Kuna uhusiano gani kati ya kula pesa ya serikali na kunenepa ovyo

Kuna uhusiano gani kati ya kula pesa ya serikali na kunenepa ovyo

Wamebadili maisha unajua tena ugali wanaudharau wakati wameula miaka 30
Sasa kubadili maisha haraka kisa wanapata za wizi, rushwa, hongo, na hata utapeli basi hapo wanaanza kujiona watakulaje ugali tena
Mda wa manyama na chips kuku au mayai na juice zilizojaa sukari za bila viwango
Matokeo yake ni kufa kwa taabu sana wakiandamwa na kisukari, BP na mengine
 
halafu kila siku kutuuliza mbona mabro mko vile vile, nina kisa cha dogo mmoja tulienda nae ughaibuni mwezi tukawekwa apartment moja tunashare jiko, aisee dogo saa kumi na moja unasikia huko jikoni keshaliamsha, saa nne kaagiza tena, saa tisa anasema njaa kali, saa mbili usiku anamalizia, mvinyo usisema utafikiri vile vitu vinaisha, anahema kwa shida huyo
Afu wengi naona wakishapata hyo miili hawawez tena kurudisha mwili ule wa mwanzo,basi unakuta mtu na mashavu yake na likitambi
 
  • Thanks
Reactions: Okk
Wamebadili maisha unajua tena ugali wanaudharau wakati wameula miaka 30
Sasa kubadili maisha haraka kisa wanapata za wizi, rushwa, hongo, na hata utapeli basi hapo wanaanza kujiona watakulaje ugali tena
Mda wa manyama na chips kuku au mayai na juice zilizojaa sukari za bila viwango
Matokeo yake ni kufa kwa taabu sana wakiandamwa na kisukari, BP na mengine
Kuna dogo nilimshangaa alikuwa anakula chips mchana na usiku
 
Wengi hatuzingatii maelekezo ya Dr. Janabi kuhusu ulaji holela, hivyo kuishia kuota vitambi!
 
Samaleykum,

Hawa jamaa zetu hasa wa umri wa kuanzia 26 mpaka 35, hiyo miili mikubwa na mavitambi yasiyoeleweka mnavipata vipi haraka haraka, na ni juzi tu mmetoka shule mkiwa wembamba kama rula, yaani mtu mnafanya kazi sawa, dili za hapa na pale mnapiga wote fresh, lakin mwenzako anafutuka tu kama kifutu sababu ya kula kula ovyo kisa pesa ipo, Mbona wale wengine ambao ni wa age hizo na wanapambana mtaani miili yao iko fresh tu,
kuna uhusiano gani kati ya kula pesa ya serikali na kupenda kula kula kisha kunenepa ovyo.

Matataizo yao ni
1) kuonekana mzee ungali kijana,
2) kupumua kwa shida na
3) kukoroma ovyo

Acheni kula kula ovyo wazee, unene kupitiliza hasa katika umri mdogo ni hatari kwa afya
Mkuu umesema wanaopambana mtaani wakati hao wa serikali ana gari, akishuka anakaa kwenye kiti anazunguka full ac, analetewa mafaili kumi anachagua kupitia moja mengine anaacha. Anavuta pesa za serikali bure tu anaenda kula junk food anarudi home na usafiri. Mwili umetulia no mazoezi na havuji jasho.
 
Hw bout rich white people?
Hii ishu huwezi ijibu inabidi umjue binadamu from his core being , what control him na ndio mana wenzetu Wana elimu or deep understanding ya human nature ndio mana Wana conquer hiyo hali. Atakayeweza nijibu kitalaaamu nampatia ten la voucher hapa lipo kwa mpesa.
Pia atakuwa ni rafiki yangu

Jiulize why Mo ,musk,jeff benzos, Dogo wa Facebook,Sergei,Obama, yaani wale matajiri wote wakubwa wa dunia ni wembamba kwa asilimia kubwa Ila bongo.
Akiwa na kipato cha $1k-$10k per month ananenepa mbaya ,.

Hao watu wanaingiza hata Dola $500k - 1M per day Ila hawanenepi ama wao hawajajipata .

Yaani bana mtu anatoa jibu rahisi mno yaani na ubongo wake unamdanganya ama kumuaminisha kuwa Yuko sahihi.
Bongo mtu anaingiza $400 kwa mwezi ana ka ist kake, ana hang key, anabeba mademu masikini kiakili wanaoshoboka na iyo key, jamaa akiipaki mcity pale anavimbaje anaona Maisha akayamaliza
 
Mtu akifanikiwa alafu akashindwa kubalance diet haimake sense.

Anyway maisha ni kuchagua
Nikiona kijana anakitambi huyo namuweka kundi la wazee kwasababu hata uwezo wake wa kufikiri unapungua
 
Back
Top Bottom