Kunena kwa lugha ni nini? Na nini hutokea pale mtu anaponena kwa lugha?

Kunena kwa lugha ni nini? Na nini hutokea pale mtu anaponena kwa lugha?

Umeichukulia kimwili ndio maana

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hiyo ndiyo maana halisi ya kutokea dhana nzima ya kunena kwa lugha. Hao wanaojifanya kwamba wamefikia level ya juu ya ufunuo wa Kimungu ni uongo.
Mungu hana lugha ya kusema ukiongea kwa lugha hii ndiyo anakuelewa zaidi, kwake hakuna matabaka wala upendeleo wa aina yoyote labda kama unazungumzia miungu na sio Mungu.
Ndiyo maana unaweza kupeleka maombi yako kwako kwa kikerewe, kichaga, kinyakyusa na bado ukapata jawabu stahiki kutoka kwake.
Hii iliwezekana wakati ule na ilitukia hivyo kwa dhima ya kuhakikisha neno linafika mahali pote Ulimwenguni.
Ndiyo maana huwezi kusikia hayo mambo kwenye Kanisa Catholic sababu wanajua hayana tija wala uhalisia kwasasa zaidi ya kutumika kama dhana ya kutapeli wasio na uelewa wa Maandiko.
Unaongea lugha ambayo unaowahubiria hawaeielewi ili iweje?
 
Unataka kunena kwa lugha? Ni rahisi sana wewe fanya kama ifuatavyo;

1. Hakikisha unaongea.

2. Ila uongee lugha ambayo wewe mwenyewe huijui, hujui maana yake wala hujawahi isikia mahali popote pale.


Ukifanya mambo mawili hayo hapo juu👆 utakua una nena kwa lugha
 
Nafkiri kichwa cha habari hakija kamilika .... ungesema kunena kwa luga isiyo eleweka .... nini kita tokea .... ngoja ni seme ivi kwe swala lolote linalool husu imani au kufanya meditation kuna namn flani unaingia kiroho outomatic wengine hadi jasho lina watoka sas hiyo process karibu kila dini ina tafsiri yake baada ya kuwa katika hali hiyo
 
Hiyo ni dalili kubwa ya magonjwa ya akili inaitwa HALLUCINATION
Ukiona unasikia sauti za ajabu pasi na kujua nini kinazungumzwa basi ni ndio kiataalamu inaitwa Shizophrrnia
Kimsingi asilimia kubwa ya walokole hamnazo kuna mmoja hapa jirani alizimia kisa hajala siku 3 kisa yesu kamtokea kamwambia afunge siku 5 jiulize wee unamjua yesu kweli kama sio ukichaaa ni nini yaan usile siku 5 hawa walokole wana magonjwa ya akili na asilimia kubwa ni wanawake
sawa ibilisi bin shetani.
 
Ninavyojua mimi hawa wanaosema wananena kwa lugha wengi sio kweli maana ukiisoma matendo ya mitume(kitabu) kinaelezea kuhusu kunena kwa lugha na kila mtu alisikia kwa lugha yake!

Sasa hii ya shibhobhobho, shalabhashi! Hata wanenaji hawajui wanaongea nini!
Nikwambie kitu....kwenye kila jambo huwa kuna namna ya kulifikia kwa urahisi. Kwa mfano ukitaka kufungua nati ambayo ina kutu...njia rahisi ni kutumia kimiminika kama mafuta(hydraulic) au maji...zipo njia nyingine lakini hiyo yaweza kuwa rahisi zaidi.
Ujue sisi viumbe tuna roho(pumzi ya uhai),ila kuna viumbe wana sifa zaidi ya hiyo...wana utashi/akili/fikra/mawazo/mitazamo/hisia/nafsi.....na hao ni sisi wanadamu.
Sasa matumizi yetu ya akili(rejea concept ya ego) yamekuwa juu sana kiasi cha kuivuga roho (remember roho ni nguvu tu...sio kitu shikika/oneka. Matumizi ya akili yanapozidi ndio matatizo mengi hutokea. Yanatokea kwa sababu tunaikandamiza nguvu yetu (roho).
Sasa basi watu wakaja na mbinu ni namna gani tutaziamsha nguvu zetu za kiroho...ili tuziishi Kama ilivyo kusudiwa.
Kutamka...shaghabhala sijui shendalabooo....sio uchizi...kuna maneno ukiyatumia akili/mawazo yanakuwa kama yanapoa/yanaenda masafa ya chini sana kwa wachache akili inasimama kabisa kabisa...
Kunena kwa lugha kunaitwa mantra(nadhani ni kihindi)
Kuna maneno/neno ukiyatumia unaifikia vizuri sana ndani yako.
Mfano wa maneno hayo ni kama
Om om om
Dabaga dabaga dabaga
Yahoo yahoo yahoo
Kwa kawaida ni maneno ambayo dunia nzima inaweza ikayatamka kwa sauti inayofanana.
Naweka pozi
 
Kama ni ugonjwa (schizophrenia) kwanini uwatokee walokole tu?

Kwanini hatusikii watu wa dini zingine wakinena kwa lugha?

Au huo ugonjwa unawachagua walokole tu?
Mafundisho ya ukole ndio yanafanya uwe na schizophrenia ukiingia tu akili yako inabdailika inaanza kupata magonjwa ya akili kutokana mafundisho kwa hiyo shida kubwa ni mafundisho yao ndio yanasababisha
 
H
Hii kidogo inakuja kuja lakini kwanini hii phenomenon haitokei kwenye aspects zingine za maisha kama kusikiliza muziki, kucheza nk?

Kwann iwe kwenye ulokole tu? Mbona dini nyingi wanakaa maakini kwenye ibada mda mrefu na nyimbo za kumsifu na kuabudi zinakuwepo pia

Hili tatizo ni common kiasi gani? Kwanini halitokei kwa waislam,wabudha,wayahudi au wasabato?

Inamaana mamilioni kwa mamilioni ya walokole wanaonena kwa lugha Wana hili tatizo?
Hii inatokea vizuri Sana kwenye muziki kwa kuusikiliza au kuucheza. Shida ni moja tu...hatufuati kanuni tukaifikia hiyo hali. Tunacheza ili mradi,unacheza huku unakunywa,unakula,unawaza waza sana,umekodoa macho kwa wengine...ushacheza muziki ukiwa umefumba macho?😁😁😁
 
Sisi Wakatoliki hatunaga hizo swaga. Hivyo nitakuwa muongo kuwasemea hao wanenaji. Labda waje wanenaji wenyewe watusimulie hali wanayojisikia.
Katoliki hakuna ibada za kiroho wala maombi ya kiroho humo mna ibada za litrujia tu
 
Sisi Wakatoliki hatunaga hizo swaga. Hivyo nitakuwa muongo kuwasemea hao wanenaji. Labda waje wanenaji wenyewe watusimulie hali wanayojisikia.
Mnafanya hivi eeh[emoji120][emoji24]
Screenshot_20231010-055903.jpg
 
Ukiwa chini (deep) kabisa ya maombi, na u msafi rohoni, mtu mwenye HAKI, ni lazima roho mtakatifu akushikie katikati ya maombi, ile nguvu ni kubwa kiasi inakufanya uanze kuongea mambo usiyoyajua, unakuwa kwenye hali ambayo huwezi kuielezea.

Sisi wakristo tumepewa nguvu hii ambayo ki ukweli inatusaidia sana kupambana na maadui zetu, its working, its free if you need it ..100% sure.
 
Ni upotoshaji tu na ukanjanja wa kuwapiga noti watu wenye imani haba na kutoelewa mafundisho yaliyoandikwa kwenye Biblia.

Wajanja ndiyo hupita humo na kukunja noti kiulaini kabisa kupitia uposhaji unaofanywa na makanisa ya leo yanoyojiita ya kiroho.

KUNENA KWA LUGHA KULIANZAJE KIHISTORIA?

Ukisoma kwenye Biblia kunena kwa lugha kulitokea siku ya Pentekoste ( Yaani siku ya Hamsini baada ya Kupaa kwa Yesu).

Katika maandiko tunaona kuwa ujumbe wa neno la Mungu ulikuwa umepokelewa katika jamii moja lakini dhima ilikuwa ni ujumbe huu usambae Ulimwenguni kote. Yaani kwa mfano, tuchukulie kwamba ujumbe wa neno la Mungu ulifikia Tanzania ambapo lugha inayotumika kwa mawasiliano ni Kiswahili, lakini ujumbe wa neno la Mungu ulitakiwa ufike Djibout, Malawi, DRC, Ethiopia na kwingineko Ulimwenguni ambapo hata hawakijui Kiswahili.

KULITOKEAJE?

Kunena kwa lugha kulitokea kwa wale Mitume sio kwa kubadili na kuacha kutumia lugha zao za asili au walijifunza lugha za Mataifa waliyoenda kuhubiri, la hasha, bali walitumia lugha zao za asili lakini waliokuwa wakihubiriwa waliupata ujumbe kwa kuusikia kwa lugha zao wenyewe.

Yaani tukirejea katika huo mfano hapo juu, ni kwamba, wewe Petro Mtanzania ukiwa unazungumza Kiswahili chako sanifu kabisa lakini unawahubiria watu wa DRC na wao wanasikia ujumbe unaowapa kupitia lugha wanayoielewa wao mfano, Kilingala, au Kifaransa.

Kwahiyo ni kama leo hii baada ya kuja teknolojia Uhutubie pale UN lakini wawakilishi wa Oman wanakusikia unaongea Kiarabu kilichonyooka, au Ujumbe kutoka Rome unaona unagonga kile Kilatini chenyewe kabisa, au wajumbe kutoka Brazil wanaona unakibomoa kireno ipasavyo.

Na kwa njia hiyo ndivyo ujumbe wa neno la Mungu ukaweza kuenea Ulimwenguni kote na maandiko kuweza kutafsiriwa katika lugha mbalimbali kulingana na sehemu ujumbe wa neno la Mungu unapelekwa

UPOTOSHAJI WA MAKANISA YA LEO YANAYOJIITA YA KIROHO:
Viongozi wengi wa hayo Makanisa hawaijui dhana ya kunena kwa lugha kwa mapana yake, na kama wanafahamu basi wanatumia ujinga wa waamini wao kufanya upotoshaji wa Makusudi kwa Maslahi yao binafsi.

Ukienda kwenye Makanisa ya leo yanayojiita ya kiroho yamejaa upotoshaji juu ya dhana hii ya kunena kwa lugha kwa kukuta hao viongozi wa makanisa hayo wanaongea lugha ambazo hata waumini wao hawazielewi nini wakimaanisha au ujumbe gani unatolewa kupitia matamshi hayo.

Nachelea kusema usikute hata wao hawajui ni kitu gani wanaongea na wala hawajui hiyo lugha gani wanatamka.

NB: Kunena kwa lugha sio kama kupandisha mashetani na kuongea vitu visivyoeleweka, bali ni njia iliyowatukia Mitume katika zama hizo ili neno la Mungu liweze kufika mahali pote Ulimwenguni.

Kwa ulimwengu wa sasa sidhani kama hiki kitu bado ni applicable.
That is your opinion, but the Bible suggest otherise, about speaking in tongues [emoji24]
 
Hakuna cha kunena kwa lugha wala nini.Mfano mimi nikiamua kusali kwa kisukuma ,wewe kisukuma haukijui hapo utafikiri ninanena kwa Lugha.
 
Back
Top Bottom