Kuwapa watoto majina ya kigeni Kizungu/Kiarabu ndio usasa au kutojitambua?

Kuwapa watoto majina ya kigeni Kizungu/Kiarabu ndio usasa au kutojitambua?

Waafrika tumepoteza dira , angalia mtu anaondoa ngozi yake ya asili ili aonekane Kama mzungu ! Ni uuuuungwana ?
 
Mwita hapa kutoka mara

Mtu mrefu ajabu.

Jina la kiyahudi naitwa solomon.

Hakuna mwafrika mwenye jina moja katika zama hizi za kubatizana

Tushatishwa bila ubatizo na kuzaliwa upya huendi mbinguni
 
Acha zako wewe,kwani lazima uwaze kwenye negativity Tu

Lulu
Furaha
neema
Waridi

Haya siyo majina mazuri ya Kiswahili ya kuwapa watoto mkuu? Wenzetu wapo ulaya lkn Wana wanawaita watoto "Dele Ali " " wale" na rotimi

Tuondoe hii dhana ya kila jina la Kiswahili ni Baya na kina mikosi asee!!!
Mkuu mbona Povu???
Mwanao umemwita Lulu nini
 
Wakoloni wamefanikiwa sana kutawala Afrika enzi za ukoloni baada ya mkutano wa berlini na sasa kiuchumi na kifikra.

Silaha moja wapo kubwa ya kumtawala mtu ni kumfanya aache asili yake na utamaduni wake audharau afuate wako. Ukimaliza hatua hiyo hatokuwa na nguvu ya kukupinga tena.

Wazungu wamefanikiwa katika hilo, leo majina ya asili, dawa asili, chakula asili, utamaduni asili unaonekana ushamba au ni uchawi...vyakuja vinatukuzwa, hakika tupo katika hasara.

Kina chief Mkwawa na Kinjikitile huko walipo wanasikitika walipigana bure tu.
 
Siwezi kushangaa sana ukisema hivyo.

Kwa sababu Watanzania wengi wamezoea maisha ya kijima, ya kufuatiliana fuatiliana, maisha ambayo mtu haamui mambo yake mwenyee, mambo yanaamuliwa na jamii, maisha ya kuzongana, kuchunguzana, kufuatiliana.

Ni hivi, mtu ana haki ya kuamua anampa mtoto wake jina gani.

Ukianza kumuingilia kwenye hilo, unamuingilia kwenye mambo ya ndani ya familia yake.

Wewe kama hupendi jina fulani, tafuta mtoto wako umpe jina unalolipenda wewe.Na mtu akikuingilia katika hili, hata wewe nitaitetea haki yako hii ya msingi.

Kwa nini uanze kulazimisha mtu baki achague jina unalolipenda wewe na asilolipenda yeye?

Yani mtu katafuta mtoto kivyake, jina umpangie sheria wewe?

Wewe mtu akikupangia jina la kumpa mtoto wako usilolipenda wewe, analolipenda yeye, utaona sawa?

Acheni mambo ya zama za ujima kila kitu kinaamuliwa na kijiji.

Jina la mtoto lisipopitishwa na kikao cha kijiji huwezi kumpa mtptp hilo jina.

Huu ndiyo mwanzo wa kusema wote tupigie kura CCM, kwa sababu mwenyekiti wa kijiji kasema.

Groupthink.

Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya groupthink ya aina hii na umasikini.
Mimi nimeita wanangu majina ya kienyeji

Jambo la kuchekesha watu ambao ndio nilitakiwa niwacheke eti wao ndio wananicheka mimi, hapo ndio nilipojenga tabia ya kuwapangia kama wanavyonipangia

Yaani mtumwa wa kifikra ananicheka niliyejitambua, sijui weusi tukoje
 
Kuna fahari na raha kubwa kufurahia asili yako. Hujisikiii mnyonge na huwezi kujidharau hata ukidharauliwa na yeyote. Mimi ni Mnyakyusa kamili na majina yangu yote ni ya Kinyakyusa, yaani Gwandumi Gwappo (Gwapponile) Atufwene Mwakatobe Mwakimenya. Asili yangu ni Mwakaleli, wilayani Rungwe, mkoani Mbeya

Nawasikitikia ambao asili ya majina yao imepotea kabisa. Mathalani Abdul Salmin Amour Juma, Victor Robert Willy Henry au Longinus Lawrence Recocatus Deogratius.

Nasikia zamani wakoloni walikuwa wanakataa waafrika kubatizwa au kuandikishwa shuleni kwa majina yetu ya asili. Tumerithi hata visivyo riziki!
Wanyakyusa hatunaga shobo na uzungu
 
Mwita hapa kutoka mara

Mtu mrefu ajabu.

Jina la kiyahudi naitwa solomon.

Hakuna mwafrika mwenye jina moja katika zama hizi za kubatizana

Tushatishwa bila ubatizo na kuzaliwa upya huendi mbinguni
Usifikiri matatizo yako wote tunayo

Binafsi sina jina la kibeberu na haitakaa itokee huo moto wa milele mtachomwa mnaoamini
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]amepewa jina la kikatuni
 
Habari salamu sio ndefu nimechefukwa mtoto wa dada yangu kapewa jina Moana, jina la kikatuni cha Disney nikapata maswali sana, kwanini hadi leo tunaendelea kushikilia majina ya wageni? Majina mazuri ya Kiswahili, lugha za asili yameisha au ndio tunayaona ya kizamani na hayafai kitu?

Kuna uhusiano gani kati ya kuwa Muislamu na kumpa mtoto jina la kiarabu? Au mkristo kumpa mtoto jina la Kizungu kama Frank, Aboubakar, Sameer, Chris, Dorice, Khadija

Kwanini sio majina ya kichina au kihindi? Labda dini ni kitu chema lakini isiondoe u-Afrika wetu. Tujitafakari.
Wewe mfuasi wa shetani.majina yote ni ya dini kuu mbili.uislamu na ukristo.sasa uafrika wako upo wapi?wahindi wanaabudu ngombe,wachina wanaabudu jua.isitoshe kama unao watoto wape majina unayoyataka.mmoja mwite mavi,mwingine mkojo,Ngombe,Kondoo,pakan.k. Upo huru.Sasa nimeelewa kwa nini makampuni ya simu yalipandisha gharama za Internet.mijitu inaandika upuuzi tu.
 
Wewe mfuasi wa shetani.majina yote ni ya dini kuu mbili.uislamu na ukristo.sasa uafrika wako upo wapi?wahindi wanaabudu ngombe,wachina wanaabudu jua.isitoshe kama unao watoto wape majina unayoyataka.mmoja mwite mavi,mwingine mkojo,Ngombe,Kondoo,pakan.k. Upo huru.Sasa nimeelewa kwa nini makampuni ya simu yalipandisha gharama za Internet.mijitu inaandika upuuzi tu.
Umeamua kuandika matusi na hukuelewa nilichoandika,nimekusamehe
 
Sahizi mtoto ukimuita majina kama masanja, mabula, misoji, minza, rhobi na mengineyo mengi unaitwa mchawi pia unaabudu mizimu. Wengine huenda mbali na kudai mizimu ya mababu huwafuata watoto, acha tusonge hivi hivi.
Kwenye mizimu inaweza kuwa na ukweli mkubwa!

Unaweza kushangaa mtoto anaandamwa na mapepo kumbe jina tu la ukoo ulilompa ndio chanzo! Maana unamfungamanisha na maagano ya kichawi ya ukoo!

Bora umuite Bahati au furaha au malaika.

Unaweza kumuita mtoto majina kama Tanzanite, au Africa, au Dhahabu, au Almasi au simba nk.
 
Hata hao wachina wana majina ya kizungu,. Kiarabu na asili (roots). Kinacho kuchanganya ni lugha na herufi, kumbuka kila jina lina maana yake jaribu kutafuta dictionary halafu tazama tafsiri za majina na maana yake bila shaka huta hangaika kuelewa ni kwanini ulipewa jina ulilo kuwa nalo.
 
Back
Top Bottom