Kuna mtu amewahi kupata kazi ya maana kwa kutumia waganga wa jadi?

Kuna mtu amewahi kupata kazi ya maana kwa kutumia waganga wa jadi?

Haya mambo yapo kuna jamaa angu alitafta kazi mda mrefu bila mafanikio interview nyingi lakini wapi, kuna siku tulienda kwa babu mmoja, alimpa dawa moja ivi ilikua kama unga akamwambia siku akienda kwenye interview, aweke ile dawa chini ya ulimi afu asiongee chochote mpaka wale wanao mpigisha interview waanze wao kuongea. Wakianza tu ameze ile dawa ndo aongee, akafanya hivo alifaulu ule usaili akapata kazi mpaka saiv maisha yake yemesimama hatari Kiukweli aya mambo yapo
connection naomba kaka maisha ya kitaa yameninyoosha
 
Mbona kuna watu wanaomba Mungu kabla ya safari na wanapata ajari na wengine kufa. Maombi yao yalisaidia nini.
Sawa,lkn tunapomuomba MUNGU kutusaidia ktk jambo fulani huwa tunaruhusu pia Mapenzi yake kutimizwa, Sasa yanapotokea hayo haina maana kuwa MUNGU hakuweza kutunusuru au hatupendi,bali wakati mwingine huruhusu hayo kwaajili ya Sifa na Utukufu wake.
 
Sawa,lkn tunapomuomba MUNGU kutusaidia ktk jambo fulani huwa tunaruhusu pia Mapenzi yake kutimizwa, Sasa yanapotokea hayo haina maana kuwa MUNGU hakuweza kutunusuru au hatupendi,bali wakati mwingine huruhusu hayo kwaajili ya Sifa na Utukufu wake.
Wewe mlokole..nenda kaanzishe uzi wako..uite waumini ndio uanze kuwahubiria ukisanye na sadaka huko..huu uzi sio wako.

Unlesaa kama uko na uzoefu wa kushare nasi kuhusiana na waganga wa kienyeji..mana walokole wengi mmejificha kwenye ulokole kumbe kwa waganga mnatimba kama kawa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Sawa,lkn tunapomuomba MUNGU kutusaidia ktk jambo fulani huwa tunaruhusu pia Mapenzi yake kutimizwa, Sasa yanapotokea hayo haina maana kuwa MUNGU hakuweza kutunusuru au hatupendi,bali wakati mwingine huruhusu hayo kwaajili ya Sifa na Utukufu wake.

Kama anajua yeye kwa mapenzi yake hawezi kukinga na ajari kwa nini ana ruhusu tumuombe
 
Kama anajua yeye kwa mapenzi yake hawezi kukinga na ajari kwa nini ana ruhusu tumuombe
Hakuna linalo mshinda Mungu kwahiyo Sio kila unaloliomba kwa Mungu basi ni lazima litimie vile unavyotaka wewe Mungu anajua lililobora na heri kwako hata kama wewe utaliona nibaya au halijakupendeza
 
Hakuna linalo mshinda Mungu kwahiyo Sio kila unaloliomba kwa Mungu basi ni lazima litimie vile unavyotaka wewe Mungu anajua lililobora na heri kwako hata kama wewe utaliona nibaya au halijakupendeza

Sasa kwa nini ana ruhusu kuombwa ikiwa anajua hawezi timiza. Unaaminisha ata mabaya pia Mungu anayapa kibali?
 
Mganga mwenyewe anamuomba Mungu amsaidie.
Halafu huyo mganga angekuwa anaweza kujiganga kwa nin hajajiganga ili yeye mwenyewe aweze kuwa na kazi nzuri zaidi ya hiyo ya kupiga matunguri?
 
Hakuna linalo mshinda Mungu kwahiyo Sio kila unaloliomba kwa Mungu basi ni lazima litimie vile unavyotaka wewe Mungu anajua lililobora na heri kwako hata kama wewe utaliona nibaya au halijakupendeza
Kuna jamaa yetu ni ustadhi kasota sana kitaa,kila mishe anayogusa haitiki.
Lastly akaamua kuingia jeshini,nako akawa anaona wenzake alioingia nao wanampita tu vyeo ilihali nae alikuwa na degree tena ya uhandisi wa mawasiliano, akaona isiwe tabu, akazama zake hapo Bagamoyo sijui kwa mtaalamu gani,hajakaa hata mwezi zikaja nafasi za cadet nae jina lake limo.saivi tunavyozungumza ni captain wa jeshi na keshaenda mission mbili nje ya nchi.kwa kifupi maisha super kwa sasa.
 
Ngoja nakuja mkuu. Ila sitaki yule anayeomba hela. Malipo ni baada ya kufanikiwa.
Pia kumbuka ili iyo ifanye kazi ni Imani yako tu. Twaweza pewa wote Ila isifanye kazi kwako kwangu ikafanya
Njoo Simiyu huku,uje na nywele za Albino kilo 10 tu,Mkuu..Ni kupeleke kwa mtaalamu.
 
Back
Top Bottom