Kwa tabia hii una tofauti gani na Ibilisi?

Kwa tabia hii una tofauti gani na Ibilisi?

Naam ibilis

Mungu aliumba kila kitu lkn kwakuwa yeye ndio muumbaji basi huwezi sema ana sifa mbaya

Yeye anajinasibisha na sifa sifa nzuri nzuri kabisa
Na je kila kilichopo duniani mungu aliumba yeye au matokeo ya fikra za watu
 
Taja jambo moja ambalo ibilis kafanya na mm nakuwa anauofanya binadamu picha limenza kala tunda kaambiwa usile tunda yeye kala baada ya kula tunda akawa uchi unadhani wazinifu wa sasa walipata ujasiri kama sio kwa baba yao adam alipoambiwa usile yaan usifanya yeye anfanya
"Basi akawateremsha wao kutoka kwenye daraja zao kwa hadaa, na wakati walipouonja ule mti zilidhihiri tupu zao{baada ya kuwa ni zenye kusitiriwa} na wakaingilia {wakaanza} wanajifunika majani ya mti huko peponi na akawaita wao mola wao akiwaambia je! kwani sikuwakatazeni kula mti huo? na kwani sikuwaambia nyinyi hakika shetani Iblis Bin Shetan kwenu nyinyi ni adui mwenye kudhihirisha uadui?.."

Quran 7:22


uasi wa aadam alayhi ssalaam ni kwa ushawishi wa shetani unayemsifu hapa.
 
Naheshimu maoni yako mkuu

Karibu sana
Huo mfano wa CEO ndo umekosea.

Nina real life experience, nlikua kiongoz sehemu fln kwenye branch mojawapo ya barrick, yalonikuta sitosahau, lkn usijepoteza muda wako na masikini, watu wa chini ni watu wa chini tu. Bora wakuone una kiburi kuliko kuwajalu halafu haohao waje wasababishe yakutokee puani.

Nlipoteza cheo kisa huo upuuzi na sitorudia tena kujifanya najali watu wa chini, wapande ladder wenyewe wafike
 
"Basi akawateremsha wao kutoka kwenye daraja zao kwa hadaa, na wakati walipouonja ule mti zilidhihiri tupu zao{baada ya kuwa ni zenye kusitiriwa} na wakaingilia {wakaanza} wanajifunika majani ya mti huko peponi na akawaita wao mola wao akiwaambia je! kwani sikuwakatazeni kula mti huo? na kwani sikuwaambia nyinyi hakika shetani Iblis Bin Shetan kwenu nyinyi ni adui mwenye kudhihirisha uadui?.."

Quran 7:22


uasi wa aadam alayhi ssalaam ni kwa ushawishi wa shetani unayemsifu hapa.
Hili andiko lilikuja uadui wa iblis na mwanadamu pale alipoambiwa amsijidie na hapo adam yupo na hawa mm nataka adam anapuliziwa roho na iblis kuwa adui unipe hilo andiko sio unipe andiko baada ya adam kuumbwa
 
Naam ibilis

Mungu aliumba kila kitu lkn kwakuwa yeye ndio muumbaji basi huwezi sema ana sifa mbaya

Yeye anajinasibisha na sifa sifa nzuri nzuri kabisa
Jibu jepesi ni kuwa allah anaumba vitu anavyovipenda na asivyovipenda pia, ameumba mema hali ya kuwa anayapenda na ameumba maovu hali ya kuwa anayachukia na amemuumba ibliys, firauni, qaarun, haaman na umayyah ibn khalaf na wenzie na hali ya kuwa anawachukia.

Haulizwi kwa anayoyafanya kwani yeye hafanyi kitu kwa upuuzi bali anafanya mambo yake kwa hekima iliyotakasika kabisa, سبحانه و تعالى عمّا يقولون علوّا كبيرا
 
Hili andiko lilikuja uadui wa iblis na mwanadamu pale alipoambiwa amsijidie na hapo adam yupo na hawa mm nataka adam anapuliziwa roho na iblis kuwa adui unipe hilo andiko sio unipe andiko baada ya adam kuumbwa
Wakati malaika wanamwambia allah atamuumba mwanadamu atamwaga damu na kufanya ufisadi katika ardhi yeye aliwajibu mimi ninayajua yale msiyoyajua, wanawachuoni wametaja kuwa ni kuwa mnaye nyie kati yenu mwenye kiburi na muovu mno na hamumjui mpaka pale alipodhihirisha kiburi chake wakati amepewa amri ya kusujudu naye ni Iblis Bin Shetan na wala kutokudhihiri uovu wake kabla aadam hajaumbwa hakubadilishi kitu.
 
Wakati malaika wanamwambia allah atamuumba mwanadamu atamwaga damu na kufanya ufisadi katika ardhi yeye aliwajibu mimi ninayajua yale msiyoyajua, wanawachuoni wametaja kuwa ni kuwa mnaye nyie kati yenu mwenye kiburi na muovu mno na hamumjui mpaka pale alipodhihirisha kiburi chake wakati amepewa amri ya kusujudu naye ni Iblis Bin Shetan na wala kutokudhihiri uovu wake kabla aadam hajaumbwa hakubadilishi kitu.
kumbe wanachuoni sio mungu kama wanchuoni hamna kitu hao sio ndio leo wanabishana na kutofautiana habari za mwezi mtume anasema usifunge siku ya iddi kuna waislam wanafunga kupitia hao wanchuoni hao wanchuoni ni fitna hawanaa wanachojua kila mtu anvuta kwake sunni anampinga shiya na ahmadiya anawapinga wote unaweza kuona wanachuoni hamna kitu kama quran haijasema iblis alimchukia adam wakat wakupuliziwa roho hayo maneno usiyatumie tena maana ukiyatumia nitakuuliza umeyatoa wapi
 
Mkuu hizi ni ngano na hekaya tu. Chanzo cha wanadamu wote siyo Adam. Kama adam alikuwa binadamu wa kwanza nipe sababu ya kwanini wengine ni weusi wengine weupe
Mwanadamu anapotumia akili yake kwenye mambo yaliyomzidi kimo, uzito na umri ndio matokeo yake haya.

Mkuu babu yako huwezi kumjua mpaka utambulishwe na wanaomfahamu hata kama una akili za namna gani, vilevile habari za kale huwezi kuzijua mpaka usome historia sahihi hata kama una akili kubwa kiasi gani, mwisho mtu wa nyuma ya ukuta wako huwezi kumjua mpaka utoke ukachungulie hata kama una akili za namna gani, sasa nakujibu.

"Enyi watu! hakika sisi tumewaumba kutokana na mwanaume mmoja na mwanamke mmoja, na tumekufanyeni kuwa ni mataifa na makabila mbalimbali ili mpate kujuana, hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu mbele za allah ni yule mchamungu zaidi kwenu, hakika allah ni mwenye elimu, mwenye khabari zote."

Qur'an 49:13
 
kumbe wanachuoni sio mungu kama wanchuoni hamna kitu hao sio ndio leo wanabishana na kutofautiana habari za mwezi mtume anasema usifunge siku ya iddi kuna waislam wanafunga kupitia hao wanchuoni hao wanchuoni ni fitna hawanaa wanachojua kila mtu anvuta kwake sunni anampinga shiya na ahmadiya anawapinga wote unaweza kuona wanachuoni hamna kitu kama quran haijasema iblis alimchukia adam wakat wakupuliziwa roho hayo maneno usiyatumie tena maana ukiyatumia nitakuuliza umeyatoa wapi
Usidhani umetoa hoja nzito, kwani quran ndio ushahidi pekee si kuna hadithi za mtume muhammad? haufahamu wewe kuwa ibliys alikuwa anamchezea aadam akimuingilia mdomoni na kutokea kwenye tupu yake ya nyuma wakati huo hajapuliziwa roho ameumbwa tu kwa udongo na ameachwa akiwa maiti?.

Sasa nakuuliza kwani kuna faida gani kujua alikuwa muovu kabla ya kupuliziwa roho aadam na baada yaani ndio nini, kuna faida gani?.
 
kama sababu ni hii basi shetani alionewa.
ushahidi unaonyesha sababu ya binaadm kuwa bora mbele za Mungu ni ya upendeleo zaidi wala sio ya uwezo na viwango.shetani kwa daraja alilokuwepo na uwezo alio nao inaonyesha wazi kumsujudia adam ilikuwa ni kumdhalilisha.

by the way,bible inasema shetani alifanya kiburi pia lakini si kumsujudia adam,bali kujaribu kujiinua hata mbele za Mungu baada ya kupewa nguvu kubwa,cheo na vipaji,akajiona anaweza akafanya jambo[emoji23],kilichompata kikawa kimempata,akafukuzwa na kuja kukaa duniani,lakini kwa hasira akatamka kwamba hakuna jambo jema la Mungu ataruhusu lifanyike mbele yake anaona.
 
Huo mfano wa CEO ndo umekosea.

Nina real life experience, nlikua kiongoz sehemu fln kwenye branch mojawapo ya barrick, yalonikuta sitosahau, lkn usijepoteza muda wako na masikini, watu wa chini ni watu wa chini tu. Bora wakuone una kiburi kuliko kuwajalu halafu haohao waje wasababishe yakutokee puani.

Nlipoteza cheo kisa huo upuuzi na sitorudia tena kujifanya najali watu wa chini, wapande ladder wenyewe wafike
Kwanza pole Sana mkuu Kwa huo mtihani

Hata nami nilitaka kurogwa Kwa kuwasaidia hao wakulungwa

Lakini

Tukiwahukumu wote tutakuwa tunakosea,naamini kuna wengine ambao sio wabaya kiasi Hicho

Ila

Uzoefu unaonyesha watu WA juu ndio huwa na viburi zaidi mkuu
 
kama sababu ni hii basi shetani alionewa.
ushahidi unaonyesha sababu ya binaadm kuwa bora mbele za Mungu ni ya upendeleo zaidi wala sio ya uwezo na viwango.shetani kwa daraja alilokuwepo na uwezo alio nao inaonyesha wazi kumsujudia adam ilikuwa ni kumdhalilisha.

by the way,bible inasema shetani alifanya kiburi pia lakini si kumsujudia adam,bali kujaribu kujiinua hata mbele za Mungu baada ya kupewa nguvu kubwa,cheo na vipaji,akajiona anaweza akafanya jambo[emoji23],kilichompata kikawa kimempata,akafukuzwa na kuja kukaa duniani,lakini kwa hasira akatamka kwamba hakuna jambo jema la Mungu ataruhusu lifanyike mbele yake anaona.
Mkuu kama ulivyosema na kutoa mfano hapo huyu shwaini hajaonewa wewe mwenyewe umetoa mfano katika Biblia jinsi alivyo haribu

Anastahili kupita huku huyo.
 
Tabia iliyomponza Ibilisi ni KIBURI. Baada ya kuambiwa na Mwenyezi Mungu amsujudie Adam sijida ya heshima basi yeye alikataa Kwa kujawa na Kiburi kwasababu yeye alijiona Bora Sana .

Na alipoambiwa kwanini ulikataa kumsujudia Adam akasema;

Mimi ni Bora nimeumbwa Kwa Moto na yeye ameumbwa na Udongo

Kwahiyo Ibilisi akajiona yeye ni Bora zaidi ndio maana akakataa amri ya ya Mola wake.

Na Mwenyezi Mungu anasema hakika Kiburi ndio vazi lake kwahiyo yeyote ambaye analeta kiburi basi anafanya kosa kubwa Sana.

Na ili ujue Kibri ni kosa kubwa Sana mpaka Mwenyezi Mungu akamhukumu Ibilisi aende Motoni ,ebu tuangalie Ibilisi alikuwa wa namna gani.

Inasemwa Ibilisi alikuwa anafanya ibada Sana kiasi ambacho hakuna sehemu yoyote katika ardhi hakuacha Kusujudu,alisujudu kila sehemu Kwa AJILI ya kumwabudu Mola wake

Lakini

Pamoja na yote hayo basi Kiburi kikamuweka mbali na Mola wake na kuhukumiwa adhabu mbaya kabisa


Sasa baadhi yetu nasi tuna Uibilisi Fulani hivi ingawa ukitutazama machoni tunaonekana kama watu vile lakini tumejawa na Kiburi kupindukia katika Maisha yetu.

Kisa wewe ni CEO sehemu Fulani basi unajiona wewe ndio wewe, unajiona mpanaaa na wengine wote unawaona hawana maana kabisa,husikilizi shida za wafanyakazi wako,hujali mahitaji Yao kwasababu wewe ndio kila kitu hapo,usichojua ni kwamba kila kitu kina mwisho na IPO siku hiyo nafasi utaiacha, kwahiyo usitumie cheo kunyanyasa watu .

Malecture mpo? Nyie nanyi huwa mnajiona mko juu Sana kwasababu Maisha ya taaluma ya mwanachuo yapo mikononi mwenu basi mmejawa na Kiburi kuwa angamiza wanafunzi wenu tena saa nyingine kwasababu za kipuuzi Sana,machoni mnaonekana kama watu lkn mna Uibilisi Fulani hivi.

Madaktari na Manesi mpo? Nyie nanyi kwakuwa afya za binadamu wenzenu zipo mikononi mwenu basi Kiburi ni sehemu ya Maisha yenu. Mko radhi wagonjwa wafe au waendelee kupata maumivu kwasababu Tu ya kiburi chenu,tena hawa manesi ndio balaa kabisa,mnayowafanyia wanawake wenzenu huko sehemu za kujifungua yaani Mungu Tu ndio anajua kwakweli, acheni Kiburi mwisho wenu utakuwa mbaya Sana.

Wana usalama kwanza nawapa Salute Kwa heshima yenu! Lakini nanyi pia huwa mnazingua Sana mnapokuwa katika majukumu yenu,kwa nafasi yenu huwa mna Kiburi Sana kwakuwa mna nguvu ambayo mmepewa na Katiba,niwakumbushe Tu ubinadamu ndio kila kitu katika Maisha IPO siku utaacha hayo majukumu na utarudi mtaani na huenda karma itafanya kazi yake.

Hiyo ni mifano michache Tu ambayo nimeitumia lkn watu viburi ambao Wana Uibilisi ndani yake wapo wengi Sana na wanakiburi Sana Kwa nafasi zao hadhi zao walizo kuwa nazo.

Niwakumbushe Tu kwamba Kiburi ni vazi la Mwenyezi Mungu kwahiyo unapokuwa Kiburi ni kana kwamba unataka kuchukua vazi lake nadhani mwisho wake unaujua utakuwaje.

Niwakumbushe nyie ni viumbe wa Allah hamna mnachokimiliki hapa duniani, kwahiyo muishi vizuri na watu na muwatendee wema daima dawamu ili muwe na mwisho mwema.

Ni hayo tu!

Kazakh destroyer
adriz
Msonjo
baby zu
reymage
To yeye
Mademoiselle
Shukran kwa ukumbusho akhy, Allah akulipe kheri.

Mtume Swalla llahu allaihi wasallam- alipoulizwa ni nini kibri akasema:-
" Ni kuikataa haqi(kweli) na kuwadharau watu".

Tuzitakase nafsi zetu na maradhi haya ya moyo, yaliyokuwa mabaya kabisa, na Mwanadamu anatakabari kwa kipi hasa!

Allah subhaanahu wataa'la anasema:-

"Wala usitembee katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala kufikia urefu wa milima."(7:37).
 
Manesi wengi wa leba ni mawakala wa kuzimu ni maajenti, ndugu YAKO akiingia leba tafuta Mchungaji kabisa na mfunge Ili kukilinda kiumbe chake kisicho na hatia plus mama wa mtoto. Yaani huko hospital ndipo ibilisi amejaa, kila hospital ina mkuu wa pepo anaemiliki anga hilo. Hospital ni njiapanda ya kifo. Life and death.
Roho ya ukatili ya manesi wanapewa na boss wao shetani.
 
Shukran kwa ukumbusho akhy, Allah akulipe kheri.

Mtume Swalla llahu allaihi wasallam- alipoulizwa ni nini kibri akasema:-
" Ni kuikataa haqi(kweli) na kuwadharau watu".

Tuzitakase nafsi zetu na maradhi haya ya moyo, yaliyokuwa mabaya kabisa, na Mwanadamu anatakabari kwa kipi hasa!

Allah subhaanahu wataa'la anasema:-

"Wala usitembee katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala kufikia urefu wa milima."(7:37).
Swadakta Al akhy

Shukrani Kwa neno zuri toka Kwa mtukufu WA daraja
 
Dawa ya kiburi ni kaburi, thus waislamu na wakatoliki wanaagizwa kusafisha makaburi. Hii kitu uondoa roho ya kiburi na kujiona wewe si lolote.
Madhehebu mengine ukizika umezika hakuna kurudi nyuma
 
Manesi wengi wa leba ni mawakala wa kuzimu ni maajenti, ndugu YAKO akiingia leba tafuta Mchungaji kabisa na mfunge Ili kukilinda kiumbe chake kisicho na hatia plus mama wa mtoto. Yaani huko hospital ndipo ibilisi amejaa, kila hospital ina mkuu wa pepo anaemiliki anga hilo. Hospital ni njiapanda ya kifo. Life and death.
Roho ya ukatili ya manesi wanapewa na boss wao shetani.
Swadakt mkuu

Umesema kweli kabisa watu ambao tungetarajia wawe faraja kwetu wamegeuka kuwa maibilisi wakubwa
 
Ukisoma vizuri kitabu cha ARBAIN HADITHY NNAWAY kuna hadihi inasema mtume anasema INNAMAL AMALU BI NIYYAT hakika kila tendo kwa niya na mtu hunuiya anayofanya maana ni kwamba angalia nia ya mtu wengi wenu nyinyi waislam na wakristo ni majina tu matendo yenu zero wazinifu wao wasengenyi wao wezi wao wanafki wao sasa kuna tofauti gani kati ya iblis na waislam au wakristo wa sasa
Noma sana!
 
Back
Top Bottom