Kuna kiashiria chochote cha tabia kwa mtoto anayenyonya kidole?

Kuna kiashiria chochote cha tabia kwa mtoto anayenyonya kidole?

Ndo hivyo wakuu, naomba nisaidiwe hilo!. Najua kuna wataalamu na wazoefu wa kung'amua tabia humu.
Mtoto ni wa kike, still todler (2+ yrs). Mtoto huyu halali kama hayanyonya kidole chake gumba cha mkono wa kushoto huku mkono wa kulia akiutumia kumfinyafinya mama yake (au yeyote aliyemshika). Na sehemu anayopenda kumfinya aliyemshika ni kwny kiwiko cha mkono.
Ukimtoa kidole hiko halali na lazime akupigie kelele za kilio. Huhakikisha analala nacho na muda pekee wa kuweza kumtoa ni wakati wa amelala fofofo!
Ilikuaje hadi akafikia hatua hiyo?
 
Sina scientific research ila kwa uzoefu wangu watoto ambao wananyonya vidole kwa umri mrefu wanakuwa na shida kwenye IQ yao. Ama anakuwa mzubaifu, mzito kiakili, mpole kupitiliza au mnyonge. Na mara nyingi hujiliza sana.
Tazama anavyokuwa ananyonya kidole anavyopigwa na butwaa au mshangao. Huwa naona ni weakness ya kupambana nayo mapema kwa mtoto.
 
Hili ni tatizo maana kunyonya kidole mwisho la kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni jambo ambalo linanifikirisha sana masan hata first born wake yupo chuo lkn ananyonya kidole mpaka muda anajisahau kabisa, inasemekana hata mimi nilikuwa na tatizo hilo Ila fimbo na pili pili zilitumika haswa.
 
As long as other developmental aspects go well, sioni kama ni tatizo. Ataacha tu kama watu wanavyoacha tabia nyinginezo; kudeka, kujikojolea, punyeto n.k
 
Mdogo angu alikua ananyonya kidole gumba cha mkono wa kulia, alikua anakatazwaa sana had kuchapwa fimbo akikutwa, ila akikaa mda ananyonya tena,

Alikuja kuacha akiwa Sec O level, ilitokea tyuuh akaacha. Ko hata huyo ataacha yeye mwenyewe, ila wengine wanaendelea had ukubwani.
 
Mimi nilikuwa nayonya vidole viwili mpaka miaka 18 nikaacha mwenyewe mimi nilikuwa nayonya huku nafinya finya sikio la kulia, mpaka leo linakujika lenyewe mpaka watu wananishangaa😃
 
Haina shida mkuu. Hiyo inaitwa sucking reflex ambayo ni hali inayoanzia tokea mtoto akiwa tumboni, huanza kuanzia mwezi wa tatu wa ujauzito.

Wataalamu wanasema hali hiyo hujijenga ili mtoto atakapozaliwa aweze kunyonya. Ndio maana ukiona viumbe hai wengi hawafundishwi kunyonya auto tu akiipata chuchu anafanya yake.

So wanasema kitu chochote kikigusa (hard palate) sehemu ngumu juu ndani ya mdogo hiyo suck reflex inatokea ana anajikuta ananyonya.

Hiyo hali inaweza kuendelea kwa mtoto mpaka miaka kadhaa hata baada ya kuacha kunyonya.

I stand to be corrected.
Nilijifunza chuoni hii kwenye saikolojia. Hiyo nguvu ya kunyonya huzaliwa nayo viumbe vyote vinavyonyonya. Ndiyo maana mbuzi, ng'ombe na nguruwe vikizaliwa tu hakuna mwalimu wa kumfundisha kunyonya. Wanyama pori ni zaidi huanza kunyonya ndani ya dakika 5 baada ya kuzaliwa. Nguvu hii huitwa libido energy au conscious activity kama sijasahau mana nimesoma zamani. Ni sawa na hamu ya kufanya mapenz Kwa wanyama huzaliwa nayo na hawafundishwi, paka, njiwa, kuku, huyo mtoto muda ukifika ataacha na akikua ataanza kufanya mapenz bila kuingia darasani kufundishwa. Mungu katuumba hivyo.
 
Haina shida mkuu. Hiyo inaitwa sucking reflex ambayo ni hali inayoanzia tokea mtoto akiwa tumboni, huanza kuanzia mwezi wa tatu wa ujauzito.

Wataalamu wanasema hali hiyo hujijenga ili mtoto atakapozaliwa aweze kunyonya. Ndio maana ukiona viumbe hai wengi hawafundishwi kunyonya auto tu akiipata chuchu anafanya yake.

So wanasema kitu chochote kikigusa (hard palate) sehemu ngumu juu ndani ya mdogo hiyo suck reflex inatokea ana anajikuta ananyonya.

Hiyo hali inaweza kuendelea kwa mtoto mpaka miaka kadhaa hata baada ya kuacha kunyonya.

I stand to be corrected.
Ahsante sana kiongozi!!
 
Hili jambo kuna muda nahisi kama ni ugonjwa, Bro wangu Ana miaka zaidi ya 40 lkn kuna muda anajisahau ananyonya kidole hasa akiwa peke yake.
Dah, bro vp tena huyo?!!!🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom