Kwa tabia hii una tofauti gani na Ibilisi?

Kwa tabia hii una tofauti gani na Ibilisi?

lakini huoni mungu alimdhalilisha iblis maana iblis tayri alikuwa mtu mkubwa na aliumbwa kabla ya adam alikuwa anaitwa ABAA SAJID baba wa kusujudu ni sawa na ww uwe na cheo flani na hadhi kubwa katika nchi na na umri upatao miaka 50 halafu raisi wa nchi akwambie mwamkie mtoto wa miaka 20 kisa amejibu swali vizuri huo udhalilishaji wa kijinsia
Ndio mitihani hiyo ya maisha mkuu.

Nakumbuka baada ya Magu kuingia madarakani akawatupa baadhi ya watu mikoani.

Baadhi wakawa humble akawarudisha na kuwapa madaraka makubwa.

Wakati mwingine unashushwa ili upandishwe.
 
Haya mambo mi naonaga ni kama tunapigwa changa la macho tu.
 
Mkuu kuna faida kutoka katika hadithi ya abuu hurayrah kwamba mtume swala na salaam ziwe juu yake amesema:

".لا تسبوا الشيطان وتعوذوا بالله من شره"
"msimtukane shetani, na muombeni hifadhi allah kutokana na shari yake"


ameipokea imaam daaraqutni na wametofautiana wanachuoni kunako usahihi wake, naona vyema mkuu tukamuita pasi na kumtukana na allah ameweka uadilifu katika kila kitu.

Na allah ndiye mjuzi zaidi.
Shukrani Al akhy nimejifunza kitu hapo

Asante sana
 
Hakuna nia kwenye kujiita jina baya namna hiyo sisi tumekatazwa kuitana majina mabaya kwenye quran.

".....wala msivunjiane heshima, wala msiitane kwa majina ya kejeli, ni uovu ulioje kutumia jina baya baada ya kuwa mmeamini......"

Qur'an 49:11

Bali zimepokewa athari nyingi kutoka kwa mtume swala na salaam ziwe juu yake akiwabadilisha watu majina baada ya kuwa wana majina ya kijaahiliya yenye maana mbaya kama matatizo, shida, nuksi n.k na akiashiria majina yana athari kwa mtoto.

Wewe unatoa wapi ujasiri wa kujiita ibliys bin shetani? haya hapo juu tumeona unamkosoa allah eti alikosea sana kumwamrisha ibliys kumsujudia aadam, hujakutwa na athari ya jina ulilojibandika bado?.
Kwanza sijui kawaza nini mpaka kajiita Ibilisi yaan anajinasibisha na adui mkubwa WA Allah
 
Ibliys hakuonewa bali alifanya kiburi cha hali ya juu mbele ya mola wake, malaika wabora na watukufu walikubali kumsujudia aadam yeye ni nani akatae wakati ni jini tu miongoni mwa majini? ukiwa na kiburi na husda umechukua sehemu katika tabia za ibliys na ukiwa mwepesi wa kuomba msamaha na maghfirah umechukua sehemu katika tabia za baba yako aadam alayhi ssalaam.

"Na kumbuka tulipowaambia malaika msujudieni aadam! wakasujudu isipokuwa ibliys yeye alikuwa miongoni mwa majini basi akaifanyia uovu amri ya mola wake....je! hivi mnamfanya yeye na kizazi chake kuwa ni vipenzi kinyume na mimi na hali ya kuwa wao kwenu ni maadui? si ubaya ulioje mbadala huu kwa wenye kudhulumu!!!!.."

Qur'an 18:50


Maneno mazito mno haya yenye kutetemesha nyoyo za wale wenye chembe ya iymaan katika vifua vyao.

Mkuu kwa kumalizia sisi waanadamu ni watukufu mno na wenye daraja ya juu miongoni mwa viumbe wa allah, na katika uislamu kukidogesha na kukidharau kile ambacho allah amekitukuza ni ukafiri.

"Kwa hakika tumewatukuza wana wa aadam, na tumewabeba wao nchi kavu na baharini {kwa kuwapa vipando vya nchi kavu na baharini}, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa juu ya wengi miongoni mwa tuliowaumba.."

Qur'an 17:70

Allahul mustaan.
Al akhy ulipwe malipo stahiki Kwa mambo matamu unayotupa wallah tunastafidi Sana mkuu
 
Ndio mitihani hiyo ya maisha mkuu.

Nakumbuka baada ya Magu kuingia madarakani akawatupa baadhi ya watu mikoani.

Baadhi wakawa humble akawarudisha na kuwapa madaraka makubwa.

Wakati mwingine unashushwa ili upandishwe.
Kweli mkuu
 
Hakuna nia kwenye kujiita jina baya namna hiyo sisi tumekatazwa kuitana majina mabaya kwenye quran.

".....wala msivunjiane heshima, wala msiitane kwa majina ya kejeli, ni uovu ulioje kutumia jina baya baada ya kuwa mmeamini......"

Qur'an 49:11

Bali zimepokewa athari nyingi kutoka kwa mtume swala na salaam ziwe juu yake akiwabadilisha watu majina baada ya kuwa wana majina ya kijaahiliya yenye maana mbaya kama matatizo, shida, nuksi n.k na akiashiria majina yana athari kwa mtoto.

Wewe unatoa wapi ujasiri wa kujiita ibliys bin shetani? haya hapo juu tumeona unamkosoa allah eti alikosea sana kumwamrisha ibliys kumsujudia aadam, hujakutwa na athari ya jina ulilojibandika bado?.
Afadhali umelisemea na ndio maana ilibidi nimuulize alichonipa ni jibu la swali au laa, manake twahusiwa kujipamba na mazuri yeye kajipa jina baya akidai nia
 
Nilikuwa busy kiasi halafu usiwazungumzie wanachuoni wetu kama wanafunzi fulani wa day care, hao ni watu waheshimiwa na warithi wa mitume kwasababu mitume hawajarithisha dirham wala dinar bali wamerithisha elimu, na wapokezi wa hiyo elimu ni wanawachuoni wabobezi kwenye elimu hata allah جلّ و على akauunganisha ushahidi wake na wa malaika na wanawachuoni kuonesha hadhi yao na nafasi mbele zake.

"Ameshuhudia allah ya kwamba hapana muabudiwa wa haki isipokuwa yeye tu, na malaika na wenye elimu {nao wanashuhudia hilo}, hali ya kuwa yeye ni mwenye kusimamia uadilifu, hapana muabudiwa wa haki isipokuwa yeye mwenye nguvu na mwenye hekma.."

Qur'an 3:18

Kwa kukuweka sawa kuna madh-hab nne mbele ya ahlu sunnah nayo ni madh-hab ya imaam abuu hanifa, imaam maalik, imaam shafiiy na imam ahmad allah awarehemu wote, hawa wametofautiana katika mambo ya kifiqhi tu na wala hawajatofautiana katika itikadi, so ukitoa mifano ya mwezi na swala ya idi au mwezi wa kitaifa na kimataifa watakucheka watu wenye maarifa siku nyingine usirudie.

Tukirudi kwa ibliys alielaaniwa zimetujia khabari kwa wingi kwenye quran juu ya uovu wake na azma yake ya kuwapoteza wana wa aadam mpaka siku itakapofika ajali yake, wala hakuna faida kujua alikuwa muovu kabla ya kuamrishwa kusujudu kwani hilo halibadili chochote.
Ma shaa allah, allah akuhifadhi
 
Kwanza sijui kawaza nini mpaka kajiita Ibilisi yaan anajinasibisha na adui mkubwa WA Allah
Tuna vijana ambao baada ya kupata maarifa fulani wanatakabbar na kujiona wanaweza kuhoji chochote na kumuhoji yeyote akiwemo allah سبحانه tena bila uoga hata chembe, basi kwa hilo wanafanya wanayoyataka wao ikiwemo hilo unalosemea.
 
Afadhali umelisemea na ndio maana ilibidi nimuulize alichonipa ni jibu la swali au laa, manake twahusiwa kujipamba na mazuri yeye kajipa jina baya akidai nia
Matumizi mabaya ya hadithi za mtume swala na amani ziwe juu yake, hadithi inasema hakika matendo yote huzingatiwa kwa nia, kwa maana malipo yake yatapatikana kwa lile ulilonuia, so umenuia nini kizuri kwa kujiita ibliys mwana wa shetani?.

Hapo ndio nukta ya mzozo.
 
Hakika, allah amlipe kwa muda wake, yan natamani kila siku kuwe na nyuzi za hivi nae atusomeshe ma shaa allah , allah amemfahamisha mengi
اللهم لا تؤاخذني بما يقولون، واغفر لي ما لا يعلمون ،واجعلني خيرا مما يظنون
 
Ila mungu alikosea sana kusema adam amsujidie iblis maana adam kaombwa na udongo dhalili wakati iblis kaumbwa kwa moto na ukitoa jambo la iblis kukataa kumsujudia adam hana jambo baya alilowahi kufanya hapa duniani wakati huyo mwanadamu ana mabaya kila kukicha na baadhi umeyataja kwa makundi ya watu wanaofanya mabaya kunzia madokata wanausalama viongozi

Nakumbuka malaika walimwambia mungu usiumbe mtu binadamu kwakuwa atakuja kuleta fitna mauvo mabaya duniani ila malaika hawakuwahi kumwambia mungu usimuumbe iblis utakuja kuona iblis hana baya ila watu ndio wabaya ila ushauri wako mzuri saana kwa jamii
malaika huwa hasemehewi . wewe ungekuwa huli, hunywi,hulali,huchoki,hunahisia za mapenzi,huna haja na hela, huoi, haufi, nk utafanya dhambi gani sasa?
 
Back
Top Bottom