sababu ya business interaction ya raia wa nchi zote mbili mtazania akita anaenda kununua mafuta ya kupakaa upande wa Zambia na mzambia akitaka anakuja nunua mchele upande wa Tanzania .kwa upande wa border Rwanda tz kuachia warwanda kuja kufanya kazi tz hivyo ndivyo inapaswa kuwa kwa nchi pande zote kwa baadhi ya kilometres free border movement ili ku create business opportunities kwa wakazi wa maeneo hayo ya mipakani.

Mtoa mada kataja sehemu husika alipoyaona yaliyofyongo na yanayoendelea.

"2. Upande wa Rwanda taratibu zote katika kila idara yaani forodha, afya, polisi, immigration, usalama nk ni wazi na hakuna rushwa."

Kwamba Kwa wenzetu ni hivi ila kwetu, na bado haikufikirishi? Kwamba huna taabu hata na hili ila mleta mada?

Tutakuwa tumerogwa!

Maelezo gani yakunasibu wewe?
 
Back
Top Bottom