Kwa mujibu wa Biblia, unaweza kujikuta wewe ni mmoja ya watu ambao Mungu aliwakataa hata kabla hawajazaliwa

Biblia iko zigzag. Mungu ana wateule wake, tangu mwanzo anajua wewe ni wa kundi gani. Mwandishi mwingine anasema unapo kufa ndio unajua umejiwekea historia gani!
 
... kinyume chake ndio ingekuwa ajabu; Mungu asiwafahamu walio wake!? Zingatia; kabla ya kuumbwa ulimwengu alishaumba viumbe wengine na waliomtii anawafahamu toka enzi hizo (kabla ulimwengu kuumbwa) hadi sasa. Hao ndio walio wake.
 
Ili kuwasaidia wale wanaoweza kupotoshwa na bandiko lako,..

Walio wa Mungu ni wale waliouacha uovu, kama ukisoma mstari mzima 2Timotheo 2:19, imeandikwa "Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake, Na tena kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu"
Kila mwanadamu amepewa nafasi ya kuwa wa Mungu, hakuna ubaguzi, Yohana 3:16, " Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili KILA amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele"
Tena Yohana 1:12" Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu" Neno KILA na WOTE hayaonyeshi ubaguzi.

Kuna watu wanaojipambanua kuwa ni wa Mungu, lakini Mungu ana muhuri wake wa kumtambulisha mtu kuwa ni wake, nao ni utakatifu, ndiyo maana akasema anawajua walio wake, na siku ile ya hukumu atawaambia wale watumishi wanaohubiri na kuombea watu wakati wao ni walevi, wazinzi, waongo, n.k kuwa "Sikuwajua ninyi kamwe, ondokeni kwangu ninyi mtendao mauvu..." Mathayo 7:23.

Hapo anawafukuza kwa kutokuwajua kwa sababu gani? kwa sababu ya kutenda uovu.
Maandiko haya yatakusaidia pia Yohana 10:26-27.
 
Hii nilimsoma katika The Children of the matrix yule father ata lecture zake kama kichwa umekaza huwezi kumuelewa kabisa.
 
KWA ninavyojua MUNGU ana sifa ya OMNIPOTENCE mwenye nguvu zote, omnipresence aliyeko kila mahali, alafu kuna omniscience anayejua kila kitu. Anafahamu kabla hata ya kuwepo tumboni mwa mama yako. Kwanini tusiseme kwamba kuanzia adamu anatenda dhambi mpaka kufikia DUNIA ilipo MUNGU alikuwa anafahamu itakuwa hivi? Jaman mimi huwa najiuliza tu ila naamini katika uwepo wa MUNGU. Naomba mwenye jibu anisaidie tuelimishane
 
Nitajuaje Mungu ananitambua ili nimuabudu? Mtu unaweza kupasua Sala mchana na usiku kumbe hakutambui na wala hajui kama upo duniani. Atheists ndio wanaoishi kwa raha, wao hawaangalii makunyanzi.
 
Hizi dini kuzifuata mkuu sharti uwe si mtu wa kuhoji na kutumia logic.
ngoja mfia dini aje hapa atudadavulie juu ya hayo mambo 3.
  1. Tumezaliwa na dhambi ya asili kwaiyo we are just unworthy piece of s##t from day we arrived on the planet.
  2. You can only be saved by believing in the savior , and that means doing what the priesthood tell you to do.
  3. If you don't do that , you will be condemned to the bowels of hell forever.
KIUKWELI UHITAJIKUWA NA IQ kubwa kutambua kuwa kunajanja janja inafanywa na jamii ya watu kuwahadaa waAFRICA.
 
Nitajuaje Mungu ananitambua ili nimuabudu? Mtu unaweza kupasua Sala mchana na usiku kumbe hakutambui na wala hajui kama upo duniani. Atheists ndio wanaoishi kwa raha, wao hawaangalii makunyanzi.
Dini ni mipango ya watu kupiga hela, kukuamulia jinsi ya kuishi, kufikiri na kuamua mambo.

Ukifuata dini unakua kama liloboti.
 
Una weza kuwa binadamu ila sio mtu , mtu anatokana na utu , kama huna utu wewe sio mtu ila ni binadamu. Ili uwe mtu inakupasa uwe na utu , ila kuwa binadamu ni lazima bila hata kuwa mtu.
 
Shida yenu huwa mnaisoma Biblia na kuitafsiri vile vile na Mara nyingi huwa mnakosea katika tafsiri zenu.

Oyaa Biblia sio kitabu Cha kawaida Kama vitabu vya shuleni.Hicho Ni kitabu kitakatifu Sana na Mara nyingi huwa nashauri kabla hujaifungua Biblia na kuanza kuisoma, muombe Mungu akupe uwezo wa kuelewa kile utakachokisoma bila kupotosha maana iliyokusudiwa.
 
MKUU kabla ya kusoma biblia kuna prior knowledge itakupasa uwenazo.

nimegundua unakaFEAR flani ndani yako
 
ungesema tatizo hatuishi na kufuata maagizo tuliyopewa kwenye biblia ningekuunga mkono.
 
Saa nyingine ukisoma sana mambo ya dini unaweza kuchanganyikiwa. Kwa mfano Yesu alimwambia Petro utanikana.. sasa kama ilikuwa hivyo si angemuepusha tu Petro hilo lisitokee? Ukienda agano la kale wale waisrael walipotoka Misri hawakuwa na pa kufikia kwahiyo walikuwa wakikuta mji wanaushambulia na kuwaua wenyeji wote.. kiongozi wa yale mauaji ya kutisha alikuwa akiitwa Joshua. Na kwenye mchakato wa yale mauaji alikuwa na usaidizi wa karibu sana wa Mungu. Dini zetu za mizimu nadhani ni bora sana kwasababu hazina huu upuuzi wa kupanikisha watu.
 
Nahuko kuchanganyikiwa ni sehemu ya ajenda ya walioandika hicho kitabu.

don't take it too serious bro.
kinamafundisho mengi na mazuri sana pia kina burudani kibao drama za kutosha.

japo iliniuma mussa hakutoboa kufika nchi ya ahadi.
hahahahaha
 
Agano la Kale ni Jino kwa Jino na Jicho kwa Jicho

Agano Jipya ni Upendo, ukipigwa kofi kushoto geuza kulia na usirudishe kofi, ukipokonywa koti mpe na shati, akikupora viatu mpe na soksi, akikuchojoa suruali msusie na boksa kabisa kisha baki uchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…