Kumekucha bomoabomoa Ubungo-Kimara ndani ya 90m za hifadi ya barabara

Kumekucha bomoabomoa Ubungo-Kimara ndani ya 90m za hifadi ya barabara

Kwani sheria inasemaje kuhusu kujenga kwenye hifadhi ya barabara? Siyo kila kitu kulalama tu, wabongo bana, hatunaga jema
Kwenye hizo nyumba kuna umeme wa TANESCO?
 
Siyo kila Maamuzi tu ni ya Kuilaumu Serikali Mkuu. Na bahati nzuri wakati Wewe ukitaka 'Kuichongea' Serikali kwa Wakazi wa huko ila Wananchi wenyewe wanajua na walishajiandaa kwa hayo Maamuzi baada ya hata Wao wenyewe Kugundua kuwa Wamejenga Kiholela japo kuna ambao wamejenga Kihalali na hao ama Wameshalipwa au Watalipwa Fidia na Mamlaka ( Serikali ) husika.
Unaushahidi na haya unayoyasema hapa!?
 
Sheria ya mita 90 as road reserve ilizikuta baadhi ya nyumba , hapo mwanzo road reserve ilikuwa mita 30.
Hizo nyumba hazikuwepo 1937 maana sheria hiyo ni ya 37 kuhusu eneo tajwa
 
Hahaaaaa yaan nikimwangalia SAMIA namuonea huruma tu maana hajui lolote maskini ye anajipigia tu misele hajui kuwa kuna wenzie wanamchonganisha na wanachi kwa makusudi kabisa

walianza umeme, wamekuja mafuta, haya makato ya line za simu, bado hapo makato ya luku haya sasa bomoa bomoa karibu kila mkoa yeye yupo yupo tu haelewi lolote maskini mzanzibari wawatu, hazijui fitna za wabara huku yeye anaamini wapo pamoja wanaimba wimbo mmoja kumbe wenzie wana hama tune taratibu kwa ustadi mkubwa.

Yaan wananchi huku hawamwelewi kabisaa na wamesha anza kumchukia kwa sasa maana tangu ashike nchi vitu vya msingi tena vinavyo gusa wananch moja kwa moja vimeanza kupanda bei
Mkuu unajidanganya Sana.Huyo Mama anajua kila kitu kinachoendelea na kinafanyika kwa Haraka zake.Hao unaofikiri wanabadilisha tone ni ujinga wako kuamini hivyo maana hawana uwezo wa kumuondoa mama.Kuna jamaa zako walitaka kumuondoa Mama Unajua waliomuweka Mama hapo?.
NB:Nchi hii hakuna raisi aliyewekwa na wananchi toka tupate uhuru. Hao wananchi waendelee na harakati za kusaka tonge maana hawaelewi kuwa Mama anaendeleza Ilani ileile aliyoinadi yeye na Mwendazake.
 
Anaandika ukweli. Ni ukomavu na ustaarabu kuandika ukweli bila ushabiki. Ni jamii ikiwa hivyo, nimsingi mkubwa wa maendeleo na ustawi wa watu. Ushabiki ubaki kwenye masuala ya starehe na ushereheshaji, lakini si katika maisha na uhai wa binadamu.
Hii id imekua HACKED au...😳😳😳😳
Mbona unaandika kwa staha sana, sio kawaida yako!😀😀😀😀
 
Watu wa kimara sijui wameikosea Nini serikali .

Tuliokaa kimara tangu miaka ya 90 tumeshuhudia bomobomoa nyingi Sana .
 
Tusijote ufahamu.Serikali zote zimekuwa zikivunja nyumba za watu wanaojenga karibu na barabara wakati wote. Tofauti na utawala wa jiwe serikali nyingine angalau zilijitahidi kutafuta nani alikuwa na makosa kati ya wasimamizi wa mji na waliojenga na fidia zikikuwepo kwa waliostahili kupata.

Tatizo la jiwe ni kutotaka kufuata utaratibu na sheria.Jiwe hakufuata sheria alipobomoa Kimara, alidharau amri ya mahakama iliyoweka zuio la kubomoa mpaka mgogoro uishe, hakutaka kusikia suala lolote la fidia.
Heheheh walisema JPM katili kavunja nyumba zao! Sasa Mama anaupiga mwingi sana na atatuvusha[emoji28]
 
WAENDE WAKAWAWEKEE ALAMA YA INAPOISHIA HIO MT ZAOO WASIWAFANYE WATZ WAJINGA ....UWEZI MWAMBIA MTU UKO TISINI AMA 120 WEKA ALAMA ISOME HAPA.MTU AJUE ANAISHIA WAPI KUVUNJA.........

HAPO NDIO MTAELEEWA WIMBO WA TUONANEEE PARADISOOO TUONANEEE PARADISOOO X3 KWENYE MJI WA RAHA KWANN INAIMBWA MSIBA NI TU..
Mpwa mpwa mpwaa

Mbn kama jana nlikuona kama ww mitaa ya top garage sema nlishindwa simama maana nlikuwa kwenye gari la lift 😂😂😂

Ova
 
Back
Top Bottom