Kushabikia Polisi kuua watuhumiwa, ni ujinga uliopitiliza

Kushabikia Polisi kuua watuhumiwa, ni ujinga uliopitiliza

Kwa sasa katiba mpya haikwepeki kweli, je wananchi kwa makundi mbalimbali wapo tayari kuidai au ndo unabaki wajibu wa wa wanasiasa(hususani CHADEMA) kuidai ?

Jiulize mkuu walioko madarakani wapo tayari kukubali kupokonywa tonge mdomoni maana katiba iliyopo Kwa sasa inawabeba wao waendelee kutawala

Mkuu walioko madarakani hawawezi kukubali kirahisi kupokonywa matonge mdomoni. Hili ni letu kuamua kunyoa au kusuka.
 
Miye ni mhanga wa panya road. Huenda nawachukia kuliko wewe. Ila si sahihi kuwauwa wao wala watuhumiwa:

Kama tunataka Katiba Mpya, Tusiionee "Haya" Haki ya awaye yote
With due respect mkuu. Mimi siungi mkono polisi kujichukulia sheria mkononi lakini nina exception.

Kama huwa unasoma posts zangu, mimi sikuwahi kumuunga mkono hayati JPM kwa mambo mengi, ila alichokifanya Kibiti niliunga mkono.

Huwa kuna hali ikifikia sheria hazifuatwi ili kutatua tatizo kwa haraka, naomba kwanza uelewe kuwa sheria zetu bado zina mapungufu mengi, mapungufu hayo yanawapa mwanya wahalifu kurudi mtaani na kuendeleza uhalifu. Hawa panya road wengi walishawahi kufikishwa mahakamani, lakini wamerudi mitaani, na wengine gerezani lakini wamerudi tena, kuendeleza uhalifu ule ule, tena kwa majigambo kwamba hakuna wa kuwafanya kitu, watu tulianza kuhisi labda wanashirikiana na baadhi ya polisi!

Sasa mkuu, katika hali kama hiyo, nini kifanyike? Unajua procedure za mahakamani. Kuna mtu ni mhalifu kabisa, na katenda uhalifu kabisa, lakini ushahidi wa kumpa hakimu unaweza ukaleta changamoto, panya road akarudi tena mtaani, unataka hivyo?

Kama kweli wewe ni mhanga wa panya road, ni lazima utumie falsafa ya Pragmatism, The end justifies the means! Matokeo ndio yahalalishe njia iliyotumika, huyo uliyemnukuu, Mwalimu Nyerere, was a pure pragmatist, aliwahi kumhukumu kunyongwa mtuhumiwa aliyemuua mkuu wa mkoa wa Iringa bila kumpeleka mahakamani.

Ni kweli kuna madhara, lakini lazima tulinganishe madhara na faida, baada tukio la september 11, marekani waliruhusu mtu anaeshukiwa kuwa gaidi kupigwa risasi on sport! Sisi ni kama nani kujidai tunajua mno haki za binadamu, na nikuambie, mtu akihisiwa ni panya road, aidha atakuwa ni mvuta bangi au mbwia unga, ni ngumu kwa mtu wa kawaida kuhisiwa!

Inaumiza sana kwenye nchi huru, watu tuishi kwa uoga na hofu, tukihofia vijana waliokataa kwa maksudi kufanya kazi halali, na kuamua kukaba.

Na kwa maelezo tajwa hapo juu, ninasema bila kumung'unya maneno, mtu yeyote atakaehisiwa ni panya road apigwe risasi mara moja. WE WANT TO STOP THIS, ONCE AND FOR ALL.
 
Panya-road wanaua raia na kupora mali zao. Polisi wao wanawaua ti hao Panya-road lkn hawapori mali mali zao.

Polisi wa nchi hii wana huruma sana Sana. Hawa Panya-road ni wa kuua Kisha kuwabaka kabisa
Duuu! Punguza hasira mrembo.. Hadi kuwabaka!?
 
Panya-road wanaua raia na kupora mali zao. Polisi wao wanawaua ti hao Panya-road lkn hawapori mali mali zao.

Polisi wa nchi hii wana huruma sana Sana. Hawa Panya-road ni wa kuua Kisha kuwabaka kabisa
Mmoja wa delinquent JF member, haya ndio matokeo ya kulelewa na familia zenye ukatili,na bila shaka ulifundishwa chemistry na hesabu pale sengerema sec.school na yule mkuu wa ukatili
 
Naunga mkono hoja
P
Kaka Paskali,
Mbona binafsi naona kama extrajudicial killings safari hii kama zimekuwa dedicated kanda ya ziwa? Au kuna kitu na-miss? Very worrying trend.

Kama mwandishi wa habari za kiuchunguzi hope pengine kuna observation utakuwa umeshaona.

I stand to be corrected.
 
Kustaarabika kwa jamii au taifa ni kufuata sheria na kanuni walizojiwekea kwa kuzingatia maadili na utu.
Hizi fikra za kupiga na kuua hadharani ni uthibitisho wa kukosa ustaarabu (jamii bado Ina ujima fulani).
Watu waovu waliostaarabika watatenda uovu wao kwa akili na kificho.
 
Kustaarabika kwa jamii au taifa ni kufuata sheria na kanuni walizojiwekea kwa kuzingatia maadili na utu.
Hizi fikra za kupiga na kuua hadharani ni uthibitisho wa kukosa ustaarabu (jamii bado Ina ujima fulani).
Watu waovu waliostaarabika watatenda uovu wao kwa akili na kificho.
Cc: Mjuni Lwambo
 
Asiyefunzwa na Mamaye ufunzwa na ulimwengu... Wahenga.!

Mtoto mwenye hekima umfurahisha Babaye Bali mwana mpumbavu ni mzigo Kwa mamaye.. Me Biblia

Kwa hili nawapongeza police .
Imagine umejichanga changa huku na huko umejenga au umenunua ka TV Kako na Redio, Mara paap Panya Road hawa hapa... Au ndo unatoka kwenye mizunguko yako ya Kila siku ya kutafuta na jinsi Watanzania wengi tulivyo vipato vyetu ni hakuna kuhumwa Wala kupumzika ni Nguvu zako ndo kula kwako, Sasa unakutana na Panya Road na familia inakutegemea .

Police fanyeni kazi yenu ipasavyo tokomeza hivyo vikundi kabla avijakomaa na kuwa vikundi vya kigaidi na kuvuruga Amani ya nchi yetu.

Mnaosema sijui ni sababu ya vijana kukosa ajira , ni wapi/ nchi Gani ambayo imeajiri wananchi wake wote.? Kuna Panya Road wengine Wana 17/18 years uwo ni mda wa kuwa shuleni au kuwa kwenye uangalizi wa wazazi wao ....

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Mmoja wa delinquent JF member, haya ndio matokeo ya kulelewa na familia zenye ukatili,na bila shaka ulifundishwa chemistry na hesabu pale sengerema sec.school na yule mkuu wa ukatili

Huyo mwamba kwa hakika kaniacha hoi. Katiba Mpya kwa hakika ingali mbali. Huyu ni Sexless sembuse Countrywide au Bia yetu?
 
Asiyefunzwa na Mamaye ufunzwa na ulimwengu... Wahenga.!

Mtoto mwenye hekima umfurahisha Babaye Bali mwana mpumbavu ni mzigo Kwa mamaye.. Me Biblia

Kwa hili nawapongeza police .
Imagine umejichanga changa huku na huko umejenga au umenunua ka TV Kako na Redio, Mara paap Panya Road hawa hapa... Au ndo unatoka kwenye mizunguko yako ya Kila siku ya kutafuta na jinsi Watanzania wengi tulivyo vipato vyetu ni hakuna kuhumwa Wala kupumzika ni Nguvu zako ndo kula kwako, Sasa unakutana na Panya Road na familia inakutegemea .

Police fanyeni kazi yenu ipasavyo tokomeza hivyo vikundi kabla avijakomaa na kuwa vikundi vya kigaidi na kuvuruga Amani ya nchi yetu.

Mnaosema sijui ni sababu ya vijana kukosa ajira , ni wapi/ nchi Gani ambayo imeajiri wananchi wake wote.? Kuna Panya Road wengine Wana 17/18 years uwo ni mda wa kuwa shuleni au kuwa kwenye uangalizi wa wazazi wao ....

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app

Unajua Kuna tofauti ya panya road na washukiwa wa u panya road?

Unaona je turasimishe kikatiba Ili iwe kwa mujibu wa sheria polisi kuuwa watuhumiwa wakijisikia kufanya hivyo?
 
Huyo mwamba kwa hakika kaniacha hoi. Katiba Mpya kwa hakika ingali mbali. Huyu ni Sexless sembuse COUNTRY wide au Bia yetu?
(Yawezekana sijaelewa lkn naomba nitoe utetezi wangu). Mm siyo katili lkn panya road wameboa Sana. Wameua mpk vikongwe wakiwa wamepumzika vyumani mwao. Inauma sana.

Ndiyo maana napendekeza polisi wawaue Panya-road kila wanapokamatwa
 
(Yawezekana sijaelewa lkn naomba nitoe utetezi wangu). Mm siyo katili lkn panya road wameboa Sana. Wameua mpk vikongwe wakiwa wamepumzika vyumani mwao. Inauma sana

Natumai unajua tofauti ya panya road na washukiwa wakiwamo wa panya road.

Unaonaje basi kama ingerasimishwa kwa mujibu wa katiba polisi kuwauwa watuhumiwa kwa mujibu wa sheria Ili tuachane na kelele hizi?

Si unajua yanayotokea sasa ni kinyume cha katiba iliyopo mkuu?
 
Back
Top Bottom