Kupoteza uwezo wa kunusa yaweza kuwa/ni dalili za mwazo za COVID19

Kupoteza uwezo wa kunusa yaweza kuwa/ni dalili za mwazo za COVID19

Kinachokupotezea sense of smell ni yale mafua yanaoambatana na hiyo Covid19...



Cc: mahondaw
 
Wakuu Kichwa cha Habari Kinajieleza.

Nina takriban wiki na siku 2 Sasa Nimepoteza uwezo wa kunusa na taste, yani hata harufu ya perfume sihisi kitu.

Najua humu Jf, tuna wataalam na wajuzi wa mambo,watatusaidia tiba na ushauri pia.

Karibuni wataalam.

Sent using Jamii Forums mobile app
===
Wakuu Habari.

Kama wiki 2 ziliopita nilikumbwa na mafua. Sio makali sana ila naamini ni kwa sababu nilitumia mashuka yenye vumbi.

Sasa bwana, narudi home nikapitia dukani nikanunua perfume fulani. Nafika home najipuliza haitoi harufu ata kidogo. Nikajua nimeuziwa feki. Nikasema kukikucha nitaenda lalamika. Duh, bahati mbaya umeme ulikatika jana yake, nikawa nimezima friji niliogopa ukirudi vibaya utaunguza friji (sina stabilizer) uliporudi nikawa nimesahau kuwasha iyo jioni nalifungua vitu vyote vimeoza Ila hakuna harufu ata kiduuuchu. Yaani ata kiduchu.

Hapo ndio wasiwasi ukaanza. Angalau sukari na chumvi kwa mbaaali nasikia ladha ila vitu vingine sio harufu wala ladha KABISA.

Dalili zingine ni kifua kwa mbaaali kinabana, mwili upo fresh tu.

Nikahisi naweza kua na Corona so nikajitahidi mazoezi kuruka kamba, malimao na machungwa kunywa, chai ya tangawizi.

Nimejifukiza mwarobaini na mpera ila nikaona vinanitesa tu nikaacha.

Case ya kupoteza izo sense mbili, kuna jirani yangu pia amepata na amesema ila yeye imerudi.

Nilitumua baadhi ya dawa za kifua, mafua na maumivu pia nilishauriwa. (AMPICLOX, CETRIZINE NA PARACETAMOL).

Sahivi naendelea poa kabisa ila nimejitenga. Niliogopa sana nikajua ni Corona.

PS: Kunusa na Ladha bado sijarudi ila izo dawa nimeacha kutumia.
Asanteni sana.
 
Kumbe corona ilikugonga mkuu? Pole sana nafikiri sasa utamweshimu Rais wako Magufuli.
Sijapata corona lakini mimi sioni tatizo kupata corona as long as natibiwa na kupona/kufa. Ni kawaida kuwa na tatizo la kunusa unapokuwa na mafua. Ni kwa vile hujui kitu.

Mbona Jiwe ameweka karantini Chato, total lockdown kama haogopi kufa. Polisi wamemwagwa lundo kuzuia watu kutoka nje.. nenda twita kasome

Majariwa alipeana mkono na Shah wa Mafia aliyekufa. Unasemaje?
 
Nilipigwa na hyo kitu wiki karibu tatu sisikii harufu wala ladha ku google nakuta eti wanasema dalili ya COVID 19 aseee...

Nilikua nakohoa sana pia

So nikapiga

Amplicox Dozi nzima

Asubuhi maji ya limao

Kusukutua na Chumvi na maji vuguvugu kwny koo kila bada ya masaa kadhaa

Kunywa Tangawizi mbichi ya kusaga iliyochanganwa na vitunguu saumu..

Kumung'unya viksi kingo

Baada ya wiki karibu tatu ndio harufu na ladha vikarudi na kifua kukohoa kukakoma mana ilikua kukohoa hadi mbavu zinauma.
Vita ilikua kali sana sa sujui ndio corona au lah
NB niliji lock down mwenyewe kama mkulu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom