Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Mkuu George Betram Kuna wazo pale juu kakupa kaka mshana jr naomba ulifanyie kazi.

Sijajua upo mji gani na chuo gani, lkn nakushauri jiingize ktk biashara ya mitumba.

Anza na bidhaa za mitumba za wadada. Usinunue BARO, nenda kwa ile style ya KUPOINT zile unazoona zina ubora. Kwa upande wa nguo, kama ungekuwa DSM, ni kujihimu pale Karume alfajir ya kila Jumamosi, KUPOINT. Kwa hiyo laki5, inatosha kuchota laki 3 na kuanza biashara huku ukipima upepo ulivo.

Ukirudi chuo unaziongezea ubora kwa kuzipiga pasi. Uuzaji wako unakuwa ni wa kuwafuata wateja wako hostel kwao, chumba kwa chumba!

Ndani ya biashara hii utaanza kupata oda za wateja wako nini wanataka ukawaletee kutoka sokoni. Wadada wengi hawana muda wa KUZURURA ktk masoko ya mitumba.

Nimekushauri ujihusishe na bidhaa za wadada kwa vile ktk maisha ya Chuo, wadada wanaongoza KUSHINDANA KUVAA kuliko men. Pia wadada kama utakuwa makini hamtasumbuana sana ktk malipo.

Wanaume baadhi wawapo chuo huweka pembeni hobby ya mavazi na wengi huigiza HIP HOP ama UGUMU lkn nyuma ya pazia wanamaanisha.
Ahsante sana kaka Slim5 bila shaka nitalifanyia kazi wazo hili...
Lakini umenifanya nicheke sana mkuu..!
 
Ebana laki moja ni ndogo kidogo, unaweza kufanya biashara ndogo ndogo inategemea uko Katiba mazingira gani na una connection zipi. Unaweza chukua mashirt, T-shirt, boxers, nguo za wadada , Sox za kiume, viatu vya mtumba vya wadada, kadet , skirt nzuri mtumba first clasa, jeans, nguo za office za mtumba, mashuka ya mtumba, pochi za wadada.. nk unachukua bidhaa kko au karume, then unatfuta soko unauza!! Kuna watu wanaishi hivyo miaka yote
nitafanyia kazi wazo lako
na vipi bei naweza nikapata kwa sh ngapi
 
kwa hili swali lako nakushauri usifanye biashara kabisa, fuga kuku
why nifuge kuku na mimi interest yangu ni biashara
nimeuliza bei za jumla ili nilinganishe kutokana na eneo nililopo kuwa nitapata faida au lah
mfano viatu vya kike kwa bei ya jumla hapo karume
but poa
 
Naomba mchango wa kima wazo, nina laki 5 nifanye issue gan?
Npo .....Dodoma (UDOM)
Age ..... 27
Plz tia neno...............
 
Mkuu ngoja nikupe kitu ambacho kipo humu jf, humu siku zote Wana zarau mtaji mdogo tena wengi wao ni wale ambao hawana dira ya nini cha kufanya ila wapo ambao wapo sensitive wapatakupa kile chenye maono. Kitu cha kufanya fanya utafiti kwa sehemu ambazo unatembelea hasa vijijin Kuna fursa nying Sana.... Embu jiulize mhindi na mwarabu ndo huwa na hii tabia ya kukimbilia vijijin Kuna nin kijijin,,,,,,?! Mbona mim na wew tunapakimbia lakin wagen wanapakimbilia..... Laki tano nikubwa Sana huko vijijin nenda kaangalie fursa huko ni kipi kinauhitaji mjini ambacho kipo huko shamba,.... Juzi nilikuwa huko nikakuta Lita ya maziwa n 500 na bado hayapati mteja lkn hayo maziwa mjini kikombe kinaanzia jero to buku,,,,,,, zipo nyingi sema mi c mwandishi mzuri ila kitu muhimu usikubali kukatishwa tamaaa na wachache ambao wanataka kupata buku lakin kashindwa kutumia akili ili apate hamsin na kila siku yeye anasubir kumbe ndo wenzake wanamuacha hivyo yeye kila siku kesho kesho
Gud idea
 
Mungu Awabariki sana uzi huu,hapa hata ukisema una shilingi hamsini unataka kufanya nini,hamna atakayekubeza,utapewa ushauri nini ufanye,mnawakomboa watu wengi sana ki fikra katika ujasiriamali,mnatoa ile dhana nzima kuwa mpaka uwe na mamilioni ndo ufanye biashara
 
Hii posti nimeikuta humu humu, kama imani yako inaruhusu na una mtaji wa kma laki 5 basi fanya research then anza hivi kama jamaa anavyotoa ushuhuda wake...


Ufugaji wa nguruwe ulivyonipa utajiri na kujitegemea

Habari wanaJF

Tafadhali kwa wale wasiopenda jina hilo hapo juu samahani sana.

Mimi nimefuga nguruwe, nilianza nikiwa niko chuo kikuu mwaka wa pili pale UDSM kwa mtaji wa shilingi 500,000/=

Nilianza kujenga zizi kwa shilingi laki tatu tu na nikanunua makinda ya nguruwe mawili jike na dume kila mmoja sh. @40,000 (mradi niliufungua nyumbani mkoani Kigoma). Fedha zilizobakia nilitafuta mfanyakazi wa kuwalisha hao nguruwe. Nilimlipa sh. 40000 kwa mwezi. Kati ya laki 5, zilibaki 80,000 ambazo nilianza kwa kunulia chakula cha nguruwe.

Baada ya hapo nguruwe niliwapandisha wakazaa watoto 10. Kati ya hao madume yalikuwa 4 na jike 6. Baada ya hayo makinda kukua sikuuza makinda ya jike. niliamua kupanua mradi hivyo nilipanua zizi! Hapo ilikuwa baada ya miezi tisa tu.

Baada ya kupanua mradi niliuza madume 3 nikanunua vyakula (maharage yaliyooza na mashudu) ya kulishia nguruwe waliobakia.

Baada ya miezi 18 nguruwe waliongezeka baada ya kuzaa tena (yale majike 6 na dume 1). Nikaendelea kupanua zizi maana nilijikuta nina nguruwe 30. Kumbuka nguruwe sita wote walizaa. Mmoja makinda 6, mwingine 5, mwingine 5 mwingine 4 mwingine 7 na mwingine 2, na lile dume 1. Jumla nguruwe 30.

Nazidi kupanua mradi na chuo nimeshamaliza kwa sasa nasimamia mwenyewe!

Hakika kwa sasa mimi ni tajiri!

Amini usiamini mimi sio masikini tena!

siku njema.
 
Heshima kwenu wakuu
Nina laki tano nataka kuanzisha Biashara..naogopa kukurupuka
Wazoefu nisaidieni je naweza kuanzisha Biashara gani ikalipa?
Naishi Mburahati
 
Back
Top Bottom