Kwa CCM kuingiza siasa kwenye taifa stars, dua langu ni kesho tuaibishwe na Morocco

Kwa CCM kuingiza siasa kwenye taifa stars, dua langu ni kesho tuaibishwe na Morocco

Inabidi viongozi wa CCM wajue kuwa Tanzania ni nchi yenye vyama vingi vya siasa, iache kuvamia kila tukio la kitaifa kuwa la CCM.

Kitendo cha kuingiza kampeni za uchaguzi 2025 kwenye kutafuta nafasi ya Kombe la Dunia 2026, sisi tusioiunga mkono CCM tutaanza kufunga na kuomba dua ili tufungwe katika michezo iliyobaki kuanzia kesho, amina.
Michezo ni burudani tu hata hiyo kesho wataoenda wataenda km kuangalia burudani tu ila sio kwenda kushinda hatuwezi kuwafunga hata kusuluhu na hao Morocco viwango vyao ni vikubwa sana.
 
Michezo ni burudani tu hata hiyo kesho wataoenda wataenda km kuangalia burudani tu ila sio kwenda kushinda hatuwezi kuwafunga hata kusuluhu na hao Morocco viwango vyao ni vikubwa sana.
Hukumsikia Msigwa?
 
Hizo story ilikuwa zamani, kwenye chaguzi tunaona kinachoendelea Wala sio Siri tena. Ccm inaigiza kufanya siasa kwa sababu kinapata upendeleo wa Dola kufanya siasa. Lakini uhayawani unaoendelea kwenye chaguzi zetu, haukipi jeuri ccm kuwa inakubalika hivyo. Na kadiri uchaguzi unavyotokea kuheshimiwa, ndio ccm inavyopoteza uwakilishi wake.

Ndio maana tunataka tume huru ya uchaguzi, ambayo itaweka uhalisia wa ccm kukubalika kwake. Na kwakuwa ccm inajua ukweli huo haiko tayari kwa tume huru ya uchaguzi, Wala katiba halisi ya wananchi. Machafuko tu ama mapinduzi ya kijeshi ndio yataionyesha ccm Iko mazingira gani hapa nchini.
Kila sekta serikali Inapambana kuleta hali bora zaidi kuanzia maji mpaka afya.

Zahanati zinajengwa Kila mahali viwanja vya ndege vinajengwa kila mahali elimu unashughulikiwa kila mkoa,
Umeme unasambaa kwa kasi ya radi, madaraja na reli zinaendelea kujengwa kila kanda ya Tanzania.

Chungeni sana, mnazeeka na vinyongo pamoja na chuki vitu ambavyo haviwasaidii.
 
Hao huwa wanajigawa wenyewe hakuna mtanzania anayehusika hapo.
Sisi mashabiki wao tunafurahia sana namna wanavyoshindana wakiwa humu ndani.

Wanapotoka huko nje wanaendeleza huo ugomvi wao. Tazama wanamuziki wa kinigeria wanatambulishwa kimataifa.

Wanaitwa Nigerian artists wakiwa kwao wanaweza kuwa wanajigawa kwa makundi lakini wakiwa nje ya nchi wao ni kitu kimoja.

Watanzania tunapenda sana kuendekeza chuki za kijinga.
 
ccm ndio zao ndio yale ya madogo wa Zanzibar u15 kukamatishwa mabango ya chama baada ya kuchukua kombe na wakati wa kwenda uganda waliwapeleka kwa mabasi
Walitoka Zanzibar na Basi mpaka Uganda??

Hapo walistahili kushinda.
 
Kila sekta serikali Inapambana kuleta hali bora zaidi kuanzia maji mpaka afya.

Zahanati zinajengwa Kila mahali viwanja vya ndege vinajengwa kila mahali elimu unashughulikiwa kila mkoa,
Umeme unasambaa kwa kasi ya radi, madaraja na reli zinaendelea kujengwa kila kanda ya Tanzania.

Chungeni sana, mnazeeka na vinyongo pamoja na chuki vitu ambavyo haviwasaidii.
Huo ni wajibu wa serekali yoyote sio hisani. Tusichotataka ni kutawaliwa na ccm kwa shuruti. Kwani lazima mkae nyie madarakani wakati watu tumewachoka?
 
Huo ni wajibu wa serekali yoyote sio hisani. Tusichotataka ni kutawaliwa na ccm kwa shuruti. Kwani lazima mkae nyie madarakani wakati watu tumewachoka?
Pambaneni mpate ridhaa halali ya wananchi sio kulialia humu JF. Na uongozi wa CDM hauna usafi wowote na pia mwenyekiti Mbowe ni tawi la usalama wa taifa hivyo hao mnaowaamini kuwa ni viongozi wa kuiondoa CCM ikulu ni matawi tu ya chama kinachodaiwa kuchokwa na wananchi. Ni masuala magumu kuliko tunavyoyachukulia.
 
Back
Top Bottom