one b
JF-Expert Member
- Jun 30, 2017
- 1,483
- 3,727
ππππ...Nilianza kuvuta picha kuwa hata mahusiano niliyokuwa nayo kuyumba kwake ni issue ya kipato...kwanza nilikuwa sina source yeyote ya income at dat tym...lakin nilikuwa napambana nipate 5,000 au 10,000 au 20,000 na muda mwingine sipat kabisaa..Endelea mkuu hali ikaendeleaje mbele mpaka leo
Nakumbuka 2015 mwez wa 7 ndio nakata ngebe ya chuo..na utawala mpya unaingia...bank cash nilikuwa na laki nane na ushee..na hyo semistr ya mwisho nilijibana sana caz nilikuwa mnufaika wa bodi nikiamin itanisaidia baada ya ya kuhitimu...
Sasa hapa ndio niliamin hicho hicho kidogo lakin bado watu wanakitaka...nimemaliza vizur mtihan wa mwisho nakumbuka ilikuwa majira ya saa mbil kasoro..siku hyo tulipangiwa upanga pale..narud home vizur na kwa furaha sana..caz kile chuo ni konyo..,sikuwah taman kusoma tenaa...sio kwa mateso yalee...
Basi najirudisha nyumban taratibu..nadaka gar za mwananyamala na drop manyanya mdogo mdogo naingia scan karibu na Mzee kigogo wa zeze....ile nafungua tu getto napawe hongera na mpangaji mwenzangu yule anae kaa na boyfriend wake...nakumbuka kwa kipindi hicho hyo dada alikuwa anafanyia Smile cjui ipo mikochen if am nt mistkn..tukapiga story nyingi sana na kati kat ya story..alipigiwa sim akawa anaongea nikamuacha hapo na mimi nikaingia ndan...nikapumzika kidogo tuu huku nikijisemea sasa rasmi nimeingia mtaani...
Kidogo kama dk 10 hiv kupita yule dada akanigongea..khee B una bahati sana kuna simu nimepokea hapa kuna rafiki yangu ametoka china ameonganishwa kwenye project flani hivi sasa kaniambia kama una mdogo wako kuna kamchango unaktoa thn unaingia...na kweli yule dada alikuwa na mdogo wake wa kiume na usiku wakati amepata hilo dili asubuh yake mdogo wake wa kiume aliondoka kurudi kwao shinyanga..na alikuwa muhitim wa mzumbe sasa sikumbuki ni diploma au certificate...so kwa huo muda tunao ongea mdogo wake alikuwa bado hajafika shinyanga...akampigia simu akamwambia shukia kituo chochote kikubwa thn kesho uanze tena safar ya kurud dar..
Eeh sister nikamwambia inakuaje sasa akaniambia hyo project inaenda miez sita..miez 6... na mwez mmoja ni trainng na miez iliyobakia ni field...mmh malipo?? Malipo ni laki 150,000 kwa siku mmh eeh tunaipataje hyo kaz? Nikamuuliza..akasema rafik yake amemwambia atoe laki sita...nikamuuluza so unamtolea dogo?( mdogo wake anaitwa kelvin) ila anajiita keivooo...akaniambia b ningekuwa na hela ningekutolea lakin ningependa sana muwe na kelv maana mjini hapa kelvin hajui mitaa mingi so atateseka...duu kichwa kinapatw ganz pesa kweli nilikuwa nayo..laki nane tuu..na nilikuwa nimeipangilia kufanya kitu mpaka pale vyet vitakapo toka..
Nikamwambia sister hebu ngoja kwanza nitakujibu kesho...nikarudi geto ni ndan humo humo..nikaoga thn nikaenda kula huku mawazo kibao..,nilikuwa na kawaida nikitoka kula mida ya saa nne mpaka tano...kuna sehemu nakuja nawaangalia madogo fulan hivi wakifanya mazoez ya kudance..walikuwa wanajitahid sana na kuna baadhi wameongia kwenye lebal kubwa sana za muziki akiwepo somebody Nyigu huyu yupo wcb..mfupi hivi kipindi hicho dahππ kweli usione vyaelea..walikuwa wanajituma sana..kipind hicho yupo nahis ni boyfriend wake anajiita Abdu jini..
Basi zikapita siku kama mbili hivi keivoo akawasili pale nyumban...tukapiga story fresh na nikmuuliza umeongea na sister wako akajibu ndio..amenipambania kaz aisee..yaan jamaaa anapenda magar haswa..akawa ashapigia mahesabu kabisaa ile posho ya project...Huku akinena hyo kaz nikifanya mwez mmoja na nusu tuu naagiza alteza...basi story za hapa na pale..tukatoka tembea tembea mtaani..yaani akiona rim za magar anaulizia..huku akiwajibu wauzaji nipeni mwez nakuja kubeba...ππ
Jioni dada yake akarudi nikamwambia sister ongea nae basi hyo rafiki yako mimi nina laki tano..anisaidie ikabid ampigie lakin alikataa..basi yule sister akanimbia b nitakuongezea hyo laki mdogo wangu...bas chapu nikadandia gar studio mpaka kwa machen pale kuna ATM ya crdb..nikatoa laki 6 thn laki nikaitenganisha...nikaja home nikampatia..akachanganya na ya mdogo wake akatuma...
Muda kama wa dk 20 mbele ikaingia msg kwenye simu yangu nahitajika training...eneo kibadamo hotel karibu na stendi ya ubungo..,mida ya saa mbili na nusu...Nikapiga yowee la hatari sasa hapa chuo tuu umemaliza hata wiki haijapita nishapata kazi...aah nilifurah sana nikaanza kumpigia mchiz wangu mmoja hivi na nikamweleza kila kitu...dah jamaa akaniambia ngoja aongee na wazaz wake..nikasema poa..
Kevoo usiku ule alikuwa hatak hata kulala tupo nae getto..akaniuliza unapafaham hapo kibadamo nikamwambia kama ipo karibu na ubungo nitapajua tuu ...
Asubuh ikafika nikajiandaa na kevoo nae akijiandaa tukasepa mpaka ubungo..ile kupiga jicho kulia naiona Mic hotel,Kagame hotel na kibadamo pia..nikamwambia ile pale tukaanza pandisha pale..fika mapokez kuuliza wakatueleza twende floor ya mwisho kabisa ..tukadandia lift pale mpaka juu..
Kufika pale kuna kama kaukumbi flani hivi watu wasio pungua 80 mpaka 100 yaani wapo wa mama, wababa,vijana..yaan kwa kifup kwa walio hitim kwa huo mwaka 2015 tena kuna wengine bado walikuwa wakiendelea na mitihan..so tulikuwa wachache..maana kwenye kujitambulisha pale wengi ni wafanyakaz na wahitimu wa miaka ya nyuma..
Basi imefika mida ya saa sita tukapangwa mstari tukapewa 20,000 kila mtu kwa ajil ya siku hyo..dah nikasema maisha si ndo haya..lakin nilijiuliza sasa angekuja mzaamiaji wangejuaje..?caz yaan hakuna cha majina wala nn..yaan pesa waligawa kutokana na idadi ya mule ndani...but sikuwaza sana na pale ndio nilichochea kuwapigia watu simu...kuwaambia wajiunge...kesho yake tena wakaongezeka tena..yaan tukawa wengi lakin siku hyo waligawa 15,000 kwa kila mtu..na huku wakitupatia vijarida vinavyo husu hyo project makumbuka project ilikuwa ikihusu maswala ya mass media and communication....
πππ hebu nicheke kwanza..wale jamaa ni wajanja sanaa..afu kingine ukishuka pale chin magar ni mengi watu wameacha kaz zao kuja kufanya ile project...kevoo muda wote hata tukiwa tunarud anaeaza magar tuu...sasa hapa na mim nilifanya ujinga kidogo..kwanza nilipiga simu home (mkoa) nikawaambia nimepata kazi...nikataja mpaka kiasi nitakacho lipwa lakin sikuwaambia nimetoa shngap ili niipata ile kazi(kosa)...kupitia zile jeur za siku tatu ilinifanya hata kile kiasi kilichobaki bank nisikitumie kwa nidham...ππ yaan nishakuwa don au naenda kuwa don soon..