Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

Naamini hakuna uwanja wa Dini,
Wanaweza kutumia hata huo wa Mkapa ila sasa kwanini siku hiyo ya game?

Sio kwamba wameweka Siku ya Mpira ila Ratiba tu zimeingiliana kwani hiyo ya Mashindano ya Qur-an ilikwisha pangwa kabla ya ratiba ya Mechi ya Simba na wageni wa Kimataifa kualikwa ila hii ya Mpira ndiyo ikaja baadae.

Hivyo Tayari Uwanja ulishalipiwa na Mikataba ya Matangazo ya Moja kwa Moja ya TV yameshalipiwa na Wafadhili/Wadhamini wameshaweka hela hivyo wasimamizi wa uwanja wanashindwa kuyasimamisha.
 
Lakini Uwanja ni kwa ajili ya Mpira,
Hata huko FIFA inajulikana ni uwanja wa mpira sio Dini..

Kwahiyo Busara hapo ingetumika walau yafanyike siku moja kabla au baada,

Lakini siku ya mechi hapa Kuna lawama zinaenda kutokea..

Takbiiir

Utakua hujui au kuna Kitu unafichwa:

Miongoni mwa mambo yanayofanywa viwanja vya Mpira ambayo sio mpira wa Miguu Dunia Nzima na si Tanzania tu.

1) Michezo ya Rugby
2) Sherehe za Kitaifa (Uhuru, Muungano n.k.)
3) Matamasha ya Muziki
4) Ngumi za kulipwa
5) Mashindano ya Riadha/Mbio
6) Kufanya maonesho ya Silaha za Kivita na Gwaride.
7) Mashindano mbali mbali yakiwemo hayo ya Qur-an.

SWALI KWAKO: Ni kweli hujawahi kuona popote uwanja wa Mpira kufanyiwa shuhuli yoyote isiyokuwa ya Kimpira au umeamua kuficha ukweli hata ukasema ule ni uwanja wa mpira na sio wa Dini?
 
Tunajua sote jinsi mchezo huu ulivyo muhimu kwa Simba na Taifa kwa ujumla, ndio wa kwanza katika historia ya Nchi yetu kutumia teknolojia ya usaidizi wa Video kwa Mwamuzi (VAR).

Zaidi ya hayo Sheria za CAF zinataka uwanja kuwa wazi angalau saa 72 kabla ya mchezo.

Pamoja na kwamba Wanasema saa 7 kamili hao washindani wa Quran watatolewa kwa usaidizi wa Polisi...

Lakini naona kabisa hapa kuna lawama zinaenda kutengenezwa sisi Waswahili tunajijua katika kutunza muda.

Lakini vipi kama mtu akaingia then akagoma kutoka ili aangalie mechi?

Lakini vipi kama hayo mashindano yakachelewa kwisha baada ya saa 7?

Ndio maana nauliza kuna ulazima haya mashindano kufanyika Lupaso?

N.B
Sina nia ya kukashifu Dini ya mtu.

Ngoja waje...

Cc: Otterhound
 
Watu wataingia bure lakini uwanja umekodiwa Watu waeshalipiwa kila Kitu Wetu waingie bure ndiyomana Wenye Uwanja hawezi kuyahairisha au kuyahamisha.

Hebu jaribu kufuatilia matangazo yao utaona Masponsor kibao pale wametoa mamilioni kulipia uwanja na Matangazo ya Moja kwa moja ya Television hivyo wanaosimamia Uwanja hawawezi kuhairisha kwasababu ya mechi ya mpira hata siku moja wakati kuna hela Cash wameshazinyaka wakichanganya na za mechi ya Simba tayari wameshanasa double payment hapo.

Ndugu uwanja ni Biashara hule.
Pitch itakua na hali gani !!!!?
 
Upo sahihi Nchi haina Dini ndiyomana wale hawawakilishi Nchi bali ule uwanja wamekodi kama VENUE tu na sio sehemu ya Dini.

Hata Diamon anaweza kukodi uwanja ule ule kama VENUE akapiga show ya mziki ingawa nchi haina Mziki.
Mziki Anaofanya Diamond hata Mimi na Wewe Tutaenda bila Kujali Imani zetu,Mpira Hivyo Hivyo hebu Niambie Hayo Mashindano Wataenda Watanzania wenye Imani tofauti. Kukodisha Uwanja wa Kitaifa Kufanya Shughulia Isiyo ya Kitaifa na Ikaacha Shughuli ya Kitaifa si Jambo Jema

Shughuli Hii Wangeifanya Kwenye Misikiti Yao maana Ipo Mingi Tu na Inauwezo wa Kujaza Waumini wao tu bila Kuathiri burudani za Watu wasiokuwa na Imani Yao
 
Ndiyo maana najivunia kuwa Mkatoliki. Tukiwa na shughuli zetu, tunafanyia kwenye makanisa yetu, au kwenye viwanja vinavyo zunguka hayo Makanisa.

Sasa hawa wenzetu, sijui wanakosea wapi!

Hakuna Kanisa wala Msikitini wenye uwezo wa kubeba watu Wanaoingia kwa Mkapa, wala hakuna Kiwanja mbadala chenye uwezo wa kubeba Watu wanaoingia kwa Mkapa ndiyomana hawajakodi Chamanzi wala uwanja wa Uhuru.

Hivyo nawewe ukipata shughuli yenye Watu wengi zaidi basi utakodi kwa Mkapa.

Narudia tena idadi ya Wanaofika/Wanaohudhuria ni wengi kiasi ya kwamba kwa Mkapa inajaa hivyo hayawezi kufanyika Msikiti wowote.
 
Hapo dar si kuna viwanja viwili wangetumia usiohusika na mechi
Vyote vitajaa, kumbuka kuna mashindano ya Qur'an yalishafanyika kipindi cha Mwenda zake mgeni rasimi alikuwa Bwana Majaliwa, Mwendazaka alikuwa anafuatilia kupitia TV mubashara.

Mashindano ya mwaka huo yalijaza watu viwanja vyote viwili, MZEE Magufuli akawaomba waislamu aende kuwa mgeni rasimu kwenye mashindano ya mwaka uliofuata.
 
Tunajua sote jinsi mchezo huu ulivyo muhimu kwa Simba na Taifa kwa ujumla, ndio wa kwanza katika historia ya Nchi yetu kutumia teknolojia ya usaidizi wa Video kwa Mwamuzi (VAR).

Zaidi ya hayo Sheria za CAF zinataka uwanja kuwa wazi angalau saa 72 kabla ya mchezo.

Pamoja na kwamba Wanasema saa 7 kamili hao washindani wa Quran watatolewa kwa usaidizi wa Polisi...

Lakini naona kabisa hapa kuna lawama zinaenda kutengenezwa sisi Waswahili tunajijua katika kutunza muda.

Lakini vipi kama mtu akaingia then akagoma kutoka ili aangalie mechi?

Lakini vipi kama hayo mashindano yakachelewa kwisha baada ya saa 7?

Ndio maana nauliza kuna ulazima haya mashindano kufanyika Lupaso?

N.B
Sina nia ya kukashifu Dini ya mtu.
Ratiba ya Mashindano kufanyika yalishapangwa kabla ya droo ya mechi ya Simba v/s Orlando haijapangwa.
 
Kwani kipi kilianza!? Kunankimoja kimekuja ghafra..!? Simba na Wasauzi ilijulikana kabla, mashindano hayo vipi!?

Naanza kuona lawaza za UDINI zitaelekezwa kwa wasio waislamu

Ratiba yaashindano ya Qur-an yapo kwenye Kalenda ya kila Mwaka hivyo ndiyo ipo mwanzo! Hiyo ya mechi ya Simba imepangwa juzi tu baada ya Simba kushinda mechi na USGN na kufuzu hatua ya Makundi.
 
Lakini Uwanja ni kwa ajili ya Mpira,
Hata huko FIFA inajulikana ni uwanja wa mpira sio Dini..

Kwahiyo Busara hapo ingetumika walau yafanyike siku moja kabla au baada,

Lakini siku ya mechi hapa Kuna lawama zinaenda kutokea..

Takbiiir
Unahisi nani alaumiwe,
Ndio uwanja wa mpira kweli lkn mbona sijawahi kukusikia ukilisema hili wakati wa maonesho mengine tofauti na mpira, kama vile makongomano ya kidini yanayofanyika pale na maonesho ya miziki?
 
Pitch itakua na hali gani !!!!?

Itakuwa salama! Kumbuka Majeshi wanatimba gwaride na Mabuti yao na bado inabaki Salama.

Kuhusu usafi uwanja una wafanyakazi wake wa kufanya usafi na maintanance hivyo mkwanja wameshapokea watafanya usafi.
 
Mziki Anaofanya Diamond hata Mimi na Wewe Tutaenda bila Kujali Imani zetu,Mpira Hivyo Hivyo hebu Niambie Hayo Mashindano Wataenda Watanzania wenye Imani tofauti. Kukodisha Uwanja wa Kitaifa Kufanya Shughulia Isiyo ya Kitaifa na Ikaacha Shughuli ya Kitaifa si Jambo Jema

Shughuli Hii Wangeifanya Kwenye Misikiti Yao maana Ipo Mingi Tu na Inauwezo wa Kujaza Waumini wao tu bila Kuathiri burudani za Watu wasiokuwa na Imani Yao
Asiyekuwa na Imani hajalazimishwe aende! Asubiri mashindano ya Qur-an yamalize ataenda kuangalia mbungi.

  • Mashindano ya Qur-an sio shughuli ya kitaifa kwasababu hayawakilishi Taifa.
  • Pia Mechi ya Simba sio shughuli ya Kitaifa kwasababu haiwakilishi Taifa

Only ikicheza Taifa Stars ndiyo shuhuli ya Kitaifa kwasababu inawakilisha Taifa.
 
Hakuna anayesema hayana muhimu, Ila kwa nini lazima yafanyike uwanja wa Taifa yasifanyike hata uhuru?

Hayo mashindano ya quran yangepelekwa kufanyikia uwanja wa uhuru



Uwanja wa Uhuru ni Mdogo hauwezi kutosha kwa Watu wanaohudhuria.

Kumbuka kwa Mkapa wamelipia Watu wote waingie Bure ndiyomana umeona Serikali imemute hawawezi hamisha Mashindano ya Qur-an
 
Back
Top Bottom