Kuwapa watoto majina ya kigeni Kizungu/Kiarabu ndio usasa au kutojitambua?

Kuwapa watoto majina ya kigeni Kizungu/Kiarabu ndio usasa au kutojitambua?

Kukosoa kunatakiwa kuwe katika msingi wa mantiki.

Sasa kama mtu hapendi hayo majina unayopenda wewe unamkosoaje? Unamlazimisha apende kitu unachopenda wewe?

Nani kakupa haki ya kukosoa jina la mtoto wa mtu baki?

Ulimsaidia kuzaa? Una ubia kwenye hiyo ndoa au mahusiano hayo yaliyopelekea kumzaa huyo mtoto?

Hao unaotaka kuwapangia majina ya watoto wao walishawahi kukupangia wee jina la mtoto wako?
Mleta mada ana hoja unalazimika kupinga sababu umeshachemka ila kimsingi huna sababu wala hoja ya msingi
 
Tatizo si jina tatizo ni kwamba tunapenda watu wafate mawazo yetu na si furaha zao.
Yeye akimuita moana,frank, charity na wa kwako ukamwita ndondocha, chungu, tabibu halafu wote mkakaa kimya bila kuzodoana itapendeza.
 
Wewe c uncle wake muite "Tabu, Shida, Masumbuko na Sikujua au watoto wako wape haya ili ufurahi na roho yako
Acha zako wewe,kwani lazima uwaze kwenye negativity Tu

Lulu
Furaha
neema
Waridi

Haya siyo majina mazuri ya Kiswahili ya kuwapa watoto mkuu? Wenzetu wapo ulaya lkn Wana wanawaita watoto "Dele Ali " " wale" na rotimi

Tuondoe hii dhana ya kila jina la Kiswahili ni Baya na kina mikosi asee!!!
 
Mleta mada ana hoja unalazimika kupinga sababu umeshachemka ila kimsingi huna sababu wala hoja ya msingi
Siwezi kushangaa sana ukisema hivyo.

Kwa sababu Watanzania wengi wamezoea maisha ya kijima, ya kufuatiliana fuatiliana, maisha ambayo mtu haamui mambo yake mwenyee, mambo yanaamuliwa na jamii, maisha ya kuzongana, kuchunguzana, kufuatiliana.

Ni hivi, mtu ana haki ya kuamua anampa mtoto wake jina gani.

Ukianza kumuingilia kwenye hilo, unamuingilia kwenye mambo ya ndani ya familia yake.

Wewe kama hupendi jina fulani, tafuta mtoto wako umpe jina unalolipenda wewe.Na mtu akikuingilia katika hili, hata wewe nitaitetea haki yako hii ya msingi.

Kwa nini uanze kulazimisha mtu baki achague jina unalolipenda wewe na asilolipenda yeye?

Yani mtu katafuta mtoto kivyake, jina umpangie sheria wewe?

Wewe mtu akikupangia jina la kumpa mtoto wako usilolipenda wewe, analolipenda yeye, utaona sawa?

Acheni mambo ya zama za ujima kila kitu kinaamuliwa na kijiji.

Jina la mtoto lisipopitishwa na kikao cha kijiji huwezi kumpa mtptp hilo jina.

Huu ndiyo mwanzo wa kusema wote tupigie kura CCM, kwa sababu mwenyekiti wa kijiji kasema.

Groupthink.

Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya groupthink ya aina hii na umasikini.
 
Kuna fahari na raha kubwa kufurahia asili yako. Hujisikiii mnyonge na huwezi kujidharau hata ukidharauliwa na yeyote. Mimi ni Mnyakyusa kamili na majina yangu yote ni ya Kinyakyusa, yaani Gwandumi Gwappo (Gwapponile) Atufwene Mwakatobe Mwakimenya. Asili yangu ni Mwakaleli, wilayani Rungwe, mkoani Mbeya

Nawasikitikia ambao asili ya majina yao imepotea kabisa. Mathalani Abdul Salmin Amour Juma, Victor Robert Willy Henry au Longinus Lawrence Recocatus Deogratius.

Nasikia zamani wakoloni walikuwa wanakataa waafrika kubatizwa au kuandikishwa shuleni kwa majina yetu ya asili. Tumerithi hata visivyo riziki!
Alafu kuna baadhi ya nchi za afrika tena watumiaji wa lugha za wazungu unakuta majina yake yoote ya asili adi raha na hawajali lakini sisi sasa!!
 
Tatizo si jina tatizo ni kwamba tunapenda watu wafate mawazo yetu na si furaha zao.
Yeye akimuita moana,frank, charity na wa kwako ukamwita ndondocha, chungu, tabibu halafu wote mkakaa kimya bila kuzodoana itapendeza.
Umeweza kuupata mzizi wa fitina mkuu.

Watu wanapenda ku control wengine.

Mtu akiamua kumpa jina analotaka mtoto wake, mtu baki anapungukiwa nini?

Ni kutaka ku control watu tu.

Kwa msingi huu, kesho watataka watu wapigie kura chama fulani, kwa lazima, usipopigia si mzalendo.

Wanaanza polepole kuingilia uhuru wa watu.
 
Sasa wameacha, labda upende mwenyewe au wazazi. Bahati mbaya majina mengi tunawapa watoto wasiokuwa na maamuzi au uwezo wa kuhoji chochote
Hivi wakristo waliacha kubatiza kwa kubadili jina la asili na kumpa mtoto jina la kizungu?

Ni utaratibu wa kizumbukuku sana
 
Umeweza kuupata mzizi wa fitina mkuu.

Watu wanapenda ku control wengine.

Mtu akiamua kumpa jina analotaka mtoto wake, mtu baki anapungukiwa nini?

Ni kutaka ku control watu tu.

Kwa msingi huu, kesho watataka watu wapigie kura chama fulani, kwa lazima, usipopigia si mzalendo.

Wanaanza polepole kuingilia uhuru wa watu.
Upo sahihi kabisa. Si mzalendo na unapigwa risasi.
 
Umeweza kuupata mzizi wa fitina mkuu.

Watu wanapenda ku control wengine.

Mtu akiamua kumpa jina analotaka mtoto wake, mtu baki anapungukiwa nini?

Ni kutaka ku control watu tu.

Kwa msingi huu, kesho watataka watu wapigie kura chama fulani, kwa lazima, usipopigia si mzalendo.

Wanaanza polepole kuingilia uhuru wa watu.
Mawazo kamwe hayawezi kufanana,,sisi tumeona lipi jema ,wewe pia una mtazamo wako,,je no vibaya kusema unachoamini sahihi???kufikiria tofauti nawewe no umasikini???hakuna anaelazimisha,Ni maoni tu,,Kama unavyosema Hakuna Mungu,huwa unalazimisha au unaeleza unachoamini???
 
Naongezea:
Upendo
Imara
Utukufu
Maua
Faraja
Hekima
Kunegunda
Mashauri
Ambangile
Mboka
Mobali
Nk.
Acha zako wewe,kwani lazima uwaze kwenye negativity Tu

Lulu
Furaha
neema
Waridi

Haya siyo majina mazuri ya Kiswahili ya kuwapa watoto mkuu? Wenzetu wapo ulaya lkn Wana wanawaita watoto "Dele Ali " " wale" na rotimi

Tuondoe hii dhana ya kila jina la Kiswahili ni Baya na kina mikosi asee!!!
 
Mawazo kamwe hayawezi kufanana,,sisi tumeona lipi jema ,wewe pia una mtazamo wako,,je no vibaya kusema unachoamini sahihi???kufikiria tofauti nawewe no umasikini???hakuna anaelazimisha,Ni maoni tu,,Kama unavyosema Hakuna Mungu,huwa unalazimisha au unaeleza unachoamini???
Kama unajua mawazo kamwe hayawezi kufanana kwa nini unalazimisha majina unayotaka wewe kwa watu ambao mawazo yao hayafanani na yako?

Unaji contradict.

Upande mmoja unakubali mawazo kamwe hayawezi kufanana.

Upande wa pili unataka kulazimisha majina unayotaka wewe.

Unajua hata umesimamia wapi?

Nilitegemea mtu anayejua kwamba mawazo kamwe hayawezi kufanana awape wengine uhuru kuwapa majina wanayoyataka watoto wao.

Wewe unafanya kinyume.

Unajua mawazo kamwe hayawezi kufanana, halafu unataka kulazimisha majina unayotaka wewe.
 
Habari salamu sio ndefu nimechefukwa mtoto wa dada yangu kapewa jina Moana, jina la kikatuni cha Disney nikapata maswali sana, kwanini hadi leo tunaendelea kushikilia majina ya wageni? Majina mazuri ya Kiswahili, lugha za asili yameisha au ndio tunayaona ya kizamani na hayafai kitu?

Kuna uhusiano gani kati ya kuwa Muislamu na kumpa mtoto jina la kiarabu? Au mkristo kumpa mtoto jina la Kizungu kama Frank, Aboubakar, Sameer, Chris, Dorice, Khadija

Kwanini sio majina ya kichina au kihindi? Labda dini ni kitu chema lakini isiondoe u-Afrika wetu. Tujitafakari.


Ungeanza wewe mwy kuonyesha mfano... lakini unanyoshea kidole wengine wakati huoni boriti jichoni pako...

Unajiita Forest Hill hapa JF
Na kama umetahiriwa basi huna mamlaka kuongelea hilo jambo maana umefata mila za kigeni...
 
Kwa sababu English is more romantic.

Mfano " BABY I WANT TO GIVE YOU A SURPRISE"

Sasa wewe jifanye unapenda Sana kiswahili igeuze sentensi hiyo kwa kiswahili halafu mwambie demu wako " MTOTO MCHANGA NATAKA NIKUPE MSHANGAO"!!!

Majina ya kibantu hayanaga swaga. Mtoto anaitwa KAJUNJUMELE!!!! That's amount to child abuse!!!
 
Ungeanza wewe mwy kuonyesha mfano... lakini unanyoshea kidole wengine wakati huoni boriti jichoni pako...

Unajiita Forest Hill hapa JF
Na kama umetahiriwa basi huna mamlaka kuongelea hilo jambo maana umefata mila za kigeni...
Hujasoma vizuri,,sio kila la wageni baya, Kuna ya kuiga,na Kama nimetahiriwa wakati nipo mdogo,au nikaitwa Solomon au Suleiman,sio kosa langu..na kujiita Forest Hill hapa,nimekosea(maoni yangu)....wewe unasemaje??
 
Ukishaanza kuwaamulia watu baki majina ya watoto wao ujue ndiyo unaelekea kuwapangia mke wa kuoa/ mume wa kuolewa na chama cha kupigia kura.

Kitu cha muhimu kabisa ni kila mtu awaachie uhuru wa kujiamulia wengine, kama na yeye anavyoachiwa uhuru huo huo.

Yani wewe unayependa majina ya Kiafrka utaonaje ukipanga kumuita mtoto wako Baraka, halafu akaja mtu akakwambia hilo jina si zuri, jina zuri ni Jayden?
 
Habari salamu sio ndefu nimechefukwa mtoto wa dada yangu kapewa jina Moana, jina la kikatuni cha Disney nikapata maswali sana, kwanini hadi leo tunaendelea kushikilia majina ya wageni? Majina mazuri ya Kiswahili, lugha za asili yameisha au ndio tunayaona ya kizamani na hayafai kitu?

Kuna uhusiano gani kati ya kuwa Muislamu na kumpa mtoto jina la kiarabu? Au mkristo kumpa mtoto jina la Kizungu kama Frank, Aboubakar, Sameer, Chris, Dorice, Khadija

Kwanini sio majina ya kichina au kihindi? Labda dini ni kitu chema lakini isiondoe u-Afrika wetu. Tujitafakari.
Kuna shule wanangu wansoma ayaaaa kama unasomewa majina halafu uko darasa lingine huwezi amani kama ni waafrika watoto wenye majina ya kabila ni wanangu tu na wanaonekana mastaa
 
Back
Top Bottom